Moisemusajiografii
JF-Expert Member
- Nov 3, 2013
- 43,960
- 77,533
Hivi siku hizi nazeeka au ni nini? Stories za kitoto nazichukia sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
We acha tu mkuu naishia Kupita kama hivi.Ulidhani ni Nida huku au sio
Usimdharau yeyote kwa outward appearance,utakuja kuumbuka....heshimu mtu yeyote aliye mbele yako hata kama anaokota makopo
Hakuna hata ndevu za Uchebe, nenda gym ukaongeze minofu au uwe unavaa nguo za kichungaji suruali ndevu hadi chini inaburuza😁😁😂Mimi kuna siku tena ni zaidi ya mara moja inanitokea, mara ya kwanza ilikuwa pale nje ya wizara ya ardhi niliegesha gari pembeni nikanunue gazeti narudi nakuta wale majamaa wamelifunga.
Nikaanza zozana nao wao jibu wanalonipa kamwite mwenye gari. Yani kila nalowambia wananiambia mwenye gari atalipa we unahangaika nini kamwite mwenye gari, dah ila mwisho nikampa 20,000 akalifungua nikasepa.
Mara nyingine nilikuwa pitiliza mataa wakati taa zimezuia, kumbe mbele kuna traffic, akandaka. Akaanza kunisngekuwa na boss wako usingefanya hivi na maneno mengi. Baadae, akaniomba leseni na kadi ya gari nikampatia akakuta kadi ya gari ina jina sawa na leseni.
Akasema kumbe gari lako nikamjibu ndiyo, akaishia kucheka akasema yani watoto wa kishua bwana mnakula maisha kwa pesa ya baba zenu. Mimi nikacheka tu akaniandikia faini nikasepa huku nikiwaza ungejua mimi mpambanaji tu.
Mara nyingine niliacha gari lilikuwa na matatizo na mimi nina haraka nikalipaki pembeni ya barabara nikachukue boda boda, kumbe huku nyuma askari wakapita lipo, wakapita tena lipo ikabidi watanaze times ambaye katelekeza gari akalichukue mimi sikuwa na habari.
Narudi baadae kulichukua nikiwa na fundi, gari silioni, namuuliza muuza matunda ndiye akaniambia wamelibeba wamelipeleka kituo cha polisi cha kawe. Kesho yake naenda kawe mkuu wa kituo akawa ananizngua kuwa nikamtafute mwenye gari, mpaka nilipofungua nikamwonyesha kitambulisho na kadi ya gari majina yana match. Aliniambia tu niwalipe waliolivuta nisepe tu.
Yani mimi nina mwili mdogo kama wa Mrehemu Ruge Mtahaba, nakutana ma mazarau sana maana hata nikivaa suti haikai ni kama imetundikwa tu.
Ndevu na nywele zangu hazinaga ushirikianao, hivyo nywele huwa nanyoa kila wiki zikae size ya chini kabisa, ndevu naziacha lakini ziko kidevuni tu nazo hata niziache miezi hazizidi kimo flani.Hakuna hata ndevu za uchebe, nenda gym ukaongeze minofu au use unavaa nguo za kichungaji suruali ndevu hadi chini inaburuza😁😁😂
Yeah maana huwezi jua nani atakusaidia kwa wakati gani, ni wachache wanalitambua hilo, ila tuliozoea kutembea sehemu mbalimbali katika kusaka maisha, tulilijua hili mapema sana, unafika sehemu hujui pakuanzia ila ghafla unasaidiwa na mtu ambaye hukuwahi kutegemea.100% kila mtu ni muhimu hapa duniani. Hata kama ni mshona viatu inabidi kumheshimu sana
miaka mingi zamani kama 10 imepita nilikua nafanya kazi mahali kama mtu wa Sales...sasa jioni dakika chache kabla ya kufunga akaja jamaa mmoja kavaa kawaida tu yule jama alikua mstaarabu sana sasa mm nikawa namjibu shortcut sana plus muda umeisha nataka kusepa halafu nikaona kama hawezi nunua mzigo wenyewe ulikua kama wa 32 hv mwaka 2010...nikamtupa jamaa nikamwambia kesho uje ulete document flani ...akaniuliza nije saa ngapi? nikamwambia saa nne asubuhi jamaa akaga na mm nikamsahau..
Lahaula saa nne kamili bwana jamaa kaja kapiga magwanda hatari aisee...kumbe ni kanali wa jeshi kachafuka..plus ana bodyguard au dreva (sikujua diference)..aisee jamaa kumbe alikua head of logistic wa JWTZ Tanzania nzima..(alinipa card) yule jamaa alipata huduma ambayo hajawahi pata mahali...akawa mshkaji wangu mno aisee...
ila sisi wabongo tun tabia ya kujudge mtu kwa muonekano au mavazi yake mno aisee na nahisi jamaa alijua ile siku ikabidi kesho yake anikomeshe...tokea ile siku mpaka leo naheshimu kila mtu..na imenisaidia sana deals nyingi mno...
Stori za ulimbukeni.Hivi siku hizi nazeeka au ni nini?Stories za kitoto nazichukia sana.
ki NGO chenu ambacho ni hayati kwa sasa tangia mwaka 2015[emoji28][emoji28][emoji28]It was a suprise kwangu.
Jirani yangu aliokuwa wanajifanya ni Boss wa Ikulu mtaani muda wote kanuna na miwani yake mieusi alikuja kunihudumia Chai Ofisini kwa Mama Salma Kikwete wakati wa WAMA, kumbe Alikuwa Office attendant pale tena wale wa oya oya na mie na wenzangu tulienda kupeleka project paper ya ki NGO chetu ambacho ni Hayati kwa sasa kuanzia 2015.
alikua anataka ale tunda lako kimasiharahii kitu bwana kuna mzee alikua anakujaga home kavaa kiraia tu ananiambia nimchumie pilipili kwenye ki garden cha home nikawa nampa nikiwa form six enzi hizo sasa bwana siku moja nimewai kuamka nikakaa nje wazee wanaenda job du yule mzee si akapita kumbe alikua meja general tena mkuu wa jkt tangu siku ile nikawa namuogopa alafu yeye bado anataka story na mimi manake hapo home kulikua na kibaa cha mangi tunakunywa bia hapo story nyingii sema mshua alikua taita so ni mshkaji wake
Eti huyu msichana ni mvulana mkuu....kitu kama Jana walisema ni mvulana org.
"Eti akasoma kwa utulivu" daa [emoji1787][emoji1787]sisi wengine baada ya hapo ndio huwa tunafunga vioo mazima,yaani fanya kama hatujawahi kukutana.
mimi jamaa alinisimulia hii tabia ya kudharau mikakati ya mtu katika maisha yake, usione mtu kazini yupo yupo tu miaka inaenda ukamdharau kwamba hana mipango, utajichanganya.
jamaa anasema wameanza kazi mwaka mmoja na huyo mshikaji wake, yeye akawa amepanga nyumba ya gharama kama 250k,usafiri wa kusumbulia watumjini nk. mwenzake yupo yupo tu. nyumba katafuta ya 120k, gari hakununua nk.
wamefanya kazi kama miaka 8 hivi. baadae siku moja wanapiga story jamaa yangu sasa akaanza maneno ya kumsimanga jamaa, oooh we vipi bana hela hatuoni wapi unapeleka, upo upo tu kama mshamba.jamaa akakereka ikabidi amuonyeshe salio bank, akasoma kwa utulivu ilikuwa ni 68mil, kwenye simu kuna 7mil.
baada ya pale jamaa siku yake iliharibika sana.
hapana mkuu alikua anapenda pilipili za home tu akishakula vyombo anachukua pilipili anaenda zake home
mvulana mkuu nafanya social experimentEti huyu msichana ni mvulana mkuu....kitu kama Jana walisema ni mvulana org.
Ulizidi kukonda na kuchakaa...kuna mdada mmoja mkenya wanaishi Germany sasa ukimuona utazani beki tatu hana alama ya kutoka ulaya...amechakaa mMara nyingi Sana ,alikuja rafiki wa mfanyakazi wangu wa dukani infact wote wa tatu Ni age mate Japo naweza kuwa nimewapita Kati ya miaka mitatu au minne hivi wote wawili
Basi hako kadada kakaja vipi Geee akimanisha huyo Sasa mfanyakazi wangu poa mzima Karibu Sana hapa ndo napofanya kazi aah pazuri Karibu Sana ,Mimi hata salamu ya Mambo hakunipa ......
Yule Gee Sasa mfanyakazi akamtambulisha Karibu huyu ndo boss wangu ,akapigwa na butwaaaa paaaaap,akasema shikamoo na goti la kuibia nikamwambia kwa mkato marahaba(shikamoo yake ilikuwa ya mshutuko Mana infact tumelingana)
Akakosa pozi rafikiye akamtoa
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Ulizidi kukonda na kuchakaa...kuna mdada mmoja mkenya wanaishi Germany sasa ukimuona utazani beki tatu hana alama ya kutoka ulaya...amechakaa m
Hadi kero....ndio umenikumbusha huyu ndugu yetu mkenya.