Joseph lebai
JF-Expert Member
- Jul 19, 2017
- 8,452
- 8,670
Pole sana ndugu Yangu.Salaam wanajamvi,
Jamani naomba mnipe ushauri kutoka kwenu hasa kwa wale waliofanikiwa kimaisha.
Kwanza naweza sema hapa Tanzania kusoma sana ndo kuukaribisha umasikini tu.
Kijana mimi wa kitanzania mwenye elimu ya Bachelor degree na Postgraduate Diploma hadi sasa nagonga 30 years sina cha maana ninachomiliki katika maisha yangu.
Sijui kwa sababu nimetumia muda mwingi kusoma, au hii familia niliyozaliwa ya umasikini ndo chanzo hata sijui.
Nilisoma kwa mkopo wa serikali na postgraduate nikafadhiliwa kwa kujua kwamba nikimaliza nitaingia kwenye system kupitia ualimu wa masomo ya arts imekua ndivyo sivyo.
Umri unaenda sina mtaji sina ndugu wa kuniwezesha kwa chochote kazi zimekua ngumu so nategemea kudra za Mwenyezi Mungu labda nitafanikiwa.
Najishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato lakini hakikidhi mahitaji napata hela ya kula, kulipa kodi miezi 2 2 au 1.
Nina mtoto anaishi kwa mama yake, najisikia vibaya kumwona mwanangu anakua lakini hadi sasa baba yake similiki chochote kitakachomsaidia, mama yake ndo anauwezo kwa sasa wa kumjengea mazingira bora coz kipato chake kinatosha kabisa.
Sina ninachomiliki jamani, naombeni ushauri njia bora ya kuishi, namna ya kufanya ili nami niweze kutoka katika dimbwi hili la umaskini, nakiri kwamba nimesoma na kwa sasa sina ndoto tena ya kutaka kuajiriwa nina ndoto ya kujiajiri lakini sijui wapi napata mtaji, labda itokee nipate ajira ya uhakika ya kupata salary bila usumbufu hapo nitajipanga kudunduliza hela nipate japo mtaji.
Umasikini mbaya sana. Na elimu ya Tanzania inachochea umasikini.
Nipeni ushauri jamani ili mwaka 2018 niwe mtu mpya nijue nini nifanye nami nimiliki japo biashara hata ya kuuza juice, banana power hata shujaa vodka.
Ushauri tafadhali, sihitaji maneno ya kejeli nina frustration zangu.
NAWASILISHA
Asante mkuu kwa kunitia moyo,be blessed chiefPole sana ndugu Yangu.
Maneno yako yameugusa moyo wangu.
Wakati nilipomaliza shule, nilikaa Kitaa, hadi nikaona kusoma hakuna faida. Nilishindwa maisha na rafiki zangu bodaboda, nikajiuliza maswali bila majibu japo sikuwa njaa sana ila nilijiona vibaya mno.
Kwa sasa, niko vizuri kiasi changu. Huwa nikijitathmini na kucheck nilipofikia, napiga magoti na kumshukuru huyu Yesu Kristo tunayemuabudu.
Usikate tamaa ndugu Yangu, Mungu hajakusahau. Ipo siku yako tu.
Madini hayaNahisi shida yako ni malengo na mtazamo wako wakimaisha mjomba.
1. Ulivo kuwa unasoma ulisoma kwa malengo yapi??...Je ulijitahidi kwa nguvu zako zote kuwa mmoja wa wanafunzi bora darasani kwako?? Ulijenga urafiki na wanafunzi wenzako na waalimu wako??
2. Je..hapo kwenye kazi yako ya sasa unafanya kwa malengo yapi? Unajitahidi kwa mfanyakazi bora au unaweka jitihada zozote za ziada kuwazidi wenzako?? Je wewe ni kwanza kufika, wa mwisho kutoka?? Unafanya kazi hata wikiendi au sikukuu ukihitajika?? Mahusiano yako na wenzako na boss yakoje?? Unatambua thamani yako kama mfanyakazi?? Je, mwajiri wako akitaka kufukuza watu kazini...je atakufukuza kirahisi au wewe ni mtu tegemeo sana kwake??
3. Kama umejiajiri, unafungua ofisi yako au biashara yako saa ngapi?? Na je unafunga saa ngapi?? Ubora wa huduma yako kuwazidi wengine ukoje?? Je ni mcheshi, mchangamfu na mtu wa watu.... au ni mtu mwenye stress na mawazo mda wote? Je unawapa wateja wako sababu yakuja kwako na wasiende kwa wengine??
4. Kwenye kila hatua ya maisha..jiulize unataka kufanikisha nini....na nini unachokifanya cha ziada kuwazidi wengine kufanikisha malengo yako. Wasomi ni wengi, uwe msomi bora.....wafanyakazi ni wengi uwe mfanyakazi bora......mamantilie ni wengi uwe mamantilie bora......machinga ni wengi uwe machinga bora....n.k..........FANYA KITU CHA ZIADA KILA SIKU UJE UTUPE MREJESHO BAADA YA MWAKA.
Mkuu laiti ungeona smartphone yangu huwez amini ndo nacomment apa. Bando lenyewe ni free basics na mb 450 wiki nzima kutoka halotel, jero tu. Ni umasikini usiopingikaNaona kama unamiliki smartphone na unaweza kununua bundle we sio maskini
Nicheki 0685580057kuni unauzia wapi mkuu?? nna shamba langu maeneo ya vigwaza nlitaka kukata miti nichome mkaa ila mlolongo nlopewa huko maliasili ilibid niweke pause kwanza,,vibali ulipataje??
Real ...uko sirious tufanye kaz mkuu ???......nicheki ka utawezamkuu maisha yanatupiga mjini hapa..
acha tu tuseme
Uko tayar tupige job sirious mkuu ??Pole mwaya, mm mwnywe umri umeenda kama ww sins ninacho miliki
Wewe si ndo unamiliki nyumba inayotakiwa kupigwa mnada na ACB kwa deni la million 20? Kwann wamdanganya mwenzio kwamba huna unachomiliki?Pole mwaya, mm mwnywe umri umeenda kama ww sins ninacho miliki
Usiwalaumu watu wa hivyo mkuu anatamani sana kuwasaidia ndugu zake, ila hizo pesa hana mamlaka nazoYaan mkuu una akil sna , hakika halio ndo hali halisi haswa
Nina kaka angu yupo uk hapa bongo ana majumba hayana idadi
Ma eka ya mashamba had mengine hayajui
Ila kumseidia mtu shida yaan kukupa kamtaj hawez labda sh 10000 ili sku yapili umuombe tena aone huwezi ishi bila yeye nikaona. Bora nijiongeze saiv sina habar nae kabisa japo km ni kaka baba mmoja ma mmoja ila sina mawasiliano nae tena nafanya yangu
Jaman chonde chonde msitegemee vya ndugu mtakufa masikini
Wewe sio mjanja, ni bonge la mjinga hata kama unafanya shughuli zakoWe siyo graduated ni graditude huwezi kuwa zoba kwa kiasi hicho nikimuona MTU ana degree halafu analalamika ajira natamani nimtemee mate huna Tina kwa taiga hili kabisa .si ajabu umeacha mashamba kijijini nawe IPO mjini unabanana na washua wakati umeacha Mali ,Mimi na degree ya HRM nibahatika kufanya field wilaya flani hadi Leo nafanya shughuri zangu kwenye wilaya hiyo na sina mpango wa kuajiliwa kabisa .