Wanabodi,
Sitaki kuingia ndani kwenye technicalities zilizopelekea wagombea wa upinzani kuenguliwa, bali natoa wito kwa rais Magufuli aingilie kati hali hii au yeye mwenyewe kama rais wa JMT, au kupitia kwa msaidizi wake Waziri Jaffo wa Tamisemi, ayafumbie macho makosa yote madogo madogo ya wagombea wote wa vyama vyote walioenguliwa kwa sababu zozote, ziwe ni za kweli za halali au ni figisu, ayafute na watoe amnesty ya jumla kwa kila aliyegombea apitishwe tuu hivyo hivyo despite all the odds ili Tanzania tuingie kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani kwa ushindani wa haki, uwazi na usawa kwa vyama vyote kutendewa haki sawa, kwa demokrasia kuachwa kufuata mkondo wake, hivyo waliosusa wote kwa kuweka mpira kwapani warudi uwanjani kipute kipigwe.
Ushindi mnono na mtamu wa raha ni ule ushindi unaotokana na ushindani halali wa haki unaopatikana kwa kuendeshwa kidemokrasia kwenye uwanja ulio sawa, level playing ground na sio uwanja tange, wala sio ushindi wa mezani!.
Hivyo natoa wito kwa serikali ya CCM, chini ya Jemedari wake, JPM, kiukweli labisa, hata kabla ya uchaguzi, CCM tayari imeishashinda kwa ushindi wa kishindo sio tuu huu Uchanguzi wa Serikali za Mitaa, bali hadi Uchanguzi Mkuu ujao wa mwakani 2020 kutokana na sababu za ki political social dynamics ya Magufulification nilizoeleza lakini ili CCM iweze kuufurahia huo ushindi kwa furaha ya kweli na hivyo kusheherekea ushindi huo, lazima CCM ishinde kwenye ushindani wa kweli, ushindani wa haki na ushindani wa usawa na sio kupata ushindi kwa kufanya figisu ili washindani wako wasuse, watie moira kwapani na wewe upewe ushindi wa mezani. Ushindi wa hivi sio ushindi mtamu, wala hauleti raha ya kudumu kwasababu karma itaingilia kati!.
Nakuomba Rais Magufuli jifanyeni kama mnacheza na watoto, wafungulieni njia watoto wote washindane kwa haki, washiriki kwenye uchaguzi huu na wa haki kwa uhuru na kwa haki sawa kwa vyama vyote despite mapungufu walionayo ili hata uchaguzi Mkuu wa mwaka kesho, wakati Watanzania watakapo irejesha Tanzania kwenye mfumo wa Chama kimoja CCM, iwe ni Watanzania wenyewe ndio wameamua kuichagua CCM kwa kishindo cha haki kupitia uchaguzi huru na wa haki ulioendeshwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi ulioendeshwa kwenye uwanja sawa na tambarare wa ushindani, na sio CCM ishinde katika ule ushindani wa kugombea kisu cha makali kuwili, huku mshindani mmoja ameshika kwenye mpini na mshindani mwingine kwenye makali. Hivyo CCM ishinde kihalali kwa kufuatia kazi nzuri ya rais JPM na serikali yake na sio kwa sababu CCM ndio iliyokamata mpini!.
Hivyo Tanzania tukiamua kufanya uchaguzi huru na wa haki, unaofusta mfumo wa uchaguzi wa kidemokrasia ya ukweli, tunaweza. Mimi naamini kabisa kwa mambo makubwa na mazuri ya Rais Magufuli anayoyafanya, we have nothing to lose rais Magufuli akiruhusu demokrasia ikashamiri, akatoa haki sawa kwa vyama vyote kufanya siasa ikiwemo kuondoa zuio batili la mikutano ya siasa, bado rais Magufuli anaweza kuyaleta maendeleo yote aliyokusudia at the same time huku akiruhusu demokrasia nayo ikashamiri, ila ukweli utaendelea kubaki ni ukweli daima kwa katiba hii, Tume hii, sheria hii ya uchaguzi na kasi hili ya rais Magufuli, CCM bado itaendelea kutawala Tanzania milele.
Naomba nimalizie kwa ile kauli ya thread hii
"Ushindi Mtamu ni Ushindi Unaopatikana kwa Ushindani Wa Haki Kwenye Uchaguzi Huru na Wa Haki, Unaendeshwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi na Unaofanyika Kwenye Uwanja Sawa wa Ushindani wa Kisiasa, Sio Ushindi wa Mezani!. Mheshimiwa Rais, Dr. John Pombe Magufuli, aka.JPM, Kasi Yako ya Maendeleo ya Tanzania Unaoifanya, Utailetea CCM Ushindi Kishindo Katika Uchaguzi Wowote, Tunakuomba Please Please Please, Ruhusu Tuu Ushindani wa Haki, Wazi na Usawa Kwa Vyama Vyote,
Utabarikiwa Zaidi na Zaidi, na Tanzania Tutabarikiwa.
Paskali