Ushauri wa Bure: Wamiliki wa Radio Clouds FM ya Dar es salaam

Ushauri ulioutoa wangepaswa kuulipia lakini wewe umefanya favour, thanks for that!
Mwenye masikio na asikie ushauri huu wa BURE.
 
M naamin clouds n moja ya redio zenye vijana wny ubunifu na vipaj ndan yao, ila tatizo lipo kwa baadh ya watangazaja ambao hawafuat maadil sahihi ya utangazaja ambpo wanafikia ha2a ya kutukana hadharan, ktu ambacho knaleta matabaka ya aina ya wasikilizaj. kna kile kpnd cha raha za roho, wamesogeza muda il kuwapa nafas wny rika sahih kusikiliza, ni uamuz sahh japo lugha wanaitumia imepitiliza uki compare na pillow talk cha times. All in all, wanapaswa kupunguza uhuru mkubwa kwa presenters wao il kuepeuka matatizo km hayo. hongeren clouds kwa kaz nzuri.
 
Mwenyew nshaachaga kuisikilza hiyo radio station long time ago!hata'sikumbuk tena sauti zao!manake ni kichefuchefu

hii radio ilikuwa nzuri sana miaka ya nyuma,lakini mabadiliko yameanza siku si nyingi sana zilizopita,naona wamegundua hilo ndo maana wamechukua watu wawili kutoka radio one,tuwape nafasi tuone itakuwaje!
 
Mkuu jaribu kusikiliza na kutazama clip hizi za vipindi vya BBC. Tena wewe uko huko UK nadhani unajua zaidi yangu. Hii BBC nadhani ni kama TBC lakini wana vipindi vyenye maneno kama hayo. Sasa wewe ukishangaa Clouds inabidi nikushangae wewe.

Inabidi ujue customer wanataka nini sio kila kipindi kiwe too official au tooo formal. Tutaboreka.

Russel Howard Good knews.

Top gear

Hiyo ni mifano so clouds wana matatizo madogo madogo kama ilivyo TBC, ITV, radio one na wengine . Sio mtaalam wa radio lakini ukniuliza station gani zinahitaji reform nitaanza na TBC
 
Last edited by a moderator:
Kila kituo cha redio kinakuwa na walengwa wake. Na kila kipindi huwa na walengwa wake pia.

Clouds FM si redio ya umma. Si redio ya umma kwa maana ya kwamba heitegemei ruzuku ya serikali kujiendesha. Kwa kiasi kikubwa inategemea hela za wadhamini wa vipindi na matangazo mengine ya biashara.

Sasa kama mtu ana matatizo na redio hiyo kwa nini wasipeleke ushahidi huko kwa wahusika walio na dhamana ya kutoa mwongozo wa kisheria na taratibu kuhusiana na vyombo vya habari?

Kutokukipenda kituo cha redio kwa sababu ya vipindi vyake ni jambo moja, na kusema eti wanavunja maadili au sijui wanakiuka sheria ni jambo jingine. Kwanza maadili hayaangozwi na sheria. Miiko ya fani ndo huongozwa na sheria. Mtu kama unaona Clouds FM wanavunja sheria basi kusanya vielelezo vyako na vipeleke TCRA.

Ukivipeleka huko na vikapuuzwa na wewe kwenye moyo wa moyo wako unaona kabisa una hoja nzuri basi anzisha kampeni kubwa yak u-raise awareness kuhusiana na hayo unayoyapinga dhidi Clouds. Unaweza ukaandika mabango na kwenda mbele ya ofisi za TCRA au ukaitisha maandamano dhidi ya Clouds yatakayoanzia, kwa mfano, kutoka ofisi za TCRA hadi pale Mikocheni kwenye ofisi za Clouds.

Si mnajidai mna nia njema? Si mnajidai mna hoja yenye mshiko? Basi kama hayo yote ni kweli sidhani kama itawawia vigumu kufanya hayo. Kuishia kulialia hapa JF haisaidii sana. Sasa sana mnaishia kuonekana wafa maji tu.
 

Hapo hata mimi nakuunga mkono kwa kweli kuna baadhi ya watangazaji wanaboa sana kama yule sijui ndio anaejiita Diva?.... Haeleweki anaongea kiswahili ama English? Mimi simfahamu kabisaa!! Hivi huyu Dada target audience yake ni kundi gani? Hii lugha anaongea wanaomfahamu ni masharobaro na masista duu ambao ni wachache kwenye jamii yetu, kwa hiyo utakuta mtu anabadilisha station na hawa cloudsfm waelewe mtangazaji kama huyu anawapunguzia audience rating. Kama alifanya interview ya kuajiriwa kweli alitumia lugha pumba kama hii tunayomsikia akiongea redioni?
 

Kama huelewi anachoongea basi ujue wewe si mlengwa wake. Badilisha tu stesheni usikilize upendacho. Redio zipo nyingi siku hizi.
 
Kama huelewi anachoongea basi ujue wewe si mlengwa wake. Badilisha tu stesheni usikilize upendacho. Redio zipo nyingi siku hizi.
Na ndio ninavofanya, nilipohisi simuelewi nilibadili station, isipokuwa haya yalikuwa maoni yangu na nafikiri hapa nina uhuru wa kutoa maoni ama? Mbona mkali mkuu ama una hisa Clouds?
 

Nduka: Hapo kwenye RED Hebu fafanua zaidi, nahisi kama kuna kwenda nje ya hoja hapa. Lakini pia nadhani ingekuwa ni hekima na busara kupinga hoja aliyokuja nayo Radio Producer kwa kueleza wazi kwa mifano. Hili haliko hivi kwa sababu hizi na zile. Nachokiona hapa ni kulalamika na nikitafakari zaidi nagundua kama kuna some sort of interest na Radio inayozungumziwa hapa. Coz naona personal attack badala ya Hoja yenyewe.
Help please ili kutuweka wazi na huru ili tuone haya aliyokuja nayo huyu ndugu ni uongo. Personally nasikiliza baadhi ya vipindi vya clouds fm na kuna vitu ambavyo sivikubali na sitavikubali hata siku moja, lakini pia nina rafiki zangu kadhaa ambao walishaacha siku nyingi sana kusikiliza clouds fm kwa baadhi ya sababu ambazo amezitaja Radio Producer.

 
Hukuwa na sababu ya kuwapongeza kwa kuwa na watangazaji wabunifu wakati umethibitisha ni wabovu,hawajivunii kulumba kiswahili,pamoja na hayo nakupa kongole kwa thread yako,binafsi siipendi hii radio!
 

Mkuu nimeipenda sana mistari yako! teh teh teh teh
 

Daima mtu mwenye mawazo mabovu huzungumzia mawazo mabovu na kutetea mawazo mabovu! Kabisaa mtu wa hivi hapendi ushauri mwema kwake ama kwa wengine! Ushuri wa clouds unakuuma nini wewe kimbenga?
 
Ushauri ulioutoa wangepaswa kuulipia lakini wewe umefanya favour, thanks for that!
Mwenye masikio na asikie ushauri huu wa BURE.

Daima media nyingi bado hazijazoea kupokea feedback, wakipewa feedback wanasema wivu!
 

Sidhani hata kama wanayo ile Regulations content ya Broadcasting! TCRA nao usingizi tu!
 
hii radio ilikuwa nzuri sana miaka ya nyuma,lakini mabadiliko yameanza siku si nyingi sana zilizopita,naona wamegundua hilo ndo maana wamechukua watu wawili kutoka radio one,tuwape nafasi tuone itakuwaje!

Ikiingia madarakani serikali ya watanzania wapya radio kama hizi sidhani kama zitaendelea kuunguruma!
 

Mkuu wewe endelea kusoma post utajifunza siwezi kukoment chochote maana wewe umesema hapo kwa red!
 
Last edited by a moderator:

Ungekuwa unaelewa maana ya ushauri hata usingeandika haya madude uliyoandika! Kama wewe ndo mtangazaji wa clouds shida kubwa najua hamjui kupokea feedback toka wa wasikilizaji ndio maana mnang'ang'ana na tu na mnachokifanya! Sisi ndio wasikilizaji wenu tunataka mfanye mabadiliko ili turidhike tufuraihie na radio yetu wewe unaleta matope tu! Ole wako nikutane nawewe radio moja watu wa hivi mimi huwa nawalima chini tu!
 

Mimi nimesema kunauwezekano mkubwa kwa PM anapata chochote cha kuruhusu madude yaendelee!
 
Kama huelewi anachoongea basi ujue wewe si mlengwa wake. Badilisha tu stesheni usikilize upendacho. Redio zipo nyingi siku hizi.

Huwa hatuna lkugha kama hiyo kwenye radio. Kila kitu kinachozungumzwa na msikilizaji awe targeted audience au bonus audience ni feedback! Elewa feedback zaweza kuwa negative au postive zote huwa tunapokea! na tukipokea hatumtukani aliyezitoa tunaziingiza followup na kuzijadili! Sasa wewe nakushangaa sijui unabishia nini tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…