T11
JF-Expert Member
- Oct 11, 2017
- 5,101
- 4,560
[emoji23][emoji23][emoji23]
Ongea na PA wangu.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ongea na PA wangu.
Hausemi kazi yako. Why?
ulimchana kuhusu dharau zake??Nilikaribishwa na binamu zangu me nikaenda, kufika nikakuta wageni ambao ni mama yao mkubwa na mama mdogo, mdogo wao pia mzazi mwenzie yule me mkubwa. Kuna wanaonijua pale na wengine hawanijui Ila wananisikia. Baada ya kutambulishwa hakuna aliyenijali kabisa hadi nikajisikia unyonge yaani ni wale vijana ndio walinihudumia kila kitu hawakuwa na muda na Mimi kabisa hao ke. Ikapita kama mwaka mmoja hivi dogo akataka kuoa wakafanya kikao kwa mama ya mdogo Mimi sikwenda niliwaambia chochote watakachohitaji nitatoa Ila sitofika hapo, baadae muoaji akaniomba harusi iingilie nyumbani kwangu baada ya wiki mbili watakwenda kwenye chumba chao nikawakubalia. Ikawa kila akiulizwa swali bwana harusi mtarajiwa anajibu nitamuuliza dada X. Ikabidi wamwambie huyu X aje hapo atudhirishie kama kwenye yeye atabeba mzigo huo na haya mengine unayoyataja, akanipigia simu palepale nikajibu Jumamosi ijayo nitakuja kweli nikaenda nikaulizwa yote nikakubali. Nikawaelekeza kwangu hivyo wakaja tukafanya harusi wakaondoka [emoji3][emoji3][emoji3]. Kuanzia hapo heshima juu. Maana wote walihudhuria, kubwa na Kali yule aliyekuwa ananipandisha na kunishusha siku iso na jina akanieleza matatizo yake ya ugonjwa nikamugharamikia. Hadi sasa heshima juu. Nashukuru simdharau mtu ila napenda kuwa mkweli na sijutii hilo, hivyo jibu langu mtu anaweza fikiri nimemdharau
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.
Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.
Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.
Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.
Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.
Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.
Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.
Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?
Bimdash unashombo mzigo kama uwendi chooni we F.Huyu ni msomi aliyekosa direction, lzm adate[emoji16]
Wewe ndio hujaelewa kwanini nimeuliza.
Shukrani tubarikiwe wote sweetie[emoji122][emoji122][emoji122] barikiwa
Hapana mkuu wale ni ndugu hata hivyo jinsi walivyo tahayari inatoshaulimchana kuhusu dharau zake??
Kama hujaelewa hutoelewa endelea na menginemkuu hata cjaelewa hii story yako ase
Hongera Boss. Inaonekana wewe ni mstaarabu sana na umepata exposure kubwa kwa nchi za wenzetu ndio maana hukujali sana hata pale ulipodharaulika.Binafsi nina visa vingi nimewahi kumbana navyo vya kuchukuliwa powa. Hapa nitataja vinne tu.
1.Nakumbuka nilihamia sehemu fulani ofisi flani mahali fulani.
Kwa vile nilikuwa mgeni sikuhama na kitu chochote zaidi ya mi mwenyewe.
Basi nikawa na tabia ya kwenda kula kwa mama ntilie ugali wa buku japo pale jirani kulikuwako na mgahawa mmoja wa kiwango cha juu kwa ajili ya watu wa tabaka la juu .
Wateja wenzangu wengi wao walikuwa bodaboda na machinga. Yule mama ntilie pamoja na wasaidizi wake walikuwa wababe na kauli mbaya kwa wateja wao, kiujumla kwao mteja alikuwa sio mfalme bali lofa.
Jioni moja nikaomba niongezewe mboga kidogo ili nimalizie ugali wangu lakini nilijibiwa kwa jibu la dharau sana mpaka wateja wenzangu wakanicheka.
Tangu siku hiyo nikahamia kwenye mgahawa wa wadosi nikawa nakatiza kwa mamantilie naingia mgahawa wa kishua. Yule dada akawa anapatwa na mshangao kama haamini kama ninauwezo wakula kule.
Lakini pia akaanza kuniona na kampani za watu fulani ambao wanafahamika na ni maarufu eneo lile. Tangu kipindi hicho akawa anajichekesha chekesha kwangu maana alisha fahamu nafasi yangu ndani ya jamii yao ila nashukuru sikuwahi kumshobokea hata kwa salamu.
2 Nikiwa ofisini, kwa vile nilikuwa mgeni, siku moja aliingia mteja ofisini akanikuta nimekaa kwenye meza yenye ya wageni, nilifanya hivyo ili kujipatia mazingira ya urelax kwa assigment niliyokuwa nafanya kwa muda ule. Ili kufanikisha hilo kiti changu na meza yake ninavyotumia kufanyia kazi vilibaki wazi hivyo ikawa kana kwamba mi ni mgeni na boss hayupo maana kiti hakina mtu.
Mara nikaona jamaa amefungua mlango ghafla nakuanza kuuliza bila hata kusalimia. Jamaa akawa ananiuliza huku akinyosha kudole kwenye kiti cha boss " jamaa yuko wapi" nikamjibu "katoka kidogo" Mara nikaona PS anaingia ofisini na kuniuliza "huyu mgeni hajakuona kwani mbona kasema hakuna mtu"? Nikamjibu mwambie aingie.
Basi yule jamaa akaingia ila hakuwa na confudence tena maana alishavurugika kisaikolojia japo nilijitahidi kumjenga kisaikolojia na kumuhuumia vizuri.
3.Siku ingine nafika ofisini nakuta wamama wawili wamekaa kwenye benchi wanamsubiri mwenye ofisi, nikasimama na kawasalima vizuri kwa utulivu, mmoja kajibu kwa kujilazimisha kwa kubetua mdomo yaani ni kama wananishit wanaona nawapotezea muda maana wanamsubiri boss wamweleze kilio chao. Basi nikaingia ofisini kidogo kama dk 3 kisha nikatoka nnje mara nikasikia PS anawambie " nyie mbona hamwingii?, anaondoka huyo! Mara nasikia kwa nyuma watu wananikimbilia huku wanaita kwa sauti za unyonge" baba samahani tunashida na wee! Nikasimama na kuwaomba twende ofisini tuongee. Niliwahudumia vizuri japo walisha potewa na confidence maana nafsi ziliwasuta maana waliuchukulia poa mwonekano na umri wangu nadhani.
3. Juzi kati nilipanda basi kuelekea mkoa fulani. Kwa vile nilipandia njiani nikapata siti jirani na dada wa makamo bonge. Nikamsalimia vizuri ila hakuitikia kwa kutoa sauti bali akatikisa kichwa tu . Baada ya mwendo wa safari ndefu, nadhani mdada alinisoma na kugundua alini underate kwa makosa. Basi akaanza kujitahidi kuniongelesha mara ooooh, "samahani kaka eti hapa ndo wapi," ooooh, "kaka hivi we ni mwenyeji ............"(anataja jina la mji tunaoelekea) Sikumshobokea , nami nikawa namjibu kwa kutikisa kichwa tu huku niko bize na simu yangu.
4.Juzi nimehudhuria harusi ya jamaa yangu. Nilikuwa peke yangu kwa vile wife alikuwa na udhuru.
Basi nikaelekezwa kwenye meza moja ambayo tayari ilikuwa na wenza wawili (umri kati ya 30 na 35) Basi nikawasalimia kwa sauti huku nikivuta kiti na mie nikae. Yule mdada aliitikia lakini mwanaume hakuitikia.
Ukaja muda wa kugobganisha glasi kila mtu na jirani yake , kwa vile nilikuwa sina mtu mingine zaidi yao nikagonganisha nao glasi lakini naona yule mkaka kama hataki . Ok, shughuli ikaendelea naona jamaa yuko bize na kushikana shikana na mpenzi wake nami niko bize na simu yangu.
Tumekula chakula tumemaliza mi sikuwa na haraka ya kuondoka ukumbini maana nilikuwa bado namalizia kinywaji changu. Basi baada ya kumaliza kula naona msela ananyanyuka anamvuta demu anamwambia "twende zetu acha hiyo" demu akaiacha redbull ambayo ndio kwanza ameifungua. Kwa vile tulikuwa mimi na wao pale mezani nilitarajia angalau " broh sie ngoja tutangulie"!
Bada ya kama dk 15 namimi nikatoka ukumbini ili nirudi home maana ilikuwa yapata saa 7 za usiku. Nafika karibu na parking, nawakuta wale mtu na demu wake bado wapo kumbe wanasubiri bodaboda huku wakipata adhabu ya kipupwe cha usiku . Nikawapita kwa karibu, nikaingia kwenye usafiri wangu nikawasogelea nikashusha kioo kidogo na kuwaaga "jamani mi natangulia, naona nyie bado mpo". Sijui kama walijibu ama la ila nilichogundua niliona msela amekosa confidence na amekuwa mnyonge saana.
Yawezekana kuwa na madhaifu ya kibinadamu ila kujisocialize na watu bila kujali hadhi zao ni faida kwako kuliko hasara.
Mkuu usingemalizia kwa kusema una mwili mdogo,ningekwambia mimi.Mimi kuna siku tena ni zaidi ya mara moja inanitokea, mara ya kwanza ilikuwa pale nje ya wizara ya ardhi niliegesha gari pembeni nikanunue gazeti narudi nakuta wale majamaa wamelifunga.
Nikaanza zozana nao wao jibu wanalonipa kamwite mwenye gari. Yani kila nalowambia wananiambia mwenye gari atalipa we unahangaika nini kamwite mwenye gari, dah ila mwisho nikampa 20,000 akalifungua nikasepa.
Mara nyingine nilikuwa pitiliza mataa wakati taa zimezuia, kumbe mbele kuna traffic, akandaka. Akaanza kunisngekuwa na boss wako usingefanya hivi na maneno mengi. Baadae, akaniomba leseni na kadi ya gari nikampatia akakuta kadi ya gari ina jina sawa na leseni. Akasema kumbe gari lako nikamjibu ndiyo, akaishia kucheka akasema yani watoto wa kishua bwana mnakula maisha kwa pesa ya baba zenu. Mimi nikacheka tu akaniandikia faini nikasepa huku nikiwaza ungejua mimi mpambanaji tu.
Mara nyingine niliacha gari lilikuwa na matatizo na mimi nina haraka nikalipaki pembeni ya barabara nikachukue boda boda, kumbe huku nyuma askari wakapita lipo, wakapita tena lipo ikabidi watanaze times ambaye katelekeza gari akalichukue mimi sikuwa na habari. Narudi baadae kulichukua nikiwa na fundi, gari silioni, namuuliza muuza matunda ndiye akaniambia wamelibeba wamelipeleka kituo cha polisi cha kawe. Kesho yake naenda kawe mkuu wa kituo akawa ananizngua kuwa nikamtafute mwenye gari, mpaka nilipofungua nikamwonyesha kitambulisho na kadi ya gari majina yana match. Aliniambia tu niwalipe waliolivuta nisepe tu.
Yani mimi nina mwili mdogo kama wa Mrehemu Ruge Mtahaba, nakutana ma mazarau sana maana hata nikivaa suti haikai ni kama imetundikwa tu.
Eheee kumbe na mimi najulikana!! Sasa mamaaa na mimi naomba nikujue hapa hapa, kama unaogopa raia njoo ndani ya sanduku!!!Wee nakujua jamanii
Kwanini?Mkuu usingemalizia kwa kusema una mwili mdogo,ningekwambia mimi.
watu wenye miili midogo na wembamba hudharaulika sanaKwanini?
Hatari sanawatu wenye miili midogo na wembamba hudharaulika sana
hasa ukute una kamwili kadogo halafu kuvaa kukupitie kushoto.
Angalau wewe hata visa vyako vina muelekeo hubabaikiBinafsi nina visa vingi nimewahi kumbana navyo vya kuchukuliwa powa. Hapa nitataja vinne tu.
1.Nakumbuka nilihamia sehemu fulani ofisi flani mahali fulani.
Kwa vile nilikuwa mgeni sikuhama na kitu chochote zaidi ya mi mwenyewe.
Basi nikawa na tabia ya kwenda kula kwa mama ntilie ugali wa buku japo pale jirani kulikuwako na mgahawa mmoja wa kiwango cha juu kwa ajili ya watu wa tabaka la juu .
Wateja wenzangu wengi wao walikuwa bodaboda na machinga. Yule mama ntilie pamoja na wasaidizi wake walikuwa wababe na kauli mbaya kwa wateja wao, kiujumla kwao mteja alikuwa sio mfalme bali lofa.
Jioni moja nikaomba niongezewe mboga kidogo ili nimalizie ugali wangu lakini nilijibiwa kwa jibu la dharau sana mpaka wateja wenzangu wakanicheka.
Tangu siku hiyo nikahamia kwenye mgahawa wa wadosi nikawa nakatiza kwa mamantilie naingia mgahawa wa kishua. Yule dada akawa anapatwa na mshangao kama haamini kama ninauwezo wakula kule.
Lakini pia akaanza kuniona na kampani za watu fulani ambao wanafahamika na ni maarufu eneo lile. Tangu kipindi hicho akawa anajichekesha chekesha kwangu maana alisha fahamu nafasi yangu ndani ya jamii yao ila nashukuru sikuwahi kumshobokea hata kwa salamu.
2 Nikiwa ofisini, kwa vile nilikuwa mgeni, siku moja aliingia mteja ofisini akanikuta nimekaa kwenye meza yenye ya wageni, nilifanya hivyo ili kujipatia mazingira ya urelax kwa assigment niliyokuwa nafanya kwa muda ule. Ili kufanikisha hilo kiti changu na meza yake ninavyotumia kufanyia kazi vilibaki wazi hivyo ikawa kana kwamba mi ni mgeni na boss hayupo maana kiti hakina mtu.
Mara nikaona jamaa amefungua mlango ghafla nakuanza kuuliza bila hata kusalimia. Jamaa akawa ananiuliza huku akinyosha kudole kwenye kiti cha boss " jamaa yuko wapi" nikamjibu "katoka kidogo" Mara nikaona PS anaingia ofisini na kuniuliza "huyu mgeni hajakuona kwani mbona kasema hakuna mtu"? Nikamjibu mwambie aingie.
Basi yule jamaa akaingia ila hakuwa na confudence tena maana alishavurugika kisaikolojia japo nilijitahidi kumjenga kisaikolojia na kumuhuumia vizuri.
3.Siku ingine nafika ofisini nakuta wamama wawili wamekaa kwenye benchi wanamsubiri mwenye ofisi, nikasimama na kawasalima vizuri kwa utulivu, mmoja kajibu kwa kujilazimisha kwa kubetua mdomo yaani ni kama wananishit wanaona nawapotezea muda maana wanamsubiri boss wamweleze kilio chao. Basi nikaingia ofisini kidogo kama dk 3 kisha nikatoka nnje mara nikasikia PS anawambie " nyie mbona hamwingii?, anaondoka huyo! Mara nasikia kwa nyuma watu wananikimbilia huku wanaita kwa sauti za unyonge" baba samahani tunashida na wee! Nikasimama na kuwaomba twende ofisini tuongee. Niliwahudumia vizuri japo walisha potewa na confidence maana nafsi ziliwasuta maana waliuchukulia poa mwonekano na umri wangu nadhani.
3. Juzi kati nilipanda basi kuelekea mkoa fulani. Kwa vile nilipandia njiani nikapata siti jirani na dada wa makamo bonge. Nikamsalimia vizuri ila hakuitikia kwa kutoa sauti bali akatikisa kichwa tu . Baada ya mwendo wa safari ndefu, nadhani mdada alinisoma na kugundua alini underate kwa makosa. Basi akaanza kujitahidi kuniongelesha mara ooooh, "samahani kaka eti hapa ndo wapi," ooooh, "kaka hivi we ni mwenyeji ............"(anataja jina la mji tunaoelekea) Sikumshobokea , nami nikawa namjibu kwa kutikisa kichwa tu huku niko bize na simu yangu.
4.Juzi nimehudhuria harusi ya jamaa yangu. Nilikuwa peke yangu kwa vile wife alikuwa na udhuru.
Basi nikaelekezwa kwenye meza moja ambayo tayari ilikuwa na wenza wawili (umri kati ya 30 na 35) Basi nikawasalimia kwa sauti huku nikivuta kiti na mie nikae. Yule mdada aliitikia lakini mwanaume hakuitikia.
Ukaja muda wa kugobganisha glasi kila mtu na jirani yake , kwa vile nilikuwa sina mtu mingine zaidi yao nikagonganisha nao glasi lakini naona yule mkaka kama hataki . Ok, shughuli ikaendelea naona jamaa yuko bize na kushikana shikana na mpenzi wake nami niko bize na simu yangu.
Tumekula chakula tumemaliza mi sikuwa na haraka ya kuondoka ukumbini maana nilikuwa bado namalizia kinywaji changu. Basi baada ya kumaliza kula naona msela ananyanyuka anamvuta demu anamwambia "twende zetu acha hiyo" demu akaiacha redbull ambayo ndio kwanza ameifungua. Kwa vile tulikuwa mimi na wao pale mezani nilitarajia angalau " broh sie ngoja tutangulie"!
Bada ya kama dk 15 namimi nikatoka ukumbini ili nirudi home maana ilikuwa yapata saa 7 za usiku. Nafika karibu na parking, nawakuta wale mtu na demu wake bado wapo kumbe wanasubiri bodaboda huku wakipata adhabu ya kipupwe cha usiku . Nikawapita kwa karibu, nikaingia kwenye usafiri wangu nikawasogelea nikashusha kioo kidogo na kuwaaga "jamani mi natangulia, naona nyie bado mpo". Sijui kama walijibu ama la ila nilichogundua niliona msela amekosa confidence na amekuwa mnyonge saana.
Yawezekana kuwa na madhaifu ya kibinadamu ila kujisocialize na watu bila kujali hadhi zao ni faida kwako kuliko hasara.
[emoji1787][emoji1787][emoji28][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]nmemwona,naona anajifariji labda akiamka itakua kweli
Ndo yy huyu shostKumbe ni YEYE[emoji1781][emoji1781][emoji1781]
@Sivan kamu hia[emoji1787][emoji28][emoji28]Madeni yako ulilipa?