Leonel Ateba Mbinda
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 644
- 2,695
Hawa wachezaji ndugu viongozi wa Simba wametoka kwenye vilabu vyao wakiwa na mafanikio makubwa sana, mimi hainingii akilini leo striker Steven Mukwala aonekane hana meno wakati alikuwa mfungaji bora, alikuwa akishika mpira mabeki wa timu pinzani wanamhara, sio mshambuliaji mjinga mjinga huyu Mukwala, Steven Mukwala ni mmoja wa washambuliaji hatari hapa Afrika, mwingine ni Jean Charles Ahoua, huyu ni MVP kule Ivory Coast.Ahoua ni mtu hasa na kiungo mshambuliaji wa kweli sio masihara.
Wachezaji hawa wa kigeni waliosajiliwa katika timu yetu ni wachezaji bora, wana viwango, wana uwezo na mategemeo makubwa ya kuleta heshima ndani ya timu yetu.
Hii Simba hii sio timu ya masihara ingawa wengi wanabeza, timu imekamilika hasa, kulia Kijiri kushoto Valentine, Chamou au Hamza dala Che Malone, six Kagoma ama Okajepha, winga Mutale winga Kibu au Balua au Chasambi au Karabaka, kiungo Debora, mshambuliaji Mukwala ama Ateba, kiungo namba 10 Ahoua au Awesu unaifungaje Simba hii viongozi wangu wa Simba?
Kwanini nimeandika hivi, jana tumemsajili Ateba kuungana na Mukwala kuongeza nguvu, lakini nachotaka kusema kuwa jina la Ateba tayari liko mezani kwa kamati ya ufundi ya Utopolo, Utopolo wana idara kabisa ya kufifisha nyota za wachezaji wa Simba.Utopolo wao wanaamini wakiiizima Simba basi wataendelea kutawala soka la bongo mielele na mielele.
Wachezaji wetu wanahitaji chanjo na kinga kama walivyo wachezaji wa Utopolo, tusipowakinga huyo Ateba pia atakuwa akikosa mabao kila siku.
Striker kama Freddy Michael leo anaonekana kama mchezaji wa mtaani kutokana na kufunikwa nyota yake, haya mambo msiyapuuze viongozi wangu.
Mo Dewji atachoka maana amefanya kila mnachokitaka ili sisi tupate furaha, biashara zake Mo zinategemea sana Simba kufanya vizuri, Simba ikifanya vizuri na biashara na uwekezaji wa Mo utakwenda vizuri, leo Mo hatawaelewa endapo tutafanya vibaya, mpeni ushirikiano Mo ili fedha anazotoa zionekane zimekwenda kihalali, wachezaji hawa wanahitaji kufanyiwa dua na ipigwe kunuti ya kweli ili kama kuna mpumbavu anahujumu wachezaji wetu ajue kuwa Simba hatutaki utani,.
Tumewaponda akina Babacar Sarr na Sadio Kanoute leo wako na Benchika wanaupiga mwingi, Babacar alikuwa kila siku anafunga bandeji mguuni leo anaonekana kule Algeria anafanya mazoezi bila bandeji na hana majeraha yoyote, Simba kulikuwa na nini hadi awe na majeraha mara kwa mara hata akicheza anakuwa amefunga bandeji, nani anawafanyia uhuni wachezaji wetu.
Lingine ni uwanjani wetu Bunju, kule Avic Town jamani haruhusiwi kuingia mtu kule, kama huna shughuli marufuku kuingia, uwanja wetu wa Bunju uko karibu na makazi ya wananchi, mtaweka mazindiko lakini inakuwa ngumu sana kwa sababu kuna majirani wako karibu na uwanja wanapenda Yanga, kwahiyo na kwa vile uwanja hauna usalama wa kutosha mtu kuingia mle na kubeba mchanga ama nyasi kwend kuzifanyia ndumba ni easy tu.
Nimewahi kushauri hapa kama tutaendelea kutumia uwanja wa Bunju kujiandaa kuikabili Yanga hatutawafunga milele, hilo nawahakikishia, fuatilieni na fanyeni tathmini tangu tufungwe goli lile na Morrison hadi leo tumewafunga Yanga mara moja tu kwa mabao ya Kibu na Inonga, zaidi ya hapo ni sare na kufungwa tu.
Soma Pia: Wachezaji wapya wa Simba wanahitaji muda ili kuzoea mazingira ya ligi yetu, tafadhalini sana mashabiki wa Simba
Mwisho, kwanini Yanga wawe wanatufunga sana utawala huu wa GSM? Kwanini nyie viongozi hamfanyi utafiti? Kwa sababu nawahakikishia Oktoba 19 pia hatutawafunga na watatutandika kama kawa? Nani anatuhujumu hadi tunapocheza na Yanga tunakuwa wanyonge namna hii, nyie viongozi na friends of simba mnadhani sisi washabiki tunapenda hali hii, tutaendelea kuwa malofa kwa Yanga hadi lini, Je mmeamua kuua upinzani wetu na Yanga? Yanga atufunge mara tatu mfululizo, katufunga 5, katufunga 2, katufunga 1 na bado ataendelea kutufunga, nyie mnaona kweli ni sawa hiyo?
Tuwalinde wachezaji wetu kwa nguvu zote, wachezaji hawa wakija lazima tuhakikishe hakuna ubaya wanaofanyiwa kiutamaduni ili kulinda afya na viwango vyao, vinginevyo kila msimu tunatengeneza timu mpya, kila heri dhidi ya Tabora United.Nitakuwepo uwanjani kushuhudia kiama tutakachowashushia Tabora siku hiyo.
Wachezaji hawa wa kigeni waliosajiliwa katika timu yetu ni wachezaji bora, wana viwango, wana uwezo na mategemeo makubwa ya kuleta heshima ndani ya timu yetu.
Hii Simba hii sio timu ya masihara ingawa wengi wanabeza, timu imekamilika hasa, kulia Kijiri kushoto Valentine, Chamou au Hamza dala Che Malone, six Kagoma ama Okajepha, winga Mutale winga Kibu au Balua au Chasambi au Karabaka, kiungo Debora, mshambuliaji Mukwala ama Ateba, kiungo namba 10 Ahoua au Awesu unaifungaje Simba hii viongozi wangu wa Simba?
Kwanini nimeandika hivi, jana tumemsajili Ateba kuungana na Mukwala kuongeza nguvu, lakini nachotaka kusema kuwa jina la Ateba tayari liko mezani kwa kamati ya ufundi ya Utopolo, Utopolo wana idara kabisa ya kufifisha nyota za wachezaji wa Simba.Utopolo wao wanaamini wakiiizima Simba basi wataendelea kutawala soka la bongo mielele na mielele.
Wachezaji wetu wanahitaji chanjo na kinga kama walivyo wachezaji wa Utopolo, tusipowakinga huyo Ateba pia atakuwa akikosa mabao kila siku.
Striker kama Freddy Michael leo anaonekana kama mchezaji wa mtaani kutokana na kufunikwa nyota yake, haya mambo msiyapuuze viongozi wangu.
Mo Dewji atachoka maana amefanya kila mnachokitaka ili sisi tupate furaha, biashara zake Mo zinategemea sana Simba kufanya vizuri, Simba ikifanya vizuri na biashara na uwekezaji wa Mo utakwenda vizuri, leo Mo hatawaelewa endapo tutafanya vibaya, mpeni ushirikiano Mo ili fedha anazotoa zionekane zimekwenda kihalali, wachezaji hawa wanahitaji kufanyiwa dua na ipigwe kunuti ya kweli ili kama kuna mpumbavu anahujumu wachezaji wetu ajue kuwa Simba hatutaki utani,.
Tumewaponda akina Babacar Sarr na Sadio Kanoute leo wako na Benchika wanaupiga mwingi, Babacar alikuwa kila siku anafunga bandeji mguuni leo anaonekana kule Algeria anafanya mazoezi bila bandeji na hana majeraha yoyote, Simba kulikuwa na nini hadi awe na majeraha mara kwa mara hata akicheza anakuwa amefunga bandeji, nani anawafanyia uhuni wachezaji wetu.
Lingine ni uwanjani wetu Bunju, kule Avic Town jamani haruhusiwi kuingia mtu kule, kama huna shughuli marufuku kuingia, uwanja wetu wa Bunju uko karibu na makazi ya wananchi, mtaweka mazindiko lakini inakuwa ngumu sana kwa sababu kuna majirani wako karibu na uwanja wanapenda Yanga, kwahiyo na kwa vile uwanja hauna usalama wa kutosha mtu kuingia mle na kubeba mchanga ama nyasi kwend kuzifanyia ndumba ni easy tu.
Nimewahi kushauri hapa kama tutaendelea kutumia uwanja wa Bunju kujiandaa kuikabili Yanga hatutawafunga milele, hilo nawahakikishia, fuatilieni na fanyeni tathmini tangu tufungwe goli lile na Morrison hadi leo tumewafunga Yanga mara moja tu kwa mabao ya Kibu na Inonga, zaidi ya hapo ni sare na kufungwa tu.
Soma Pia: Wachezaji wapya wa Simba wanahitaji muda ili kuzoea mazingira ya ligi yetu, tafadhalini sana mashabiki wa Simba
Mwisho, kwanini Yanga wawe wanatufunga sana utawala huu wa GSM? Kwanini nyie viongozi hamfanyi utafiti? Kwa sababu nawahakikishia Oktoba 19 pia hatutawafunga na watatutandika kama kawa? Nani anatuhujumu hadi tunapocheza na Yanga tunakuwa wanyonge namna hii, nyie viongozi na friends of simba mnadhani sisi washabiki tunapenda hali hii, tutaendelea kuwa malofa kwa Yanga hadi lini, Je mmeamua kuua upinzani wetu na Yanga? Yanga atufunge mara tatu mfululizo, katufunga 5, katufunga 2, katufunga 1 na bado ataendelea kutufunga, nyie mnaona kweli ni sawa hiyo?
Tuwalinde wachezaji wetu kwa nguvu zote, wachezaji hawa wakija lazima tuhakikishe hakuna ubaya wanaofanyiwa kiutamaduni ili kulinda afya na viwango vyao, vinginevyo kila msimu tunatengeneza timu mpya, kila heri dhidi ya Tabora United.Nitakuwepo uwanjani kushuhudia kiama tutakachowashushia Tabora siku hiyo.