S3 epi 12
Mama namjua hata hanipi shida Sana, alivyosema hivyo yule mama jirani Sasa akaanza " na we muache kijana wangu bana ", akaniambia njoo tukae hapa, kufika akaanza Sasa kujisemesha.... " Ila sio mbaya kuliko kuja kurundika watoto Wana damu tofauti tofauti wanakua na tabia za ajabu ajabu tu, Bora hata Sasa tupate wajukuu wengine hapo hapo"
Is this supposed to make me feel better? Hapana!!! Bado Nina mawazo makali Sana hapo, kuja kumcheki maza nae anankata jicho tu, akaanza
"Uzuri mimi kipindi kile mlivyokua mnaenda kuoa na baba zako bila kunishirikisha nilikuambia kabisa yatayowapata msinihusishe, na wewe una baba wengi tu ila kutwa unafanya mambo Yako na hao ambao hawana akili maana mnajuana akili wenyewe"
Nikaona Hawa wananchanganya tu nikaaga nikaingia zangu ndani, kufika ba mdogo nae anapiga, ananiambia Kwa aina ya huu msala we rudi tu huku tuunganishe nguvu maana huku Kuna balaa, nikamwambia siwezi kurudi mwanza mpaka nipate plan kwanza, yeye aendelee kupambana tu huko, hapo naanza kumwambia mimi huku nimemaliza kazi yangu wewe kilichokushinda ni nini, ananiambia " we Mzee huku ni pa moto mpaka yule Mzee niliyeenda nae alitaka kukimbia" nikamwambia acha niwaze Sasa tutajua Cha kufanya....
Hapo Simu ya G haipatikani nikaamua nitulie tu Sasa nafanyaje, nikapata wazo la kumpigia yule dada wa kazi wa mtoto nikasema hapana hapa ntaharibu anaweza kua na mama mkwe acha kwanza nikae kimya
Zinapita dakika, Simu inaita, kuangalia anapiga yule dada ya mgahawa rafiki yake na Rachel wa kipindi kile, hapo tulikua tunaongea nae Kwa nadra Sana, nikasema eeheee hapa pamekucha, nikapokea pale tukaanza salimiana analeta story za hapa na pale hapo namsikilizia tu najua Hana jipya itakua ni mambo ya G tu, basi badae anaanza Shem uko wapi? Nikamwambia nimesafiri, anasema Sasa "Shem ndo umefanya nini tena huku? Rachel kanipigia analia anasema mama yake ana Hali mbaya naona umeamua kumuua mama yake Sasa" .... Hapo nashangaa tena, mimi tena namuua mama yake?? Tukaongea pale ananiambia Rachel kesho anakuja huku..... Nikamwambia sawa hebu niache nipumzike kesho nikipata wasaa ntakupigia tuongee tukiwa tumetulia
Hapo nawaza Sasa ndo nimefanya nini? Mbona Kila kitu kinaenda ovyo tu, nawaza huyu Rachel akija atamfanya nini G? Huyu si anaweza hata kumpiga mpaka mimba itoke, akili ya kurudi mwanza inanijia, ila Sasa naenda kufanya nini Sina hata plan kabisa.... Nikasema acha ntajua
Hio siku sikulala, umiza Sana akili, badae nikapata wazo, katika wale wazee tuliowakuta tulivyoenda kujitambulisha Kuna wawili tulibadilishana namba, mmoja hakuwahi kuntafuta ila Kuna mmoja ni Mzee wa makamo Sana aliniambia Rachel ananiita mimi Babu, Sasa huyo Mzee Kuna kipindi nipo kazini aliwahi kunipigia akaniambia mwanangu jino linanisumbua nisaidie Hela nikalitoe, nakumbuka nilimtumia pesa kiasi, hio siku jioni nikarudi nikamwambia Rachel, akachukia kweli akaniambia Hawa nawajua ukiwaendekeza shida zao zote utakua unapewa wewe, akachukua Simu akawablock wote wawili
Ambae hafai Leo, ipo siku atafaa tu, kesho yake ikabidi Sasa yule Mzee nimtoe kifungoni(blacklist) nikampigia nikamkumbusha pale akawa kanikumbuka, nae anasema alipoteza Simu nikasema afadhali asije kua alikua ananipigia Simu inadunda, basi sikumwambia chochote nikamwambia yule rafiki Yako( ba mdogo Sasa) yupo mwanza mimi nimesafiri alisema akuone akusalimu kabla hajaondoka akasema sawa, badae nikamtumia yule Mzee kama elf 50 hapo sijamwambia kwamba Nina msala mwingine na mabinti zake, nikasema huyu ngoja nimuweke karibu badae anaweza kua msaada kwangu
Ba mdogo nae namcheki, ndo Nampa plan b, akaonane na yule Mzee mahali, wapige zao vyombo badae tu ndo amueleze Sasa, maana swala la kurudi Kwa mama mkwe lishakua haliwezekani tena, huyo Mzee ndo ataenda kuongea nae Sasa, wakae kifamilia watupe jibu Sasa, ba mdogo akasema " sawa hakuna shida Bora hata maana na mimi nilikua nataka nikuambie Kwa yule mama nisingeenda tena wale majirani wakali kweli wasije wakanibadilikia"
Ba mdogo nae mission town hapo ananiambia " angalia Sasa uniongezee balance kidogo si unajua napambana" namwambia sawa kesho ntakutumia
Yule dada co worker nae badae ananipigia anauliza yule Binti(G) uliyeniletea mbona hajaingia kazini? Hapo namzuga hebu ngoja nijaribu kuwauliza Sasa, akaniambia unaona Sasa ndo shida ya kuleta watu Kwa kujuana, nikamwambia tulia ntakurudia nikipata jibu, akasema sawa
Sasa kesho ba mdogo akakutana na yule Mzee, hapo nimeweka Simu standby nasubiri wakimaliza kuongea ba mdogo aniambie mambo yameendaje, kabla hata hawajamaliza ba mdogo anatuma sms " we Mzee Fanya uje tu huku, hii kazi uliyonipa siyo ya kufanywa na mtu mmoja, hapa ndo tumejichanganya kabisa"