USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

Msifanya hii issue ni ya Regia Mtema; John Malecela pia alishafaidika na hii ya Ubunge wa kuteuliwa baada ya wananchi wake kumkataa alipowaambia wapanda treni "YOU CAN GO TO HELL" alikosa Ubunge lakini akateuliwa na Rais...

Kwahiyo akaendeleia na Raha ya kupata Ubunge wa Chee... Kwanini Mwanae haweki hiyo historia sasa???
 
Gaijin ebu fafanua hiyo sayansi ahaa aaa JF siku hizi ukileta za kuleta unatandikwa ngumi za utosini.

Ana wakilisha interest za chama.

Kwa sababu kwanza wananchi wa Kilombero walimkataa jimboni. Pili, hata wanawake wanaounga mkono CHADEMA hawakumchagua, aliteuliwa 'kisayansi'.
 
Ana wakilisha interest za chama.

Kwa sababu kwanza wananchi wa Kilombero walimkataa jimboni. Pili, hata wanawake wanaounga mkono CHADEMA hawakumchagua, aliteuliwa 'kisayansi'.

Duh! Umemaliza kila kitu..

Naogopa tu wasije wakaku-ban maana umesema yote hiyo sayaynsi iliyoko cdm?
 
Ana wakilisha interest za chama.

Kwa sababu kwanza wananchi wa Kilombero walimkataa jimboni. Pili, hata wanawake wanaounga mkono CHADEMA hawakumchagua, aliteuliwa 'kisayansi'.
Haaa! haa! hapana mkuu wangu tusifanye dhihaka hili sii swala la Regia Mtema ni mfumo wa utawala ktk bunge letu ambao haufai kabisa...Chadema walilazimika kuchagua wabunge kutokana na mfumo huu kupitishwa. Yeye na wabunge wengine wengi wa viti maalum ni kati ya walofaidika na mpango huu wa Utawala, sasa kinachotakiwa ni sisi kuuliza wanawakilisha kina nani?

Kama wanawakilisha vyama hapo ndipo tunarudi kuelewa kwa nini muswada wa Katiba mpya umeshindikana kupitishwa kwa sababu CCM ina wabunge wengi wa viti hivi kukiwakilisha chama badala ya wananchi. Pia swala zima la Katiba mpya limekuwa la kisiasa zaidi ya ukweli kwamba huu ni mwongozo wa nchi nzima na wananchi ndio wanatakiwa kuwa chanzo cha katiba mpya.
 
Mkuu umejuaje kama haikuwa sababu? W.J.Malecela kazungumzia ujumla wa mfumo huu hakusema Regia wala nngu007..Mfumo haufai na tuujadili na sii W.J Malecela kama ulivyofanya wewe. Unaona haki kumjadili Malecela lakini siii Regia?
 
Picha nzuri au mbaya...wewe unapenda demokrasia kamili au nusu yake??


kama wakigombea wakashindwa, basi hiyo ndiyo sauti ya wapiga kura....!

Demokrasia wewe unaipima kwa vipi?
 
Gaijin ebu fafanua hiyo sayansi ahaa aaa JF siku hizi ukileta za kuleta unatandikwa ngumi za utosini.


Hapana mkuu mie nanukuu maneno ya Kitila pamoja na viongozi wengine wa chama walosema kuwa uchaguzi wa wabunge wa viti maalum Chadema haukuwa wa upendeleo, kwa sababu walichaguliwa kwa "mfumo wa kisayansi"

Mie sikuona "usayansi" wake ndio maana nikaweka hizo alama.
 


Hivi hujui vitimaalum vinawakilisha nini? Ni kwelim mfumo dume umetupumbaza sana wabongo. Kuna maeneo wanawake wanakubalika kwa lolote kuna maeneo hawakubaliki, hata hivyo kushinda kwao si ndo kusema mfumo dume haupo kuna mambo mengi yapo nyuma. Ngoja nikuulize swali hivi ingekuwa kuna uwakilshi wa wanaume kwa mikoa au hata wilaya na wale wa majimbo wapo tungesema nini katika hilo?

wabunge wa vitimaalumu hawateuliwi kamwe, kaperuzi vizuri, ndo uje na hoja ya kusema atamwakilisha yule aliyemteua. au nikuulize nani anateua vitimaalumu?
 
Katiba Mpya pia izuie Wabunge kuoana Kama ilivyotokea kwa Wazazi wako na Ubunge uwe na Kikomo kama Urais sio mpaka mtu anazeekea Bungeni kama Mzee Malecela.
Nilifikiri mtu akiwa mbunge anakuwa na busara! ona sasa fyongo unazomwaga, umezidi kuaibisha na kudharaulisha ubunge wa viti maalum, suala la wabunge kuoana halina mantiki yeyote katika muktadha huu, bora ungejenga hoja kuonesha umuhimu wa viti maalum na sio huu ushuzi uliotujambia humu ndani,shame on you! sikutegemea mtu kama wewe uje na hoja ya kumshambulia mtu kifamilia wakati yeye ametoa hoja ambayo iko very general,shame on you once again!
 

ahsanteni kwa kujitambua ninyi wachache lakini wengi wenu wapenda vya bure mwishowe wanatumikishwa kama robo war.
 


Sijakataa kama hatuwezi najua tunaweza sana tena kushinda hao wababa na kamwe si nga'ng'anii viti maalumu , suala ni kuwa watanzania bado hatujamkubali mwanamke kwa 100% awe kiongozi, nachelea kusema kuna baadhi ya maeneo hata mwanamke awe mzuri kiasi gani hawatamchagua. Utasikia we mwanamke tu utaniambia nini? Shida yangu kubwa ni hoja ya mchanganyiko(ratio) bungeni.
 

Ni kweli kuwa Chadema walilazimika kuchagua hao kwa sababu mfumo upo tayari, lakini chama hakijaonyesha kutokubaliana na mfumo huo uliopo.

Katika sera na ajenda zao za hatua zinazofaa kuchukuliwa ili serikali ibane matumizi, hatujawasikia kulitaja hili hata wakati mmoja ikitoa picha kuwa wapo sambamba na CCM katika kuukubali mfumo huo. Ukiangalia pia wabunge waliochaguliwa na Chadema kushika nafasi hizo, huoni tofauti yoyote na CCM. Wote wamejaza ndugu, jamaa na marafiki
 
Ana wakilisha interest za chama.

Kwa sababu kwanza wananchi wa Kilombero walimkataa jimboni. Pili, hata wanawake wanaounga mkono CHADEMA hawakumchagua, aliteuliwa 'kisayansi'.
uncalled for mwalimu....
 
uncalled for mwalimu....

Its the truth! Tatizo letu Watanzania hatutaki kusema ukweli kisa tunaogopa kuumiza hisia za watu.

Yeye ni public figure na ninachokizungumza sio siri wala kuingilia maisha yake binafsi; ni facts ambazo zipo wazi na kila mtu anazijua.
 


Wapo wa majimbo wantia saini na kuondoka, wpowapo tu? hivi bungeni ni suala la utetezi wa majimbo tu? hakuna masuala ya kitaifa? mbona mi ndo naona ni mengi kuliko kutetea hayo majimbo mnayosema. Na hata sioni maendeleo ya majimbo yha hao vidume eti mbunge katetea. Jamani yote hii kisa mwanamke ndo kapewa hiyo nafasi, wanume roho zinawatokaaaa.

VITIMAALUM VIDUMU MILELE, JK TUNAUNGAA MKONO HOJA WA KUFANYA WANAWAKE WAFIKIE 50% BUNGENI TENA KWA NGUVU YA KUPEWA IWE KWA UKIMADA, UKE, USHOGA, MERITS, GOD KNOWS.

 

mifumo mifumo mifumo m kila kitu mfumo, what's this!? mfume dume,mfume kristo, i can't understand and am confused! kwa nini kuna mfumo dume,ulianzaje mfumo huo na kwa nini isiwe mfumo jike!? jibu lake nadhani halina tofauti na ukijiuliza kwa nini nchi za magharibi(ulaya) zimeendelea kuliko Afrika, walitutawala-kwanini sisi hatukuwatawala wao!? which is which!? mfumo dume ulikuja automatically,by will au kwa kutumia nguvu? na kama kwa kutumia nguvu kwanini wanaume wawe na nguvu kuliko wanawake na isiwe viceversa?
 
Mkuu umejuaje kama haikuwa sababu? W.J.Malecela kazungumzia ujumla wa mfumo huu hakusema Regia wala nngu007..Mfumo haufai na tuujadili na sii W.J Malecela kama ulivyofanya wewe. Unaona haki kumjadili Malecela lakini siii Regia?

Opportunist... Kwanini asiongelee NEC kwanini baba yake Bado ni Mjumbe CC ya CCM na wakati ameshaenguliwa?

Kuna Ulafi fulani ukiwa ndani ya vyombo hivyo Nchini... Angeanzia Ndani ya Chama Cha CCM kama anataka kusafisha sio juu juu tu na pick and point...
 

Hivi unajua kuwa sasa hivi wapiga kura tanzania wengi ni wanawake? Sasa wameshindwa nini kuwapigia kura wanawake wenzao? Na akina Makinda na Mdee wanashinda kwa kura za akina nani? Hoja yako dhaifu ndugu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…