Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

S3 epi 13


Sasa mimi nakuaga na maamuzi yangu nikashafanya hata iweje siwezi kubadili, nikapiga mahesabu story za Kanda hizo kweli nazijua, katika kukaa mwanza Kuna msiba ulitokea wa rafiki yangu alifiwa kwao nikamsindikiza, Ile kufika center akukutana na wajomba zake pale tukaanza kupiga bia kwanza kabla hatujafika msibani, mmoja wao akazidiwa akashindwa kwenda kuzika, kesho wamekaa kikao mjomba anaambiwa lala chini apigwe viboko mjomba kagoma hapo na watoto wake wapo kabisa, badae wakatumwa vijana waende bomani kwake wachukue ngombe watatu kama faini, Mzee kuskia ivo akashuka tu chini wakamlamba viboko, hivyo kwanza nikasema hata mbingu ishuke swala la mimi kwenda kwenye Hilo tambiko siwezi kujaribu, Hawa watu swala la viboko hua ni la kufikia tu



Muda ukaenda Sasa mawazo yamehamia Kwa G, najiuliza huyu mtu yupo wapi? Hapo imefika usiku ulizia naambiwa hajaja, kazini najua hakufika maana yule dada bosi wake alinitumia sms " naona huyu Binti ni kama hataki kazi, na Leo hajaja".... Nikawaza pale nifanye nini Sina Cha kufanya, nikiwaza misala inayonisubiri mwanza nachoka kabisa



Sasa Kuna muda naona namba mpya inapiga, kabla sijapokea nawaza hapa inawezekana ni G huyu, au ukute mama mkwe au Rachel maana hao wapo blacklisted, au ni mtu mwingine tu, nikaona ngoja nipokee, nikawa naskilizia sauti kwanza mbinu za kibaharia, nikaja kujua ni Rachel... Nikakata simu



Nakaa kidogo zikaanza mvua za sms Sasa.... Lawama kama zote, mara nataka kumuua mama Yao, yaani maneno kama yote naonekana mimi ndo Malaya Dunia nzima, ila Sasa paliponichosa zaidi akaniambia kuanzia Leo hesabu huna mtoto tena na mimi, D naondoka nae na hutokaa uje umuone tena labda nikiwa nimekufa, ukitaka hata mahakamani tutaenda..... Nikasema mbona hili balaa Sasa, hapo nikapigwa na biti akaniambia " yaani we dawa Yako Iko jikoni ni swala la muda tu utanitambua vizuri"


.

Nikawaza sasa huku nafanya nini, mbona kule mambo ndo yanazidi kuharibika, G nae yupo wapi? Nawaza mtoto kweli akiondoka huyu Rachel naanza kumtafutia wapi, nikakata shauri hapa inabidi nirudi mwanza tu nikapambane na hizi ishu maana kukimbia sio suluhisho kabisa



Nikatoka zangu pale Kuna bar nikaenda piga piga gambe pale, narudi Nina mawazo Sana... Navuta hisia za nyuma naona kama nimeharibu maisha yangu mwenyewe, sijui nikapata hisia gani bana, nikachukua Simu nampigia Mary mara upande wa pili inapokelewa naskia sauti ya kiume, naambiwa huyu kapumzika mpigie kesho!!! Basi tu Kuna ka roho flani ivi kakaingia nikajiskia vibaya nikasema maisha ndo hivo lazima yaendelee



Kesho yake napiga plan jinsi ya kumuaga mama Sasa, nikaita fundi pale nikapiga nae hesabu arudishie rangi ukuta wa fence ulianza kupauka nikampa Hela za material pale, hua tuna utaratibu Kila tukirudi nyumbani na sister ni kujaribu kurekebisha chochote pale nyumbani, badae mama namuaga namwambia kesho narudi mwanza.... Akaanza kucheka, namuuliza unacheka nini we Mzee, ananiambia " hivi Kwa akili zako ulitegemea flani(ba mdogo Sasa) ndo ataenda kurekebisha ujinga uliofanya? Naona umeamua kwenda mwenyewe"


Hapo kumbuka simuambii chochote kinachoendelea, nikampotezea tu, badae akaniita akanipa zawadi za mjukuu wake tukakaa Sasa akaanza kunipa ushauri, kaniambia kua makini Sana mwanangu huko upo ugenini watu wanaweza kukufanyia Hila usichukulie mambo kirahisi nikamwambia sawa....




Kesho mimi huyo safarini narudi mwanza, njiani kuulizia si kazini Wala nyumbani G haonekani, nikasema nikifika ntajua.... Nikafika salama Sasa hapo tupo na ba mdogo tukaanza kupanga mbinu pamoja, jioni tunatoka nampeleka mahali anakataa ananiambia twende sehemu flani ndo Kuna watoto kule, nikamuambia naona ushakua mwenyeji, wewe ndo maana kazi ilikushinda unawaza watoto tu....


Sasa nafika mwanza G nae kimya tu sijui hata yupo wapi, ila nikawa najipa moyo huyu kwao watakua wanajua yupo wapi la sivyo wangenisumbua Sana.....




Wale wazee wakaja kumpigia ba mdogo hesabu pale tukakamuliwa pesa sijui ndo na Hilo tambiko, hapo namwambia ba mdogo we tutoe tu tutaona mwisho wake ni nini, akasema sawa tukapanga siku wakaja kuzichukua, Sasa kama bahati yule dada wa kazi wa mtoto nae sio mjinga alishakuja kujua nini kinaendelea pale, akaja akapata taarifa Kwa kuskia skia kumbe G alienda Kwa shangazi yake mmoja akawa amekaa huko, nikasema afadhali Sasa najua mtu yupo salama na nini



Hapo karata iliyobaki tuwasubiri hao wazee wafanye Hilo tambiko lao, wakae Sasa na mama mkwe kifamilia wao ndo watatupa jibu nini Sasa kifanyike pakawa hakuna ujanja zaidi ya kusubiri, hapo na mimi siku zinaenda nawaza hii ishu inatakiwa iishe kabla likizo haijakata...



Hapo siwezi hata kwenda kumuona mtoto yaani ni vurugu mechi tu


Zikapita kama siku 2 nipo na ba mdogo home mara G huyo kaja na mama Fulani nilikua simjui, tukawakaribisha pale ndo akajitambulisha kua ni shangazi yake( upande wa baba Sasa).... Yaani mama mkwe wanaitana wifi, Sasa tumeongea pale mimi nipo kimya hapo baba mdogo nae anajikuta ana busara muda wote yeye ndo anaongea pale wanamskiliza, Sasa sijui ndo ma wifi hawapatani au yule shangazi ni kama alikua mtulivu Sana, anamwambia ba mdogo Hawa ni watoto wetu haya yashatokea Sasa tufanyaje, ni kwenda nayo tu hivo hivo, nikasema afadhali Sasa hata na huyu



Siku ya kufa nyani Sasa.....


Tumekaa pale geti linagongwa, ba mdogo alikua karibu na mlango wa kutokea mara kainuka kaenda kufungua, badae sijui ni kama nilipatwa na wazo gani nikasogeza pazia nijue ni nani anagonga, geti kufunguliwa namuona Rachel na yule rafiki yake wa mgahawa, ba mdogo akasalimiana nao pale sijui aliwaambia nini yeye akawa anakuja wao wamebaki tu pale karibu na geti ila washaingia, jamaa kuingia ndani hakujali hata kama tuna wageni ni kama alipata wenge ivi ananiambia "mzee mwaka huu wa kwetu"
Mwaka Huu Mpk Ibirisi Atutoe Roho 🤣
 
S3 episode 15



tukapiga hesabu sasa pale na ba mdogo, Hawa mbona wanatuchanganya, tufanye kipi Sasa, karatu zetu tulishazitupa Kwa wale wazee wao ndo wamalize Kila kitu,huku tena tunaitwa Kwa mama mkwe, tushike kipi, hapo ba mdogo nikamwambia ni Bora nikamsize kwanza mama mkwe maana hata hivo yeye ndo kama atakua na maamuzi ya mwisho, kumalizana na wale wazee bila kufika muafaka na huyu mama Bado itakua kazi Bure tu hakuna la maana tutakua tumefanya...... Hapo namwambia ba mdogo acha niende tu mwenyewe maana tushawakwaza Hawa tukisema tena ndo tunaenda wote wakati mtu kashatuweka wazi kua usije tutazidi kuleta misuguano tu, ba mdogo nae Sasa " Hawa wakijua uko mwenyewe watakusumbua Sana, ndo maana mimi npo huko wajue una mtu nyuma Yako, hakuna Cha kwenda mwenyewe kwanza hatujui wao kule wameandaa safu gani"




Sasa hapo nawaza hata tukienda huko ndo kukutana na kina Rachel hapo Kuna kikao kweli au itakua ugomvi tu na kutiana aibu, G hapo Sasa nasiliana nae na ye Sasa ni kujidekeza tu anajifanya kama yeye ndo ana mawazo kuliko mimi, hapo namtuliza tu mambo yatakaa sawa, nikamwambia mama kaniita anataka nikaongee nae, akawa kama hana amani kabisa akaniambia kua makini tu kaka maana mama nae akishakutana na Rachel huwezi Jua wamepanga wakuitie nini



Kesho imefika tumejiandaa ba mdogo kashajitundika zake suti mimi hapo nimevaa casual tu, ndo tunajiandaa kwenda, Sasa bana wale wazee sijui walikua wanatuona vipi bana, labda walishajadiliana kua tumeyavuruga hivo bila wao hatuna namna tena, au kwasababu hizo pesa za tambiko tulitoa bila hata ku bargain kitu wakaona Hawa tushawashika, imagine hapo wametupigia mahesabu ambayo Kwa akili timamu ni kama hayatekelezeki mtu huwezi kulipa pesa zote hizo, alafu hatujakaa hata siku hio siku tukiwa tunajiandaa wakampigia Simu ba mdogo kua badae wanataka jibu hizo pesa zinawakilishwa lini, ba mdogo anawaambia subiri tujipange jamaa wanamuambia mahesabu tuliyopiga hayana mjadala tunataka mpaka badae mue mmetupa jibu lini hizo pesa zitawakilishwa.....




Hapo ba mdogo amekata Simu namuuliza hivi Hawa watu hata kama ni kupeleka hizo pesa tunapeleka Kwa utaratibu upi Sasa? Tunawapelekea wao? Au mama? Au vipi? Na baada ya hapo nini kinafuata Sasa? Ikabidi awapigie tena, "hizo pesa tukishapanga tarehe sehemu ya kuwasilisha ni kule Kwa mama au?" Ba mdogo anauliza, yule Mzee akaanza kujiuma uma pale Kuna Mzee mwingine nadhani alimpokonya Simu watakua labda walikua wameweka loud speaker.... Huyu Mzee Sasa hapindishi maneno 'hivi nyie kikao mmekaa na sisi, sa ivi mnauliza maswali gani Sasa, hii kesi imeshafika ngazi ya ukoo Kila kitu kinafanyika huku"

Ba mdogo akawaambia ntawarudia, wakasisitiza mpaka badae mue mshasema lini mnakuja..... Tukabaki tunashangaa Hawa mbona Wana haraka hivi....... Ba mdogo nae Sasa anaanza kunipa mbinu za kivita, ananiambia hizo pesa wanazotaja hata taahira hawezi kuzitoa, Hawa ngoja tukiona wanatuletea upumbavu we Kaa kimya endelea kuwasiliana na mwenzako(G) wao waache tuone Sasa watatufanya nini, maana naona washatuona wajinga....



Ikafika muda tumeenda, tukapokelewa pale na kijana mmoja ila tukaelekezwa Kuna nyumba nyingine kubwa ndo tuingie sio upande ule wa wapangaji( Kwa kina Rachel).... Kufika ndani tunamkuta mama mkwe Sasa ametandikiwa mkeka sebleni pale amejilaza yupo na wamama wawili, mmoja sijawahi kumuona na mwingine mtu mzima nishawahi kumuona kama mara 2 japokua hatujawahi kuongea.....




Tukasalimu pale mama mkwe anaitikia kinyonge ni kama vile anaumwa, tukakaribishwa tumekaa pale, badae yule mama wa makamo Sasa( nikaja kujua ndo mwenye nyumba) ndo akaanzisha maongezi, akaanza mbali kweli jinsi wanavyojuana na mama Rachel, alivyowaona Rachel na G wanakua na historia nyingine ndefu ndefu, Sasa akawa anasema kama makosa ndo yashafanyika, maji yakimwagika hayazoleki, akadai amekaa Sana kamshauri mama Rachel hili jambo aangalie namna ya kulimaliza maana linahusisha watoto wake... Basi pale yule mama akaongea maneno mengi tu Sana tukawa tunamsikiza tu



Badae Sasa akanigeukia, kumbe taarifa zote za sisi kukutana na wale wazee, tulivyopigwa faini la tambiko na Yale mahesabu tulivyopigiwa mama mkwe alikua anazo, lakini hakuambiwa na wale wazee sijui hata nani ndo alimpenyezea, Sasa yule mama ndo akawa ananiambia naskia mmeenda kule mmefanya hivi na hivi akanieleza Kila kitu, Sasa akaanza kuniambia, "mwanangu kua makini utapoteza muda wako Bure na pesa zako alafu matatizo yatabaki pale pale, huyu mama tangu namjua ameishi hapa miaka mingi sana tushakua kama ndugu, amelea watoto wake Kwa shida hakuna hata ndugu ashawahi kusogeza mguu hapa kumpa msaada wote, Leo hii watoto wamekua wakubwa ndo wanajifanya kimbelembele ndo waonekane na wao ni wazee wao"



Yule mama akawa anasisitiza niangalie Namna tu ya kujua tunayamaliza vipi huku upande wa mama mkwe maana wale wazee hawana Mamlaka yoyote Kwa Hawa kina G kwanza mama Yao hataki hata kuwaskia, Sasa katika maongezi ndo tukaja kujua kumbe hata Ile million laki 3 tulioacha Ile siku ya faini ya Rachel ilileta shida maana tuliwapa wale wazee kumbe hapo washajiwekea mgao mkubwa( wazee wa fursa)



Ba mdogo nae ni mtu anapenda kurahisisha Sana mambo, akawa anamwambia yule mama Sasa " tumekuelewa ulivyotuambia, na Kwa jinsi nilivyokuona naamini hili swala limeshaisha, labda tu mama mtoto( mama G Sasa) aseme jambo tujue utaratibu ukoje"



Sasa yule mama mwenye nyumba akadakia " huyu mwacheni kwanza naona hata Hali yake sio nzuri ngoja akae sawa tutatafuta siku tuongee"



Hapo mama mkwe kajilaza tu hajatia neno tangia tufike na mimi hapo nipo kimya tu naona mambo sijui ya kuanza kuomba msamaha hapa ni ujinga tu, tukaendelea kuongea pale badae nikatoka nikaenda upande wa wapangaji namkuta dada wa mtoto yupo nje pale namwambia mlete mtoto nimsalimu, ile anaingia ndani namskia Rachel anamwambia " mwambie huyo mtoto anataka kulala" basi yule dada anakuja kuniambia dada anasema mtoto anataka kulala, nikajua tu huyu anataka Shari mi sikusema kitu nikarudi kule ndani.....


Sasa nafika ndani wale wazee nao kumbe wanampigia ba mdogo akawa kama ananionyesha Simu lakini akawa hawapokelei, nao wanazidi kupiga tu mpaka nikawa nawaza huenda Hawa wazee nao wameweka mitego huku wanajua tumekuja huku bila wao, maana walishatuambia tusije huku wao ndo watamaliza mambo yote, au nikawa nawaza huenda Rachel ndo kawaambia maana huyu najua fika hataki suluhu kwenye hili jambo



Badae wakamtumia Sasa ba mdogo sms "nyie si mnajiona wajanja, nadhani mmekosa ukoo wa kuchezea, safari hii lazima tuwafunze adabu" ba mdogo akawa kanipasia Simu nisome, Sasa naye hakujali hata tupo ugenini akajikuta karopoka " Sasa na mimi wananijumlisha tena?"
Umo si ulitaka mwenyew 🤣
 
Sikutuma ujumbe

Kuhusu zawadi,ni nyingi hadi natamani niwapatie ndugu wa kike lakini suala la kumpelekea wewe ni hapana maana kuna nyingine natakiwa nimvishe kwa mikono yangu sasa wewe utaweza?🤣

Nimtume kijana alete umfikishie baadhi?
😹😹😹 Weeh.!! Tule tudude twa kambakamba 🤭

Mpelekee mkanitafutie na auntie mwaka usiishe huu wifi anitume embe na udongo 😹
 
S3 epi 16



Tukazuga pale tukaaga tukaondoka, hapo kumbuka mama mkwe tangia tufike zaidi ya salamu hajatia neno, basi pale nikaona hapa kazi ipo, ba mdogo nae analalamika Hawa wazee mbona siwaelei nikamwambia Mzee hii ishu tushaianza wote usijifanye kama haikuhusu, ingekua kazi rahisi ungedhani nilishindwa nini kuimaliza mpaka nikakuita wewe uje huku



Nikampigia Simu G tukakutana mahali hapo tupo na ba mdogo tumekaa mahali tu, nikamuelezea yaliojiri akawa ananiambia naomba Sana haya mambo yaishe salama Nije tu kukaa kwangu..... Hapo Sasa ndo akili yangu inakuja kwamba kumbe baada ya Hili sakata Kuna kupewa huyu Binti tena, hapo namuuliza na kazini Sasa vipi huendi, akaniambia hapana mi siwezi tena akili haipo sawa mpaka nijue mwisho wa hili jambo ni nini, sawa tukakaa pale badae G akaaga akaondoka, ba mdogo nae hua hayupo serious kabisa, hapo tuna majanga ye akaanza matani " Mzee hapa upo sawa kabisa, huyu mtoto hata pesa zetu tutatoa Kwa halali kabisa"


Nikawa nashukuru tu at least nipo na mtu anajua nayopitia tunaweza hata kushauriana, ba mdogo hapo tushatiana kiburi kua Hawa wazee tuachane nao kwanza maana tushaambiwa kule wao hawana Mamlaka yoyote, na kama Hilo tambiko sijui Hela tulishawapa ni kama wanatafuta namna ya kufanya hili jambo liwe fursa kwao



Basi zinapita siku, wazee wanapiga Simu sisi tupo kimya tu hapo nawaza Hawa watakua na plan gani mbona walishatupa vitisho vingi, Rachel nae alisharudi geita nilifanya kuambiwa mtoto akawa kamucha pale kwao, G Bado yupo Kwa shangazi huko..... Kuna siku nikapigiwa namba mpya kumbe ni yule mama Sasa wa Ile siku mwenye nyumba akawa ananiambia mkipata wakati mnijulishe ni lini mje nyumbani tuongee.... Nikamwambia sawa ntakujulisha...... Hio siku nimekaa pale mara napigiwa Simu na mkuu wangu kazini, Sasa nikawa nawaza huyu anataka nini ila sikushangaa Sana maana Kuna kipindi unakuta upo likizo unapigiwa tu Simu unakuta mtu uliyemuachia nafasi Kuna maelezo anataka kutoka kwako..... Sasa napokea tumepena salamu pale na nini, anaanza kuniuliza " hivi policy za kazi si mnazijua wote, mambo yenu private ni marufuku kufika kazini"



Namuambia Hilo nalielewa, maana kweli kazini kulikua na policy za kijinga kweli mambo Yako ya nyumbani ukileta kazini wanakua na zogo kweli, Kuna kipindi Kuna mfanyakazi Ali apply zile emergency Loan akaandika anahitaji ada Kwa ajili ya watoto wake, yaani alichambwa ofisi nzima mpaka ikawa aibu, Hawa wajinga shida za nyumbani ukiondoa maradhi au kifo walikua hawataki kuskia



Sasa kumbe wale wazee wameenda pale ofisini napofanya kazi, aliyewaelekeza huko hata sielewi ni nani, nikashangaa kwanza nikaona mpaka Sasa Hawa wamefika mbali, uzuri tu pale ofisini mkuu akawasikiliza akawaambia mbona hapa naona ni mambo private sielewi sisi tunahusika vipi, mtafuteni muongee kifamilia, Sasa hapa nao washanitia dosari kazini, na ukizingatia hii ishu sikuwahi kumuambia mtu



Ba mdogo Sasa namuuliza Hawa wazee tunadeal nao vipi maana naona Sasa tunatiana aibu tu Sasa na ukizingatia swala la kuongea nao tena tushaliweka pembeni, ba mdogo ananiambia waache kwanza hao tutajua namna ya ku deal nao



Ikafika siku tukaja kwenda Kwa mama mkwe kule, same routine... Tukafikia Kwa yule mama hio siku yupo tu yule mama na mama mkwe hapo nipo na ba mdogo, mama mkwe kama kawaida baada ya salamu yeye yupo kimya tu, yule mama Sasa ndo muongeaji, akaniambia "mwanangu hapa sitaki mambo yawe mengi Wala nini ndo maana hata unaona tupo wenyewe tu hatukutaka watu wengi maana haya mambo yashakua ya aibu, huyu ashakua mama Yako inabidi ifike mahali tu msameheane maisha yaendelee, hapa sisi Wala hatuwezi hata kuanza kukaa vikao vya kupigana faini Wala nini, wewe ni mtu mzima Wala sio mtoto nendeni tu mjipange mje na chochote sisi tutapokea Kwa mikono miwili, Ili huyu(G) awe amepata baraka za mzazi Sasa, hapo ba mdogo nae akadakia akajifany anaongea maneno yake ya busara pale mimi hapo nipo kimya tu naitikia tu..... Tukaongea pale tukawa tumemaliza





Sasa Mila za huku Kanda ya ziwa Kuna muda hua sizielewi, kuna kitu kinaitwa nzengo, Hawa ni majirani wote ambao mnakua mnaishi mtaa Mmoja, omba Sana kugombana na mtu yoyote ila sio Hawa watu, nilishazoea tu kuhudhuria matukio mbalimbali ya mtaani pamoja na kutoa michango pale panapohitajika, sasa hio siku napigiwa Simu nifike Kwa Mzee mmoja ni karibu ninapoishi, tukatoka hapo nipo na ba mdogo, Sasa Ile kufika hio nyumba nashangaa tena nakutana na lile jopo la wazee...... Nikabaki nashangaa Hawa wananitafuta nini
Halafu wewe ni mstaarabu sana na una hofu ya Mungu. Vinginevyo ungewakimbia na hakuna chochote wangefanya
 
Sema nimesoma hii story yako comprehensively nimekuja kugundua anguko la sisi wanaume ni umalaya na pombe, nadhani ungekuwa mbali sana kimaisha kama ungetulia na Marry,nevertheless,imaginary Marry ni mwanamke mzuri,humble, mtamu,sexy,romantic and one of a kind, ni dhambi kuruhusu kuolewa na kutombwa na jamaa mwingine,with due respect, I hereby commanding you to send her dials to my inbox,Marry anahitaji mwanaume kama mimi,nitumie na namba ya Samira pia nione kama nitaweza kuwatomba kwa ujumla wao,I hope life linazidi kukufunza na utakuwa baba bora,by the way kwa aliyepo Arusha tuonane tunajidili hali ya uchaguzi wa mwenyekiti wa Chadema kwa kina,preferably mwanamke ili walau tutombane at the end,umofia kwenu
Mkuu naona ushapiga cha nyumbani kabisa
 
Back
Top Bottom