Ushauri wangu kwa Wanasiasa wa kweli walio ACT Wazalendo na CHADEMA

Ushauri wangu kwa Wanasiasa wa kweli walio ACT Wazalendo na CHADEMA

CCM wanatumia kila njia kuwatongoza ACT na CHADEMA ili waingie kwenye serikali na ubunge, kwa kinachoendelea bado kwa upande wa Zanzibar hali imekuwa ngumu zaidi na zaidi kila kunapokucha haswa kunapotokea vifo vinavyoendelea vya wahanga wa ulioitwa uchaguzi Mkuu.

Upande wa Tanganyika au tuseme Tanzania bara kumetokea sintofahamu ambayo itahitaji wakuu wa CHADEMA kutoa kaulimbiu ya kilichotokea kama kina baraka au hakina baraka kuhusiana na wabunge wanawake wa kuteuliwa kuingia bungeni.

Zanzibar kila kijiwe hakipo tayari kuona ACT inaingia kwenye serikali ya Rais Hussein Mwinyi,wananchi walio wengi wanasema kila mtu abebe mzigo wake kwa maana hawataki kuona wala kusikia ACT inaingia kwani hakuna faida na zaidi wanadai hakukuwa na uchaguzi wa aina yeyote kilichotokea ni kuwaharibia watu muda wao.

Kuna habari kuna kundi kubwa la walioteswa huko Pemba ambao hali zao zimekuwa tete na zinazoashiria kupoteza maisha wamehamishiwa hospitali za Dar es Salaam ili lifanyike la kufanyika kuokoa hali zao baada ya Hospitali za Pemba kuelekea kushindwa kuwatibu kwa majeraha waliyopewa na vikosi vya SMZ.

Haiwezekani kwa ACT kujiunga na serikali ya Rais Hussein Mwinyi hata dakika moja utakuwa ni usaliti kwa wanachama wa ACT na wapiga kura.

Wanachokitafuta CCM ni kwa vyama hivi kuingia katika serikali zao haramu ili waitangazie dunia kuwa uchaguzi umekuwa ni wahalali na walioshindwa wameshindwa kihalali,zilikuwa ni peresha za kushindwa tu ,sasa wametulia na wameshaingia kwenye serikali kama haitoshi wataandika mabarua makubwa makubwa kupeleka kwa mabeberu kuwa kila kitu shwari na hakuna tena mvutano watanzania wote ni wamoja huku wakionyesha picha za kideo wabunge wa upinzani kushiriki serikalini.

Chadema fukuza chama wabunge wote waliopokea hela na kununuliwa kwa bei mbaya na hata maalim akienda kuingia kwenye serikali atafukuzwa chama.

CCM moja ya faida watakayoipata kama hawa ni kuingiza fitina ndani ya vyama na kusababisha viongozi na wanachama kufarikiana.
 
Jiandae kwa lolote kiongozi....

Watanzania tunatabia ya kutopenda kukosa vyote.
👣
 
CCM wanatumia kila njia kuwatongoza ACT na Chadema ili waingie kwenye serikali na ubunge ,kwa kinachoendela bado kwa upande wa Zanzibar hali imekuwa ngumu zaidi na zaidi kila kunapokucha haswa kunapotokea vifo vinavyoendelea vya wahanga wa ulioitwa uchaguzi Mkuu...
Umeongea point tupu mkuu
 
Bahati mbaya ikiwa asubuhi kila mtu ana msimamo, mchana wanapungua na ikifika jioni wengi unagundua maamuzi yao yalikuwa siyo yenye faida na kumsaidia mwananchi bali kila mtu anaangalia familia yake itaishije.

👉 HAKUNA SIASA HAPA AFRIKA.
 
Mkuu;
Hawa vijana wanaofanya ''schoolboy politics'' hawawezi kukuelewa!

Mtu anayedhani anajua wakati hajui ni vigumu sana kama sio haiwezekani kumuelimisha na kukubali kuelimika!

Yaani anafikiri nchi inaendeshwa tu kinadharia huku yeye akiwa nyuma ya keyboard/keypad!
Eti schoolboy politics??? Kweli Ccm mmejimilikisha hii nchi.

Endelea kukebehi jitihada za watu wanaotaka maendeleo ya kweli ya Watanzania na Tanzania kwa ujumla. Hujui kuwa jitihada hizi zina faida kwako wewe na kizazi chako chote. Siku moja utakuja kujiona ulivyo mjinga.
 
Hata ACT watajiunga soon, saiv wanasubir hali ya hewa ipoe kwanz
 
Unajua wanasiasa wa Africa wanafanya wanachama kama macartoons vile si ajabu hawa kwenye vikao vyao vya siri wanakubaliana lakini kwenye hadhara wamejipanga huyu sema hivi ,wewe sema hivi ,yule sema hivi . Kwa asili ya wenye chama cha chadema wapo kwa ajili ya FWEZA kile chama ni kama mradi
 
CCM wanatumia kila njia kuwatongoza ACT na Chadema ili waingie kwenye serikali na ubunge ,kwa kinachoendela bado kwa upande wa Zanzibar hali imekuwa ngumu zaidi na zaidi kila kunapokucha haswa kunapotokea vifo vinavyoendelea vya wahanga wa ulioitwa uchaguzi Mkuu...
Guys huwa mnasemaga Sana..na hapa narudia tena..hizo hoja zako ni mufilisi..now watu wako busy kuangalia ni kwa namna Gani chama kitaendelea mbele..maana jua kama.wanakataa kuingia serikalini..inamaana vyama vitakufa njaa..havitapewa ruzuku za kujiendesha..so mnapofikiria hoja zenu karibun kuliangalia hili..

CDM wameona mbele..kwamba sawa tayari tumeshabakwa..tufanyeje.ili kujitibu majeraha hayo..lazima waje na mikakati B na hoja hapa sio kutafuta sijui uhalisia wa uchaguzi.

Soon, ACT Wazalendo nao wataungana na CCM kule znz Ili kujaribu kukiuhsiha chama kwa miaka mitano ijayo..

So haina maana kukubali kwao inamaana Kama mnavyofikiria..kumbuka pia huwezi kuitoa CCM ukiwa nnje ya serikali..
 
Wengi tunamuani tatizo ni kile kilichojificha nyuma ya pazia!
Huyo uliyemtaja hana credibility yeyote ya kusema lolote na akaaminika. She has lost everything. Hakuna kitu ata simamia bungeni na kukisema akaaminika tena!!
 
Huu ushauri wangu hauhusishi wanasiasa njaa/ Wanasiasa Maslahi, bali wanasiasa kweli wenye uchungu na nchi yao. Waliopo kwenye siasa kwa dhumuni la kuleta itikadi mbadala inayoenda kuleta mabadiliko ya kweli nchini katika maendeleo ya wananchi yanayoongozwa na demokrasia ya kweli na sio wanasiasa maslahi, wanaochukulia siasa kama ajira au sehemu ya kujijenga kimaisha na kikipato....

Mtaji wa chama chochote ni watu

CCM kinabaki kuwa chama imara chenye misingi imara, chama cha wananchi wote, chama chenye uthubutu wa kukemea maovu na kusema hapana kwa mwanachama yoyote anayedhani ni mkubwa kuliko chama na kuliko Tanzania.

Kuendelea kuuongelea upinzani usiokuwepo na kuendelea kuamini vikundi vya kisiasa visivyokua na misingi ya uzalendo ni kujilisha upepo

Pole Lord denning
 
Nani mkweli ktk siasa upinginie siasa utakua na akili timamu kweli
Siasa ni biashara ya kisayansi mtu hufanya kwa malengo yake binafsi kisingizio kutetea wananchi na kuafuta haki, bado watu wataumia sana kutafuta maslahi binafsi kwa njia ya kisiasa
 
Kama ulimsikiliza Mheshimiwa Kibudu Paramagamba na kumuelewa ,Tanzania kutoshirikiana na mabeberu inamaana itakufa ? Kama hivi vyama kwa kutegemea ruzuku basi havifai kuwepo na havifai kuaminiwa na wananchi ,ni vyama vingapi vipo na havina ruzuku, ruzuku ni jinga la moto kutegemea ruzuku ni sawa na ng'ombe aliefungwa puani anakovutwa ndiko anakoelekea hawezi kukataa.

Ila kwa Zanzibar mbona wamekaa bila ya kushiriki na wameibuka kidedea na kudhibiti kampeni za uchaguzi kama ungekuwepo basi leo hii kungekuwa na hadithi nyengine.

kama chama kina wananchama na viongozi na wanachama wanasikilizana mbona michango ya wanachama ni hela nyingi tuu ! Huna haja ya ruzuku, ruzuku inakaribia ni sawa na rushwa,na tunaona imewaghilibu hao wanawake.

ACT wazidi kudinda hadi CCM waelewe ,hakuna masihara kuhusu maisha ya watu,watu zaidi ya hamsini inatetesiwa kuwa wamepoteza maisha na mamia hali zao ni za mguu ndani mguu nje ya dunia ,wapo Muhimbili huko CCM wanahangaika nao.

Kusema huwezi kuitoa CCM ukiwa nje ya serikali hilo sio kweli, ukweli huwezi kuitoa CCM ukiwa ndani ya serikali na ndio maana kukaanzishwa vyama vya upinzani na ndio maana CCM hawavitaki vyama vya upinzani ni suala la muda tu subiri mpaka bahari itakapoamua kuchafuka kikwelikweli haya ya sasa ni mawimbi ya kawaida tu na yanaelekea kila siku zikizidi kuchafuka .

*** Kama ACT watagomea kuingia serikalini na Chadema kuruhusu au kubariki, nakuhakikishia ACT watazidi kujizolea wanachama zaidi kwa msimamo huo na hata viongozi andamizi wa CHADEMA wenye msimamo madhubuti wataelekea ACT.

Kuiogomea CCM katika kuingia serikalini ni pigo takatifu,pigo ambalo litaenda sanjari na harakati za kudai haki amani na umoja wa kitaifa na kuliondoa tabaka linalojijenga la CCM,

Kama hao Chadema wameruhusu hilo kwa kweli watakuwa wanahangaishwa na hela na sio kwa ajili ya wananchi na hao walijipeleka kama ni kwa njaa zao basi wapewe siku kama hawatorejea wanafukuzwa mbona kuna watu wengi wanahitaji kugombea hizo nafasi watu na heshima zao.
 
Tuache uongo kwa nchi za Afrika hasa Tanzania siasa ni ajira kama zilivyo ajira nyingine.
 
Back
Top Bottom