Ushauri: Umri unaenda sina ninachomiliki

Siku ukiadili mindset na kujua kwamba u are reaponsible for ua future na ukaacha kutupa lawama kwa mtu yoyote itakuwa ni siku kubwa maishani mwako
 
Pole sana kijana, mara nyingi ugumu unakuwa kwenye mind zetu kuliko uhalisia. Hebu amua kujiajiri kwa kuanza kidogo kidogo na mtaji mdogo. Kuanza na mtaji mkubwa sio muhimu wengi unawaona wanabiashara kubwa walianza mbali kidogo kidogo, hivyo basi wewe kwa akili uliyo nayo na utayari unaweza kufanya chochote na kufika mbali sana ndani ya muda mfupi.

Wekeza kwenye kutatua changamoto wachana na mazoea ya kuwa umesomea digrii fulani unapswa kuajiriwa sekta fulani. Fikiria kuna fursa fulani nawezaje kutoa solution na kupata kipato.

Kuna mdau ameeleza kufanikiwa ni suala la unatatua changamoto ipi na sio yale mazoea ya naijiriwe wapi ndani ya miaka 10 utashukuru kwanini ulikosa ajira maana utapiga hatua kubwa sana.
Kesho ukiamka andika mambo ma 2 au 3 unayotaka kuyafanya kisha yafanyie utafiti, baada ya hapo amua lipi la kufanya.
Kisha andika unahitaji kuanza na vitu gani, endelea kuainisha unavipataje hivyo vitu. Unaweza shangaa kumbe unaweza na mambo sio magumu kama unavyohisi.
 
Chief kama una soft copy msaada
 
Mjinga Mkubwa wewe
 
Umenena hamna kitu chenye dhamani kama afya njema mengine mungu anajua juu yetu sisi.
 
Nakuunga mkono kuna siku nilikuwa naenda kutafuta ajira mahari nikiwa kwenye daladala nikawa najihisi mtu nisiye na bahati, pembeni yangu alikaa dada fulani alikuwa na kidonda shingoni Kwa nyuma nikawa naongea nae na kumuuliza kulikoni hicho kidonda akanijibu kuwa anaumwa kansa. Ilibidi nimshkr MUNGU na kujiona mweny bahati Kwa kunipa afya njema maisha yanabadilika sana huwezi jua kesho yako..
 
Kati ya watu usiotakiwa tegemea ni
Ndugu (Tumbo Moja au W Mbali)
Familia
Marafiki

Ukiwategemea Hawa utakufa masikini, hata wawe nacho hawawezi kukusaidia zaidi watapenda uwe hivyo ili uwaheshimu
Naomba niongezeee kidogo,hakuna ndugu anayetaka Ndugu yake afanikiwe kimaisha bora mtu baki anaweza kukusadia ukatoka kimasha sio Ndugu.
 
Hahaha pole ila usikate tamaaa maisha ni safari ndefu, na utakacho pata kitakuwa chako haswa siyo vile vya "daddy gave me" unajua eeeh, halafu familia ni factor kubwa japo siyo validy kivile labda kama una wadogo home unasaidia kuwa somesha au kutunza wazazi nk!! Kikubwa komaaa mali inatafutwa mdogo wangu, mbona wewe ni billionea anza sasaa weka malengo
 
Mtaji mkubwa kupita yote ni afya njema. Pili ni akili yako na utashi wako. Unaweza kuanza na zero na baada ya muda ukawa milionea. Mfano unaweza kuhamia mahali pafaapo kwa kilimo ukawa unapiga kazi yako na hata ukachanganya na vibarua with determination unatoka. Ziko njia nyingi usipoangalia hivyo vyeti.
 
Ninachokupongeza ni kwamba mtaji muhimu na mkubwa ambao ni Uzima na Uhai.. Miaka achana nayo wewe ni mzima kuna siku mambo yatakaa Sawa tu.
 
Nimekuelewa sana mkuu thumb up!
 
Kati ya watu usiotakiwa tegemea ni
Ndugu (Tumbo Moja au W Mbali)
Familia
Marafiki

Ukiwategemea Hawa utakufa masikini, hata wawe nacho hawawezi kukusaidia zaidi watapenda uwe hivyo ili uwaheshimu
Inategemea na ndugu wa aina gani. Wengine ni mayatima wamelelewa na kusomeshwa na ndugu. Jitazame wewe na ndugu zako kaka...sio wote ni wabaya.
 
Mizunguko ya Kutafuta Ni Mingi Kuna Siku Unapata Kuna Siku Unakosa, Katika Yote Usikatee Tamaa Stay Committee, Muda wa Mafanikio Unakuja, Endelea Kumwomba na Kumwamini Mungu Aliyekupa Uzima.
 
Umeongea point sana. Wasiosoma sana wanatuzidi mbali sana katika elimu ya biashara nimejifunza sana hili. Wasomi huwa tunaangalia sana mitaji mikubwa. Ndio maana matajiri wengi hawana elimu kubwa ya darasani.
 
Nahisi shida yako ni malengo na mtazamo wako wakimaisha mjomba.

1. Ulivo kuwa unasoma ulisoma kwa malengo yapi??...Je ulijitahidi kwa nguvu zako zote kuwa mmoja wa wanafunzi bora darasani kwako?? Ulijenga urafiki na wanafunzi wenzako na waalimu wako??

2. Je..hapo kwenye kazi yako ya sasa unafanya kwa malengo yapi? Unajitahidi kwa mfanyakazi bora au unaweka jitihada zozote za ziada kuwazidi wenzako?? Je wewe ni kwanza kufika, wa mwisho kutoka?? Unafanya kazi hata wikiendi au sikukuu ukihitajika?? Mahusiano yako na wenzako na boss yakoje?? Unatambua thamani yako kama mfanyakazi?? Je, mwajiri wako akitaka kufukuza watu kazini...je atakufukuza kirahisi au wewe ni mtu tegemeo sana kwake??

3. Kama umejiajiri, unafungua ofisi yako au biashara yako saa ngapi?? Na je unafunga saa ngapi?? Ubora wa huduma yako kuwazidi wengine ukoje?? Je ni mcheshi, mchangamfu na mtu wa watu.... au ni mtu mwenye stress na mawazo mda wote? Je unawapa wateja wako sababu yakuja kwako na wasiende kwa wengine??

4. Kwenye kila hatua ya maisha..jiulize unataka kufanikisha nini....na nini unachokifanya cha ziada kuwazidi wengine kufanikisha malengo yako. Wasomi ni wengi, uwe msomi bora.....wafanyakazi ni wengi uwe mfanyakazi bora......mamantilie ni wengi uwe mamantilie bora......machinga ni wengi uwe machinga bora....n.k..........FANYA KITU CHA ZIADA KILA SIKU UJE UTUPE MREJESHO BAADA YA MWAKA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…