Ushawahi kujifanya mjuaji ukaja kuumbuka?

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] mchungaji alikuwa na makusudi sana aisee
 
Aiseee!
 
😂 😂 😂 😂
Umenichekesha sana mdogo wangu, hiyo tabia na My Mom alikuwa nayo, niliwahi pika ubwabwa mbichi nililishwa mpaka nikawa nalia, nikapika ugali mbichi nikalishwa mpaka mdada tuliyekuwa tunaishi naye, akanitetea kwa Mama ndiyo nikaumwaga, nikapika uji una mabonge nilinyweshwa chupa nzima mpaka nikahisi kutapika..!
Namshukuru sana yule mwanamke lakini, maana akili ilinikaa hasa.!!

Kuhusu kuumbuka, siku hiyo nimefika kwa bamdogo ugenini, wakawa wanataka kupika mboga halafu ni tembele, basi nikajitia sogeeni tu mie ndiyo nitapika, nafanya utani pale na mbwembwe kibao wanakaukia kucheeeeka.!
Basii nikawasha zangu jiko la gesi, bwaaana bwaaana.!! Ule mjiko kumbe unazingua bwana haupunguzi moto, yaani sikutoa tembele nilitoa 'rojo la tembele' na imagine limeshika chini,

Niliona aibu, nikawa mpole na ile 'ki-ere-ere' yote ikaniisha, nilishindwa hata kutazama watu usoni, nikajiuliza aliyenituma niseme nitapika hapa ugenini kwa watu ni nani.???
 

Wapi kashata yakheeeeeeeee
 
Mwana kuli find Mwana kuli get😂😂
 
Haha binti phoneix we are together [emoji3]
 
Nimeingia kwenye daladala ilikuwa kituoni inasubiri abiria nakuta wameachia mziki mnene hadi kero.

Basi nikawafokea nyie vipi mbona makelele watu tumechoka bana hebu punguzeni sauti konda akaja juu Nami nikaja juu mara kumi yake wakazima mziki.

Gari limejaa likaondoka konda ameanza kukusanya nauli kujisachi nimesahau wallet.

Nimejisachi kila mifuko yote minne ya suruali na miwili ya shirt mara kumi kumi hamna kitu. Konda akaniwashia moto upya siwezi kujitetea wala kumuambia chochote bahati nzuri akapatikana msamaria akanilipia ila konda alinisema safari nzima.
 
Mimi maza angu hakua mama wa kuchapa,alikua n mama wa adhabu Nakumbuka zamani alishatukataza kuangalia TV bila yeye kutoa ruhusa,siku hiyo tumezoea mama akirudi si atarudi na Gari atapga Honi tukiskia tutazima tv tutakausha kimya.

huo ndio mtindo wetu tukiskia tu honi piiiii,unakimbia getini kufungua huku nyuma usharudisha kila kitu eneo lake,unasambaza madaftari mezani kuonyesha kwamba ulikua unajisomea,si unajua zileee..

Basi bwana! hiyo siku bi mkubwa gari sijui kaacha wapi "anajua mwenyewe" kaingia kupitia geti la nyuma "anafunguo zake" huku kumbuka tulishakatazwa angalia TV bila ruhusa,basi ghafla bin vuu Mama huyu hapa sebleni,Pale sebule yote inakua ndogo,moment kama hizo huwa naombaga MUNGU aje hata MGENI,ila ndio hivyo haji cha mgeni wala nini

Basi bana baada ya kudakwa tuliulizwa tu swali 1,Nilisema nini? "tukajibu" akatuambia nyie si mnapenda sana TV sasa subirini,Akatoka akaenda chumbani kwake kisha akarudi akaenda Chumba chake cha maombi,Maza angu n maza wa prayer kwa sana "ana chumba chake special hicho" basi akaenda akafungua kisha akachukua TV ya chumbani kwake akaipeleka kwenye ile chumba yake ya maombi.

Alipomaliza akaja seblen ambapo alituacha,akatuuliza tulikua tunaangalia nn? tukamdanganya "tukamtajia limkanda la Yesu" akasema uchukueni nifateni,Tukauchukua ule mkanda tukamfata hadi kwenye chumba chake,akatuingiza akasema sasa ingien mkae humu ndani muangalie huo mkanda mpk mchoke,Tukaingizwa Tukafungiwa.

Kile chumba ni master,Dada wa kazi akaambiwa awe anapika chakula kingi,basi tukiletewa asubuhi msosi mle ndani tunakaa humo ndani mpk usiku muda wakutoka kwenda kulala,Usiku ukfka tunaletewa chakula tule tukmaliza usiku kbsa saa 4 tunafunguliwa tukalale chumbani,asubuhi ikifka tunarudi jela yetu,Ile adhabu ilidumu mwezi mzima wa LIKIZO huwezi amini likizo nazionaga fupi,ila hamna likizo nliona ndefu kama hii tuliiyofungiwa chumba kimoja tunaangalia mkanda wa yesu.


Tangu hapo sijawahi kwenda tofaut na maagizo ya mazaaa,yule mama ana ma adhabu ya JKT Halafu mshua wangu alivyogo boya na yeye hata haingiliagi kesi ambazo mazaa anaishughulikia,mi ananiboaga kweli yani,badala hata antetee et akirud kazini jioni anakuja kwenye ile chumba unamskia anasema "hi my sons" ananiboaga basi tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mama yangu alikuwa Ni mkali ,yaani ukizingua unachezea bakora Africa mashariki na kati hazijawahi kutokea....![emoji23][emoji23]

Nakumbuka kipindi nipo form four home kilikuwa na deki yenye upande wa VHS na DVD, ujio wa CD za DVD ukawa ule upande wa VHS hautumiki sana...

Sasa si unajua utundu wa ukijana Tena,nikaunganisha waya waya zile ikawa unauwezo wa kurecord kitu kinachooneshwa kwenye tv,dhumuni Ni kurecord nyimbo channel 5 enzi hizo hata cable ikiwa haijalipiwa tuwetunachek,

Basi ile kitu ikawa Ni tabia natafuta mikanda ya zamani naifuta narecord nyimbo zangu,mwanzoni alipiga mkwara baadae akazoea naona hata yeye akawa anapenda tunaangalia familia nzima maana nakumbuka kulikuwa na mazishi ya kiongozi mkubwa duniani aliomba nimrecodie,ila nilikuwa makini kuchagua mikanda,maana kuna mikanda yake alikuwa anaipenda hagusi mtu

katika kurecord pia tulikuwa na mikanda yetu sisi vijana wakiume tulikuwa tunarecord video za ngono,Kuna channel ilikuwa inapatikana kwenye Cable ikifika usiku inaonesha movie za ngono ,na ile mikanda ilikuwa inafichwa geto,

Sasa bwana Kuna siku mama katoka kuwapokea wageni wametoka kijijini,Sasa usiku baada ya kumaliza kula watu wote tupo sebuleni ,baada ya taarifa ya habari ya ITV kuisha Mimi kiherehere changu nikasema ngoja niweke mkanda wa rose mhando umburudishe mama na wale wageni maana mama alikuwa anampenda kweli

Lahaula mkanda unaanza rose mhando kipande Mara kinakuja kipande Cha ngono,kumbe Kuna mtu alirecord pasipo kujua Ni mkanda wa rose mhando...
Kwanza nilianza kuona Giza sebule nzima,nilikimbia kwenye tv hata sielewi nifanye nn,nilijikuta nimechomoa waya Hadi ukutani...

Bahati nzuri sisi watoto wakiume tulikuwa tunalala nje Basi nilivyotoka sikurudi Tena nyumbani nilisingizia nipo kambini najisomea kwa ajili ya kuanza na mitihani mpk nilivyomaliza form four.....
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Umezingua ata muislam najua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…