Ushauri wa Bure: Diamond saidia baba yako

Ushauri wa Bure: Diamond saidia baba yako

Kweli wewe naye mtu. Bado una utoto mwingi au kichwa bongo fleva. Maana mwenye hekima na busara hawezi ongea upuuz huu.
Hakuna kitu kama hicho ... niupuuzi mkubwa huu ..mzazi unapaswa kumlea mwanao nakumpatia mahitaji yake ya msingi yatakayo muweza kumpatia msukumo wakuweza kuzifikia ndoto zake ",

Hata kama ni mzazi masikini komaa na family yako ipatie matunzo hata kama ni haba na uionyeshe upendo" watoto wakija Julia wataelewa tu kwamba mzazi wetu ni masikini lakini hakuwahi kutu telekeza alikuwa pamoja nasi katika kila hali "

Sasa kama wewe ni mzazi halafu uliikimbia family yako" na kumuacha mtoto wako akipitia tabu za maisha ", hakika haustahiki kuonewa huruma na dunia .... acha yakukute mazito

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujajua maumivu ya kukataliwa na mzazi wewe tena hilo neno la kumdharau futa.
Ni maumivu yasiyoelezeka wewe unazungumza tu kwa sababu ulipata malezi ya wazzi wote.

Kupewa pesa si tatizo yule mzee pesa anapata, tatizo ni msamaha ni kitu kigumu sana mwanadamu kukitoa, haihitaji media ili kupata msamaha anahitaji wasuluhishi shauri yake.
Diamond hajawahi kukataliwa acheni fixi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu mwenyewe hawezi kumsamehe shetani.
Kufikia hapo mungu kanifundisha kutosamehe, roho nzuri nishaona ni udwanzi, Diamond anaufala wake ila kwenye kutomsamehe mzee wake hajakosea, haiwezekani utelekeze familia hata wanyama pori wanatunza familia zao. (mimi nimekulia nyumbani malezi ya baba na mama ningetelekezwa sijui ingekuwaje).

Namkubali Malcolm X ila baada ya kuslimu akapata akili akasema
"Ima Muslim because its a religion that teach me to respect everybody and treat everybody right and it also teach me an eye for an eye and tooth for tooth"
mambo ya kusamehe sijui staying positive in a negative situations hapana aisee.
 
Baba mtu apambane na hali yake kama tu either
1.alimkana dai akiwa mdogo
2.aliwaita wachawi na kuwafukuza wasimuombe msaada wowote enzi anajiweza
3.alimtaka au kumshawishi mama dai aichoropoe mimba ya dai(hii style ya enzi na enzi eti itoe haraka)
4.hakumjali kijana wake enzi za utoton.

enyi wababa acheni kuwatelekeza watoto madhara yake ndo haya ya mzee mzima kulia kwenye media kila kukicha
 
Mungu mwenyewe hawezi kumsamehe shetani.
Kufikia hapo mungu kanifundisha kutosamehe, roho nzuri nishaona ni udwanzi, Diamond anaufala wake ila kwenye kutomsamehe mzee wake hajakosea, haiwezekani utelekeze familia hata wanyama pori wanatunza familia zao. (mimi nimekulia nyumbani malezi ya baba na mama ningetelekezwa sijui ingekuwaje).

Namkubali Malcolm X ila baada ya kuslimu akapata akili akasema
"Ima Muslim because its a religion that teach me to respect everybody and treat everybody right and it also teach me an eye for an eye and tooth for tooth"
mambo ya kusamehe sijui staying positive in a negative situations hapana aisee.
Simpendi diamond ... lakini kwakuwa katika maisha yangu nilichagua kuwa positive ... katika hili niko kwenye upande wake ....

Majuzi nilikuwa na bishana na watu kuhusu suala hili hili tweeter ", na hatimae walielewa tu "

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnakazana tu " oohh vitabu vya dini vime sema. .vitabu vya dini Vimesema"...... sasa kama baba aliyakimbia majukumu yake ya kulea' Mnauhakika gani kuwa diamond anajua hayo mafundisho yaliyopo kwenye vitabu vya dini"........,

Kwa sababu Ni jukumu la mzazi kuhakikisha kuwa anampeleka mtoto wake kuanza shule" iwe inayotoa elimu dunia au ya huko sijui ndio akhera"......., so kama hayo mafundisho hayajui", hamuoni kuwa hawezi kutambua umuhimu wa hicho mnacho muambia", na hapo hapo lawama tena zinarudi kwa baba huyo huyo maana alishindwa kumpatia mtoto wake elimu ili aweze kuyajua hayo mafundisho ya imani ".... so wakumlaumu ni huyo mzee sio domo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaume leeni familia mnatelekeza watoto afu saizi unakuja tia huruma kwenye media pole sana baba diamond you weep what u have sawn gademn mkomage ....mnatelwkeza watoto wakikua na mafanikio ndo mnaleta pua zenu huku mnatia huruma heheheh

am better here
 
Hakuna kitu cha thamani hapa chini ya jua kuliko kusamehe..inakuweka huru,inavunja maagano ya kishetani,inaleta heshima,inakupa hadhi mbele za Mungu na wanadamu.
Daudi aliwahi kuandika Ee bwana Kama usingelirehemu,ni nani angesimama mbele zako?lakini kwako kuna msamaha ili wewe uogopwe"
Binafsi sishindwi kusamehe kosa lolote lile hata la mtu nisiyemjua..napendaga sana kusamehe kwa sababu inanipa furaha na amani.
NB:simanishi kuwa huwa sikasiriki,ila siwezi kuishi na kisasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naandika nikiamini kwa namna moja au nyingine ushauri huu utamfikia huyu kijana Diamond. Yeyote asiye na maelewano na wazazi/mzazi wake pia inamuhusu. Na wazazi wanaotelekeza vizazi vyao pia wanaweza kujifunza jambo.

Mimi ni mmoja kati ya watu wanaopenda namna Diamond anavyojituma katika kazi pamoja na ubunifu katika muziki na biashara ya muziki. Pia amekuwa mstari wa mbele kusaidia vijana wenzake, hususan waliotoka katika hali duni kimaisha kama ilivyokuwa kwake, kupata maendeleo kupitia sanaa. Tumeshuhudia hali kadhalika mara kadhaa akirudi maskani Tandale na kuwasaidia wakazi wa huko, kidogo alicho jaaliwa, na mengine mengi mazuri.

Yapo pia mambo kadhaa ambayo sifurahishwi nayo kuhusu yeye, lakini nitalizungumzia hili la kumtelekeza Baba yake. Nimeona mahojiano ambayo baba Diamond amefanya na online TV moja. Ni wazi kwamba huyu mzee alitibuana na demu wake Sandra - mama Diamond, akatimka nyumbani na kutelekeza familia. Anasema wakati huo Diamond alikuwa na akili yake nzuri tu, hivyo huenda Diamond aliathirika sana kisaikolojia kwa Baba yake kutokomea kusikojulikana na kuwaacha yeye na mama yake hawana hata unga robo. Kutokana na maelezo yake aliyotoa na mazingira ya nyumbani kwake, huyu mzee ana hali ngumu. Baba Diamond sasa hivi anafanya biashara ya kukopa viatu vya mtumba Ilala, anarudi kwake magomeni anaviosha na kung'arisha kisha anatembeza mtaani, yaani Mmachinga typical. Anapoumwa kwa mfano, anakuwa hana hata fedha ya matibabu, hivyo kugeuka ombaomba. Kutokana na maelezo ya Mzee mwenyewe, majirani na mdogo wake Diamond anayeishi na baba yake, Diamond kufika kwa mzee wake ni tokea yuko na Wema!

Kilichonifanya kuandika huu uzi ni kwamba Baba Diamond ameomba msamaha kwa makosa aliyoyafanya. Tena amesema kwa uchungu kabisa, kwamba hata Mwenyezi Mungu husamehe. Kwa nini , yeye asisamehewe?. Binafsi naona imefika wakati Diamond akunjue moyo wake na kumsaidia Baba yake. Katika Qur'an, ipo wazi kabisa, kwamba baada ya Mwenyezi Mungu, wanafuata wazazi. "Be grateful to Me and to your parents; to Me is the [final] destination." (Quran 31:14). Mzee Abdul alikosea kumtelekeza mtoto Diamond, haijalishi walitibuana nini na mama Diamond. Diamond hajui nini hasa kilitokea. Mzee ameomba msamaha, anapaswa kusamehewa na maisha yaendelee.

Diamond rudisha maelewano na umsaidie baba yako. Amejutia na ameomba msamaha. Kwa sasa haikupunguzii chochote kumsaidia mzee wako aishi maisha ya kawaida, ya angalau ajue familia yake itakula nini jioni. Utakuwa na amani, Itakuongezea heshima katika jamii, na zaidi utapata credit kwenye daftari lako la Akhera. Maisha yenyewe ndiyo haya. Ukiishi sana 80. Ukiishi zaidi ya 80 ni maumivu tu, uwe na hela au huna. Akifa huyu mzee katika hali hii, Diamond utaaibika Duniani na akhera.
Kwanza nikuambie siku zote Mungu hatoi laana endapo mzazi haja timiza majukumu yake na mimi nakuambia na nimeshuhudia mzazi akikupa laana au akinung'unika basi kama kweli Mzazi alitimiza majukumu yake ya malezi lazima Kuna baya litamkuta mtoto, kilio cha mzazi Mungu anakisikia sana.

Hivi nikuulize Mondi leo angekuwa hana kitu huyu mzee angemtafuta?

Haya basi tufanye Mondi kakosea, lkn ukirudi kwa Doreen lawama ni zile zile mpaka akamtukana matusi makubwa kwenye kipindi cha Shilawadu, sasa ww hujiulizi mtu mmoja lkn anarudia kosa lile lile kwa watoto wawili tofauti ambao amezaa na wanawake tofauti, huoni huyu mzee ni type zile za kuzalisha na kutambaa.

Mimi nakuambia kama huyu mzee angekuwa responsible kwa Mondi na Doreen nina uhakika Mondi yangemkuta mabaya sana kwani laana ya mzazi haimalizi hata mwezi (nishashuhudia kwa watu watatu tofauti) lazima impate mtoto, lkn huyu mzee tokea aanze kulalamika ana miaka zaidi ya mitano lkn Mondi kila siku anazidi kutusua, kutoka kuwa mwanamziki mpaka CEO.

Kiubinadam na kidini hata mm napenda Mondi amsamehe mzazi wake, ila approach ya mzee hata mimi nisingemsamehe. Mimi mtaani Kuna mzee mmoja, mdogo wake alimtelekeza mtoto, babu wa huyu mtoto aliwafuata ili kujua hatma ya mwanae na mjukuu wake lkn walimjibu hovyo nakumfukuza. Yule mtoto kakua kamaliza chuo, baba yake kaanza kumfuata babu yake ampatanishe na mwanae alitimuliwa na mpaka akatumia njia kibao akachemka. Kaka yake huyo jamaa kamfuata mzee wangu, sababu baba na babu wa huyu binti wanaheshimiana sana akatafuta na wazee na ndugu ambao yule babu anawaheshimu wameenda wakaongea na kuyamaliza.

Tatizo huyu mzee anakosea kwenda kwenye vyombo vya habari, alafu anaonekana hata yy mwenyewe ni bado anatabia za kisela (nineshamuona ktk interview mbili) na ndio maana hata yy mwenyewe anashindwa kuwatafuta watu au ndugu ambao Mondi na mama yake wanawaheshim ili wamsaidie ktk kupatana na mwanae. Lakin kama angeitumia hii njia kimya kimya nina uhakika wangemsamehe. Ila hii kila siku kwenye vyombo vya habari hata mimi simkubali.
 
Back
Top Bottom