Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Umenikumbusha mbali sana!

Father yangu anapenda sana swala la undugu, yeye mtu wa mbali kabisa atakuambia 'kamtafute huyo ndugu yetu kabisa'.

Wakati nimepangiwa kazi mkoa fulani, kuna ndugu yake father alikuwa Meneja wa litaasisi likubwa sana(kafariki now). Father akapiga kelele sana mtafute huyo mtu ni ndugu yetu kabisa usikae kipweke. Akawasiliana nae kabisaa kumwambia uwepo wangu huko. Akamjibu poa.

Siku, nimetoroka ofisini fresh nikaenda ofisi yao fasta ili sasa kumsalimia na kutambuana, kufika getini nikajitambulisha kama mgeni wa nani kwa walinzi.

Akapigiwa simu (extension) kutoka getini kutaarifiwa ujio wangu, yaan namsikia kabisa anahoji ni nani huyo akaambiwa kila kitu ila mwisho wa siku akawaambia walinzi mwambieni sipo na msimruhusu kuingia.

Angewaambia kwamba mwambieni nipo busy, ningemuelewa ningemtafuta siku ingine ila kitendo cha kusema eti mwambieni sipo! Nilikata mguu na sikutaka hata kumjua tena, father alipiga kelele sana wala sikuhangaika tena.

Hamadi! Kuna mkulu mmoja alikuja kwa ziara ya taasisi yetu na kwenye majumuisho akaomba wakuu wa taasisi zote za umma na binafsi pale mkoani waalikwe! Ilikuwa inaanza saa moja jioni.

Kwenye utambulisho tulianza sisi, tuliokaa high table jirani na mkulu tena MC anakutaja we unapungia. Wao waalikwa wakajitambulisha wenyewe, unapewa mic unajitaja unatokea taasisi gani na cheo chako. Coz namjua jina nipolisikia jina lake tu nikawa makini kumuangalia maana sikuwahi kumuona physically.

Kumbe naye aliponisikia akawa makini kuniangalia.

Kwenye coctail party anajileta leta kinoma halafu anashangaa sana na kuniuliza, kumbe we ndo mtoto wa fulani?! Mi namjibu vyema kabisa na hakuficha mshangao wake.

Baada ya siku ile alinitafuta yeye, tukawa na undugu imara! Alianza yeye kuja home ndo nami nikaenda kwake.

Moyoni nikajua alinikwepa awali akijua kinachofuata ni kuombana misaada akidhani ndiyo naanza maisha!
Du[emoji26]
 
Heshimu yeyote bila kujali umemkutaje. Vingine havipo kama unavyoviona/kufikiria.
Dada zetu wanachemka sana hapa.
Mkuu kuna wanawake hawaonagi mbele, wanafikiri situation ya mtu kuwa hohehahe ni permanent.....ikibadilika wanashangaa......Kuna mwanamke alinikataa katakata nikiwa chuo katakata yaani asee acha tu.......last year nilikuwa na chat nae ananiambia ananipenda namwambia mimi nishaoa anasema hivyo hivyo anataka awe side chick......she is pretty ana kazi yake na maisha yake.....lakini sahivi age ishatembea hakuna mdau anatangaza nia, halafu kazi yake ni porini hamna wadau hata wakumuona.....nadhani anataka anitegeshee mimba......
 
Mkuu kuna wanawake hawaonagi mbele, wanafikiri situation ya mtu kuwa hohehahe ni permanent.....ikibadilika wanashangaa......Kuna mwanamke alinikataa katakata nikiwa chuo katakata yaani asee acha tu.......last year nilikuwa na chat nae ananiambia ananipenda namwambia mimi nishaoa anasema hivyo hivyo anataka awe side chick......she is pretty ana kazi yake na maisha yake.....lakini sahivi age ishatembea hakuna mdau anatangaza nia, halafu kazi yake ni porini hamna wadau hata wakumuona.....nadhani anataka anitegeshee mimba......
Hahahahaha

Sent from my SM-N910W8 using JamiiForums mobile app
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiiiiiiiiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale obey waniambie Wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
Ulitisha mkuu
 
Mkuu kuna wanawake hawaonagi mbele, wanafikiri situation ya mtu kuwa hohehahe ni permanent.....ikibadilika wanashangaa......Kuna mwanamke alinikataa katakata nikiwa chuo katakata yaani asee acha tu.......last year nilikuwa na chat nae ananiambia ananipenda namwambia mimi nishaoa anasema hivyo hivyo anataka awe side chick......she is pretty ana kazi yake na maisha yake.....lakini sahivi age ishatembea hakuna mdau anatangaza nia, halafu kazi yake ni porini hamna wadau hata wakumuona.....nadhani anataka anitegeshee mimba......
Nipe namba zake plz
 
Huyo katibu mkuu nae atakuwa siyo mstaarabu tu. Kusalimia watu kwake ni shida? Ni mmoja wa wale waliolewa madaraka.
Lakini salamu sio lazima mkuu. Maana hata ukimsalim mtu akakujibu hayuko salama utamsaidiaje mkuu?
 
Kuna mpangaji mwenzangu tulikuwa tunaishi vzri sana ila sasa ni muongo mnafiki sana akawa anatangaza kwamba mimi na wife tuna maisha magumu tuna lala chini Mungu mme wake anajua kutafta pesa niliumia mwzi wa 8 mme wake amefumaniwa akapigwa mpka kufa mwanamke alikuwa haongeagi na majirani baada ya kupata taarifa za mme wake kuawa akaanza kuomba msamaha
 
Umenikumbusha mbali sana!

Father yangu anapenda sana swala la undugu, yeye mtu wa mbali kabisa atakuambia 'kamtafute huyo ndugu yetu kabisa'.

Wakati nimepangiwa kazi mkoa fulani, kuna ndugu yake father alikuwa Meneja wa litaasisi likubwa sana(kafariki now). Father akapiga kelele sana mtafute huyo mtu ni ndugu yetu kabisa usikae kipweke. Akawasiliana nae kabisaa kumwambia uwepo wangu huko. Akamjibu poa.

Siku, nimetoroka ofisini fresh nikaenda ofisi yao fasta ili sasa kumsalimia na kutambuana, kufika getini nikajitambulisha kama mgeni wa nani kwa walinzi.

Akapigiwa simu (extension) kutoka getini kutaarifiwa ujio wangu, yaan namsikia kabisa anahoji ni nani huyo akaambiwa kila kitu ila mwisho wa siku akawaambia walinzi mwambieni sipo na msimruhusu kuingia.

Angewaambia kwamba mwambieni nipo busy, ningemuelewa ningemtafuta siku ingine ila kitendo cha kusema eti mwambieni sipo! Nilikata mguu na sikutaka hata kumjua tena, father alipiga kelele sana wala sikuhangaika tena.

Hamadi! Kuna mkulu mmoja alikuja kwa ziara ya taasisi yetu na kwenye majumuisho akaomba wakuu wa taasisi zote za umma na binafsi pale mkoani waalikwe! Ilikuwa inaanza saa moja jioni.

Kwenye utambulisho tulianza sisi, tuliokaa high table jirani na mkulu tena MC anakutaja we unapungia. Wao waalikwa wakajitambulisha wenyewe, unapewa mic unajitaja unatokea taasisi gani na cheo chako. Coz namjua jina nipolisikia jina lake tu nikawa makini kumuangalia maana sikuwahi kumuona physically.

Kumbe naye aliponisikia akawa makini kuniangalia.

Kwenye coctail party anajileta leta kinoma halafu anashangaa sana na kuniuliza, kumbe we ndo mtoto wa fulani?! Mi namjibu vyema kabisa na hakuficha mshangao wake.

Baada ya siku ile alinitafuta yeye, tukawa na undugu imara! Alianza yeye kuja home ndo nami nikaenda kwake.

Moyoni nikajua alinikwepa awali akijua kinachofuata ni kuombana misaada akidhani ndiyo naanza maisha!
Imeniuma sana hii...inafanana kabisa na mimi
 
Mi kuna mwaka flani nilipewa promotion kwenda kuwa branch manager mkoa flani. Sasa sabab nilikua bachelor nikauza vitu vyote nikabaki na mabegi ya nguo nikapaki kwenye ndinga nikaamsha. Nikafika mkoani mida ya sa 9 na mafuta yalikua yamekaribia kuisha nikasema nikachomoe mpunga kwenye atm ya hiyo bank ninayofanyia kazi. Nilivomaliza kutoa hela na muda wa bank bado nikasema niingie kumsalimia branch manager aliyepo maana tulikua tunafahamiana. Ile kuingia reception mdada mmoja matata sana ndo yupo pale na pembeni kaka jamaa mwingine..nikamsalimia akaitika vizuri tu,nikamwambia naomba kuonana na meneja..akainua macho kuniangalia...akanambia sema shida yako...nikamwambia shida yangu ni personal,akasema huwezi kumuona ..tena kwa madharau. Na yule jamaa wa pembeni akaniangalia akaendelea na ishu zake.Nikamwambia basi sawa ntampigia simu,akanijibu kwa kejeli kumbe namba yake unayo...yule jamaa wa pembeni akacheka..nikasepa nikaenda kuchkua hotel. Jion nikamcall meneja nikamwambia nipo nishafika akafurahi sana maana kama nilimsurprise na skumwambia kama nilifika ofisin. Jioni akanitafuta tukapiga vyombo huku akinionesha machimbo. Kesho yake asubuhi kwenye morning talk akawaambia staff meneja mpya kashafika atakuja mchana kuwasalimia. Mchana wake nikaibuka... Hahahahaaaa basi wapenzi wasikilizaji mtamalizia wenyewe kilichofuata.

Kisa cha pili ni sehem nilipoenda kupanga room maana sikua na familia na vitu niliuza so nikazama kama ninja...wakawa na madharau yao mi sina time nao mpaka wamekuja kujua badae sana ndo wanajichekesha maana hata gari nilikua silazi pale hapakua na parking.
Ulitisha mkuu
 
Niliwahi kwenda ofisi fulani (kampuni ya simu) kwa ajili ya kuonana na mtu wa marketing kuna mradi ofisi yetu ilikua inafanya nao.
Sikua na appointment kwa makusudi ili nijionee wanavyohudumia wateja maana mradi ulikua unahusisha kutoa huduma kwa wateja ambao ba sisi wanatuhusu.
Nilifika na kukaa zaidi ya dakika 10 bila kua attended af si mnajua kuna maofisi Mlinzi anamamlaka utasema meneja anavyoamrisha [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]. I was very patient na observe tu. Meneja alikua na ka meza kake kwenye kona....I walked to him nikamsalimia "Habari kaka"....hakuhangaika wala kujibu salamu akauliza "Una shida gani???" Nikamsahihisha nikamuambia "Sio kila anaekuja ana-shida ungeniambia karibu ni kuhudumie kisha mimi ndio ningesema kama nina shida ama nahitaji huduma nyingine"....kabla hajapata nafasi ya kujibu nikajitambulisha.
Natamani kuchora picha uso wake ulivyotahayari ila itoshe kusema aliona aibu [emoji1].
 
Mwaka 2012 wakati nipo kituo cha Tembon - Mbezi wingu la mvua likatanda ghafla kwa sababu nilkuwa naelekea maduka tisa ikabidi nikodishe bajaji fasta ili hata mvua ikinyesha kabla sijafika nisilowe basi bhana wakati naita bajaji kwa pembeni mbali kidogo na nilipo alisimama manzi fulani hivyo baada ya kuelewana na bajaji nikapanda nashangaa haondoki kumbe anasubria manzi apande anajua niko naye hadi nikamwambia mbona unazubaa au unataka mvua inikute hapa wala hakusema kitu akawasha chombo tukasepa wakati tupo njian ndo ananiambia ninaonekana ni mtu wa totoz hivyo alijua yule niko nae, nikwambia ndo maana umenipga parefu unajua nipo na demu siwezi kuchomoa yaan muda wote alibaki kunishangaa kwamba kumbe mi mstaarabu kuliko alivyonidhania mtu wa totozi
 
Mkuu kuna wanawake hawaonagi mbele, wanafikiri situation ya mtu kuwa hohehahe ni permanent.....ikibadilika wanashangaa......Kuna mwanamke alinikataa katakata nikiwa chuo katakata yaani asee acha tu.......last year nilikuwa na chat nae ananiambia ananipenda namwambia mimi nishaoa anasema hivyo hivyo anataka awe side chick......she is pretty ana kazi yake na maisha yake.....lakini sahivi age ishatembea hakuna mdau anatangaza nia, halafu kazi yake ni porini hamna wadau hata wakumuona.....nadhani anataka anitegeshee mimba......

Huo mstari wa mwisho umebeba kila kitu. Nimemuonea huruma japo simjui. Maisha yanabadilika mno dah
 
Uzi mzuri huu.unafundisha sana
Mnoooo.... kwa miaka yangu kadhaa ya kuishi nimeona mambo ya kutosha kunifunza kuto dharau/ kushusha thamani mtu.
Asubuhi napo ingia mzigoni sina kale katabia kakupita mlinzi au mfagizi kama sio mtu; nasalimia na kuulizia hali ya familia kisha naendelea na siku yangu. Dereva , mhudumu wa chakula wote nawapa heshima inayostahili.
Nishawahi ingia kwenye mgahawa nikamsalimia mdada vizuri tu na kumtania kirafiki kisha nikaagiza...Huwezi amini aliniambia hicho usile sio fresh bora ule chakula flani ni fresh na kimepikwa vizuri. Ningeingia kwa nyodo na dharau ningejulia wapi hayo [emoji3]
 
Back
Top Bottom