Aisee yaani mule mule, wangu alipokutana na ndugu zangu kwenye msiba she pretended and played an angel mpaka mama na ndugu zangu wakaning'ang'aniza baada ya mazishi niondoke nae kuja nyumbani kwangu mkoa ninaofanyia kazi. Nikamwambia sawa wazee wamekukubali kumbuka hatuna muda mrefu so utakaa kwangu mwezi mmoja then utarudi nyumbani kwenu tukiwa tunasomana, akakubali. Wazee wakawa wanashinikiza nijipange ili tutume watu wakajitambulishe na kila mara wanaongea nae kwenye simu wanamwakikishia kuwa kijana wetu atakuoa maana tayari ana kazi, maisha mazuri na umri unazidi kwenda.
Aisee huyu binti kichwa kilimpanda na hapo ndipo nilipoanza kuona rangi zake kama nilivyoelezea huko juu. Hakuna kitu nisichokipenda kama kupangiwa ratiba, kukaguliwa simu yangu na nikiiacha tu na ikaita kama niko mbali kidogo bhasi ataiwahi na kupokea na akiona ni mwanamke tu baada ya hallo yeye ataanza na "Mke wa Fyddell hapa naongea, nikusaidie nini?" Aisee.... kuna siku uvumilivu ulinishinda kwa shutuma ya kitu ambacho sijafanya eti akanikaba as yeye yupo juu yangu, nikamuonya kistaarabu tu niachie, alivyoona nimeshuka akaichukua simu na kuipiga chini kwenye carpet huku kanikaba.. ebanae hasira sijui zilitokea wapi, nilimkata kofi moja matata mpaka chini na aliponyanyuka tu akakimbilia sitting room maana hakuwahi kuniona katika ile hali ya hasira vile. Mimi sikumjali zaidi ya kuvaa tshirt then nikaondoka zangu nje nikimuacha sitting room uso wake ukiwa umeumuka.
Nilimwambia nikirudi nikute umeandaa nguo zako kesho asubuhi unarudi kwenu Dar kwa wazazi wako na kabla ya kutoka nikampogia agent wa busy kumwambia anitumie control number nifanye malipo ya nauli online huku simu ikiwa loudspeaker akisikia. Nipo na washkaji tunapiga gambe nashangaa simu ya mama angu hiyo na pale kuna kelele kidogo nikaona si ustaarabu kuongea na bi mkubwa eneo kama lile. Hakuna siku ambayo wazazi wangu walijazwa maneno ya uongo juu yangu na yule girl kama hiyo siku na neno la mwisho nililoambiwa na mama ni "Ole wako umfukuze huyo binti wakati wazazi wako tumeshampenda na kumbariki". Nilichoka aisee........