Ushauri wa Profesa Janabi kuhusu krismas, kuleni kwa kuzingatia afya, msile kupitiliza

Ushauri wa Profesa Janabi kuhusu krismas, kuleni kwa kuzingatia afya, msile kupitiliza

Pesa zangu nakula Jumamosi naelekea Rombo
 
Anataka tule mapera? Sisi tuna miaka 40 tunakula pilau Kisha nyama zinafuata
 
Huyu mzee kila ushauri atakaoutoa basi asilimia 90 unagusu kula kula tu! shida nini?
 
“Watu wanaenda Krismasi na nyie wote mlioko hapa mnaenda Krismasi, wapo wa Moshi, wapo wa Arusha, wapo wa Mbeya, wapo wa Iringa na wengine Songea nyumbani kwetu, ulaji utakuwa wa kupitiliza, ulaji wa nyama utaongezeka, vinywaji vya kupitiliza kila kitu kitakuwa cha kupitiliza , wapo ambao wakirudi Januari wanaweza kurudi sawa kwa lugha za waandishi kurest lakini salamu zangu za Krismasi kuzingatia ulaji.”

Prof. Mohamed Janabi

View attachment 3175090
Huyu Prof amekuwa kama mama lishe, issues zake ni chakula tuu hana ushauri mwingine.
 
Mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi wa WHO Africa Prof Janabi amewataka Wananchi watakaosafiri kwenda kula Christmas mikoani mfano Moshi, Arusha, Iringa, Mbeya na Songea Wazingatie Ulaji wasile kupitiliza

Prof Janabi amesema hizo ndio salamu zake za mwaka Mpya

Source: East Africa TV
 
Aaah; prof siku 1? Yaani siku 1 tu ndio ilete shida..., hapana kaka, tuache tujipe pole ya mwaka mzima
 
Back
Top Bottom