Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Umetisha mkuu.
 
We kenge Mimi sio njaa kama wewe hivyo vipesa ulivyotaja havifiki hata hii niliyonayo kwulivyotaja usione Kila anayepinga jambo ni njaa kama wewe
IMG_0612.jpeg

Unataka ushindani zaidi tujuwe nani mwenye njaa hapa?.
 
Nimesoma mwanzo hadi mwisho,ila inaonekana ulikuwa unafanya blander nyingi sana.Mfano huyo Merry ulipuzia mpaka akafikia hatua hiyo kwa uzembe sana.
Mke wa ndani ukisha ona kitu hakipo sawa,una msikizia day 1 ikifika day 2 bado yupo hivyo hivyo unapiga pumbu anasahau mambo yote.Ndivyo ulitakiwa ufanye kwa Merry.

Issue ya kuwapa mimba mabinti wa 2 wa Mama moja wewe sio wa kwanza inatokea kwa wanaume wengi sana,hasa pale wadogo wa kike wa wife wanapokuja kumtembelea ndugu yao ila watu huwa wana solve yanakwisha.
Huko huko Mwanza kuna jamaa alioa Mtu na Dada yake mapacha ilitokea Issue kama hiyo.

Kuhusu huyo Grace,kwa kuwa ulikuwa na mawasiliano mazuri na Mama yake ulitakiwa umuite uongee naye wewe mwenyewe 2 tu kiutuuzima mngekubaliana yangeisha-kisha ungemuoa Grace mambo yanaisha.

Huyo Mama kilicho Muuma na Issue hiyo kujulikana na watu wengine-hivyo amepata aibu.mngemaliza yeye na ww hata kusingekuwa na Issue.
sAwa kabisa,anayakuza mambo naona umri nao ulikuwa tatzo
 
S3 epi 10


Mama namjua akianza kuongea hamalizi Leo sikumjibu chochote nikampotezea, kesho yake Sasa nawasiliana na ba mdogo yaani tunapanga mbinu utasema tuko vitani, kwanza akaniambia amefanya mawasiliano Kuna mtu kampata mwanza Mzee mmoja wa kwenda nae, akaniambia yule Mzee wa kwanza tulieenda nae wakati wa kujitambulisha Kwa Rachel hafai, anadai yule ni mlaini Sana hii vita hatoiweza inahitaji makamanda kweli, hapo mimi simbishii kitu chochote nipo kimya maana nilishamuachia msala apambane nao....



Ba mdogo akaja Sasa na idea Moja, operation ya kuua ndege wawili Kwa jiwe Moja....

Akaniambia hapa inabidi tulipue mabomu kotekote ibaki tu kazi ya kukabiliana na madhara yatakayojitokeza, jumapili akienda Kwa mama mkwe na mimi huku nikae na mama nimuambie tu Kila kitu, maana hata nisiposema akasema mama mkwe ni lazima tu atampigia mama, hapo Sasa naona nimeruka nimejichanganya tu, mama yangu namjua ataongea mpaka nyumba ipate ufa, ila nikiwaza msala wa mama mkwe kule naona Bora nipambane tu huku kule ni kwa moto zaidi, hapo Rachel yeye Bado Sasa, nawaza huyu nae hawezi kuacha ipite hivi hivi lazima tu ataleta vita ya aina yake,



Hua sifanyi kitu bila ya kua na plan b, nawaza haya mambo yanaweza yakaenda tofauti kabisa na tunavyotarajia hivo plan b yangu ni kua nikiona mambo yameharibika Sana nifanye mpango mtoto nimlete huku Kwa mama maana nilihofia Rachel anaweza pata sababu ya kumchukua mtoto....... Nikishamleta huku mimi Sasa nibaki nipambane na lolote litalokuja



Usiku wa deni haukawi kufika, jumapili hio hapo, nipo busy na askari wangu( ba mdogo) tunapanga mipango wa mwisho, nikampa idea usiende mikono mitupu nunua zawadi za mama mkwe na mtoto kwanza mpate hata pa kuanzia mkienda, Sasa ba mdogo hii ishu yeye anachukulia simple tu yaani anasema " hii ya Leo Haina Cha zawadi Wala nini, Leo tunaenda uwanja wa vita zawadi za nini tena"


Mimi huku swala la kumuambia mama likanishinda, Kuna rafiki yake mmoja mama mtu mzima Sana tulikua tunatenganishwa na ukuta tu huyu mama alikua mcheshi na simple Sana, nikawa nimeshamuambia majanga yote nikamwambia jumapili we njoo umueleze tu huyu Mzee mwenzako akasema hakuna shaka.........



Hio siku yule mama kafika Sasa home, tumekaa Kaa pale ikabidi mi nizuge nikatoka zangu nimuache Sasa afikishe msala huku, nimetoka nimekaa bar Moja nampigia ba mdogo kujua kafikia wapi, anapokea anauliza vipi wewe uko wapi? Namuambia npo bar hapa natuliza kichwa kidogo, jamaa nae anacheka anasema na si tumepitia hapa tunapiga Moja Moja kwanza hii vita sio ya kwenda ivi ivi


G hapo tunawasiliana kawaida ila sijamwambia chochote asije akavujisha taarifa akaharibu, ikafika muda ba mdogo ananiambia wapo njiani wanakaribia kufika....


Mimi ni nani??

Nikachukua Simu yangu, mama mkwe nikamtupia kwenye blacklist, Rachel nae nikamuunga huko huko.... Hapa nasema mpaka nipate kwanza feedback kutoka Kwa ba mdogo ndo ntajua Cha kuongea nao....



Basi wao wakafika kule hapo tukaacha kuwasiliana, hapo Nina mawazo najiuliza mbona nimejiingiza kwenye matatizo kiasi hiki, upande wa mama Wala siwazi Sana najua tu atasema mpaka nikome, huku Sasa Kwa mama mkwe.... Nikakaa pale yaani navyosubiri Simu ya ba mdogo ni sawa na mtu ammepeleka mwenzie labor anasubiri ajifungue




Nikiwa nashusha bia taratibu pale, mama yangu akaanza kupiga nikawa kimya tu Wala simpokelei, akapiga kama mara tatu mie kimya tu.... Nakaa kama dakika 10 naona sms kutoka kwake


" Hivi wewe hizo akili zako umezitoa wapi , mbona baba Yako hakua na akili kama hizo"


Nikawaza hapa bomu la kwanza lishalipuka...

Sijapata hata muda wa kuwaza ba mdogo nae anatuma sms

" Mzee hii Ngoma nzito, tushachemka huku"
Ba mdogo kashachomoa betri
 
Back
Top Bottom