Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

patrickk

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2012
Posts
367
Reaction score
4,003
Wakuu natumaini wote mpo salama na mnaendelea vyema kusherekea sikukuu hizi

Dah, kwa upande wangu mimi sipo sawa kabisa hapa najiona mkosefu sana na sijui hata jamii itanielewa vipi, nimekuja huku naamini kuna wakubwa na watu wenye busara naweza pata ushauri.. Nayopitia kwa sasa na jinsi nilivyokua na mahusiano imara huko nyuma ni mbingu na ardhi. Kisa ni kirefu kiasi chake hivyo naomba muwe wavumilivu

Mikosi ilianza kama miaka 7 iliyopita nikiwa nimemaliza chuo, nilikua na maisha bora sana yasiyo na misukosuko yoyote, nilianza mahusiano na mrembo mmoja tukiwa form four wote sema shule tofauti, yeye akisoma shule ya bweni ya wasichana pekee na mimi kipindi icho niko boarding school boys tupu,

Huyu binti mpaka kumpata nilitumia sana nguvu acha tu hua sitaki hata kukumbuka, ni binti ameshika sana maadili sidhani kama kuna binti wa namna hiyo endelea kufatilia huu mkasa utaelewa kwanini nakuambia hivo....ili iwe rahisi acha tumuite mary japo sio jina halisi ntajitahidi kuficha codes kadhaa

Mary alikua ametoka familia yenye uwezo mkubwa tu sana na yenye maadili mema, mama yake akiwa na wadhifa mkubwa tu serikalini na mzee wake akiwa mfanyabiashara, hatukua majirani bali nilikutana nae shuleni kwao nikiwa nimeenda kuhudhuria mahafali ya dada yangu mkubwa, bado hio siku naikumbuka kama jana kweli mapenzi yana nguvu unaweza kumuona mtu ukakaa wiki nzima bila kumtoa akilini kwako, sikufanikiwa hata kumsemesha hio siku nikawa nimeondoka na mawazo kibao tu huku namuwaza mtu ambae nilikua na imani sitokaa nije nimuone tena maishani..

Basi bana maisha yakaendelea mpaka siku nakumbuka nipo naangalia cd ya graduation ya sister kuna kipande walikua wanaimba madarasa ya chini ndipo nikamuona Mary bana, hapo nilikua nishaanza kusahau kuhusu yeye, nikamuita sister nijajikaza tu nikamuuliza unamjua huyu binti? Akamuangalia akajibu " vipi unamjua kwanini unaniuliza?" Nikamuambia hapana simfahamu ila nakumbuka nilimuona nilivyokuja shuleni kwenu kipindi kile, sister akaniambia anha huyo anaitwa Mary(disguise name) ni mdogo wake na fulani.... Akaniuliza vipi kuna nini...? Nikajibu hakuna kitu kwani wao wanakaa mkoa gani, uzuri akaniambia wanakaa mkoa mmoja na sisi tulipo, hapo mapigo ya moyo yanaenda kasi sana.

Basi kila nikipata muda nikawa namdadisi sister kuhusiana na yule binti mpaka kuna siku sister akaniambia na wewe nimechoka na maswali yako ngoja ntakuombea namba kwa dada yake, baada ya kama siku mbili sister akaja akanipa ile namba hapo nimechanganyikiwa nashindwa hata nianzie wapi,nikaja mtafuta kwa njia ya sms akanijibu nikatumia nguvu sana kujitambulisha uzuri alikua anamjua sister, akawa anakomaa tu anauliza unataka nini toka kwangu nikamuambia tukiwa marafiki itapendeza akanijibu hakuna shaka...

Nikaja kumuomba nimuone kabla shule hazijafunguliwa tukaja kuonana sehemu moja alikuja na mdogo wake ila hatukukaa sana wao wakaondoka,mawasiliano yakaendelea kwa njia ya barua kipindi hicho kishule shule sasa, kufika form 4 ndo nikaja kumfungukia hisia zangu kwake nakumbuka alikua mkali mpaka nusu urafiki ufe, lakini sikukata tamaa mpaka akaja kunikubalia tukawa wapenzi rasmi

Huyu binti alikua na msimamo sana maana hatukufanya chochote mpaka tukaja kumaliza six nakumbuka kwa mbinde nilimvunja usichana hio siku alilia sana akaniomba nisije kuacha kumuoa, kwa uzuri na tabia zake hakika nilishajihakikishia hapa mke nimepata, tukachaguliwa wote udsm hakika nilifurahi sana nikapanga ghetto huko ndo mapenzi yakawa rasmi sasa, jumatatu naenda nae chuo jioni namuacha anakaa hostel za chuo mpaka ijumaa tukitoka tunaenda wote ghetto mpaka jumatatu tena, hakika Mary alikua mzuri sana ndani ya muda watu wengi sana wakawa wanamjua, nakumbuka kuna siku nipo hall kwao tupo room wakaja wadada flani nilikua nasoma nao kozi moja Mary kuwaambia kua mi ni boyfriend wake wale wadada kila tukikutana nae lecture hall wakawa wananiambia we kaka ulimpata wapi binti mrembo vile.

To cut the story short, Mary hakuwahi kuniletea mauza uza yoyote kipindi tupo chuo, na ujinga sikufanya mwingi maana hakuna weekend yoyote ambayo sikua nae, maisha yakaendelea mpaka tukamaliza chuo mi nikapata kazi mwenye government institution moja ofisi zake zipo posta yeye akapata kazi kwenye private firm, after a while tukahamia kwenye nyumba nzima Mungu akajalia tukanunua na usafiri, asubuhi nampeleka job namuacha jioni anatoka anakuja ofisini kwangu ananisubiri mpaka natoka tunaenda wote home maana mi nilikua nachelewa kutoka, sikua na wasiwasi na Mary maana kuanzia chuo alishatongozwa sana na alikua akiniambia tu naomba uniamini siwezi kufanya ujinga

Basi tukaanza kuishi maisha ya Mume na mke rasmi, uzuri kwao wote kasoro wazazi tu ndo walikua hawanijui, na kwetu ivo ivo, tukaanza kabisa na kupanga mipango ya kutambulishana makwetu, dah kumbe bana ukipanga hivi shetani nae anapanga vile, nakumbuka kuna birthday moja nilihudhuria nikakutana na msichana mmoja wa kisomali mixture kidigo alikua anasoma chuo cha uhasibu TIA aisee najuta sana hio siku maana nahisi masaibu yangu yote mpaka leo hii nakula christmas kinyonge ivi yalianzia hapa...

Endelea kunifatilia naandika leo leo hii mpaka iishe hata kama ni saa 7 usiku.
 
Clarification- hii story ya mary nimeiandika juu juu tu kwani sio mlengwa halisi wa hiki kisa


EPISODE 2


Basi bana nakumbuka kuna sherehe nilihudhuria ilikua birthday party ya co worker mmoja ivi nikakutana na huyu binti wa kisomali hapa nadhani ndo masaibu na mikosi ya maisha yangu yalianzia hapa.... Hiyo siku tulifanya party tu wala hatusemeshana na huyo binti, ila ali catch sana attention yangu maana alikua binti mrembo haswa, tukirudi kwenye maisha ya chuo sio kwamba sikuwahi kucheat, ila nilifanya hivo na mabinti ambao niliwaweka wazi kabisa kuwa nina serious relationship wasitegemee chochote kutoka kwangu kwamba tunaweza kua serious, after that party nikapotezea kuhusiana na huyo binti( tumuite Samira)... Kumbe Samira alikua amekuja na rafiki yake mmoja ambae anadate na huyu mfanyakazi mwenzangu ambae ndo alikua na hio shehere



Huyu jamaa sikua na mazoea nae sana zaidi ya kikazi,maana wao wakitoka job walikua wanapenda kwenda pale new africa casino wanapiga zao mitungi mpaka foleni ilegee ndo wanaondoka, sasa mimi hio lifestyle sikuweza kwenda nao sawa maana nilikua tayari naishi na Mary ni kama nilikua nishaoa na kumbuka usafiri naotumia mary nae ndo alikua anautegemea.... Sasa kumbe huyu mfanyakazi mwenzangu( tumuite John) yeye bado akawa anakutana na huyu Samira na rafiki yake Samira ambae ni mpenzi wake na John, sijui sasa story zikaanzia wapi kumbe yule Samira akawa ananidadisi kwa huyu mshkaji john kila wakikutana, ikaenda mpaka wakaanza matani kila wakikutana Samira anamtania msalimie Mume wangu Patrick!!! Hapo mi sijui lolote na wala jamaa hakuwahi kuniambia chochote....



Baada ya muda huyu jamaa John tukaanza mazoea flani tukawa weekend nyingi tunapiga wote vinywaji japo nilikua najitahidi sana kumkwepa, ikaenda hivo mpaka siku akaniita jangwani kipindi hicho pa moto moto nikaenda nipo mwenyewe, nikamkuta yupo na mpenzi wake na huyo binti Samira nae alikuwepo, mabinti wameagiza juice jamaa anakunywa grants( kipindi iko bado vijana na mshahara na posho ofisini ilikua si haba).... Ile nafika nikawasalimu kisha nikaketi, huyu samira akawa anaongea kwa utani "afadhali leo Mume wangu amekuja maana kila siku natuma salamu hata sijibiwi"

Nikawa confused kwanza ila nikajikaza nikakausha tu, nikaagiza glass tukaanza kupiga shots pale mshkaji story nyingi ndo nikajua wale mabinti wako mwaka wa pili TIA pale, hapo nikawa nampiga jicho Samira la kuibia ibia mpaka nadhani akawa kama kashtuka ivi, nikaona hapa niskae kinyonge nikawaagizia chakula wakakataa wakidai wametoka kula basi nikaongeza tena pombe pale na wao nikawaongezea juice, sasa baada ya muda john nae pombe imeanza kukolea akawa anamwambia huyu samira " haya patrick huyo hapo nimechoka kila siku unatuma tuma"...


Akili yangu ikaclick tena nikawaambia mbona siwaelewi, ndo john akaanza kuropoka " bana huyu kila siku haishi kutuma salamu kwako bora umekuja leo muongee wenyewe tu" nikawaza mbona mshkaji hajawahi kuniambia au ndo alikua ananbania white, hapo nikaweka shots kadhaa nina confidence kiaina nikamgeukia yule binti nikamwaambia hebu chukua namba zangu salam zangu unipe mwenyewe basi akaandika namba kwenye simu yake akasave....


Sikukaa sana maana Mary alishaanza kusumbua nachelewa nikaaga pale mi nikaondoka zangu, nafika home ile nafungua simu nakuta samira kantumia picha zake kama 10 ivi wala hakuna ujumbe wowote, huyu mtoto alikua mzuri huwezi amini mpaka leo picha zake kuna mahali ninazo nilishindwa kuzifuta.... Nikaangalia zile picha nikawa ninawaza hapa kazi ninayo, sema nikawa najipa moyo Mke tayari ninae hapa nikipita siangalii nyuma... Nakafungua zile picha zote sikujibu chochote nikakaa kimya tu



Kesho nipo kazini, ikaingia text kutoka kwa samira "Mme mbona jana hukujibu au ulipitia mchepuko huko nini"... Nikawaza sana badae nikamuita john nikawa namdadisi kuhusu huyu binti, nikamuuliza john ina maana katika maongezi/utani wenu hujawahi mwambie huyu binti naishi na mwanamke mimi, jamaa akasema hajawahi hata kumuambia hilo swala, hapo na mimi nipo kwenye denial mode tu ila akilini samira kashaanza kuniingia... Nikawaza nikasema potelea popote acha liwalo na liwe



Nikawa sio mtu wa mazoea ya kuchat nae kwenye simu sana mpaka weekend moja nikamtafuta tukaanza kuchat

Mimi: hujambo mke
  Samira: sijambo mme, loh mwanaume ndo leo umenikumba
Mimi: kukuwaza nakuwaza sana sema nakua busy na kazi na kupambana na maisha, vipi leo una muda nataka tuonane
Samira: sijaweka vizuri ratiba zangu ila inategemea una shida gani na mimi labda naweza kuadjust ratiba
Mimi: nataka leo nimtoe mke kwenye first date ikiwezekana tuvunje kabisa undugu leo tuzindue penzi letu
(Kumbuka hapo mi naenda resi maana binti mwenyewe ndo alianza kuonyesha kunitaka)
 Samirah: Patrick hivi uko serious kweli?
mimi: nipo serious sana tu we jiandae niambie saa ngapi nije nikufate
samira: Mungu wangu Patrick mi napenda utani sana sikutegemea kama we utachukulia serious kiivo, mi nakuona kama kaka yangu sio tofauti na hapo na mimi na mtu anayekunywa pombe wapi na wapi


Heeee!! Nikabaki nashangaa tu, huyu mtu mbona simuelewi hata, mbona ye ndo ameanzisha haya mambo leo hii anaruka kiasi hiki? Basi nikashikwa na hasira pale nikapotezea, huku Maisha na Mary yapo poa kabisa wala hakuna dosari yoyote ile, nikawa nawaza kwanza nahangaika nini wakati nina mke mzuri kabisa ambae hajawahi hata kunisumbua, aisee kumbe nilikua sijui kinachonisubiri mbele
 
Episode 3

Basi bana maisha yakaendelea vizuri tu huku nipo na Mary tunazidi kupanga mipango ya kimaisha vizuri tu yaani, kwa upande wa Samira sasa sijui wanaume tuna shida gani, ni kama tunapenda challenges flani ivi, yaani ukiona binti hakutaki ndo akili inahamia kwake ukiona anayekutaka sana ndo unakua huna muda nae, ujinga ukaanza kuniingia taratibu nikaanza kumpa ratiba za kazini za uongo mpenzi wangu Mary huku nikijifanya namuonea huruma anavyotoka mapema kuja kukaa kwenye gari akinisubiri mpaka nitoke kazini, mara awe anawahi anakuja hata kunipikia usiku.... Basi tu sababu nyingi maana nikaanza kuona ni kama ananibana yanii, nikamshawishi sana tukaja kununua kagari kadogo used kwa mshkaji wangu tukawa tunamlipa kwa installments, kila mtu akawa na gari lake, hapo ndo nikaanza ujinga rasmi



sasa hapo hawa washkaji kina john wakawa ndo washkaji zangu tukitoka kazini ni kwenda kupiga gambe nikawa mtu wa kurudi home sa tano, Mary mpole kweli hawezi hata kuongea narudi ananipakulia nakula ushahidi tu wala halalamiki, mpaka siku akaanza kunihoji mbona siku izi unakunywa kila siku afu hurudi mapema, nikawa namjibu stress za kazi tu afu ofisini kuna training tunachelewa kutoka ila tunalipwa overtime mke wangu usijali, akajibu sawa mme nakuombea tu....


Mimi sasa ndo nikaanza kuhangaika na Samira, kila nikitoka kazini nampitishia vizawadi, au niwachukue na marafiki zake niwatoe out basi tu yani, siku moja akaniambia patrick unajua nakupenda sana hata marafiki zangu wananiambia you are such a good guy ila naogopa kuumizwa na wewe tena unakunywa pombe sidhani kama tutawezana, nikaanza kumdanganya tu hapa na pale ila kuhusu pombe nikamwambia point blank siwezi kuacha kwanini nikudanganye


Ikaenda enda mpaka akaja kukubali nakumbuka first kiss tulikua coco pale upepo mwanana hapo Mary wangu ananisubiri ndani sikujua hata nilimdanganya nini siku hio maana nilishakua muongo kweli, huku samira nambembeleza tukalale hoteli yeye anakazana nataka nikalale kwako mtu hata sijui unaishi wapi, nikamzuga home kuna wageni tutaenda siku nyingine



Drive ya mapenzi na pombe ni a very bad combination aisee, huku nataka nikalale hoteli kule kwa Mary sijaaga hata wala sina plan yoyote, basi bana ikafika muda hapo simu nimezima tukaenda hoteli na samira mi nawaza tu leo huyu msomali sijui mdigo kazi anayo aisee, tumefika ndani tupo comfartable tu badae kufika kitandani mwenzangu kanibadilikia, akawa haeleweki, mara analia, kuvua nguo hataki yaani nikawa hata simuelewi kabisa, namuuliza kuna shida gani hakuna analosema la maana, kila nikitaka kumvua analia, basi nikatoa begi la kazini nikatoa pc nikaweka movie nikawa nimemkumbatia tunaangalia, alivyorelax kabisa nikamuuliza samira mama kwani kuna shida gani mbona sikuelewi,huku ameziba macho na mikono akaniambia patrick sijawahi kufanya hiki unachotaka kufanya



Aisee akili ikaruka nikawa sielewi, ila moyoni nikasema hapana aisee huyu ananiona wa kuja, alivyo mrembo hivi na hili tako na hii rangi ya mtume wajanja wa dar hawajamuona nikasema patrick acha kujidanganya hapa unachezewa picha la kihindi
 
Episode 3

Basi bana maisha yakaendelea vizuri tu huku nipo na Mary tunazidi kupanga mipango ya kimaisha vizuri tu yaani, kwa upande wa Samira sasa sijui wanaume tuna shida gani, ni kama tunapenda challenges flani ivi, yaani ukiona binti hakutaki ndo akili inahamia kwake ukiona anayekutaka sana ndo unakua huna muda nae, ujinga ukaanza kuniingia taratibu nikaanza kumpa ratiba za kazini za uongo mpenzi wangu Mary huku nikijifanya namuonea huruma anavyotoka mapema kuja kukaa kwenye gari akinisubiri mpaka nitoke kazini, mara awe anawahi anakuja hata kunipikia usiku.... Basi tu sababu nyingi maana nikaanza kuona ni kama ananibana yanii, nikamshawishi sana tukaja kununua kagari kadogo used kwa mshkaji wangu tukawa tunamlipa kwa installments, kila mtu akawa na gari lake, hapo ndo nikaanza ujinga rasmi



sasa hapo hawa washkaji kina john wakawa ndo washkaji zangu tukitoka kazini ni kwenda kupiga gambe nikawa mtu wa kurudi home sa tano, Mary mpole kweli hawezi hata kuongea narudi ananipakulia nakula ushahidi tu wala halalamiki, mpaka siku akaanza kunihoji mbona siku izi unakunywa kila siku afu hurudi mapema, nikawa namjibu stress za kazi tu afu ofisini kuna training tunachelewa kutoka ila tunalipwa overtime mke wangu usijali, akajibu sawa mme nakuombea tu....


Mimi sasa ndo nikaanza kuhangaika na Samira, kila nikitoka kazini nampitishia vizawadi, au niwachukue na marafiki zake niwatoe out basi tu yani, siku moja akaniambia patrick unajua nakupenda sana hata marafiki zangu wananiambia you are such a good guy ila naogopa kuumizwa na wewe tena unakunywa pombe sidhani kama tutawezana, nikaanza kumdanganya tu hapa na pale ila kuhusu pombe nikamwambia point blank siwezi kuacha kwanini nikudanganye


Ikaenda enda mpaka akaja kukubali nakumbuka first kiss tulikua coco pale upepo mwanana hapo Mary wangu ananisubiri ndani sikujua hata nilimdanganya nini siku hio maana nilishakua muongo kweli, huku samira nambembeleza tukalale hoteli yeye anakazana nataka nikalale kwako mtu hata sijui unaishi wapi, nikamzuga home kuna wageni tutaenda siku nyingine



Drive ya mapenzi na pombe ni a very bad combination aisee, huku nataka nikalale hoteli kule kwa Mary sijaaga hata wala sina plan yoyote, basi bana ikafika muda hapo simu nimezima tukaenda hoteli na samira mi nawaza tu leo huyu msomali sijui mdigo kazi anayo aisee, tumefika ndani tupo comfartable tu badae kufika kitandani mwenzangu kanibadilikia, akawa haeleweki, mara analia, kuvua nguo hataki yaani nikawa hata simuelewi kabisa, namuuliza kuna shida gani hakuna analosema la maana, kila nikitaka kumvua analia, basi nikatoa begi la kazini nikatoa pc nikaweka movie nikawa nimemkumbatia tunaangalia, alivyorelax kabisa nikamuuliza samira mama kwani kuna shida gani mbona sikuelewi,huku ameziba macho na mikono akaniambia patrick sijawahi kufanya hiki unachotaka kufanya



Aisee akili ikaruka nikawa sielewi, ila moyoni nikasema hapana aisee huyu ananiona wa kuja, alivyo mrembo hivi na hili tako na hii rangi ya mtume wajanja wa dar hawajamuona nikasema patrick acha kujidanganya hapa unachezewa picha la kihindi
...
 
Episode 4


Basi bana nikasema acha niwe mpole ntajua tu itakuaje, sikutaka a panic tena nikamwambia its okay wala usijali, sasa nikawa nataka nionekane gentleman kumbe sina lolote, nikamwambia uamuzi unaotaka kufanya hauwezi kubadilika maishani tena kama unaona mi sio mtu sahihi ni bora tuache tu.... Akageuka akaniambia nakuamini patrick usije tu kuniangusha, basi hapo amerelax tena nikaanza romance kidogo kidogo anahema tu mpaka nikafanikiwa kumtoa nguo, katika maisha yangu sijawah kukutana na bikra ya namna ile yaani hata kidole cha kati kilikua hakipiti kabisa baada ya majaribio mengi, tukaanza kukimbizana kitandani tu abane miguu nimtanue yaani purukushani tupu mpaka asubuhi bila bila hakuna kitu hata



Asubuhi nikampeleka mpaka Kurasini huko hapo nishakua kama mwehu sikwenda hata home nikaenda kazini, nafika nawasha simu nampigia Mary ile simu inaita huku sms zinaingia kama mvua yaani, kuja kupokea anahema kulikoni uko wapi mme wangu, nikamwambia jana nilipata ajali ila sijaumia sana sema nimelala kituoni mtu wa boda ndo aliumia, dah akaanza kunipa poleh nyingi na maswali mengi tu akawa anauliza, nikamwambia relax mke wangu gari nimepeleka bodi nikija jioni tutaongea....alivyokata simu nikaanza kujiskia sina amani, nikawaza tulipotoka Mary mbona nataka kuharibu maisha kwa tamaa za ajabu tu...


Nikafanya kazi hapo akili sasa ipo kwa samira tunachat muda wote,jioni ikabidi niwahi home samira nikamwambia nina wageni leo hatuwezi kuonana nafika home Mary nae yuko busy kunikagua kama nimeumia na kunipa pole, uzuri hakua mdadasi wa magari hivo hata gari hakuhangaika nalo,


Nikawa rasmi nimejiingiza kwenye double life, huku naishi na Mary huku Samira nae haishi kupiga simu/sms na wote sitaki kuwapoteza rasmi nikaingia kwenye maisha magumu sana kuya maintain


Nikaanza mipango ya kijinga sasa, Mary nikaanza kumpanga kua nataka weekend niende morogoro vijijini huko kuna mradi nimeambiwa na mshkaji wangu ya ufugaji wa nyuki nikaangalie nione kama tunaweza kuwekeza, Mary nae tena ukimwambia mambo ya maendeleo ndo kwanza anafurahi akaniambia ni jambo jema, ilivyofika weekend mimi huyo na samira kuna hoteli moja chimbo sana tumejifungia weekend nzima simu hapo nimezima nikitaka kumpigia mary natoka nje naongea nae namdamganya network kijijini hakuna najiongelesha na mambo ya nyuki( ila maisha haya).... Acha tu...


Huku ndo nikafanikiwa kumtoa usichana samira tukaanza safari mpya ya mapenzi, mpaka leo hua najuta sana kumkuta huyu binti ni bikra maana tofauti na hapo ingekua rahisi sana kumuacha, ila nikaanza ku feel commitment kwake na nikaanza kumpenda sana, maisha yangu nikaanza kuhangaika kua na wanawake wawili na kila mmoja akijiaminisha na hana chembe ya wasiwasi kua yuko mwenyewe, nikawa najiona mjanja kumbe bana sijui kitachonikuta
 
Ngoja nipunguze details ili isiwe ndefu sana iishe leo leo

Episode 5

Katika kitu ambacho kilinipa wakati mgumu ni huyu binti samira hakua bado matured kabisa, bado alikua na mapenzi ya kitoto sana, ilifika kipindi asiponiona siku moja atalia wee mpaka awe mwekundu, marafiki zake anaokaa nao hostel sijui kwanini aliwapa namba zangu yaani akianza kujiliza utapigiwa simu na mashemeji na sms mpaka ukome, huku nae Mary sio mjinga, japo hashiki simu yangu ila alishaona nabadilika sana, akaanza kuhoji mme wangu siku hizi una ratiba sizielewi na hutaki hata tufatane we kua makini dunia hii, yote kwa yote Mary ni mwanamke nilikua nampenda sana na sikua tayari kumpoteza kabisa hayo mengine nilikua nafanya tamaa tu na ujana wa kijinga



Sasa ili kukeep up na double life ambalo nilikua nimechagua nikaja kupanga sehemu nyingine nikaweka na vitu vya ndani huko maana samira nae kila siku sababu za kutomleta kwangu ziliisha, nikaanza maisha ya kujigawa leo nalala huku kesho huku hapo mary nishamdanganya mpaka akachoka, akawa ananisemea kwa dada yangu mkubwa kila siku ananionya lakini wapi siambiliki, hapo mary hajashtuka mchezo mzima ila alikua anajua kuna jambo tu maana nilikua nimebadilika sana...


Maisha yakaenda hivo hivo mpaka siku nikafanya a grave mistake, samira siku niko nae kitandani akawa anaturecord ila hatukuwa tunasex ila ndo ivo kisses na nini, kumbe ile video alinitumia whatsap ikaji auto download ikazama gallery mi sina habari, mi sikua mtu wa picha wala nini so nikiwa na Mary hua nahakikisha tu hakuna sms mbaya wala simu za ajabu, samira kuna namna nilikua namuweka do not disturb hivyo missed call au sms zake nizikuta kwingine kabisa, tofauti na hapo sikua na mchepuko mwingine kabisa.....


Sasa siku hio Mary kaniomba simu yangu mimi najua ipo clean nimempa yupo sebleni mi nipo zangu chumbani, kumbe kakutana na ile clip bana, mpaka leo hua ananiambia hakuwahi kuamin kama naweza kumcheat mpaka hio siku alivyokutana na hio clip, basi akalia wee huko sebleni mpaka akachoka mi sina habari wala nini.... Kuja kwenda sebleni namkuta na chupa ya drosstdyhoff kwanza hakua mnywaji sana ilikua glass moja akinywa tu basi, mi sijui kinachoendelea hapo nikachukua zangu sijui pombe gani kali nikawa nakunywa Mary namtania wala hata hayupo interested


Sasa sijakaa sawa mara mtu kamaliza ile chupa nzima kubwa kaenda kwenye fridge katoa nyingine kafungua, akili ikaanza kucheza hapa hakuna usalama, nikamuuliza leo mbona unakunywa ivo wala hata hajibu anakunywa tu wine kwa kasi sana, badae nikamfata mke wangu kuna shida gani, aisee alitoa kilio hiko mpaka leo nakumbuka, akalia sana akaniambia angalia unafanya umalaya unajirekodi ili uje nionyesha, kwanini umenichoka ivo, kuja kuangalia simu sasa yaani nikachoka, niliomba msamaha kweli siku hiyo, lakini wapi mtu alilia usiku kucha, akakesha anatapika tu maana hata hakua mnywaji, hio siku amelewa anaongea vitu sijielewi, nikawa nawaza kwanini nimemfanyia hivi mke wangu, sijawahi kumuona kwenye hali hio namuonea huruma tu yaani....


Mungu akasaidia pamekucha bado analia macho yamevimba akaniambia siendi kazini leo kwanza sitaki kazi tena, nikambembeleza weee nikaenda kumuogesha nikamvisha nikampeleka mpaka kazini mi ndo nikaenda kazini na mimi, haikufika hata saa 4 anapiga analia ananiambia utanikuta nyumbani nimekufa nataka kujiua, nikasema aisee leo kazi ninayo
 
A very stupid story and betrayal man. If it's true story there is bundle or furnace of fire for you in hell, the eternity fire. Poor Brain

Do not give your strength to women, your ways to those who destroy kings.

Proverbs 31:3
Hakuna aliye mkamilifu, malipo nayalipa hapa hapa duniani endelea kufatilia na mimi nilikutana na aliyeninyoosha
 
Dah!,pole sana mkuuu

Ila namwonea huruma sana mtoto wa watu Mary

Story nzur sana ya mapenz ila ina huzunisha

Ila ya kwenye viatu vya mumeo kuna ndala zangu sjui imeishia wapi

Mimi kwenye mapenz napendaga sana kuwa mkweli maana uongo huwa siuwez,samira ningemwambia ukweli au alipozingua siku ya kwanza ningempotezea kabisa ila kuondoa jam
 
Episode 6


Hapo akili ikaanza kuwaza kwa kasi, nikakumbuka kuanzia Mary namuona kule shuleni kwao, that innocent girl leo hii anakua hivi kwasababu yangu, nikajikuta chozi linatoka,nikamtumia sms, nakuja mke wangu nakupenda, sikuaga hata mtu nikaondoka zangu ofisini kwenda nyumbani, hapo samira nae anapiga simu sipokei, sms sijibu, ikaingia roho nikaanza kama kumchukia tena samira, ila nikawaza she is just another innocent girl mimi ndo mwenye makosa, hakuna namna ya kurekebisha hapa....huyu nae akijua, amejitunza kote huko leo hii ajue nilimtoa usichana kumbe nina mke, nikasema hapa there is no winning nimejichanganya tu tena sana



Nafika home nakuta Mary ashalewa tena, analia tu, dah nikasema ndo maisha gani haya tena, ikawa hakuna namna nambembeleza tu ikabidi pombe zote nitoe ndani nikazifungia kwenye gari, imefika muda nikatoka kwenda kumtafutia chakula nae katoka kuna grocery pembeni kaenda kanunua wine tena, narud hayupo kumkuta ndo huko tena analia tu watu wanamshangaa nikajiskia vibaya sana, sikuwahi kumuona hata amelewa tangu nimjue, nikambembeleza tukaenda home, yule dada wa grocery akaniambia mdogo wangu badae uje


Nikarudi home Mary kula akagoma nikambembeleza akawa amelala, nikatoka mpaka grocery hapo kichwa kina moto nikabugia konyagi ndogo kwanza bila hata kupumzika, yule sister wa grocery alikua mshkaji wangu kiaina ila Mary hakua na mazoea kabisa na majirani, ananiuliza kulikoni wifi kafanyaje ikabidi nimueleze tu ilivyokua, nae akaanza kunchamba na mwenzake "kaka una mke mzuri hivo anafanya kazi nzuri unataka nini tena"



Akili ikaruka, kazini sijaaga, kuna Mary hapa sijui nadeal nae vipi, Kuna samira hapa nae namfanyaje, aisee sikuwahi kua na siku nzito kiasi hiko
 
Back
Top Bottom