Ushauri wa wazo la kibiashara kwa Mwanza, Dodoma na Dar es Salaam

Ushauri wa wazo la kibiashara kwa Mwanza, Dodoma na Dar es Salaam

But all in all.. nice advice atamm nmechukua kitu hapo. Tafanyia kaz from one place to another
 
Wakuu kwema?

Nina mtaji wa million mbili(2m),nimekuja kwenu kama wana jamii nikihitaji mawazo bora ya ujasiliamali kwa mikoa ya Mwanza,Dodoma na Dar es salaam,mikoa hii nimeichangua nikiwa na maana ya kuwa nipo tiari kufanya biashara moja ya mikoa hiyo sasa ni kufuatana na ubora wa wazo lenyewe ndo litaamua mkoa wa kuchanguliwa kati ya hiyo.

Naamini hapa hakishindikani kitu na nina uhakika nitapata ushauri ulio bora kabisa,basi nikualike wewe uliyeko katika moja ya mikoa tajwa hapo tujumuike katika mjadala huu,karibuni na asanteni sana.
Sio kwamba kila mwenye Pesa lazima afanye Biashara hilo ni muhimu sana.

Sasa basi.

Kwenye Biashara fanya kile unacho kipenda kutoka moyoni mwako. Swala la ufanye nini ni wewe kuumiza akili. Biashara inahitahi kuumiza mno akili tena wakati huu ambao kuna Techinolojia kubwa.

Mkuu umiza kichwa na si kwamba lazima ti ufanye kile ambacho kila mtu anafanya.

Biashara zote zina faida ilimuradi unatatua changamoto za wateja.

Hapa utaambiwa kile ambacho kila mtu anapenda. Mimi nitakuambia fuga nyoka kwa sababu tu nafuga. Kuna atake kwambia fungua Duka la kuuza mayai kwa sababu tu yeye anafanya hivyo.

Wewe umiza kichwa na ukijua kabisa kufanikiwa kutategemeana na Conmitment yako na ubunifu pia.

Make unaweza kuwa na Commitment ila ubunifu ukawa huna sasa itakuwa kazi bure tu.
 
Chif kwa sasa hakuna biashara mpya,biashara nyingi ni zilezile,
Cha msingi ni ww kufanya uchambuzi kutokana na mtaji wako ili ujue ni ipi biashara itakayo kuvutia,

Mm nimekuchagulia mwanza kwasababu ni jiji lenye mzunguko mzuri wa fedha lkn pia vitu vina bei nzuri sana,
Pia muingiliano wa wafanyabiashara wa mikoa jirani na mwanza pamoja na wa inchi jirani ni wengi,lkn pia hata ziwa,migodi,kilimo ni vitu vyenye mchango mkubwa sana vyenye kichochea uchumi wa jiji la miamba,
Hii imekaaje mkuu ..nipe na idea kabisa.
 
Nafuatilia mawazo yatakayotolewa na mimi naweza nikapata kitu.
 
Nimekaa sehemu zote mbili na niki linganisha na mtaji inakuja list hii ya biashara.

1)Mgahawa (Dodoma)
Sometime nilikuwa nashangaa wafanya Biashara wa Dom wasiofanya hii, kuna sehemu inaitwa Ng'ong'ona wanakula wanafunzi wa Chuo ukiwa serious unapiga pesa hadi utasema....what hell.

2)CarWash (DSM)
Hii ukiweka iliyo serious DSM unatusua Magari mengi then haiitaji mahesabu mengi | Kama utataka hii minipo tayari kukusapoti kuisimamisha hii tunaweza kukaa chini.
Mkuu kwema? Nicheki Pm..
 
ng
Nimekaa sehemu zote mbili na niki linganisha na mtaji inakuja list hii ya biashara.

1)Mgahawa (Dodoma)
Sometime nilikuwa nashangaa wafanya Biashara wa Dom wasiofanya hii, kuna sehemu inaitwa Ng'ong'ona wanakula wanafunzi wa Chuo ukiwa serious unapiga pesa hadi utasema....what hell.

2)CarWash (DSM)
Hii ukiweka iliyo serious DSM unatusua Magari mengi then haiitaji mahesabu mengi | Kama utataka hii minipo tayari kukusapoti kuisimamisha hii tunaweza kukaa chini.
ng'ong'ona hakikisha unajua kuroga....ila ni sehemu nzuribya biashara kama unajua mambo ya giza
 
Wakati mwingine unakuwaga na akili?
Safi sana mkuu kwa kupata wazo la kujiajiri mwenyewe.
Mawazo ya biashara yapo mengi sana lakini siyo yote yatakufaa wewe..

Biashara yoyote ili ifanikiwe inabidi ufanye biashara unayoijua na unayoipenda. Kwa nini nasema hivyo? Ukifanya biashara ambayo hauijui undani wake , inafanyikaje, risk zake itakubidi uwe na hela za kutosha ili uajiri manager atakaye manage kila kitu. Ambapo kwa mtaji wako wa 2M ni ngumu sana.

Ngoja nikupe mfano, hauwezi kufanya biashara ya kuuza nguo kama wewe haupendi mambo ya nguo au mambo ya fasheni. Kwa sababu utajikuta unauza nguo za mwaka 2000 huko na wakati zilishapitwa na wakati sasa hivi ni 2019. Inatakiwa iwe ni kitu unachokipenda hata swaga mpya ikiingia mjini ujue kabisa.

Ngoja nijitolee mimi kama mfano, tangu nikiwa mdogo shuleni nilikuwa napenda sana kusuka watu nywele, nilivyofika secondary kazi ikaendelea kusuka watu maana tulikuwa tunaruhusiwa kusuka. Nilivyofika chuo kikuu sikupata mkopo na niliwaza ni biashara gani ambayo naweza kuifanya nikiwa chuoni huku nasoma pia. Nilishauriwa mambo mengi ya kufanya , wengine wakanishauri hadi kwenye kilimo. Guess what.. Kila biashara niliyofanya ilifeli kabisa ndipo nikagundua nilikuwa najihusisha na vitu ambavyo sivijui na ikapelekea kufanya vibaya.

Akili ilinirudia kwamba Mimi ni Msusi, najua kusuka najua kupamba kumbi za ibada , sherehe nk. Ndipo nikagundua kwamba biashara ya kuuza urembo wa wakina Dada, nywele , lipstick nk hiyo ndiyo itanifaa. Nitauza rasta na pia nitazitumia hizo hizo kusuka wateja watakaokuja kusuka.

Mpaka namaliza chuo mwaka wa tatu tayari nilishafanikiwa kufungua saloon yangu mwenyewe na nikaajiri wafanyakazi. Nimejaribu kujiingiza kwenye biashara nyingine zinafeli feli tuu na kunitia hasara. Mpaka sasa nimeamua nijikite hapo hapo kwa sababu ndiyo biashara pekee ninayoijua vizuri, ninayoipenda na inayofanya vizuri. Na biashara inafanya vizuri na pamoja na kwamba nimeajiriwa ila biashara hiyo ndiyo inanipa jeuri mjini. Naipenda sana na kila siku lazima nigoogle kujua mtindo mpya ulioingia nk.

Hivyo mkuu usiangalie tuu ni wazo gani la biashara, jiangalie wewe jee ni kitu gani unakipenda? Unakijua? Na utaweza kukifanya vizuri na ukifurahia kabisa. Hapo lazima ufanikiwe.

Kama unacho kitu au vitu unavyovipenda, au hata kama unapenda kulima sema ili tujue tunakupa wazo lililo base kwenye mambo hayo.
 
Wakati mwingine unakuwaga na akili?
Kwani wakati mwingine sina akili?
Wewe mwenyewe unaelewa akili nilizonazo nilikuwa kwenye final stage ya kubadilisha akili zako nizifanye ninavyotaka sema ulishtuka mwishoni sana.
 
Wakuu kwema?

Nina mtaji wa million mbili(2m),nimekuja kwenu kama wana jamii nikihitaji mawazo bora ya ujasiliamali kwa mikoa ya Mwanza,Dodoma na Dar es salaam,mikoa hii nimeichangua nikiwa na maana ya kuwa nipo tiari kufanya biashara moja ya mikoa hiyo sasa ni kufuatana na ubora wa wazo lenyewe ndo litaamua mkoa wa kuchanguliwa kati ya hiyo.

Naamini hapa hakishindikani kitu na nina uhakika nitapata ushauri ulio bora kabisa,basi nikualike wewe uliyeko katika moja ya mikoa tajwa hapo tujumuike katika mjadala huu,karibuni na asanteni sana.

Mzaleee unamaanisha biashara yoyote wewe unataka kufanya?.
 
Nimekaa sehemu zote mbili na niki linganisha na mtaji inakuja list hii ya biashara.

1)Mgahawa (Dodoma)
Sometime nilikuwa nashangaa wafanya Biashara wa Dom wasiofanya hii, kuna sehemu inaitwa Ng'ong'ona wanakula wanafunzi wa Chuo ukiwa serious unapiga pesa hadi utasema....what hell.

2)CarWash (DSM)
Hii ukiweka iliyo serious DSM unatusua Magari mengi then haiitaji mahesabu mengi | Kama utataka hii minipo tayari kukusapoti kuisimamisha hii tunaweza kukaa chini.

Car wash dar es salaam eneo unalo??
 
Back
Top Bottom