Siwezi nikishakichoka kitu na moyo wangu ukakubali huwa sirudi nyuma..!! 😹Shemejiiiii mrudie mwana….😂
Huu upendo wa kuoneana huruma mashemeji mmeanza lini? 😹Shemeji hebu Muoneee huruma Mtoto wa Mwanamke Mwenzio, Jamaa yetu anakumiss mno!!
Shemeji sisi tunakutambua wewe tu kama Shemdarling, Hatumjui Yoyote mwingine mpe nafais nyingine MwanetuHuu upendo wa kuoneana huruma mashemeji mmeanza lini? 😹
Mzee shusha Episode, ulisema mpaka saa saba , tumeshaweka Kambi hapa. Tunakula BIA huku tunashuka na stori yako, acha uzembe
🤣🤣🤣🤣🤣Mzee shusha Episode, ulisema mpaka saa saba , tumeshaweka Kambi hapa. Tunakula BIA huku tunashuka na stori yako, acha uzembe
Kmmk 😁 🤣 🙌 🙌S2 episode 2
Sijakaa sawa dada wa mgahawa anapiga tena, " Shem upo wapi?" Nashangaa huu ushem wa lini tena, nikamuelekeza nilipo akaniambia tunakuja akakata simu. Baada ya muda kweli nawaona huyu hapo na rachel, Rachel amevaa kigauni flani ivi amejibeba kweli kweli, yule dada wa mgahawa alikua mcheshi sana akafika akaniambia " haya mtu wako huyo hapa mbembeleze mwenyewe mi nimechoka"... Nikamvuta rachel namuuliza kuna shida gani akaniambia tu we futa hio picha ndo tutaelewana, basi bana wakala pale na vinywaji kidogo yule dada wa mgahawa nikamuambia tafuta usafiri wako mapema sisi leo hatujamaliza kubembelezana... Rachel ni kama alianza kusita ila badae akakubali tukaenda kulala wote kwangu hio siku safari mpya ya mapenzi ikaanza
Kuhusu rachel sasa, ye aliishia la saba, kalelewa familia duni na mama tu na ana wadogo zake wawili mmoja wa kike alikua form 1 bado mwingine wa kiume mdogo yupo la pili, mama yake nae kazi haieleweki yani ni kujishkiza hapa na pale tu, basi tukaanza penzi la rachel sijui hata niliwaza nini miezi mitatu tu ya kwanza mimba tayari, hapo nimemchunguza kidogo sana ila nikasema sawa tu, akawa anakuja kwangu anapika, anafanya usafi kuna muda ni kama alihamia tu kwangu kabisa
Tofauti sasa nikaanza kuiona rachel kwao ndo tegemezi kwa hiyo bills zote nikawa nalipa mimi kupitia yeye, mara sijui ana michezo anadaiwa, yaani vitu ambavyo sikuzoea kutoka relationships za nyuma, ila nikawa siwazi kwani financially nilikua sipo vibaya na nawaza huyu anabeba mtoto wangu sitaki apate stress, sasa kuna siku nipo kazini, ikaingia sms namba mpya "mwanangu mna mpango gani na mwenzako na hio hali yake mtakuja lini kujitambulisha?"
Nikawa kama sielewi elewi hivi, jioni nikamuuliza rachel hii namba ya nani akaangalia akasema hii ya mama nilimpa namba yako, nikabaki nashangaa, nikaanza kuona red flags, mbona kama uswahili sasa huu, mama mkwe anaanza kuntafuta mimi alafu tena kwa sms, nikasema something is not right hizi familia nazoingia huku nitanyooshwa tu
Andika hapo na wewe punguza umalaya ✍️✍️✍️🤣🤣🤣S2 episode 5
Hilo sakata likaisha bana, Rachel jioni karudi namuuliza hao wazee ni kina nani, ye anacheka tu anasema sijui hata mama kawatoa wapi, dah moyoni nikawa nasema tu mbona hawa watu kama hawapo serious nikaanza kujuta sasa naona mbona kama nakosea, hapo mama sijamuambia anaishia kuskia tu maneno juu juu kwa watu
Baada ya kama siku 2 hivi, Rachel kuna simu yake ya zamani ilikua samsung sijui toleo gani ila zile za nyuma kidogo akawa kaniomba nimbadilishie kioo kilikua kimevunjika ili aje ampe mdogo wake wa kike yule alikua yupo form 2, sasa nikaja kutoka nayo siku naenda kazini nikaacha kwa fundi jioni nikaipitia, katika kukagua kioo kama kipo sawa nikawa nimeingia sasa kwenye simu haikua na password wala nini dah huko sasa ndo nilikutana na balaa ambalo siwezi lisahau
Nikaingia kwenye sms za kawaida aisee nilichoka, zilikua na span ya kama mwaka, ni kama sms za mwaka mzima hajikufutwa, huko nilikutana na sms za wapenzi kama wote yani, madereva wa malori, wame za watu, ma dj wa club, wafanyabiashara, vijana wa mtaani tu yaani vurugu tupu, nikapanic sana nikapita mahali nikaanza ichunguza simu taratibu, sms zile ambazo zilikua wazi kabisa kwamba ametembea nao maana unakuta wanakumbushiana kabisa waliyofanya zilikua za wanaume kama 8 ivi
Kuna kama watu 6 hizi hazina ushahidi wa moja kwa moja kama walifanya au, hapo ni sms za kawaida, nikazama whatsapp sasa... Uwiiii.... Huyu binti ni malaya sijapata kuona huko napo watu washamla sana, unakuta sms anaelekezwa njoo guest flani, mara namtuma boda akufate alafu watu tofauti, kuna moja jamaa anamuambia nakufata unipe binti anadai siwezi tumejuana leo tu mara subiri nikuandalie siku nyingine ili nikupe vizuri, jamaa akakomaa demu badae akamwabia haya nifate, ni hio namba haijaseviwa hata😔, hapo na mimi binti nishaanza kumpenda nilijikuta natetemeka tu sijawahi kuumia vile
Nikaja gallery sasa, kuna video mbaba mtu mzima wapo chumbani anampiga romance huku anamnywesha savannah, yaani kwenye hio simu nikisema nieleze mambo yote niliokuta naweza andika mpaka nikachoka maana ni mengi mno hayaelezeki,
Kuna chat nikakuta anachat na yule dada wa mgahawa yaani hapo ndo kila akienda kuliwa ndo hua anamuambia shoga yake, mpaka kuna siku yule dada wa mgahawa akamwambia "shoga yangu na we sasa punguza umalaya"
We G hujambo?Waliimbaga eeh hainaga ushemeji😄😄
Nawewe kili kulamba !!? 🤣🤣recho ni kama Elineva tu, pumbavu sana elineva
Baba mkubwa nae anatonesha kidonda 🤣🤣🤣S2 episode 6
Dah nilitafakari sana nikapata mawazo makali sana, nikawaza maisha na Mary kule dar, nikamuwaza Samira, nikawaza nimekuja kuingia kwenye balaa gani tena, uzuri napenda sana kua mtulivu kwenye situation za kupanic mpaka leo ndo niko hivyo, nikawaza sana nikajilaumu nimemtia mimba binti ambae simjui vizuri, mbaya zaidi nishaenda na kujitambulisha kwao, nikawaza sana kuhusu huyu mwanangu tumboni, badae mawazo yanakuja ni wangu kweli au? Yaani nikawa sielewi tu
Nikarudi home usiku kufika napokelewa sina hata furaha, nikampa simu yake akawa kafurahi kweli anasema ngoja nichukue na picha zangu za zamani,mi hapo namchora tu npo zangu kimya, kanipakulia nikamwambia tumbo linauma siwezi kula basi ananibembeleza hapo sina hata hisia wala amani mpaka muda tukaenda kulala, akataka tusex namuambia tu tumbo linasumbua, akaja pitiwa na usingizi, mi hapo siwezi kulala, huwezi kuamini kuanzia hapo nilipatwa na tatizo la kutopata usingizi mpaka leo linanitesa, nikaanza kumuangalia akiwa amelala, ni binti mrembo, nikaanza kuwaza zile sms, natamani hata nimnyonge!! Ila bado nawaza hiki kiumbe tumboni, au nimconvince atoe mimba nimpige chini, ntampa sababu gani, basi tu mawazo hayaishi
Nikatoka nikaenda sebleni nikamimina pombe nikaanza kunywa huko( mpaka leo nina utamaduni huwezi kukosa pombe kwangu hata kama sio za bei lakini lazima niwe na stock ndani)... Mawazo kama yote sielewi cha kufanya, sasa sijui kwanini nikawa namkumbuka sana Mary nikiwa nimelewa, Samira ikawa rahisi kumsahau labda kwa kua hatukua pamoja kwa muda mrefu, nikashika simu nikampigia Mary ikaita weee haikupokelewa, nikaachana nayo, nimekaa sebleni Rachel mara kanifata,
"Mume wangu mbona huku tena usiku na hio pombe na tumbo kulikoni"
Nikamwambia nina kiporo ofisini nataka malizia alafu nakunywa kidogo labda tumbo litakaa sawa, basi akaja pale ananibembeleza na nini hapo nawaza zile sms, nawaza ile clip yaani napata hasira basi tu, badae akarudi kulala nikawaza nikasema ntapata jibu tu hakuna haja ya kupanic
Kesho nikaenda kazini kama kawaida, natoka nikapita pale golini kwake nikampa hi tukawa tunapiga story tu pale, mara mezani nikaona ile simu niliyomrekebeshia nikamuulizia ulipata picha zako za zamani akasema ndio, basi nimekaa pale nikazuga zuga badae nikashika ile simu kuchungulia nakuta sms zote zipo tu kama jana, hajafuta hata kitu, moyoni nikasema huyu binti tofauti na umalaya mbona tena ni kama hamnazo, ni ujinga au kiburi? Yaani ushahidi wote wa ujinga wake anaacha tu na anajua naweza angalia muda wowote..... Nikajisemea moyoni... Karibu uswahilini patrick
Hasira zikapanda pale tena nikaaga nikaondoka zangu, mi huyo mpaka bar nikanywa kidogo nikakumbuka Mary alinichek sikumjibu ikabidi nimpigie, tukapiga story tu pale nikazuga nipo sawa wala hakuna shida yoyote basi badae nikarudi home siku ikaisha
Kumbuka hapo bado nadaiwa laki 3 kwa kina Rachel ambayo sikumalizia, nawaza hapo nipeleke au niachane nayo tu, nikawa najiona mjinga yaani mimi ndo naenda kulipia K ambayo watu washacheza nayo kiasi kile nikasema dah! Si niliacha K za maana dar nikakimbilia huku, acha nikome sasa
Ujinga sasa, badala kipindi cha mwanzo ndo ningeanza kumdadisi Rachel nikajikuta sa ivi ndo naanza kumhoji kuhusu maisha yake, ndo akaniambia baba yao aliwakimbia wakiwa wadogo, na yule mdogo wao wa mwisho ni mtoto wa baba mwingine, anadai baada ya kumaliza la saba hakuendelea na shule, na alipofikisha miaka 16 ndo akahamia kwa yule rafiki yake mwenye mgahawa akaanza kujitegemea, sasa nikawa namuuliza unajitegemea kwa kazi gani sasa akawa anajiuma uma akilini hapo najiambia patrick acha ujinga kwani majibu huna
Mama mkwe nae hapo alishakua free ananipigia simu tu tunawasiliana kama kawaida na nyumbani akawa anakuja freely tu, nikapanga siku nikaenda kumalizia ile laki 3 lakini safari hii nilienda na baba mkubwa(hakuwepo awamu ya kwanza).... Tukafika tukamkuta mama mkwe,Rachel na mzee mmoja safari hii hapakua na maongezi sana tukalipa ile pesa tukala pale maongezi kidogo tukaondoka
Tukapita mahali nikawa nimekaa na baba mkubwa mara from nowhere ananiambia
"Tatizo lenu vijana mnaharibu kwanza ndo mnakuja kutushirikisha, yule binti kama angekua hana mimba ningekushauri uachane nae tu"
AU ni saa9 na nusu usiku mkuu tulale kidogoWakuu samahani leo nilikua safari, saa 3 na nusu ntaanza kuziweka ntajitahidi leo ziwe ndefu
MmhWe G hujambo?
🤣🤣🤣 Umpe milion 3 na Mtu alikuwa anauza matunda huko umemkomboa umemuweka ndani so anajikuta mko level Sawa , imagine umeanza Ujenzi badala mwanamke akupunguzie majukumu ili ujenge ndio kwanza anaomba mtaji wa biashara wtf 🚮S2 episode 10
Mama namjua nikampotezea tu japo nafsi yangu ilikua inaniambia kile kile ambacho kilikua kipo moyoni mwangu, lakini kitendo cha kuendelea kufanyiwa kiburi na Rachel ch kugoma kuja nyumbani hata wageni walipokuwepo nikasema hakitapita hivi hivi, nikasema ni muda muafaka sasa wa kuacha kujifanya kijana mwema sana, mimi huyo sasa nikakata mawasiliano na Rachel pamoja na mama yake, yaani hivo tu, simu sipokei, sms sijibu, hakuna cha matumizi wala nini, kitu pekee nachokumbuka kutuma tena namtuma mtu ilikua pampers za mtoto, sabuni za kufulia, mafuta ya mgando ya mtoto na wipes!! Nikitoka kazini nachelewa kurudi nyumbani basi tu nikaanza ratiba mpya nazojua mimi
Wakalalamika sana kwa sms lakini wapi mi npo kimya tu, wanakuambia dawa ya jeuri ni kiburi, imepita kama mwezi siku natoka zangu kazini nafika nyumbani namkuta Rachel yupo na mtoto, mama mkwe na mdogo wake(Grace) wananisubiri, nikajifanya kama sijashtuka wala nini nikafungua nikawakaribisha ndani, basi na wao wakazuga kama hakuna tofauti yoyote tukawa tunapiga story kawaida badae nikamwagiza boda akaleta mahitaji pale wakawa wanapika mi nikatoka nikawaacha pale, nimerudi badae mama mkwe kashaondoka yupo Rachel na mdogo wake
Rachel ndo akawa karudi sasa kwa style hio maisha yakaendelea badae tukawa sawa tu ila ndo hivyo ukishakosa imani na mtu mnaishi kwa machale tu sana, kufupisha sana mambo japo katikati hapo ugomvi haukosekani, mtoto ndo ana kama miezi 9 ivi, ikatokea nafasi kazini za kwenda training nje, mwanzo sikutaka kwenda ila kuna bosi wangu akanishauri niende nikirudi anaweza nibadilisha kitengo chenye maslahi zaidi, nika apply zile nafasi nikakaa kimya kusikilizia majibu maana waliokua wanataka walizidi nafasi zilizotolewa
Baada ya kama mwezi majibu yakatoka nimepata nafasi ila kuondoka ilikua kama baada ya miezi miwili, na kule ni kwenda kukaa wiki 8, nilivyoona posho ambayo tutakua tunalipwa kule nikaona si haba nikapata msukumo nitafute eneo ninunue nijenge hata msingi kabla sijaondoka, nilikua na akiba yangu fulani kweli nikafanya mpango nikapata kiwanja kikubwa tu pembezoni kidogo ya jiji nikaanza kujenga msingi kimya kimya hapo sijamwambia mtu wala hata sikuona sababu....
Hapo swala la safari wanalijua sema muda bado ulikua haujafika, sasa kuna notebook moja nilikua naandika mahesabu ya site ili co monitor cost Rachel akaja kuiona akawa ananiuliza hayo mahesabu ya nini, nikamwambia kuna mahali nimenunua najenga msingi huko, akakaa kimya ni kama mtu ambae hakufurahishwa maana hata hakuniuliza ni wapi, mchana npo kazini napata ujumbe toka kwake nae kaandika business proposal yake sijui biashara gani anataka milion 3 kabla sijaondoka ya biashara yake, nikamjibu tu plain sina pesa kwa sasa huoni kama najenga
Aisee ni kama nilipalilia moto, huyu binti kumbe alikua na mdomo sana nilikua simjui vizuri