Ushauri wa kisera kuhusu watu wenye ulemavu

Ushauri wa kisera kuhusu watu wenye ulemavu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
Huwa najiuliza kama watu ambao ni wazima kabisa wa afya tena vijana; kuna muda maisha yanawapiga hadi wanashinda na njaa, hivi tunawafikiriaje ndugu zetu walemavu ambao hawana mikono, miguu, hawaoni n.k?

Katika misingi ya distribitive justice serikali kote duniani hukusanya kodi na kuzitawanya kulingana na mahitaji ya kijamii.


Badala ya hali ilivyo sasa ambapo walemavu wanaombaomba mtaani na hawapati msaada wa maana: Nashauri serikali ianzishe makambi ya kuhudumia walemavu kwa kila kitu maisha yao yote maana hawakupenda kuwa walivyo.

Ili kupata fedha ya kuwahudumia, serikali iweke kodi angalau ya Tsh.1 kwa kila huduma na naamini hakuna mtanzania mwenye ubinadamu anaweza kupinga sera hiyo.

Kwa maoni yangu maendeleo ni pamoja na utu na kuoneana huruma sisi kwa sisi hasa kwa watu wenye mahitaji maalum.

Naomba tuiuunge mkono hoja hii na tuishawishi serikali hadi ikubaliane nayo, tutakuwa tumefanya jambo la maana duniani na mbele ya Mungu tutakuwa mashahidi.
 
Katika nchi zilizoendelea, huwa wanatenga fedha kwa makundi maalum mbalimbali ikiwemo walemavu, wazeee, wasio na ajira na.k

Lakini sisi kwa mazingira yetu na uchumi wetu hatuwezi kufanya yote hayo. Lakini sioni ni kwa nini angalau hili la walemavu litushinde. Hebu tujaribuni kujiweka kwenye nafasi zao na tufikiri sisi tungekuwa ndio wao.

Yaani kwa mfano unakutana na mtu haoni kabisa, halafu yuko juani anaomba omba, hivi role yetu sisi tulio wa zima kwa watu hawa ni nini? (Kitaasisi)
 
Mkuu, kwenye policy lobbying iko hivi; kitu kikipata watetezi wengi kinauwezekano wa kuwa sera rasmi (bila kujali uzuri au ubaya wa kitu chenyewe) na kikikosa utetezi kinapotea bila kujali sana uzuri wake.

Hivyo ni muhimu kama jamii/ raia tukajenga utamaduni wa kutetea reforms kama hizi ambazo hazina madhara kwa yoyote bali faida kwa wote ili mwishowe ziwe sera rasmi. Hakika hatutakuwa na cha kupoteza bali heri kwetu sote.
Ngoja tuone...
 
Kuhusu mjadala wa kama serikali inaweza kukusanya kodi na kuwasaidia wasio na ajira ( mfano kuwalipa kima cha chini) ili waweze angalau kuishi,

Inaonekana kwa nchi za Afrika haiwezi kufanya kazi ( hata tungekuwa na uchumi mkubwa) kwa kuwa watu wengi wangeamua kutofanya kazi makusudi ili walipwe kima cha chini (bure)

Lakini kwa hili la walemavu, angalau tuna uhakika kuwa, hakuna mtu anaweza kujitia ulemavu makusudi ili ahudumiwe na serikali.

Hivyo hii inaweza kuwa moja ya sera bora kabisa kwa ustawi wa jamii ya mwanadamu.
 
Back
Top Bottom