S2 episode 11
Kurudi sasa maneno hayaishi binti analalamika nashindwaje kumpa hela ya mtaji ila ya kujenga ninayo, hapo hasira zinapanda nawaza nilimfungulia biashara akaiua kwa ujinga wake mwenyewe... mi npo kimya analalamika tu nikawa nawaza hivi huyu najenga yeye analalamika mbona ni mpumbavu sana, basi akaongea we pale maneno ya shombo ikafika wakati nikasema enough is enough, hiyo siku nilimpiga kipigo utasema nampiga mwanaume mwenzangu, binti maneno mengi ila kupigwa muoga nakumbuka alipiga sana magoti ila wapi kipigo kipo palepale, nikampigia mama mkwe simu nikamwambia njoo mfate mtoto wako mi ntamuua huku
uliza kuna nini sikujibu nikakata simu nikaondoka zangu, badae narudi nakuta hawapo na milango hata hawajafunga, chunguza nakuta kabeba karibu kila kitu chake na laptop moja nilikua natumia nyumbani tu, mama mkwe anapiga simu mi sipokei wala nini, ikafika kesho mi kimya tu, mida ya 9 akaja mtu ofisini ananiambia kuna mgeni wako, naenda namkuta mama mkwe tukasalimiana pale akaanza kunihoji baba kulikoni? nikamwambia mwambie binti yako akueleze yeye ndo anajua vizuri, basi akaanza kuongea pale ohh mvumilie tu najua ni mkorofi ila fanya kwa ajili ya mtoto tu sasa, nikamwambia mi nshachoka naomba tuongee muda mwingine nina kazi, akasema sawa akaondoka
Muda wa kusafiri ukakaribia ikabidi nitafute kuna kijana ndugu yangu aje akae pale kwangu, ilivyokaribia muda nikaenda kwa kina Rachel nikawaaga mama mkwe nikamuachia pesa za matumizi kwa ajili ya mtoto kwa huo muda ambapo sipo ikafika tarehe huyo mi nikasafiri zangu
sasa kule njia ya mawasiliano rahisi ni kutumia whatsap, mama mkwe nae mambo ya smartphone hata hayajui ana simu ndogo, Rachel tushagombama hakuna anayemsemesha mwenzake
nimekaa kule vizuri tu nakumbuka muda mwingi nilikua naongea na Mary tu atleast napata amani kidogo, sasa kuna siku naona Rachel kaweka status yupo bar usiku wanakunywa nini sijui wapo na madem flani ivi, nikasema kumekucha hapo namuwaza mtoto tu nasema huyu mtu ataniharibia mwanangu, nikajua huyu anataka attention wala hata sitamtafuta
kama mwezi npo kule nikamtuma yule kijana anayekaa kwangu akanunua simu nakumbuka ya bei ndogo tu smartphone akasajili na laini na kuunga whatsap nikamwambia aende kwa kina Rachel asifanye chochote mpaka niongee na mama yake, kweli nikafanikiwa kuongea na mama yake nikampa maagizo ampe hiyo simu Grace mdogo wake na rachel ili niweze kumonitor hata maendeleo ya mtoto akasema sawa, nilifanya hivo maana kuna kipindi cha nyuma nilitaka kumnunulia mama yake Rachel smartphone akakataa akasema hata hajui kutumia
basi mara nyingi maendeleo ya mtoto nikawa napata kupitia grace akitoka shule, japo alijaribu kumfichia siri dada yake lakini badae nilikuja gundua rachel ameshakua mtu wa viwanja mara nyingi anachelewa kurudi nyumbani, hapo nakumbuka nilikua nawaza sana kuhusu huyu mtu kuniharibia mwanangu
nakumbuka nabakiza kama wiki nirudi huku wakanipa taarifa kua mtoto ameachishwa ziwa, yaani hapo ana kama mwaka na mwezi mmoja na sehemu nikasema tu sawa moyoni nikashukuru maana huyu binti nilikua simuamini kabisa....
kupitia yule kijana nikawatumia pesa tena siku hazigandi training ikaisha nikawa nimerudi