Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Kuna siku walikuja wapima ardhi eneo ninalo ishi,wakanikuta nafua nipo kama house girl.
Katika mahojiano wakawa wanahitaji majina ya mwenye nyumba nikawatajia jina la kike ambalo ni langu.
Wakasema kwa kupanik kabisa tunatak jina la mwenye nyumba nikawajibu ndio hilo.Wakahitaji jina langu nikawapa wakaona ni jina hilo hilo,waliondoka hawaamini mpaka kesho.
 
Ungevunga baada ya kutambuana. Ungechukua point tatu vyema, kabisa. Badala ashoboke yeye ukashoboka tena kwa mara ya pili.

Kwanza anamuonea bure tu Dada wa watu, unainuka kumfuata mtu usiyemfaham kumuomba ujumuike nae akikataa unasema amekuchukulia poa???
 
mimi binafsi nachukuliwa poa sana na naendelea kuchukuliwa poa kwasababu sina mwendelezo chanya ( sina maendeleo) ila naamini wanaonichukulia poa ipo siku watajuta na kusutwa na nafsi zao juu yangu as long as bado kijana na nina ndoto na mipango kedekede yakitimia watainamisha vichwa vyao chini


ngoja nimwage hiki kisa nilichosimuliwa na mwalimu wangu. huyu ticha wangu alienda kariakoo kama sio posta kwenye maduka ya kuuza vifaa vya kielektroniki maana laptop yake ilikua na shida akahitaji kifaa flani kama spear. sasa wakati anaelekea kuingia kwenye mojawapo ya duka kubwa mlinzi akamchukulia poa kwa mwonekano wake( ticha ni mfupi, mweusi, ana mwili mdogo na ana ulemavu wa mkono mmoja sijawahi juaga chanzo cha ulemavu wake) kwa ukali mlinzi akawa anamhoji


mlinzi; weweee simama hapo, UNAKWENDA WAPI?

ticha; kwani huku watu wanakwenda wapi?

mlinzi; UNAKWENDA KUFANYA NINI HUKO?

ticha; kwani huku watu wanakwenda kufanya nini?

mlinzi; Unarudisha maswali kwangu hebu nipatie kitambulisho chako


ticha akazama kwenye begi akamtolea Id kucheki ni mwalimu wa shule ya sekondari mojawapo wilaya ya temeke. mlinzi akabaki ameduwaa nadhani alijua atakua ni ombaomba wale wa jiji maana ticha hakua smart hata kidogo.ticha kuzama ndani akamkuta mzungu sijui mhindi dukani kwa kuua kabisa mwalimu akaeleza shida yake ya kifaa anachohitaji kwa lugha ya malkia kwa ufasaha kabisa maana hiyo lugha yeye ndo mwalimu hilo somo, mlinzi akachoka. hakufanikiwa kupata alichokitafuta ila kwa lugha ya kibiashara yule mhindi akamuambia mzigo umeisha ila mpaka next week mzigo utakua umefika.



nadhani huyo mlinzi licha ya aibu zake alipata funzo kubwa kuliko sisi.



huyu ticha ni memba mkongwe huku jf na tukiwa shule alituambiaga mtandao wa kuongeza maarifa ni jamii forum sio ile ya ajabuajabu. nimekumis sana mwalimu mwaka juzi nilionana nae kwa mara ya mwisho nikamwambia saivi na mi ni mwanajf akaniambia 'kuwa makini bhana usije ukawa unabishana na mwalimu huko jf'



nakutakia kheri na uzima tele mwalimu wangu nakukumbuka sana
Asante Sana kijana,yule mlinzi hakujua kua nilikua Nina uwezo wa kumfanya house boy nyumbani kwangu
 
Nakumbuka nilikua nimeenda ku report kazini mara ya kwanza. Askari wakanifanyia ukaguzi na kufuata taratibu zote za kiusalama kuruhusiwa kuingia kwenye jengo.

Nilikua na bag nikaliacha pale kwao, ikaja kuniuliza majina yangu, nikataja la kwanza, wakatizamana, akauliza la pili, nikataja akatabasam, akaniuliza la tatu nilivyotaja akamtizama mwenzake akacheka sana. Na kuonyesha hali ya kuwa tuko mrengo tofauti wa kiimani na wao. Nakumbuka nililazimisha tabasam na kutokusema kitu nikapanda juu ofisini.

Baada ya muda kama masaa matatu hivi nikapitishwa kutambulishwa ofisi zote baadae tukamalizia kwa wale ma askari...walihofu sana lakini sikuwahi kuwaonyesha kinyongo chochote licha ya kuwa na hofu mara kwa mara kwamba ningewafanyia kitu..kuna siku nikaona niwatoe wasiwasi kwamba yaliyotokea yalishapita ila siku ingine wasimfanyie hivyo mtu mwingine. Ikaishia hapo.
 
dah na mim umenifanya nilete kisa changu ambacho hakina hata miezi miwili.
kuna mdada jina yupo katika ofisi fulani ni majirani zetu(home).Ni wale watu wanaoringa kupita kiasi ukimsalimia kama hakuoni vile( hii ishatokea kama mara 3) last time niko zangu na town anafanya kazi pale benjamin mkapa,nmemkuta yupo na wenzake wakati huo nilikuwa niko na kaka yangu mkubwa.

Nikamchangamkia ila mwenzangu kanilia buyu namtambulisha kwa bro kuwa huyu ndo jirani dah mixer mfyonyo juu hakuna siku roho ilikuwa inaniuma kama siku siyo.

sasa week kama 3 nyuma natokea moro nmeingia kama saa 6 hivi nikasema ngoja sku ya leo nikasalie pale upanga maamur ni mskiti ambao waislamu wengi sana wanapenda kuosha maiti pale na kwenda kuzikia makaburi ya kisutu.

Nilivyofika pale pakawa kama na stori za chini kwa chini kuwa muosha maiti amekimbia baada ya kuosha maiti zaidi ya tano kitu ambacho syo cha kawaida, basi kwenye maongezi maongezi ikajulikana kuwa kuna maiti kama 2 zimeshndwa kuoshwa ndugu hawajui na muoshaji kakimbia(hofu ya corona)

Basi tukajitokeza mimi na mwenzangu tukaingia chumba cha maiti tulikuwa kama wa 4,tukaiosha ile ya kwanza,then tukafata ile ya pili zote tukaandaa safi kabisa ila ile ya pili niligundua alikuwa na baba wa yule dada maringo.

wakati tunatoka kuosha ndugu wakatuvuta pembeni wakatupa kama laki 3,wenzangu walichukua ila mimi sikuchukua hata cent sasa kumbe aliyekuwa anatoa hela ni mdogo wa yule(dada maringo) ambae anaishi nairobi kaja kumzika mzee wake but hanijui.

basi tukachukua maiti tukaenda zetu kuzika makaburi ya kisutu, wakati narudi zangu maeneo ya home ndo nakuta msiba sasa huku zogo pembeni likiwa ni muosha maiti kukimbi, basi jamaa akaniona mdogo mtu tukasalimiana pale ile furaha aliyokuwa nayo akanishika mkono mpaka uwani ambako kulikuwa na dada zake na mjane akanitambulisha na jinsi nilivyowasaidia dada mtu(cha maringo) aliangua kilio kupita maeleozo akaniomba namba nkampa.

baada ya kama dakika 30 baada ya kurudi home nikatumiwa mesage kama gazeti ya kuniomba radhi/msamaha mie nka act humble tu japo kila siku anataka tuonane but kila akinipigia namwambia niko moro japo anafosi anitumie hata nauli nikaonane nae au aje yeye but namchomolea.

katika maisha usimdharau mtu kwani huwezi jua nani atakaekufaa kwani unaweza kuwa trilionea but msaada wako ukatoka kwa mwenye kupata sh 500 kwa siku
umefikia hatua nzuri ya kula kimasihara
 
Tokea hii itokee zimepita Kama wiki tatu hivi....

Baada ya kumaliza chuo huku ajira zikiwa ni ndoto za Abunawasi Kama sio Alinacha, mzee wangu aliamua kunipiga tafu ili tusije kulaumiana huko mbele. Alifumba macho akavunja kibubu akanunua trekta jipya "Massey Ferguson 275" likiwa na tela pamoja na majembe yake halafu akanikabidhi funguo na kadi na kuniambia Kama ninataka mali nitazipata shambani.

Katika kusubiri msimu wa kwenda kuzitafuta mali shambani nikaamua kulipeleka trekta kijijini kwetu maana sio mbali ili niwe nawabebea watu mizigo. maisha ni kujiongeza shekhe! Alhamdulillah, kazi inaenda vizuri hasa ukizingatia suka mimi mwenyewe! Sometimes hata mshua mwenyewe akishirikiana na mama huwa wananipiga mzinga, nawatoa kiroho safi. Kimsingi hata zile text za "Baby nikuambie kitu" siziogopi huwa nazijibu pasina shida yoyote!

Last week nilipata dili la kubeba tofali. Wakati wapakiaji wanaendelea na kazi ghafla Kuna jamaa alikuja pale site akiwa na mwanamke! Walikuwa wamependeza wenyewe, wanawaka hatari na jua lile la utosi wananukia marashi tu. Mikogo yao ilitosha kuonyesha wapo kwenye lindi la huba na mahaba yasiyoelezeka.

Wakafika pale huku wanajipukuta vumbi kwa leso, site hapataki utanashati. Basi jamaa akalitazama trekta Kama traffic anayetafuta kosa, halafu bila hata salamu japo sio lazima akaniuliza linabeba gunia ngapi za mahindi, nikamtajia gunia 35. Akatikisa kichwa kuonyesha ni uwezo mdogo sana! Mbulumundu kabisa, wakati Kijiji kizima trekta langu ndio kubwa na linabeba kuliko wengine wote! Kwanza kijiji chote matrekta yapo matatu tu na langu ndio King of the empire! Nilimvumilia maana mteja sio fala ni mfalme.

Basi akajinyonganyonga pale, akajishingondoa paleee, akajimwemwesa kwa pozi za ashuo mbele ya demu wake halafu akauliza gharama za usafiri, nikamtajia. Akasema,

"Eeh... dogo mbona unapiga sana, bosi wako anajua lakini?" Achana kwanza na ishu za bosi, kwanini aniite dogo tena mbele ya demu wake hasa ukizingatia bei niliyomtajia ni very reasonable? Why? Why always me!

Mjinga aliniharibia siku, shubamiti! Akaongeza chumvi kwenye kidonda,

"Kama vipi nipe namba ya mwenye trekta niongee nae maana nyie madereva huwa mnazingua Sana!" Itoshe tu kusema yule jamaa aliondoka kwa dharau huku akisapotiwa na demu wake! Nilipoteza pambano na sikujisikia vizuri.

Wale wanaopakia tofali ndio wakaniambia kuwa jamaa na demu wake wote ni walimu wa shule ya msingi hapo kijijini. Wanavimba sababu wamesoma. Sasa nikashangaa wanalingia elimu au ajira? Diploma ya kumfanya mtu alinge kweli? Kama wanalinga kwa sababu ya ajira, je wangekuwa makatibu wa elimu wizarani ingekuaje? Just imagine jamaa ndio angekuwa Makonda, hapo mjini Daslam mngeishije? Basi siku ikaisha hivyo kinyonge!

Juzi kati mzee aliniambia nisiache ku apply nafasi za ualimu zilizotangazwa na serikali hata Kama uwezekano wa kupata ni 0.000. So siku hiyo sikwenda bush kwenye trekta nikabaki town ili nifanye application! Nikaenda internet cafe ili mambo yaende fasta!

Kama nusu saa hizi nikasikia sauti Kama naifahamu hivi, kugeuza shingo kumbe yule jamaa na demu wake wanaingia wakiwa na jamaa mwingine. Tukagongana macho, wakatoa macho Kama mjusi kapigwa spana! Hawakutarajia kuniona pale! Dereva wa trekta na macomputer wapi na wapi? nikawapotezea!

Kumbe wamekuja kumsaidia kufanya application yule jamaa ni mshkaji wao. Walikuwa hawajui vitu vingi na mhudumu wa pale cafe hakuwa na msaada kwao akawaambia waje kuniuliza Mimi maana kaniona nafanya application. Hawakuamini kabisa! Dereva wa trekta anafanya application? Kivipi yaani?

Ulikuwa mtihani mzito kwao, liliwashuka, sura zao zikasawijika, wakakosa pozi, wakacharara, waliishiwa kwa kweli ila watafanyaje? Wakaja huku wanajichekesha wakanisalimu kwa kunipa mkono bila ajizi na Mimi nikawapa mkono na tabasamu langu la uongo usiojificha mdomoni.

Wakashangaa Sana kuona ninabonyeza sehemu ya TCU badala ya NACTE. Wakaniuliza nimesoma chuo gani, usitake kujua niliwajibu Nini ila unajua tena sisi wa UDSM tunavyojionaga tumeyapatia maisha! Niliwajibu kwa kadri inavyopaswa!

Yule binti akasema, "sio mbaya lakini, umejishikiza kwenye kuendesha trekta" nikamuangalia usoni nikamwambia hapana Lile trekta ni langu nashindwa kumuajiri dereva maana wanakuwaga wasumbufu Sana! Nilihakikisha wanajua hadi kipato changu kuwa wakiunganisha mishahara yao wote Kama mambo yakikaa sawa Mimi naingiza ndani ya wiki mbili tu.

Jamaa mkosa adabu alikosa raha. Kwenye kiti palikuwa hapakaliki mbaya zaidi demu wake aliweza kwenda sawa na upepo ali connect na Mimi vizuri kabisa! Hadi namba ya simu alinipa ili wakiwa vizuri nikawabebee mahindi yao.

Sasa hapa Nina namba ya simu ya demu, tunachati tu WhatsApp kuhusu changamoto za Maisha na fursa za baadae. Ghafla nimekuwa motivation speaker wake! Ananichukulia Kama role model wake! Sijui Kama jamaa nimemsamehe au vipi acha niendelee kuchati na demu wake kwanza!
chati nae tuu na shetani akikupitia mkubalie apite tu 😀
 
Nakumbuka nilikua nimeenda ku report kazini mara ya kwanza. Askari wakanifanyia ukaguzi na kufuata taratibu zote za kiusalama kuruhusiwa kuingia kwenye jengo.

Nilikua na bag nikaliacha pale kwao, ikaja kuniuliza majina yangu, nikataja la kwanza, wakatizamana, akauliza la pili, nikataja akatabasam, akaniuliza la tatu nilivyotaja akamtizama mwenzake akacheka sana. Na kuonyesha hali ya kuwa tuko mrengo tofauti wa kiimani na wao. Nakumbuka nililazimisha tabasam na kutokusema kitu nikapanda juu ofisini.

Baada ya muda kama masaa matatu hivi nikapitishwa kutambulishwa ofisi zote baadae tukamalizia kwa wale ma askari...walihofu sana lakini sikuwahi kuwaonyesha kinyongo chochote licha ya kuwa na hofu mara kwa mara kwamba ningewafanyia kitu..kuna siku nikaona niwatoe wasiwasi kwamba yaliyotokea yalishapita ila siku ingine wasimfanyie hivyo mtu mwingine. Ikaishia hapo.
Why walikuwa wanacheka majina yako sasa???

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
Utakuwa ni mtu wa ajabu sana muonekano wako. Hebu tutumie picha tukuone.

Enzi zetu magenius wengi ndio walikuwa wachafu wachafu wa kutokuoga, kufua na kupiga mswaki.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
nilikua napata tabu sana kuelekezwa na magenius maana midomo yao ilikua inanuka mno
 
Baada ya kumaliza Chuo mtaani kukawa na matukio ya wizi na uvamizi. Basi nikqja na idea ya kuanzisha ulinzi shirikishi. Wananchi wakasapoti nika organise vijana tukawa tunapiga kazi, mwisho wa mwezi nawa cash vijana laki na 20 kila mmoja maisha yanaenda.. Kuna Bi mkubwa mmoja anapita beria na kagari kabaya baya ila tunamsalimu na kumkirimu vyema tu. Siku moja akaniambia juma mosi uje kwangu nilipopanga pale. Tukaongea kidogo akataka kujua elimu yangu basi akaniambia kesho niende offisini kwake.. Akani business card.. Maza kumbe ni Naibu Msajiri wa High Court.. Akanioa connection moja kali na Mungu ambariki.
 
Kweli kabisa usimdharau mtu usiye mjua.

Hata mm imenitokea hiyo kuna Mkaka mmoja mtaan kwetu ukweli sikuwahi kumuelewa kabisa. Kwanza nilikuwa namuona kama hajatimia kuitwa wa kiume kwa njisi tu alivyo alivyo. Hata salamu tulikuwa hatuna.

Kuna siku moja nilikuwa nimekaa nje kwetu na shoga angu akapita huyu kaka. Nikajikuta namwambia best yng "yaani katika watu nisiowaelewa hapa duniani huyu kaka wa kwanza. " akaniuliza kwa nini, nikamwambia basi tu simuelewi katika kila kitu.

Zikapita siku za kutosha. Siku moja nimetoka zangu mishe najiandaa kuingia bafuni mara shoga angu huyoo ananiita. Nikamwambia nisubiri ndani nakuja. Niliporudi ile naingia tu kuniona akaanza kucheka hatari. namuuliza wacheka nini wewe. akajibu yule kaka usiyemuelewa hapa duniani kanipa zawadi hii nikuletee. Anaomba kukutana na ww. Looh nikamwambia muongo ww naanzaje kwenda kumsikiliza na kwa nn umepokea zawadi hii ikiwa unajua kila kitu. akasema ndio hivyo nenda ukamsikilize uku anacheka hatari.

Kweli sikwenda siku hiyo. Ilipita kama wiki mbili hivi akuacha kunitumia zawadi. Ile kitu ikanifanya niwe namfikiria sana. Nikampa nafasi nikaenda kumsikiliza. Akamwaga sera zake pale nikazipokea taratibu nikaanza nikazifanyia kazi. Nakumbuka kauli yake ya kwanza alisema "Nakupenda, sitaki kujua kuhusu mahusiano yako uliyonayo ingawa ninchojua mm hujaolewa, so nipe nafasi alafu utachagua ww yupi anakufaa." Hakuwa na mengi

Looh mpaka leo siamini nimezama mwenzenu. Alivyo kwa nje na ndani tofauti kabisa. Na sasa ndoa imetangazwa.
Kweli usimdharau mtu usiye mjua
kwahiyo unaolewa kimasikhara 😀
 
Baada ya kumaliza Chuo mtaani kukawa na matukio ya wizi na uvamizi. Basi nikqja na idea ya kuanzisha ulinzi shirikishi. Wananchi wakasapoti nika organise vijana tukawa tunapiga kazi, mwisho wa mwezi nawa cash vijana laki na 20 kila mmoja maisha yanaenda.. Kuna Bi mkubwa mmoja anapita beria na kagari kabaya baya ila tunamsalimu na kumkirimu vyema tu. Siku moja akaniambia juma mosi uje kwangu nilipopanga pale. Tukaongea kidogo akataka kujua elimu yangu basi akaniambia kesho niende offisini kwake.. Akani business card.. Maza kumbe ni Naibu Msajiri wa High Court.. Akanioa connection moja kali na Mungu ambariki.
Mkuu tutaanzisha uzi wa kuolewa kimasihara utupe kisa kamili
 
dah na mim umenifanya nilete kisa changu ambacho hakina hata miezi miwili.
kuna mdada jina yupo katika ofisi fulani ni majirani zetu(home).Ni wale watu wanaoringa kupita kiasi ukimsalimia kama hakuoni vile( hii ishatokea kama mara 3) last time niko zangu na town anafanya kazi pale benjamin mkapa,nmemkuta yupo na wenzake wakati huo nilikuwa niko na kaka yangu mkubwa.

Nikamchangamkia ila mwenzangu kanilia buyu namtambulisha kwa bro kuwa huyu ndo jirani dah mixer mfyonyo juu hakuna siku roho ilikuwa inaniuma kama siku siyo.

sasa week kama 3 nyuma natokea moro nmeingia kama saa 6 hivi nikasema ngoja sku ya leo nikasalie pale upanga maamur ni mskiti ambao waislamu wengi sana wanapenda kuosha maiti pale na kwenda kuzikia makaburi ya kisutu.

Nilivyofika pale pakawa kama na stori za chini kwa chini kuwa muosha maiti amekimbia baada ya kuosha maiti zaidi ya tano kitu ambacho syo cha kawaida, basi kwenye maongezi maongezi ikajulikana kuwa kuna maiti kama 2 zimeshndwa kuoshwa ndugu hawajui na muoshaji kakimbia(hofu ya corona)

Basi tukajitokeza mimi na mwenzangu tukaingia chumba cha maiti tulikuwa kama wa 4,tukaiosha ile ya kwanza,then tukafata ile ya pili zote tukaandaa safi kabisa ila ile ya pili niligundua alikuwa na baba wa yule dada maringo.

wakati tunatoka kuosha ndugu wakatuvuta pembeni wakatupa kama laki 3,wenzangu walichukua ila mimi sikuchukua hata cent sasa kumbe aliyekuwa anatoa hela ni mdogo wa yule(dada maringo) ambae anaishi nairobi kaja kumzika mzee wake but hanijui.

basi tukachukua maiti tukaenda zetu kuzika makaburi ya kisutu, wakati narudi zangu maeneo ya home ndo nakuta msiba sasa huku zogo pembeni likiwa ni muosha maiti kukimbi, basi jamaa akaniona mdogo mtu tukasalimiana pale ile furaha aliyokuwa nayo akanishika mkono mpaka uwani ambako kulikuwa na dada zake na mjane akanitambulisha na jinsi nilivyowasaidia dada mtu(cha maringo) aliangua kilio kupita maeleozo akaniomba namba nkampa.

baada ya kama dakika 30 baada ya kurudi home nikatumiwa mesage kama gazeti ya kuniomba radhi/msamaha mie nka act humble tu japo kila siku anataka tuonane but kila akinipigia namwambia niko moro japo anafosi anitumie hata nauli nikaonane nae au aje yeye but namchomolea.

katika maisha usimdharau mtu kwani huwezi jua nani atakaekufaa kwani unaweza kuwa trilionea but msaada wako ukatoka kwa mwenye kupata sh 500 kwa siku
Safi sana mwenyezmungu akuzidishie kheri inshaallah

Sent from my SM-A307FN using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom