Ushauri: Used Car ndo imetoka Japan iko majini inakuja

Tatizo ukaguzi ni subjective na judgemental halafu unakoenda kurekebisha gharama kubwa na huduma mbovu.

Unaweza bora utoke ukatengenezee unakojua wewe
Mzee mbona wanakupa gari lako unaenda kurekebisha unapopajua wewe then unalirudisha wanakagua tena? Pale ni ukaguzi tu kurekebisha ni juu yako.

Mimi nilipewa oil leakage nikaenda rekebisha ikarudi wakapitisha mia shilingi tano sikutoa....
 
Below 1litre pole, GDI hazina deep stick ya kucheck oil level?
 
Kuweka funguo kwenye ruksi ni aina flani ya ushamba flani hivi...
 
Oil si lazima kumwaga, mara nyingi unaweza ukahakiki mara ya mwisho huko Japan gari imefanyiwa service lini kwa kucheck service stickers huwa wanazipandika ama ndani ya 'boneti', mlangoni n.k

Kwa kuwa wameandika kijapan, unaweza tumia google camera kutranslate...
 
Asante sana mkuu, nitafuata ushauri wako
 
Hapana mkuu kitimoto, nimeiona ni gari imekaa kiutu uzima kidogo tu
Hujakosea chaguzi mkuu, hiyo gari ni ngumu balaa, na ukienda shamba unapeta tu, Mshua wangu aliichukua GDI 2009 mpaka leo anakula nayo misele, gari imeanza kumsumbua sumbua mwaka jana, Kaniambia ana mpango wa kuitia engine ya noah sijui kama zinaingiliana ila kaonesha kuwa haiachiil[emoji23][emoji23]
 
Yeah! Mungu akinijalia uhai nami hii nitakaa nalo hadi vijana walikute.Ili waje nao wanunue za kwao wasije kung'ang'a zangu sababu watazikuta zimechoka
 
Inayo lakini sikuangalia wala sikuwa na wasiwasi kuwa ingekuwa low kiasi kile.Kuna gari nasikia kuwa engine oil ikiwa imechoka au ikiwa low kuna taa inaonyesha kwenye dashboard,nadhani hao waliona mbali zaidi ili kukwepa matatizo kama hayo...
European Cars nyingi unafanya service unafanya Reset ukifika muda wa service itakuwashia tu taa.

Pia kwenye dashboard katika taarifa za gari inazoonesha pake utakuwa inakuonesha bado Km ngapi ufanye service.

Hivo.
 
hapo TRA washakukamua upo hoi, sasa jamaa wa Inspection wanakuambia kanunue tairi 4 mpya @250,000 x 4 = 1,000,000 utachagua wewe! usumbufu vs chai.
Kweli inategemea na kosa.... Lakini si zimechoka kweli??? Au wanasingizia? Ila kama haupo poa unazama ndichi unawaachia chao...
 
Ngoja ifike kwanza, ujue TBS watakuambia nini...
 
Kubwa kuliko yote.ukiingia barabarani sio unavimbaaa kwenye gari uko serious as if ndo wa kwanza kumiliki gari.

Mvua inanyesha unamuona mdada nywele zake zinalowa hata husemi chochote? Hapana unatakiwa kusimama uongee nae kwa upole.

"Dada pole unaelekea wapi nikusogeze?"

Akija kushuka sio lazima uombe no. Wewe toa msaada usepe kama humu tulivyokushauri bila gharama.

Nina imani wewe ni dereva vigezo na masharit ya barabarani unayajua. Otherwise all the best
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…