Nimekuwa nikiona kupitia luninga jinsi viongozi wa Kata, Tarafa, Wilaya, Mikoa na hata Taifa wanavyohangaika na kukamilishwa kwa miradi hii. Walipewa agizo kuwa miradi hii iwe imemalizika katika muda wa miezi mitatu.
Mimi binafsi natofautiana na agizo hili. Kwa Mhandisi anayejua maana ya ujenzi huwezi kukamilisha jengo kwa muda wa miezi mitatu. Unapojenga msingi kwanza kunatakiwa kuwe na maandalizi na hii inaweza kuchukua hata mwezi mmoja ukichukulia kuwa lazima msingi umwagiliwe maji na uwe imara.
Kujenga Boma nayo hivyo hivyo na unapokuja kumaliza mpaka plasta huwezi ukamaliza jengo kwa miezi mitatu. Ujenzi unaoendelea ni ulipuaji wa hali ya juu na baadaye tutakuja kujuta. Leo nimesoma kwenye Jamii forums kuwa Mkuu wa Mkoa fulani ametoa masaa 48 kumaliza majengo 452.
Je hii inawezekana? Tuwe wakweli tuna haraka gani? Tutekeleze miradi hii polepole na kipaumbele uwe ni UIMARA(quality).
Mimi binafsi natofautiana na agizo hili. Kwa Mhandisi anayejua maana ya ujenzi huwezi kukamilisha jengo kwa muda wa miezi mitatu. Unapojenga msingi kwanza kunatakiwa kuwe na maandalizi na hii inaweza kuchukua hata mwezi mmoja ukichukulia kuwa lazima msingi umwagiliwe maji na uwe imara.
Kujenga Boma nayo hivyo hivyo na unapokuja kumaliza mpaka plasta huwezi ukamaliza jengo kwa miezi mitatu. Ujenzi unaoendelea ni ulipuaji wa hali ya juu na baadaye tutakuja kujuta. Leo nimesoma kwenye Jamii forums kuwa Mkuu wa Mkoa fulani ametoa masaa 48 kumaliza majengo 452.
Je hii inawezekana? Tuwe wakweli tuna haraka gani? Tutekeleze miradi hii polepole na kipaumbele uwe ni UIMARA(quality).