Ushauri: Tufundishe Kiswahili na English kuanzia darasa la kwanza kwa manufaa ya taifa

Ushauri: Tufundishe Kiswahili na English kuanzia darasa la kwanza kwa manufaa ya taifa

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Tunataka English tu kiswahili kila mtu anajua

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Miye kama mwalimu siku nikipata rungu la uongozi,kiingereza kitafundishwa chekechea Hadi chuo kikuuu
 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Sijawaelewa kabisa, yaani sababu ya kufundishia Kiingereza ni mfano wa huyo mtoto wa kaka yako kenda kusoma Marekani na kapata kazi ya dollar 65 elfu kwa sabau gani? Kiingereza!
Je, ni asilimia ngapi ya Wanafunzi wetu husoma Marekani au nchiza Kiingereza kuliko sehemu nyinginezo?

Vipi kuhusu Watoto wanao kwenda kusoma Sweden, Germany, Ufaransa, Maleysia, China, India, Uturuki, Misri n.k hawa watafaidikaje na Kiingereza?

Hivi kwa nini Waafrika tunashindwa kuondokana na akili ya kitumwa? Kuna Wahindi Wangapi na Wachina, Waspanish, na mataifa mengine Marekani walofundishwa huko makwao kwa lugha zao wanashika nafasi kubwa na za juu Marekani? Hapo Tanzania kuna Wachina na Wahindi hata kiingereza hawajui na wameshika wadhifa wa juu katika ajira zetu wenyewe! Sababu ni lugha au Uelewa wa kazi husika! Hivi accounting 2 ni two sio mbili?

Isitoshe, msomi mzuri Tanzania anaweza kabisa kupata Usd elfu 3 mlaka 5 kwa mwezi Tanzania ambazo kwa maisha ya Tanzania ni sawa au zaidi ya hizo Elfu 65 Marekani, na mchango wa elimu zao kwa lugha yetu utawasaidia Watanzania hata Wananchi walioko vijijini.

Elimu haina lugha, lugha yoyote inaweza fundishie Elimu muhimu ni kutambua lugha ipi inaweza kuwapa Wanafunzi Uelewa wa haraka. Watu wanajifunza Kiingereza kama lugha ya mawasiliano tu sio Elimu. Wapo Waingereza hawajui hata kusoma na kuandika kama ilivyo Kiswahili wapo waswahili hawajii kusoma wala kuandika. Pia wapo Watu Tanzania wanazungumza kiingereza safi kabisa lakini hawakumaliza kidato cha nne. Je hawa pia ni wasomi?

Isitoshe dunia hii ni nchi chache sana zilokuwa tawala za Muingereza ndizo zinatumia kiingereza kufundishia Nyingi zipi Africa!

Kwa nini basintunabeba Kiingereza ikiwa bara la Afrika pekee kule west wamebeba Kifaransa, Kasikazini Kiarabu, kusini Angola na Msumbiji wanafundishia Kireno. Na hakuna nchi hata moja baina yetu iwe kwa Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa au Kireno wamesoma ama wana Elimu zaidi ya wengine.

Kiswahili ni lugha yetu kwa nini tunaipiga gira sisi wenyewe wakato hii Lugha pekee ni somo kubwa la Ajira duniani. Sasa hivi hakuna nchi isiyokuwa na soko la lugha hii katika vyuo na jumuiya mbali mbali (Community centre). Jumuiya ya EA na SADC pekee kuna soko la kutosha nchi zote hizi zinataka kutimia Kiswahilu kama.lugha yao ya Taita acha kufundishia!

Sisi wenye lugha ndio kwanza tunaikana kutaka Uzungu kamakwamba ukizungumza kiingereza ndio una elimu saana!. Inasikitisha sana kuona Watanzania tulivyolala!
 
Sijawaelewa kabisa, yaani sababu ya kufundishia Kiingereza ni mfano wa huyo mtoto wa kaka yako kenda kusoma Marekani na kapata kazi ya dollar 65 elfu kwa sabau gani? Kiingereza!
Je, ni asilimia ngapi ya Wanafunzi wetu husoma Marekani au nchiza Kiingereza kuliko sehemu nyinginezo?

Vipi kuhusu Watoto wanao kwenda kusoma Sweden, Germany, Ufaransa, Maleysia, China, India, Uturuki, Misri n.k hawa watafaidikaje na Kiingereza?

Hivi kwa nini Waafrika tunashindwa kuondokana na akili ya kitumwa? Kuna Wahindi Wangapi na Wachina, Waspanish, na mataifa mengine Marekani walofundishwa huko makwao kwa lugha zao wanashika nafasi kubwa na za juu Marekani? Hapo Tanzania kuna Wachina na Wahindi hata kiingereza hawajui na wameshika wadhifa wa juu katika ajira zetu wenyewe! Sababu ni lugha au Uelewa wa kazi husika! Hivi accounting 2 ni two sio mbili?

Isitoshe, msomi mzuri Tanzania anaweza kabisa kupata Usd elfu 3 mlaka 5 kwa mwezi Tanzania ambazo kwa maisha ya Tanzania ni sawa au zaidi ya hizo Elfu 65 Marekani, na mchango wa elimu zao kwa lugha yetu utawasaidia Watanzania hata Wananchi walioko vijijini.

Elimu haina lugha, lugha yoyote inaweza fundishie Elimu muhimu ni kutambua lugha ipi inaweza kuwapa Wanafunzi Uelewa wa haraka. Watu wanajifunza Kiingereza kama lugha ya mawasiliano tu sio Elimu. Wapo Waingereza hawajui hata kusoma na kuandika kama ilivyo Kiswahili wapo waswahili hawajii kusoma wala kuandika. Pia wapo Watu Tanzania wanazungumza kiingereza safi kabisa lakini hawakumaliza kidato cha nne. Je hawa pia ni wasomi?

Isitoshe dunia hii ni nchi chache sana zilokuwa tawala za Muingereza ndizo zinatumia kiingereza kufundishia Nyingi zipi Africa!

Kwa nini basintunabeba Kiingereza ikiwa bara la Afrika pekee kule west wamebeba Kifaransa, Kasikazini Kiarabu, kusini Angola na Msumbiji wanafundishia Kireno. Na hakuna nchi hata moja baina yetu iwe kwa Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa au Kireno wamesoma ama wana Elimu zaidi ya wengine.

Kiswahili ni lugha yetu kwa nini tunaipiga gira sisi wenyewe wakato hii Lugha pekee ni somo kubwa la Ajira duniani. Sasa hivi hakuna nchi isiyokuwa na soko la lugha hii katika vyuo na jumuiya mbali mbali (Community centre). Jumuiya ya EA na SADC pekee kuna soko la kutosha nchi zote hizi zinataka kutimia Kiswahilu kama.lugha yao ya Taita acha kufundishia!

Sisi wenye lugha ndio kwanza tunaikana kutaka Uzungu kamakwamba ukizungumza kiingereza ndio una elimu saana!. Inasikitisha sana kuona Watanzania tulivyolala!

Najua ni ngumu kuelewa kwa watu wengine mawazo yetu ni ya mbali kuliko maono ya wengi

Mtoto wa kama yangu ni mfano tu . Mfano mwingine ni Kenya. Uwekezaji wa Kenya kwenye teknologia uko wazi na sababu zao wamezisema wiki mbili tu nilikuwa naongea na uongozi na NALA walieleza hili. Tusikimbilie kujilinganisha na Sweden ambayo ukienda mtaani unaweza kutumia English! Ndiyo maana nimetumia mfano wa Kenya.

Kama kweli English sio muhimu ni kwanini watoto wa viongozi wote wanatumia zaidi $10,000 kuwalipia watoto tena shule za msingi? Je wanapoteza pesa au? Na kwanini watoto wa wengine wasiweze kusoma English kama watoto wao. Tujiulize maswali kabla ya kudakia vitu kishabiki

Kwanini mwigulu mtoto wake anasoma shule hii na sio ya kata?

 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Achana na Kiswahili kwa kuwa watakujuwa tu wapende wasipende. Ila weka emphasis kwenye ENGLISH tu ndiyo tutaweza ku-match na soko la ajira, teknolojia na sayansi ambavyo ni vitu vya muhimu kwenye maendeleo
 
Wameziba masikio.. limesemwa sana hili hapa!
 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Hili nalo likatazamwe. Bila mawasiliano hakuna kuelewana. Kwa bahati nzuri au mbaya, Wawekezaji wengi wanatumia lugha ya Kiingereza. Vitendea kazi (Vifaa) vingi e.g. Computers, Medical equipments, Scientific /Research etc vina maelekezo ya matumizi kwa lugha ya Kiingereza. Hata hapa kwetu (Bongo) oral interview hufanyika kwa Kiingereza. Ukienda nchi za nje documents zako ziwe ni kwa Kiingereza. Tutakwepea wapi? Hatuna budi kukubali kumeza dawa chungu.
 
Hili nalo likatazamwe. Bila mawasiliano hakuna kuelewana. Kwa bahati nzuri au mbaya, Wawekezaji wengi wanatumia lugha ya Kiingereza. Vitendea kazi (Vifaa) vingi e.g. Computers, Medical equipments, Scientific /Research etc vina maelekezo ya matumizi kwa lugha ya Kiingereza. Hata hapa kwetu (Bongo) oral interview hufanyika kwa Kiingereza. Ukienda nchi za nje documents zako ziwe ni kwa Kiingereza. Tutakwepea wapi? Hatuna budi kukubali kumeza dawa chungu.

Lakini vilevile vitabu karibu vyote vina copy za kiingereza.

Tusishangae wenye pesa wanapeleka watoto kwenye shule za English kuanzia darasa la kwanza sio wajinga! Tatizo watu wa chini hawajiulizi haya
1681749237226.png
 
Sijawaelewa kabisa, yaani sababu ya kufundishia Kiingereza ni mfano wa huyo mtoto wa kaka yako kenda kusoma Marekani na kapata kazi ya dollar 65 elfu kwa sabau gani? Kiingereza!
Je, ni asilimia ngapi ya Wanafunzi wetu husoma Marekani au nchiza Kiingereza kuliko sehemu nyinginezo?

Vipi kuhusu Watoto wanao kwenda kusoma Sweden, Germany, Ufaransa, Maleysia, China, India, Uturuki, Misri n.k hawa watafaidikaje na Kiingereza?

Hivi kwa nini Waafrika tunashindwa kuondokana na akili ya kitumwa? Kuna Wahindi Wangapi na Wachina, Waspanish, na mataifa mengine Marekani walofundishwa huko makwao kwa lugha zao wanashika nafasi kubwa na za juu Marekani? Hapo Tanzania kuna Wachina na Wahindi hata kiingereza hawajui na wameshika wadhifa wa juu katika ajira zetu wenyewe! Sababu ni lugha au Uelewa wa kazi husika! Hivi accounting 2 ni two sio mbili?

Isitoshe, msomi mzuri Tanzania anaweza kabisa kupata Usd elfu 3 mlaka 5 kwa mwezi Tanzania ambazo kwa maisha ya Tanzania ni sawa au zaidi ya hizo Elfu 65 Marekani, na mchango wa elimu zao kwa lugha yetu utawasaidia Watanzania hata Wananchi walioko vijijini.

Elimu haina lugha, lugha yoyote inaweza fundishie Elimu muhimu ni kutambua lugha ipi inaweza kuwapa Wanafunzi Uelewa wa haraka. Watu wanajifunza Kiingereza kama lugha ya mawasiliano tu sio Elimu. Wapo Waingereza hawajui hata kusoma na kuandika kama ilivyo Kiswahili wapo waswahili hawajii kusoma wala kuandika. Pia wapo Watu Tanzania wanazungumza kiingereza safi kabisa lakini hawakumaliza kidato cha nne. Je hawa pia ni wasomi?

Isitoshe dunia hii ni nchi chache sana zilokuwa tawala za Muingereza ndizo zinatumia kiingereza kufundishia Nyingi zipi Africa!

Kwa nini basintunabeba Kiingereza ikiwa bara la Afrika pekee kule west wamebeba Kifaransa, Kasikazini Kiarabu, kusini Angola na Msumbiji wanafundishia Kireno. Na hakuna nchi hata moja baina yetu iwe kwa Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa au Kireno wamesoma ama wana Elimu zaidi ya wengine.

Kiswahili ni lugha yetu kwa nini tunaipiga gira sisi wenyewe wakato hii Lugha pekee ni somo kubwa la Ajira duniani. Sasa hivi hakuna nchi isiyokuwa na soko la lugha hii katika vyuo na jumuiya mbali mbali (Community centre). Jumuiya ya EA na SADC pekee kuna soko la kutosha nchi zote hizi zinataka kutimia Kiswahilu kama.lugha yao ya Taita acha kufundishia!

Sisi wenye lugha ndio kwanza tunaikana kutaka Uzungu kamakwamba ukizungumza kiingereza ndio una elimu saana!. Inasikitisha sana kuona Watanzania tulivyolala!
Hoja ipo wazi tusome kingereza lugha ya Dunia

Lugha zingine ziada
 
Kiswahili kinakuwa sana na Tanzania tunapata heshima sana kwa lugha yetu hii. Hii naina maana tusifundishe watoto wetu kiingereza-English kuanzia darasa la kwanza. Inasikitisha sana viongozi wetu wana aminisha kwamba hakuna umuhimu wa kujua kufundisha English kwa elimu ya msingi wakati watoto wao karibu wote wanasoma shule ambazo zinafundisha kiingereza kuanzia msingi!. Hili swala halitakiwi kuwa na watu wenye uwezo na hali ya juu pekee.

Mimi sipendi sana kuongea vitu kwa hisia nitatoa mfano wa ukweli kwa familia yetu. Mtoto wa Kaka yangu amesoma Tanzania English media kuanzia darasa la kwanza amekuja huku akiwa na miaka 18 na kujiunga na community college kwa miaka miwili na baadae akaenda kumaliza degree ya Accounting Mississipi. Mwaka jana akiwa na miaka 22 kabla hajafika miaka 23 tayari kapata kazi, kampuni imempa visa maalumu ya miaka mitatu ya wafanyakazi HB1 visa, na analipwa dollar $65,000 kwa mwaka ambayo ni Tsh 152,490,003. Huyu mtoto ameweza kushindana na wenzake kupata kazi kwasababu ana uwezo mkubwa wa kujieleza na kujua kiingereza vizuri. Nasema hivi si kwa kujigamba bali kuonyesha hili sio swala la watu fulani linawezakana kwa kila mtoto kupata elimu ya hivi.

Tanzania tunaenda kwenye kushindana kampuni nyingi za teknologia mfano zinaenda kuwekeza Kenya kwasabbu ya mfumo wa elimu yao wakati Tanzania tumepata uwekezaji usiozidi $200M wenzetu Kenya wamepata uwekezaji zaidi ya $2B kwenye teknologia kuanzia microsoft, google na kampuni nyingine kubwa. Tofauti ni English tu na ukiangalia wanafunzi wetu wanaosoma english media wakienda Kenya au kuja nchi kama USA wana uwezo sawa au hata zaidi ya wale wa Kenya.

Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media. Kama tunatatizo la walimu basi tulitatue ikiwa na pamoja na kubadilishana walimu na kenya na uganda kwa sisi tuwapeleke kwa muda walimu wa kiswahili kwao na wao watupe walimu wa english

Tukishinda hapa kupigana madongo ukweli ni kwamba watoto wa masikini tu ndiyo wanakosa nafasi. Kuweni makini sana na mashabiki.
Nimeipenda hapo uliposema "Watoto wao wanasoma English medium"....umemaliza 😅😅😅
 
Lakini vilevile vitabu karibu vyote vina copy za kiingereza.

Tusishangae wenye pesa wanapeleka watoto kwenye shule za English kuanzia darasa la kwanza sio wajinga! Tatizo watu wa chini hawajiulizi hayaView attachment 2591231
Kumbe wawakilishi wetu (Wabunge)wangelipeleka mswada au utaratibu wa lazima masomo hayo yaanzie toka mwanzo chini kabisa ngazi ya chekechea kupanda juu.
Hapo ni kweli. Wanaopeleka watoto wao English medium wengi wao ndo viongozi wetu na matajiri. Hakika wanayo Agenda. Tuamke.
 
Nashauri tusiweke mazingira ya uongo ya kuaminisha wananchi kwamba tukifundisha watoto wetu english kuanzia darasa la kwanza ni kutokuwa wazalendo wakati viongozi wetu wanasomesha watoto wao english media.
Ni kweli. Hakuna kiongozi anayempeleka mwanaye kusoma shule za kata (a.k.a St. Kayumba).

Kama ndiyo uzalendo kwann wao wanazikimbia shule zinazofundisha kiswahili??
 
Sijawaelewa kabisa, yaani sababu ya kufundishia Kiingereza ni mfano wa huyo mtoto wa kaka yako kenda kusoma Marekani na kapata kazi ya dollar 65 elfu kwa sabau gani? Kiingereza!
Je, ni asilimia ngapi ya Wanafunzi wetu husoma Marekani au nchiza Kiingereza kuliko sehemu nyinginezo?

Vipi kuhusu Watoto wanao kwenda kusoma Sweden, Germany, Ufaransa, Maleysia, China, India, Uturuki, Misri n.k hawa watafaidikaje na Kiingereza?

Hivi kwa nini Waafrika tunashindwa kuondokana na akili ya kitumwa? Kuna Wahindi Wangapi na Wachina, Waspanish, na mataifa mengine Marekani walofundishwa huko makwao kwa lugha zao wanashika nafasi kubwa na za juu Marekani? Hapo Tanzania kuna Wachina na Wahindi hata kiingereza hawajui na wameshika wadhifa wa juu katika ajira zetu wenyewe! Sababu ni lugha au Uelewa wa kazi husika! Hivi accounting 2 ni two sio mbili?

Isitoshe, msomi mzuri Tanzania anaweza kabisa kupata Usd elfu 3 mlaka 5 kwa mwezi Tanzania ambazo kwa maisha ya Tanzania ni sawa au zaidi ya hizo Elfu 65 Marekani, na mchango wa elimu zao kwa lugha yetu utawasaidia Watanzania hata Wananchi walioko vijijini.

Elimu haina lugha, lugha yoyote inaweza fundishie Elimu muhimu ni kutambua lugha ipi inaweza kuwapa Wanafunzi Uelewa wa haraka. Watu wanajifunza Kiingereza kama lugha ya mawasiliano tu sio Elimu. Wapo Waingereza hawajui hata kusoma na kuandika kama ilivyo Kiswahili wapo waswahili hawajii kusoma wala kuandika. Pia wapo Watu Tanzania wanazungumza kiingereza safi kabisa lakini hawakumaliza kidato cha nne. Je hawa pia ni wasomi?

Isitoshe dunia hii ni nchi chache sana zilokuwa tawala za Muingereza ndizo zinatumia kiingereza kufundishia Nyingi zipi Africa!

Kwa nini basintunabeba Kiingereza ikiwa bara la Afrika pekee kule west wamebeba Kifaransa, Kasikazini Kiarabu, kusini Angola na Msumbiji wanafundishia Kireno. Na hakuna nchi hata moja baina yetu iwe kwa Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa au Kireno wamesoma ama wana Elimu zaidi ya wengine.

Kiswahili ni lugha yetu kwa nini tunaipiga gira sisi wenyewe wakato hii Lugha pekee ni somo kubwa la Ajira duniani. Sasa hivi hakuna nchi isiyokuwa na soko la lugha hii katika vyuo na jumuiya mbali mbali (Community centre). Jumuiya ya EA na SADC pekee kuna soko la kutosha nchi zote hizi zinataka kutimia Kiswahilu kama.lugha yao ya Taita acha kufundishia!

Sisi wenye lugha ndio kwanza tunaikana kutaka Uzungu kamakwamba ukizungumza kiingereza ndio una elimu saana!. Inasikitisha sana kuona Watanzania tulivyolala!
Hayo mataifa uliyotaja ukimtoa mchina, walikuwa watawala wetu na wametuzidi kwenye kila kitu,hebu rejea vitabu tunavyovisoma huko shuleni ni copy na paste ya mitaala ya magharibi, sasa je tutaikwepaje lugha yao eti tujiite wataalamu.

Sikia kama unataka kuwakwepa magharibi kwa hivi sasa na wewe ni Mwafrika "Anza kwa kurudisha maendeleo yako yote hadi kwenye ujima".

Tuanze na viwanda vyetu vya mawe halafu tuponde ponde vyuma baada ya kuvitoa kwenye tanuru ndipo tuanze kuandika vitabu vyetu kwa kiswahili jinsi ya kuchimba na kuboresha vyuma vyetu.

Siyo unachukua gari au simu ya mchina unataka juu kwa juu ubadilishe majina ya vifaa (baada ya wao kutengeneza) na kujiita mtaalamu....

Je utaweza kuanzia tulipoishia kwenye (ujima na ukabaila).?
 
Hoja ipo wazi tusome kingereza lugha ya Dunia

Lugha zingine ziada
Ok. Na kama Kiingereza hakipandi basi soma Kifaransa au jifunze lugha nyingine ya Kimataifa. Ila Kiingereza ni #1 kwani mifumo mingi ya uendeshaji hapa Tz hutumia Kiingereza e.g. Mahakama, Banks, Research Services, Afya n.k.
 
Ni kweli. Hakuna kiongozi anayempeleka mwanaye kusoma shule za kata (a.k.a St. Kayumba).

Kama ndiyo uzalendo kwann wao wanazikimbia shule zinazofundisha kiswahili??
Hapo tusimungunye maneno. Kwa viongozi kuwapeleka watoto wao English medium Schools ni kupandikiza Mbegu ya UBAGUZI. Kwa mfano hata siku hizi watoto wenyewe utawasikia wakizomeana " hee, huyu mwenzio anasoma ingilish". Halafu wakati huo viongozi wanakazania kujenga vyoo matundu cjui 8 etc. Badala ya kujikita kwenye Planning ya Future ya watoto hao. Watakunya kwenye vyoo hivyo miaka 7 (shule za msingi) halafu baada ya hapo inakuwaje?? Akienda Form One, mwalimu ana kazi nzito sana kwani vitabu vyote vimeandikwa kwa Kiingereza. Mwanafunzi ndo usiseme kwani lazima awe na Standard English - Swahili dictionary mkononi vinginevyo anaona maruweruwe tu.Na hizi kamusi hazina maneno ya kisayansi (Biology, physics,Chemistry) na Mathematics Jamani viongozi wetu Iweni na Huruma.
 
lugha ya kingereza itumike kufundishia masomo yote kuanzia awali mpaka chuo kikuu
pia mfumo wa mtaala usukwe upya haingii akilini kumfundisha mtu simu ya maneo ana itumia wapi? ,nadharia zipunguzwe kama si kuondolewa kabisa kuwe na mtaala unao endana na veta kila kijana awe na ujuzi pia somo la kilimo liwe ni lazima upende usipende tena liwe kigezo kikuu kupata mkopo popote pale mapori ni mengi sana tunaweza kulisha afrika mashariki na kati
 
lugha ya kingereza itumike kufundishia masomo yote kuanzia awali mpaka chuo kikuu
Naunga mkono hoja 100%+. Ikumbukwe Tz sio kisiwa. Mfano hai ni watoto wa viongozi wetu wanaosoma Eng.Medium. Kama ingekuwa sio kitu muhimu kwa nini viongozi hao waingie gharama hizo? Wanatupiga upofu sisi ngurumbili halafu wao wanasonga mbele. Itafika mahali watoto hao ndo watakuwa na vigezo kwenye nafasi za ajira ndani na nje ya Tz.(Soko la Ajira). Wakati huo watoto wa kwetu watakuwa weshapitwa na wakati.😱
emoji23.png
 
Back
Top Bottom