Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

adi Oprah Winfrey ilishamkuta.. muuzaji alikataa kumuonesha pochi ya beii akamwambia hataweza kuiafford
Kuna mchezaji mmoja wa zamani wa Southampton anaitwa James Beatty alikuwa anataka kununua Porsche 911 akapita kwenye Porsche dealership moja mitaa ya London salesman akamwambia 'you can't afford this' (bei ilikuwa zaidi ya £100,000).
Jamaa akazunguka mitaa miwili mitatu akakuta Porsche dealership ingine akachukua gari kama ile akapita tena pale alipopita mwanzo akampa middle finger yule salesman akaishia. Hapo salesman kapoteza si chini ya £5000 commission.
 
Juzi juzi nilienda kumlipa Binti yangu ada kwenye shule fulani ya watoto wa kike kufika office ya Mhasibu nikamkuta mama flani namslimia akanishusha tu akaendelea na mambo yake. Nikamsalimia mara ya pili ndo akanijibu "nimeshakusikia" nikaamua kusubiri alipomaliza mambo yake ndo akaniita "haya unasemaje?" Nikamwambia nimekuja kumlipia ada ya Binti yangu anayesoma hapa
Akashtuka "ooh kumbe sikujua"
Nikatoa bank slip ya 3.5m ambayo ni ada ya mwaka mzima Pamoja na slip ya pili yenye laki 5 ya michango
Alipoona hivyo akaanza kujichekesha mpk akawaagiza wanafunzi wamwite Binti yangu amsalimie .
 
Umenikumbusha mbali sana!

Father yangu anapenda sana swala la undugu, yeye mtu wa mbali kabisa atakuambia 'kamtafute huyo ndugu yetu kabisa'.

Wakati nimepangiwa kazi mkoa fulani, kuna ndugu yake father alikuwa Meneja wa litaasisi likubwa sana(kafariki now). Father akapiga kelele sana mtafute huyo mtu ni ndugu yetu kabisa usikae kipweke. Akawasiliana nae kabisaa kumwambia uwepo wangu huko. Akamjibu poa.

Siku, nimetoroka ofisini fresh nikaenda ofisi yao fasta ili sasa kumsalimia na kutambuana, kufika getini nikajitambulisha kama mgeni wa nani kwa walinzi.

Akapigiwa simu (extension) kutoka getini kutaarifiwa ujio wangu, yaan namsikia kabisa anahoji ni nani huyo akaambiwa kila kitu ila mwisho wa siku akawaambia walinzi mwambieni sipo na msimruhusu kuingia.

Angewaambia kwamba mwambieni nipo busy, ningemuelewa ningemtafuta siku ingine ila kitendo cha kusema eti mwambieni sipo! Nilikata mguu na sikutaka hata kumjua tena, father alipiga kelele sana wala sikuhangaika tena.

Hamadi! Kuna mkulu mmoja alikuja kwa ziara ya taasisi yetu na kwenye majumuisho akaomba wakuu wa taasisi zote za umma na binafsi pale mkoani waalikwe! Ilikuwa inaanza saa moja jioni.

Kwenye utambulisho tulianza sisi, tuliokaa high table jirani na mkulu tena MC anakutaja we unapungia. Wao waalikwa wakajitambulisha wenyewe, unapewa mic unajitaja unatokea taasisi gani na cheo chako. Coz namjua jina nipolisikia jina lake tu nikawa makini kumuangalia maana sikuwahi kumuona physically.

Kumbe naye aliponisikia akawa makini kuniangalia.

Kwenye coctail party anajileta leta kinoma halafu anashangaa sana na kuniuliza, kumbe we ndo mtoto wa fulani?! Mi namjibu vyema kabisa na hakuficha mshangao wake.

Baada ya siku ile alinitafuta yeye, tukawa na undugu imara! Alianza yeye kuja home ndo nami nikaenda kwake.

Moyoni nikajua alinikwepa awali akijua kinachofuata ni kuombana misaada akidhani ndiyo naanza maisha!

Hii nimeipenda Mtu akijifanya keki mteme tu
 
It was a suprise kwangu.

Jirani yangu aliekuwa anajifanya ni boss wa Ikulu mtaani muda wote kanuna na miwani yake mieusi alikuja kunihudumia Chai Ofisini kwa Mama Salma Kikwete wakati wa WAMA, kumbe Alikuwa Office attendant pale tena wale wa oya oya na mie na wenzangu tulienda kupeleka project paper ya ki NGO chetu ambacho ni Hayati kwa sasa kuanzia 2015.
Kikubwa ni yupo ikulu
 
Nakumbuka nilikua nimeenda ku report kazini mara ya kwanza. Askari wakanifanyia ukaguzi na kufuata taratibu zote za kiusalama kuruhusiwa kuingia kwenye jengo.

Nilikua na bag nikaliacha pale kwao, ikaja kuniuliza majina yangu, nikataja la kwanza, wakatizamana, akauliza la pili, nikataja akatabasam, akaniuliza la tatu nilivyotaja akamtizama mwenzake akacheka sana. Na kuonyesha hali ya kuwa tuko mrengo tofauti wa kiimani na wao. Nakumbuka nililazimisha tabasam na kutokusema kitu nikapanda juu ofisini.

Baada ya muda kama masaa matatu hivi nikapitishwa kutambulishwa ofisi zote baadae tukamalizia kwa wale ma askari...walihofu sana lakini sikuwahi kuwaonyesha kinyongo chochote licha ya kuwa na hofu mara kwa mara kwamba ningewafanyia kitu..kuna siku nikaona niwatoe wasiwasi kwamba yaliyotokea yalishapita ila siku ingine wasimfanyie hivyo mtu mwingine. Ikaishia hapo.
Askari gani hao wa Suma au
 
Miaka fulani nilikuwa na likizo ndefu ya chuo basi nikaona nisikae bure nikafungua kamgahawa katikati ya mji. Nilikuwa nauza bites zote, juice fresh na matunda fresh.

Nilikuwa karibu na ofisi nyingi na banks. Basi nikawa napata oda ya kupeleka bites na maziwa asubuhi pamoja na matunda.

Dada mmoja staff wa pale CRBD aliweka oda ya matunda kila ikifika saa 6 mchana, ikawa siku nyingine ukipeleka anakwambia umechelewa nishakula kwingine, au leo sili basi narudi nayo. Au ukienda siku nyingine anakuangalia tuu hapokei matunda unabaki umesimama kama sanamu na matunda yako.

Siku moja nikaenda nikiwa na shida ya kufungua joint acc, kufika kwake hata sijamsalimia kanijibu leo sitaki matunda. Nikamwambia nina shida nyingine kabla sijaeleza akajibu tena "hapa tunasikiliza za kiofisi tuu hivyo ondoka". Sijui alijua nataka msaada wa hela au vipi.

Ikabidi niwe mpole maana alikuwa peke yake kwa muda ule customer service pale. Nikamweleza nahitaji fomu kufungua joint acc na mama yangu. Akachukua fomu akanipa akaniuliza "utaweza kusoma na kuzijaza kweli na mama yako??" Nikamjibu ndio. Akaniambia viambatanisho vinavyohitajika nikaondoka kesho nirudishe fomu.

Kesho yake nimeenda na mama, kufika pale akamkaribisha akakae kwenye kiti mimi akaniambia kasubiri pale yaani pembeni, ndio mama akamwambia nimekuja na binti yangu tunafungua joint acc, kwanza alistuka akamuuliza ni mwanao kumbe mama sikujua. Akaishiwa pozi.

Basi katika kupiga stori na bimkubwa akamwambia sikujua kama una binti mkubwa, bimkubwa akamwambia mara nyingi hayupo nyumbani kwasasa yupo likizo anasoma masters huko mkoa X. Alishangaa kwa nguvu Masters?? Aliniangalia sana. Miaka hiyo bimkubwa na mzee walikuwa wafanyabiashara wakubwa sana mkoani na chapaa zipo za kutosha wanajulikana kila kona. Bank pale walikuwa wanajulikana sana.
Enzi hizo bimkubwa na mzee CRDB wana zile VisaGold so wanahudumiwa kishua....kwahiyo dada akajua huyu sio kwamba anauza matunda kwa dhiki

Dada alikosa raha sana hadi muda anatoa copies akaniambia dada kakae kwenye kiti [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] toka siku hiyo alianza na kunisalimia na kunichangamkia. Mimi wala sikumwonyesha tofauti nikaendelea kumpelekea matunda.
 
Miaka fulani nilikuwa na likizo ndefu ya chuo basi nikaona nisikae bure nikafungua kamgahawa katikati ya mji. Nilikuwa nauza bites zote, juice fresh na matunda fresh.

Nilikuwa karibu na ofisi nyingi na banks. Basi nikawa napata oda ya kupeleka bites na maziwa asubuhi pamoja na matunda.

Dada mmoja staff wa pale CRBD aliweka oda ya matunda kila ikifika saa 6 mchana, ikawa siku nyingine ukipeleka anakwambia umechelewa nishakula kwingine, au leo sili basi narudi nayo. Au ukienda siku nyingine anakuangalia tuu hapokei matunda unabaki umesimama kama sanamu na matunda yako.

Siku moja nikaenda nikiwa na shida ya kufungua joint acc, kufika kwake hata sijamsalimia kanijibu leo sitaki matunda. Nikamwambia nina shida nyingine kabla sijaeleza akajibu tena "hapa tunasikiliza za kiofisi tuu hivyo ondoka". Sijui alijua nataka msaada wa hela au vipi.

Ikabidi niwe mpole maana alikuwa peke yake kwa muda ule customer service pale. Nikamweleza nahitaji fomu kufungua joint acc na mama yangu. Akachukua fomu akanipa akaniuliza "utaweza kusoma na kuzijaza kweli na mama yako??" Nikamjibu ndio. Akaniambia viambatanisho vinavyohitajika nikaondoka kesho nirudishe fomu.

Kesho yake nimeenda na mama, kufika pale akamkaribisha akakae kwenye kiti mimi akaniambia kasubiri pale yaani pembeni, ndio mama akamwambia nimekuja na binti yangu tunafungua joint acc, kwanza alistuka akamuuliza ni mwanao kumbe mama sikujua. Akaishiwa pozi.

Basi katika kupiga stori na bimkubwa akamwambia sikujua kama una binti mkubwa, bimkubwa akamwambia mara nyingi hayupo nyumbani kwasasa yupo likizo anasoma masters huko mkoa X. Alishangaa kwa nguvu Masters?? Aliniangalia sana. Miaka hiyo bimkubwa na mzee walikuwa wafanyabiashara wakubwa sana mkoani na chapaa zipo za kutosha wanajulikana kila kona. Bank pale walikuwa wanajulikana sana.

Dada alikosa raha sana hadi muda anatoa copies akaniambia dada kakae kwenye kiti [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] toka siku hiyo alianza na kunisalimia na kunichangamkia. Mimi wala sikumwonyesha tofauti nikaendelea kumpelekea matunda.
Vipi sasa kuhusu Ph.D mkuu,
Umeshaipiga au bado kidogo?
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale Obey waniambie wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
[emoji23][emoji1787][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mimi uzuri nina adabu simdharau mtu kwakweli ila kuna Mtu aliwahi kuvuka matarajio yangu yani sikutegemea.

Maana jamaa alitaka nikamfanyie kazi fulani akanambia niandike namba atanicheki anatumia Tecno S series😂 nikadharau nikajisemea huyu nae nani🤣, siku ya kazi kaja kunichukua Offisini na Range rover sport anaishi Cliffside resiidence toure dr hakuna kazi nililipwa kama hio mtu unafanya kazi huku unakunywa Moet Chandon Shampaigne.
Sikuhizi wana ku jugde Kwa SIMU unayo tumia
 
Miaka fulani nilikuwa na likizo ndefu ya chuo basi nikaona nisikae bure nikafungua kamgahawa katikati ya mji. Nilikuwa nauza bites zote, juice fresh na matunda fresh.

Nilikuwa karibu na ofisi nyingi na banks. Basi nikawa napata oda ya kupeleka bites na maziwa asubuhi pamoja na matunda.

Dada mmoja staff wa pale CRBD aliweka oda ya matunda kila ikifika saa 6 mchana, ikawa siku nyingine ukipeleka anakwambia umechelewa nishakula kwingine, au leo sili basi narudi nayo. Au ukienda siku nyingine anakuangalia tuu hapokei matunda unabaki umesimama kama sanamu na matunda yako.

Siku moja nikaenda nikiwa na shida ya kufungua joint acc, kufika kwake hata sijamsalimia kanijibu leo sitaki matunda. Nikamwambia nina shida nyingine kabla sijaeleza akajibu tena "hapa tunasikiliza za kiofisi tuu hivyo ondoka". Sijui alijua nataka msaada wa hela au vipi.

Ikabidi niwe mpole maana alikuwa peke yake kwa muda ule customer service pale. Nikamweleza nahitaji fomu kufungua joint acc na mama yangu. Akachukua fomu akanipa akaniuliza "utaweza kusoma na kuzijaza kweli na mama yako??" Nikamjibu ndio. Akaniambia viambatanisho vinavyohitajika nikaondoka kesho nirudishe fomu.

Kesho yake nimeenda na mama, kufika pale akamkaribisha akakae kwenye kiti mimi akaniambia kasubiri pale yaani pembeni, ndio mama akamwambia nimekuja na binti yangu tunafungua joint acc, kwanza alistuka akamuuliza ni mwanao kumbe mama sikujua. Akaishiwa pozi.

Basi katika kupiga stori na bimkubwa akamwambia sikujua kama una binti mkubwa, bimkubwa akamwambia mara nyingi hayupo nyumbani kwasasa yupo likizo anasoma masters huko mkoa X. Alishangaa kwa nguvu Masters?? Aliniangalia sana. Miaka hiyo bimkubwa na mzee walikuwa wafanyabiashara wakubwa sana mkoani na chapaa zipo za kutosha wanajulikana kila kona. Bank pale walikuwa wanajulikana sana.

Dada alikosa raha sana hadi muda anatoa copies akaniambia dada kakae kwenye kiti [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] toka siku hiyo alianza na kunisalimia na kunichangamkia. Mimi wala sikumwonyesha tofauti nikaendelea kumpelekea matunda.
Inaonekana una passion sana na mambo ya misosi bila shaka wewe ni mtaalamu wa maskolodinyo
 
Back
Top Bottom