😂😂 haina presha hiyo mkuiNa unaifuatilia tu, achana nayo ulale mkuu, Mwandishi tunakusubiri tumalizie
Ba mdogooooooooo 😂😂😂😂😂
Bila picha ya ba mdogo huu Uzi ni batili mana ametisha sana.
Endelea basi tushajifunza vya kutosha hususan sisi wenye BK 😅😝😅Vyovyote watakavyoona tu mi sipo kumfurahisha mtu hapa, naamini kuna watu wanaweza kujifunza kitu Kwa niliyopitia mimi
😀😀Mbona kidume!S3 epi 11
Sms ya mama huku nikaachana mayo kwanza, shauku kubwa nataka kujua kimejiri nini kule Kwa ba mdogo, nikampigia Simu, akaikata.... Imepita kama dakika katuma sms "Mzee tulia kwanza ntakupigia, hapa ni kama tupo msibani"
Dah nikasema hiki nini tena, nikaanza ku speculate tu pale labda kimetokea hiki, labda kile basi tu mawazo hayaishi, nawaza nimchek G? Mbona ye hajanitafuta kama Kuna shida? Nikasema hapana utakuta yupo nao ntachochea moto
Sijakaa vizuri sister yangu anapiga( hio siku ilikua majanga tu).... Nikawaza huyu kashapewa umbea, ila huyu nammudu, nikapokea..... Akaanza kucheka..... "Hivi dogo una shida gani aisee? Au mganga wako kakuambia lazima uoe pale?"
Hapo namwambia "acha hizo wewe hebu tulia hapa yenyewe Nina majanga mia kidogo, mama Yako mwenyewe najua Leo sitalala ataongea mpaka kesho"
Akaendelea " ndo katoka kunpigia hapa anashangaa tu, ila dogo na wewe kiboko aisee Sasa ndo umefanya nini?"
Nikamwambia hebu tulia kwanza kichwa kikitulia tutaongea vizuri nikakata Simu, hapo Simu ya maana naona ni ya ba mdogo tu Hawa wote ni kama wananipotezea muda tu
Ikapita kama Lisaa ivi ba mdogo ndo ananipigia Sasa.... Napokea anahema kweli badae akaanza kucheka, namuuliza unacheka nini Sasa Kuna nini huko? Akaanza " we Mzee mwenzangu tunaheshimiana Sana, mbona umeniingiza kwenye msala mzito hivi? Hapo simuelewi na anavyocheka Sasa ndo ananichanganya tu, nikamwambia hebu acha mafumbo basi niambie imekuaje huko mbona sikuelewi, akaniambia ngoja nitulie basi Mzee tupo na huyu Mzee tuagize hata chakula na kinywaji maana kule hatujalamba hata maji
Hapo namuambia sawa agizeni tu ila niambie basi kwanza Kuna nini, akaanza Sasa
" Unajua Mzee hii ishu tulikua tunachukulia simple Sana ila imekua tofauti kabisa, hapa Mzee mwenzangu umeharibu Sana sijui hii Ngoma tutaicheza vipi'
Ndo akaanza Sasa kuniambia kilichotokea, wamefika pale wamepokelewa vizuri tu, akaletewa mtoto pale amekaa Kaa nae, G yupo jikoni ba mdogo anavyopenda misosi Sasa anasema anaskia harufu tu akajua hapa mambo mazuri, Ile kuzuga zuga ndo Sasa akaanza kujielezea na yule Mzee, Sasa Hawa jamaa nao sijui walivyopita bar kabla ya kwenda walishauriana nini bana, katika kumuelezea mama mkwe eti badae wanamuambia "kijana wetu naona ameamua kuzidi kuuanganisha undugu kabisa"
Mama mkwe anawauliza kivipi, ndo wakamueleza Kila kitu, naskia mama Wala hata hakuonyesha kupanic, akamuita G, G nae anakuja anashangaa tu pale amekaa ameshika Simu, mama hapo akawa mkali akachukua Simu, anamwambia we unaitwa na watu wakubwa upo busy umeshika Simu mbona huna adabu, akamnyang'anya Simu pale..... Akamgeukia Sasa G anamuuliza mwanangu nimepewa taarifa hizi na hizi, je ni za kweli? G akaitikia Kwa ishara ya kukubali Kwa kutingisha kichwa
Aisee naskia mama alipiga ukunga mmoja hatari Sana, akaanza kulia pale, anaongea mambo hayaeleweki, badae majirani nao washajaa, wanamuuliza vipi Kuna msiba mama Fulani? Mama hajibu analia tu, G nae hapo kaingia mitini sijui ndo alienda chumbani, Sasa mama analia tu hasemi nini shida majirani wanazidi kujaa....
Badae Kuna jirani akawageukia kina ba mdogo Sasa na yule Mzee "nyie wazee mmemfanya nini huyu mama?"
Hee msala ukageukia Sasa Kwa kina ba mdogo, watu Wana hasira wanawauliza nyie kina nani kwani mmemfanya nini huyu mama, hapo yule Mzee aliyeenda na ba mdogo akawa anatetemeka tu, anamwambia ba mdogo hapo mambo yashaharibika hapa dawa ni kuingia socket(kukimbia) tu....
Kuna majirani wakamkokota mama mkwe Sasa wakaenda nae kwao huko kumtuliza, ba mdogo ndo anawaambia majirani sisi ni wajumbe tu Kuna habari tumezileta Kwa huyu mama naona kidogo zimemchanganya tutakuja wakati mwengine, majirani nao Sasa wanataka kujua ni habari gani(watu wambea Sana)..... Ba mdogo akawaambia ni mambo ya kifamilia siwezi kuliongea hapa, basi wakaaga wakaondoka
Basi tukaongea pale, nikamwambia sawa nyie kuleni tu na huyo Mzee usisahau kumpa posho yake Ili kama ikitokea Kuna kurudi tena asije akakataa, ba mdogo nae Sasa "huyu Nampa posho kidogo, jinsi jasho lilivyokua linamtoka, huyu hawezi kurudi kule hata Kwa fimbo"
Nafanyaje Sasa? Nikapiga Simu ya Grace haipatikani, mama mkwe na Rachel Hawa waache waendelee kukaa blacklist kwanza mpaka Nije nipate plan nyingine....
Nikakaa pale mpaka badae nikarudi home namkuta mama amekaa nje Bado wapo na yule mama jirani Sasa, kuniona tu akaanza
"Naona kidume ndo kinaingia"
Nataka nijaribuWe zuga tu kama huelewi
ⱨ₳ⱨ₳ⱨ₳ⱨ₳ ʉ₮₳₴ⱨ₳₦₲₳ⱬ₩₳Nataka nijaribu
Jana nilikuwa saluni wakawa wanapiga story za shisha akaniuliza kma nimewah kutumia shisha nikamwambia sijawah hata kuiona live naona kwenye mitandao walicheka sana
Ngoja nijaribu hata Bangi niwe wa mjini Sasa😀
Et sterling😀😀😀S3 epi 14
Akili ikanituma hapa nisipanic wala nini, nikatoka nje Sasa, ba mdogo nae Sasa yupo nyuma yangu, nafika nawauliza " vipi tena mbona huku Kuna nini?" Sijakaa sawa Rachel huyo kashanirukia, kanishika akaanza kupiga kelele Sasa " we mwanaume umalaya wako ulishindwa kufanyia kwingine, najuta Sana hata kujujua... Mama anakufa Kwa sababu yako mshenzi wewe"
Sasa katika kitu sipendi ni kushikwa na mwanamke ile kama kibabe, Mila zetu zinakataza kabisa kuanzia tukiwa wadogo baba akikuona umekabwa na mwanamke alafu unashangaa tu lazima badae upigwe bakora, kwetu ilikua marufuku kabisa mwanamke kukukaba, likaja wazo Sasa hapo nIshapata hasira nawaza huyu nimpige kichwa au, ila nawaza kuna shangazi kule, ba mdogo ye ataelewa tu, sijui ba mdogo ni kama alishtuka akaingilia kati haraka, Sasa kelele zile shangazi nae huyu na G washatoka nje.....
Sasa sijui ni hasira au nini, Rachel anaropoka tu " kumbe huyu Malaya wako umekuja kumficha huku(yaani utasema sio mdogo wake)..... Shangazi nae hapo kaanza nyie kwani Kuna nini huku, nikaona Sasa hapa nipo kwangu Hawa wasijaribu kunletea ujinga hapa, kama kuharibu nishaharibu Sana Sina Cha kupoteza tena, Kuna jicho nikamkatia Rachel, uzuri ananijua Kuna siku nilishampiga kama mbwa mwizi, nikamwambia sitaki kelele kwangu, alafu nikamwambia haya mambo wewe hayakuhusu ukitaka kunitafuta nitafute tuongee mambo ya mtoto tu tofauti na hapo acha kuingilia mambo ambayo yamekuzidi uwezo
Tukalumbana pale, shangazi anawabembeleza Kina Rachel waondoke anawaambia ntakuja huko nyumbani tuongee, haikupita muda wakaondoka zao, tunarudi ndani G huyo mpaka chumbani, nafika nakuta analia anasema mimi Bora nijiue tu, hapo nikaona hapa ni kwenda ki askari tu, nikamwambia na we toa ujinga wako hapa, kwanza Simu ipo wapi? Ndo ananiambia hata sijui kuanzia Ile siku mama anachukua, basi nilikua na visimu vidogo ndani nikatoa kimoja na kuna laini nilikua natumia kwenye modem nikamtolea nikampa, Sasa huyu Binti nae alivyo mjinga nae anaanza kunilaumu, eti kwanini nilituma watu kwao bila kumuambia, nikawa namshangaa tu pale maana ye ndo alikua ananitisha kumuambia mama yake
Basi tukarudi sebleni ongea Sana na shangazi pale wakaaga wanaondoka, unajua familia zetu za kibantu lazima hapo utoe posho tu utasingizia hata nauli huwezi kumuacha mtu hivi hivi, tena huyu naona kabisa nimepata mtetezi, G nae nikampa balance kidogo tukaagana wao wakaenda
Ba mdogo nae huku kashaanza kuingiza miss(kuogopa).... Ananiambia Mzee tuwe makini haya mambo mbona kama ni magumu Sana, namwambia Mzee tulia mambo yatakaa sawa tu, siku hazigandi ikafika siku wale wazee wakafanya tambiko lao huko sisi tulitoa sababu kama mia hivi si mimi Wala ba mdogo alijaribu kusogeza pua huko....
Mimi huku G naongea nae tu vizuri, Rachel nae Kila siku atatumia Simu mpya kunitukana nikawa nishamzoea, Sasa wale wazee wakaja kutuita na ba mdogo, ba mdogo akaniambia mwanangu tusiwe mafala Hawa tukutane neutral ground tu( tukatae kwenda kwao) maana huwezi kujua wamejipangaje.... Akawashawishi pale tukutane sehemu nyingine badae wakagoma hapo wanasema hatuna heshima tunawaita mnaanza na kutupangia sehemu ya kukutana
Basi bana Kwa tahadhari Sana tukaja kwenda sehemu waliyotuita, hio siku haikua hata kikao aisee ni kama walikua wanatupa taarifa tu ya walichoamua wao, Sasa hapo nakutana na mahari kwanza Kwa akili ya mtoto(D), faini ya kumpa ujauzito G, faini ya kuwapa ujauzito mtu na dada yake, faini ya kutokuja kwenye tambiko, faini ya kimila sijui inaitwaje nimesahau jina lake la kilugha, mwisho kabisa mahari ya G..... Ukipiga mahesabu Sasa ndo tukachoka, unajenga ki nyumba kabisa..... Na zote zinatolewa Kwa pamoja hakuna Cha installments Wala nini
Sasa ba mdogo akawauliza vipi mama wa huyu Binti (G) mmemshirikisha na karidhia na haya mnayotuambia? Hapo Kuna kizee kikapanic " sisi ndo Kila kitu, mnatakiwa kufanya Kila kitu tutachosema sisi, hiki kikao mpo na wazee zake wewe unauliza maswali kuhusu mwanamke tena"
Tukaomba tukajipange tukapewa muda zisipite siku 21, tukaaga tukaondoka, njiani ba mdogo ananiambia Hawa wajinga hio Hela si unajenga kabisa ka nyumba kazuri wanatuona sisi mafala sio, alafu Hawa kama hawajamshirikisha mama hamna kitu, tutapigwa hela hapa kesi ibaki pale pale tu.... We si umeona wazee wenyewe wajanja wajanja
Basi sisi hao tukapita zetu bar agiza chakula pale gambe kidogo tunapeana faraja tu, mara sms kwenye Simu yangu namba mpya "mimi mama Yako(mama G Sasa) kesho uje nyumbani ila uje mwenyewe huyo baba Yako asije"
Nikamuonyesha ba mdogo Sasa Ile sms, nae anavyojikuta Sasa, akaniambia waache ujinga hao hakuna movie linachezwa bila sterling kesho mguu Kwa mguu tunaenda wote
Kuku wa kiswahili wa kizungu uliwaona hawanogi kaka 😂😂S2 episode 2
Sijakaa sawa dada wa mgahawa anapiga tena, " Shem upo wapi?" Nashangaa huu ushem wa lini tena, nikamuelekeza nilipo akaniambia tunakuja akakata simu. Baada ya muda kweli nawaona huyu hapo na rachel, Rachel amevaa kigauni flani ivi amejibeba kweli kweli, yule dada wa mgahawa alikua mcheshi sana akafika akaniambia " haya mtu wako huyo hapa mbembeleze mwenyewe mi nimechoka"... Nikamvuta rachel namuuliza kuna shida gani akaniambia tu we futa hio picha ndo tutaelewana, basi bana wakala pale na vinywaji kidogo yule dada wa mgahawa nikamuambia tafuta usafiri wako mapema sisi leo hatujamaliza kubembelezana... Rachel ni kama alianza kusita ila badae akakubali tukaenda kulala wote kwangu hio siku safari mpya ya mapenzi ikaanza
Kuhusu rachel sasa, ye aliishia la saba, kalelewa familia duni na mama tu na ana wadogo zake wawili mmoja wa kike alikua form 1 bado mwingine wa kiume mdogo yupo la pili, mama yake nae kazi haieleweki yani ni kujishkiza hapa na pale tu, basi tukaanza penzi la rachel sijui hata niliwaza nini miezi mitatu tu ya kwanza mimba tayari, hapo nimemchunguza kidogo sana ila nikasema sawa tu, akawa anakuja kwangu anapika, anafanya usafi kuna muda ni kama alihamia tu kwangu kabisa
Tofauti sasa nikaanza kuiona rachel kwao ndo tegemezi kwa hiyo bills zote nikawa nalipa mimi kupitia yeye, mara sijui ana michezo anadaiwa, yaani vitu ambavyo sikuzoea kutoka relationships za nyuma, ila nikawa siwazi kwani financially nilikua sipo vibaya na nawaza huyu anabeba mtoto wangu sitaki apate stress, sasa kuna siku nipo kazini, ikaingia sms namba mpya "mwanangu mna mpango gani na mwenzako na hio hali yake mtakuja lini kujitambulisha?"
Nikawa kama sielewi elewi hivi, jioni nikamuuliza rachel hii namba ya nani akaangalia akasema hii ya mama nilimpa namba yako, nikabaki nashangaa, nikaanza kuona red flags, mbona kama uswahili sasa huu, mama mkwe anaanza kuntafuta mimi alafu tena kwa sms, nikasema something is not right hizi familia nazoingia huku nitanyooshwa tu
😅😅😂😅😂 𝕙𝕒𝕨𝕒 𝕨𝕒𝕫𝕖𝕖 𝕟𝕚 𝕧𝕚𝕓𝕠𝕜𝕠badae wakagoma hapo wanasema hatuna heshima tunawaita mnaanza na kutupangia sehemu ya kukutana
Kama ungekuwa huna fedha ungekufa vbaya weweVyovyote watakavyoona tu mi sipo kumfurahisha mtu hapa, naamini kuna watu wanaweza kujifunza kitu Kwa niliyopitia mimi
Kwa kipi Sasa?Kama ungekuwa huna fedha ungekufa vbaya wewe
Shusha vitu mkuuhakuna movie linachezwa bila sterling kesho mguu Kwa mguu tunaenda wote