Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,277
- 8,860
Nimefuatilia kwa karibu tamasha la fiesta jana kuna jambo kubwa nimejifunza na sii vibaya nikamshauri huyu bwana mdogo Diamond kuwa marafiki wanakuwa karibu pindi mziki wako unapokuwa juu, wakijua watapata msaada flani kutoka kwako au faida flani.
Wanapogundua unashuka au una dallili za kuchokwa wanakukimbia mmojammoja au kuwa sehemu ya kukumaliza kabisa.
Nakuasa wee...kijana kipindi hiki ukiwa juu ukiwa na vimafanikio vya magari na vijumba utazungukwa na marafiki lakini baadhi yao ni wanafiki."sijadharau hizo mali zako ila kwa mimi naona ndio kwanza maisha unayaanza una safari ndefu kuitwa tajiri wa uhakika.
Kumbuka hawa clouds ni manyoka tena hatari na wenye sumu mbaya,wataonyesha unyenyekevu lakini baada ya kuanza kuonyesha dadili za kufanikiwa binafsi bila kuwategemea wao wameanza kukumaliza kisanii na sidhani kama hilo umeshaligundua muda sio mwingi hawa jamaa utashangaa hawaonekani tena kwenye mzunguko wako wa kifedha.
Jambo la msingi kwako na wasanii wengine mnatakiwa wanapokaribia kupoteza mvuto wa kisanii kama wewe mjiandae kuwa wajasiriamali.
Tatizo hufahamu kwamba kuna muda wa kupoteza mvuto kimziki kama ilivyokuwa kwa wasanii wenzako wa Tanzania na kimataifa jiandaa kwa hilo mdogo wangu kwa kuanza kuwa wajasiriamali,fungua hata kiwanda kidogo cha kubangua korosho kama biashara ya nguo ilikushinda.
Kinachofanyika sasa hivi na hao unaowaona marafiki zako"clouds"ni kumtengeneza All kiba afanane na saizi yako then wanakutupa na kukuzika wewe na mziki wako
Kwahiyo jiandae mapema baada ya dhamira yao hiyo kutimia uje uishi maisha ya raha na starehe, kama Sugu na wengine wengi...yaliyokukuta jana kwenye tamasha la fiesta iwe funzo kwako na kwa wengine wote.
Ni mimi mpenda maendeleo ya watu Kibo10
Wanapogundua unashuka au una dallili za kuchokwa wanakukimbia mmojammoja au kuwa sehemu ya kukumaliza kabisa.
Nakuasa wee...kijana kipindi hiki ukiwa juu ukiwa na vimafanikio vya magari na vijumba utazungukwa na marafiki lakini baadhi yao ni wanafiki."sijadharau hizo mali zako ila kwa mimi naona ndio kwanza maisha unayaanza una safari ndefu kuitwa tajiri wa uhakika.
Kumbuka hawa clouds ni manyoka tena hatari na wenye sumu mbaya,wataonyesha unyenyekevu lakini baada ya kuanza kuonyesha dadili za kufanikiwa binafsi bila kuwategemea wao wameanza kukumaliza kisanii na sidhani kama hilo umeshaligundua muda sio mwingi hawa jamaa utashangaa hawaonekani tena kwenye mzunguko wako wa kifedha.
Jambo la msingi kwako na wasanii wengine mnatakiwa wanapokaribia kupoteza mvuto wa kisanii kama wewe mjiandae kuwa wajasiriamali.
Tatizo hufahamu kwamba kuna muda wa kupoteza mvuto kimziki kama ilivyokuwa kwa wasanii wenzako wa Tanzania na kimataifa jiandaa kwa hilo mdogo wangu kwa kuanza kuwa wajasiriamali,fungua hata kiwanda kidogo cha kubangua korosho kama biashara ya nguo ilikushinda.
Kinachofanyika sasa hivi na hao unaowaona marafiki zako"clouds"ni kumtengeneza All kiba afanane na saizi yako then wanakutupa na kukuzika wewe na mziki wako
Kwahiyo jiandae mapema baada ya dhamira yao hiyo kutimia uje uishi maisha ya raha na starehe, kama Sugu na wengine wengi...yaliyokukuta jana kwenye tamasha la fiesta iwe funzo kwako na kwa wengine wote.
Ni mimi mpenda maendeleo ya watu Kibo10