Ushauri wana JF: Milioni 25 itatosha kumalizia nyumba yenye sifa hizi?

Du kwa kunena ni rahisi sana hebu ingia kwenye zoezi lenyewe hiyo millioni 10 utakuta imeishia kwenye bati

Hakuna acha uoga nyumba ya vyumba vi3 haifiki milioni 10,minimize cost jamani,wengi wakipata hela wanakuwa na mawenge
 
Mkubwa mbao za mnazi miaka 100 na kuendelea cha msingi ni kuchagua uliokamaa,ushawahi kwenda saba saba banda la JKT? vitanda vyao vyote ni vya minazi.
Dah, King Kong III unanipa mtihani? Ngoja nifatilie nione ukweli wa hii kitu, lakini mhh!
 
Katika ujenzi hakuna kitu kinachokula hela kama finishing ,jipange ndugu
Ni kweli usemacho, lakini finishing haiwezi kumzuia mtu asiishi humo ndani, pia lazima ujue kuwa finishing inategemeana na mtu binafsi, anataka nyumba iweje na material ya aina gani yatumike na ndio ina determine ghalama halisi ya vifaa
 
Kwa jinsi ulivyooleza hapo ningekuwa mimi, kwa hizo 25M ninge focus kwenye vitu vya muhimu ili nyumba iweze kukalika kwanza halafu mambo mengine yatajipa nikiwa humo kwangu, kuliko kuifanya nyumba iishe haraka pasipo na ubora sahihi then baada ya kuhamia unaanza kuvunja hapa na pale , na kubadili baadhi ya sehemu, hio haipendezi, so ni muhimu kufanya vitu vichache ila vya ukweli hayo mengine yataendelea nikiwa humo ndani pia kwa ubora mzuri, na ukisema uache kujenga unajidanganya maana kila siku vitu vinapanda bei fanya hivyo kama umedhamilia, focus na kuezeka kwa hizo msauzi, weka mninga milango ya mbele na nyuma vitasa vya ukweli hata kama ni sh laki 2, weka grill za madirishani na milangoni mbele na nyuma, weka condrich za wiring pia mabomba kwa ajiri ya sytem ya maji,then fanya paster, weka choo cha public then angalia kinachosalia.
Note kwako ni kwako hata kama utakaa kwenye vumbi kwa muda, kwani barabarani utembea kwenye tiles?
 

very good advice kaka
 
Natoa shukrani za dhati kwa wana JF kwa ushauri mnaonipatia, kwa hakika ni faraja kubwa na nikiri kwamba mmenipa uelewa mkubwa wa kuliendea suala labgu hili. Si rahisi kuwataja wote mliotoa ushauri wenu, lakini King Kong III nakushukuru sana kwa wazo lako la Mbao za Mnazi, Kibanga Ampiga Mkoloni(Japo aliniudhi hakumpiga mpaka afe na hivyo sasa hivi asingetusumbua tena) na ushauri wako wa mbao za Mpapai; sina shaka Brown ashika Tama atakuja kunipa ushauri wa kutumia mbao za Mgomba. Lakini niweke wazi, pamoja na kufanyia kazi rai zote, lakini nadhani hii rai yako Dancani imetulia na nahisi ndiyo nitaipa kipaumbele. Shukurani sana kwa ushauri ulio mzuri,mwepesi kuutekeleza na naona kama uko more realistic.
 

Mkuu chamajani vipi ulikamilisha?. Maana mi mwenzio nimekuwa na hiyo lakini naona imekuwa ndogo saaana. Nimeweka Bati tu, imebaki milioni 11. Kwa experience yako hiyo nifanye nini?
 
Mkuu chamajani vipi ulikamilisha?. Maana mi mwenzio nimekuwa na hiyo lakini naona imekuwa ndogo saaana. Nimeweka Bati tu, imebaki milioni 11. Kwa experience yako hiyo nifanye nini?
ushauri wangu ni tengeneza sehemu utakazotumia piga finishing ndani ya nje suburia. Kama kuna vyumba vingi tengeneza vichache unavyotumia. Vingine utamalizia baadae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…