Ushauri: Ripoti ya CAG isirudiwe tena kusomwa hadharani, inatia hasira na kuleta manung'uniko, wanaotuhumiwa hawajawahi kukamatwa

Ushauri: Ripoti ya CAG isirudiwe tena kusomwa hadharani, inatia hasira na kuleta manung'uniko, wanaotuhumiwa hawajawahi kukamatwa

Kusomwa itabidi isomwe tu maana ni takwa la katiba, ishu ifike mahali wachukue hatua na hatua zionekane kuchukuliwa.

Tatizo hata enzi za mwendazake hakuna aliyeshtakiwa
Kama awamu hiyo ndo ilikuwa hovyo kabisa.

Mwendazake hakutaka kabisa hasara zisomwe, alipenda kusikia faidaza uongo tu ili kuwa manipulate wananchi wengi ambao wana akili ndogondogo na za kinyumbu. Ndo sababu akatibuana na Prof. Assad na kumwondoa kwa kuilawiti katiba.

Charles Kichere alipoteuliwa akaona isiwe tabu, akatusomea faida hadi ATCL, plus magawio kibao kutoka mashirika mbalimbali ya umma! Lakini alipoingia mama tu Charles huyohuyo akatusomea hasara ya ATCL kuwa tangu ifufuliwe ni mwendo wa hasara tu. Na in fact ni not shirika la ndege kupata faida ndani ya muda mfupi tu baada ya kuanza kazi. Hata mashirika makubwa duniani yana struggle kwanza. Ila mwamba yeye kwa kujua aliongoza vilaza akawa anawashushia mifaida ya kwenye karatasi tu, na mdogo wake sasa naona anaadapt kwa bro mambo mengi tu.

Tutaendelea kuwa na mambo ya hovyo as long as tutaendelea kutawaliwa na green mamba.

Hizo report mimi nilishaacha kuzifuatilia.
 
Ukiacha mihemko na hisia hasi kwa kuheshimu taaluma za kikaguzi hutakaa uwaze na kuandika mfano na ulichokiandika.

Hizi ripot zinasaidia sana kukosoa, kurekebisha na kusahihisha njia ambazo hazikuwa sawa hapo awali.

Ukweli huwa na kawaida ya maumivu awali ila ukizoeleka huponya na kufanya kuwa imara. Ipo siku utaona matunda ya hizi ripot na sio vile wewe unavyotaka kwa wakati wako. Kila jambo lina njia yake na wakati wake.

Uishi umri mrefu, uje ujifunze mambo.

Mkuu umezungumza kirahisi mno kama vile sisi hatuijui serikali yetu ambayo ina matatizo yaleyale (kama ufisadi na uzembe) miaka nenda rudi.

Kwa maelezo ya mtoa mada hajaelekeza malalamiko kwa CAG na zoezi lake la ukaguzi, bali kwa wale wanaowasilishiwa taarifa (ambao ndio wenye mamlaka ya kuchukua hatua) hadharani, kwa mbwembwe ambazo mtu akiwa mgeni Tanzania/Africa atadhani kuna mijitu inaenda kunyongwa hadharani, kumbe show imeishia pale.

Na hizo hasara zinazojirudia kila mwaka, sijui ni lini huo ukosoaji, urekebishaji na usahihishaji hufanyika! Au nao ndo tuendelee kusubiri wakati wake haujafika?
 
Wanafalsafa wanatuambia: in the long run we’re all dead! Hiyo siku ya kuwajibishwa hao mafisadi itakuwa na maana endapo tulioshuhudia na kuathirika na maovu yao tutaiona. Nje ya hapo tutakuwa tumetapeliwa na kufanywa mazuzu wa karne.

Inaonekana viongozi wa CCM wanatumia mkakati wa kusukuma muda. Wanafanya kila hila kukatisha tamaa (frustrate) wakosoaji na wapinzani wakielewa kuwa baada ya muda watazeeka na kuchoka na kukaa pembeni. Vijana wao nao wataendeleza hiyo vicious circle wakizidi kutoa ahadi za uongo kwa wananchi kusukuma muda kuendeleza utawala wa kifisadi milele.

Nakumbuka mwanzo wa vyama vingi milango ilipofunguliwa, wapinzani wa Nyerere kina Kambona, Tumbo na Fundikira walijitokeza kuanzisha vyama vya siasa. Siku moja Nyerere alikutana na mmojawao akatabasamu na kumwambia “bwana wewe ndio unataka kuingia kwenye haya mambo leo hii? Wenzio tulishaachana nayo zamani!” Ilikuwa kama kejeli hivi.

Nikakumbuka kusoma jinsi Nyerere alivyosafisha uwanja wa siasa enzi zake na kubaki mwenyewe huku “maadui” zake hatimaye wakiishiwa nguvu na kutawanyikia kusikojulikana. Kisha wakajaribu kuinuka tena bila mafanikio. Bila kujua kwamba it was too late. Nikasema: Indeed, the world is not fair.

Sasa naona mafisadi wa CCM nao wanatumia janja ya muda wakiamini watadanganya vizazi na vizazi vya Watanzania kwa mafanikio. Msiwe na wasi wasi. Kuweni na subra. CCM haina mchezo na mafisadi. Ipo siku watashughulikiwa kikamilifu!
Umeandika ukweli mtupu !
 
hivi huwa husikii,wapo waliokamatwa na kufikishwa mahakamani,pia ufahamu nchi inaendeshwa kwa kuzingatia sheria,hizo ni audit queries zinatakiwa majibu na serikali huzijibu,na ndipo tunapata zipi ni jinai,zipi ni uzembe na zipi ninafutwa
Wamekamatwa akina nani na wako gereza gani ?
 
Ibaki kuwa siri ya Rais na watu wake baasi, maana kiukweli pamoja na madudu yote yanayoanikwa lakini hakuna hata mmoja aliyechukuliwa hatua.

Zaidi ya kuleta manung'uniko na hasira kwa wananchi, hakuna lolote linalofanyika , kuna haja gani sasa ya kutupotezea muda kuangalia na kusikiliza ripoti hiyo?

Acha waendelee kujitafunia mihela yetu ya bure watakavyo waendelee kutuongopea kwamba bado Nchi yetu ni Changa.

Tunawatakia Kila la heri katika ulaji huo wa Nchi.

Hapana. Endelea kusomwa kwa ajili ya kumbukumbu.
 
Mimi Huwa naishangaa jamhuri!!hivi Kuna nini huko jikoni has!?Kuna makubaliano gani hasta kati ya nyie na Rais aliepo madarakani!!?

Huwa mnamwachia nchi aiamue kama familia yake!!?hakuna mstari unaochorwa asivuke!!?

Sasa KAZI ya Cag ni nini!?mbona ripoti hazifanyiwi kazi!!?

Yaani Tatizo Huwa ni nini!!?
Ndugu kaz inafanywa sana si lazima itangazwe.ila kwemye mafail huko kunawaka moto. Unajibu hoja mpaka tumbo linauma na saa nyingine unahamishwa vijijin huko
 
Tuendelee na Mjadala , Teuzi za Hangaya zisitupoteze
 
Back
Top Bottom