Ushauri wako ni muhimu sana kwa mke wangu

Noel france

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2012
Posts
1,104
Reaction score
917
Wana jamvi habari za mchana. Wandugu uwanawaheshmu sana kwa ushauri mnaotoa. Kwani nimekwisha nufaika na ushauri wenu.
Leo ninajambo ambalo naliona kama si lakawaida kwa mke wangu. Jambo lenyewe ni kwamba:- mke wangu anaujauzito ulikia miezi mitano (wiki ya 20 ). Tatizo ni kwamba mbaka sasa anasema mtoto hajamsikia akicheza tumboni.
Binafsi ninavyo tambua kuhusu mtoto kucheza tumboni uwa kwanzia wiki ya 17.
Kwahiyo ndugu zangu ningependa kufahamu kama nitatizo ama ni hali ya kawaida?
Cc: Mzizi mkavu,washawasha, na n.k
 
Haya wataaramu mtoeni shaka jamaa,mimi nathani mwanao akizaliwa atakuwa mtoto mkimya sana,yaaani sio mtoto mtundu.
 
Haya wataaramu mtoeni shaka jamaa,mimi nathani mwanao akizaliwa atakuwa mtoto mkimya sana,yaaani sio mtoto mtundu.

mkuu umesababisha wife ashikilie mbavu zake kwa kicheko. Lakini nashukuru kwa ushauri
 
Hongera baba kijacho.
Mkeo anaenda clinic? Hebu kamata mkono muende nae clinic, mkae na dr muelezwe kila kitu.

asante bibie,kiukwel amekwisha anza kuudhuria clinic na pia amekwisha anza kutumia doz ya kwanza ya sp. Ila kule clinic walituambia tuendele kusubiri ifike wiki ya 17 ambazo zimekwisha pita na sasa wife amefikisha wiki ya 20 sawa na miezi 50 lakini toto alichezi kabisa. Binafsi nahisi uwenda labda kunatatizo. Kwahiyo nikaona nipate mawili matatu humu ili nijue wapi kwa kuanzia
 

Ni mtoto wa ngapi? Kwa mimba ya kwanza wapo wanaosikia mtoto akicheza late coz wanakuwa hawajazoea but pia inategemea na position ya mtoto katika tumbo..20 weeks is too early kuwa worried,japo ni vema umuone daktari kwa ajili ya screening.
 
Mkuu watalaamu wengine wanasema mtt anatakiwa kuanza kucheza wiki ya 20, lkn pia mama km ni ujauzito wa kwanza anaweza akashindwa kujua mapema km ameanza kucheza sababu huwa kiki zake ni za taratibu sana.. kwa uhakika kafanyeni ultra sound itasema yote.. Hongereni na kila la kheri
 
Mkuu nafikiri ukifika hospital itakuwa vizur zaid,lakin pia tumbo la mkeo likoje?kubwa au dogo sana kulinganisha na umri wa mimba?je ni mtoto wa kwanza?ukifika hospital ni vizuri ukaangalia amniotic fluid level (AFI),kama ni kidogo mtoto hatacheza hovyo as inamuwia vigumu ku-swim,na kama ni nyingi,basi huwa anacheza sana and you might have cord around the neck!
 
mbebe kila siku mkeo kama uzito unaongezeka bac hakuna tatizo kama unapungua wai haraka usichelewe kimbia hospital ukamuone daktari
 
Muhim ni ultrasound then acpende kulala sana pia inasababisha mtoto awe mvivu na anaweza kuwa hachez sana but uzuri fika hosp tu
 
Mkuu ucwe na shaka kwa miezi 5 mtt kutocheza Nina jirani yangu 1 yy Mke wake alikaa hadi miezi 8 bila kumckia Mtt akicheza kila akienda CLINIC vipimo vinaonyesha mtt yuko sawa Hadi ss ameshajifungua so Ondoa shaka mkuu kid atatoka salama2! Manake km kungekuwa na tatizo lolote Afya ya mama ingekupa majibu hata hivyo Nenda hospt kwa uhakika zaidi!
 

sawa mkuu nimekuelewa.
 
Ni mtoto wa ngapi? Kwa mimba ya kwanza wapo wanaosikia mtoto akicheza late coz wanakuwa hawajazoea but pia inategemea na position ya mtoto katika tumbo..20 weeks is too early kuwa worried,japo ni vema umuone daktari kwa ajili ya screening.

nashukuru kwa ushauri wako mkuu. Kiukweli ndiyo mimba yake ya kwanza. Ila sijakuelewa unaposema inategemea na position ya mtoto
 

tunashukuru mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…