Ushimen: Ebu ngoja leo niwape mawazo machache ya kujikwamua

Sijajua kwanini wanaachwa wafanye huo uharibifu. Sijui kwa kuwa kabila lao ni lile la yule mtukufu wa chattle.
 
asante sana bro umesahau kutupa location ya biashara ya shoeshine
 
asante sana bro umesahau kutupa location ya biashara ya shoeshine
Mkuu... ukichangamsha macho hapo nyuma, kuna maeneo nilisha yataja kabisa kwa shughuli hizo ama kama hizo
 
Naomba location ya mashamba Dodoma ambapo wanalima mazao ya horticulture (eg. Bamia, hoho,carrot,mwendokasi) na yapo maeneo gani, umbali na usafiri Ushimen Mshana Jr
 
Naomba location ya mashamba Dodoma ambapo wanalima mazao ya horticulture (eg. Bamia, hoho,carrot,mwendokasi) na yapo maeneo gani, umbali na usafiri Ushimen Mshana Jr
Mkuu, hizo kitu naona sana zinalimwa maeneo ya Zuzu.
Zuzu ipo umbali wa kilometers 7-10 kutoka Dodoma mjini, na pia huko Zuzu ndipo alipo waziri mkuu mstaafu mzee Kayanda Mizengo Pinda (pia anafanya kilimo na ufugaji).
Zuzu unaweza ukapata shamba la ukubwa wa hekari moja kwa bei ya kuanzia 1,000,000 - 1,500,000 (hii inategemea na utashi pamoja na eneo la muuzaji)
Pia kimazingira, Dodoma ni mka ambao water table yake ipo juu sana, hivyo basi unaweza ukapata maji ya kisima kwa umbali usio chini sana.
Mkuu, karibu sana Dodoma
 
Mkuu ww ni mgodi unaotembea ,hakika unatema madini adhimu sana endelea kumwanga ideas watu wazitumie hakika hawatokusahau japo hawakujui.
 
Mkuu ww ni mgodi unaotembea ,hakika unatema madini adhimu sana endelea kumwanga ideas watu wazitumie hakika hawatokusahau japo hawakujui.
Ahsante mkuu, ingawa namimi napenda nijipongeze kwa uwezo wa kumtumia Ushimen kuwasilisha kile kinacho faa kuiongezea jamii na hasa vijana maarifa.
Kwa pamoja nivyema pia tukampongeza Ushimen kwa kutuletea machache kutoka kwangu, pamoja na kwamba kuna wakati namtumia Ushimen vibaya hata anaonekana lilevi, likorofi, halina akili, linaishi kijijini, lina sura ngumu....
Pamoja sana Chief..
 
asante sana bro umesahau kutupa location ya biashara ya shoeshine
Mkuu... hii biashara watu wengi wanaidharau sana, lakini ni kitu kama ukiamua kikifanya kwa hakika hauto lala njaa mjini wakati ikikusaidia kupata pesa ya kilipia kodi ya pango pamoja na matumizi ya kula siku.

1. Ukienda pale 4 ways bar, hakuna shoe shine wa uhakika kwenye eneo lile.
Pale wateja ni wengi hasa madereva wa magari makubwa ambao hupendelea sana kupombeka mule kila jioni baada ya kupaki magari yao. Na pia hata kwakuwa ni njia panda kubwa inayo gawanyika, pale kuna mzunguko mkubwa sana wa watu na Nina uhakika ukiweka kijiwe pale pembeni ya muuza matunda bilashaka utafanya kazi.

2. Pale maeneo ya Stella Bar Nkuhungu hakuna huduma ya shoe shine, na mzuguko ama mkusanyiko wa watu ni mkubwa sana.

3. Jaribu kuweka kijiwe pale Malaika Annex, nina hakika utapata wateja wa kutosha kwasababu sisi walevi tunatabia ya kupenda kupata huduma tunazo hitaji wakati tunapata moja moto na nyingine muongeze yule.
Pale nina hakika ukiamua kuifanya kazi yako, kwanza wewe binafsi uwe nadhifu na ukawa na kandambili walau pea 4-6 amabazo sio chakavu, safi na zenye kuvutia. I'm sure utawapata wateja wa kutosha na hauto lala njaa mjini.

4. Nimechoka mkuu, ngoja nimalizie hii whatever-Vant kwa raha zangu......
 
Kuna wazo nafikiria hapa namba ya kukiweka vizuri kwenye maandishi ili lisomeke ma kuweza kueleweka...
 
Mkuu Ushimen naomba uniambie Location nzuri ya biashara ya kuchoma mahindi ukitoa area C.View attachment 1192841
Mkuu, kwanza nikupe pole na uniwie radhi kwa kuchelewa kujibu hili swali linalo hitaji muongozo.
Kwanza nikupongeze kwa kuja na wazo, then nikusaidie kwenye umaliziaji.

1. Hii biashara inafaa sana ikiwa utaweka kijiwe pale Sheli, njiapanda ya kwenda Kisasa na UDOM kupitia Dar road. Pale karibu na wachoma kuku na wewe ukijipanga ninahakika hauto jutia.

2. Ukifanikiwa kupata eneo pale njiapanda ya kwenda Ilazo na Meriwa Dar road, nina hakika utafanya biashara nzuri sana eneo lile kwasababu pana muingiliano mkubwa sana wa watu na pia ni njia kuu inayo elekea maeneo niliyo yataja hapo juu.
Na kwakuwa kuna wapita njia kwa wingi pamoja na bodaboda, pale panafaa pia kama utaweka biashara ya mihogo ya kukaanga.

3. Panaitwa 4 ways ni njiapanda inapo gawanyika kutoka Singida road kuelekea Nkuhungu.
Pale patakufaa sana kwa biashara ya kuchoma mahindi, pamoja na Mihogo ya kukaanga kwasababu watu wengi sana wanashukia na kupita eneo lile, pamoja na boda boda wapo pale kwa wingi, bila kusahau wanafunzi.
Pale ukiwa msafi, kwahakika hauto jutia.

4. Mkuu, eneo la chako ni chako sijaona mchoma mahindi na kapilipili kwa mbaali pamoja na vipande vya liomao.
Pale chako ukipata nafasi patakufaa sana kwasababu pana mzunguko mkubwa sana wa watu na pia ukiweza kuweka muhogo wa kuchoma, nina amini utafanya biashara uzuri kabisa.

Mkuu, ebu ngoja kwanza nikamae hapa, kuna kazi natakiwa niimalize leo ili nipate pesa ya kumalizia ule mjengo kule Nala.
Na madogo wanafunga shule leo, inatakiwa niangalie sehem yenye M-Pesa ili nikawatumie nauli please
 
Kwanza ahsante sana kwa mawazo yako, pili nikupe pongezi kwa kuwa mdadisi wa kuzijua fursa zilizopo Dodoma. Hakika utasaidia vijana wengi wasiokuwa na mtaji mkubwa kuanzisha shughuli itakayo waingizia kipato halali. Hizo sehemu ulizozitaja zote ni centre nzuri na nina zifahamu vizuri. Kongole kwako!

Ukimalizana na watoto. Eeeh! Kesho sasa wikiendi.... Kuna sehemu yenye kuku choma tamu zaidi Mwanga Bar[emoji41][emoji41]

 
Kwanza nikushkuru kwa pongezi kwa haya machache ninayo wafungulia vijana.
Pili niseme tu kwamba ahsante kwa kuni allocate pale kwa Mzee Mwanga kwenye kuku choma na ikiwa utafika viunga vya pale, naomba fikisha salam zangu kwa sheji yangu Secy.
Mimi leo kwakuwa vijana wamerejea, hapa napanga niwapeleke Pizzeria wakakule Pizza na pia wacheze na kubembeya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…