Ushindi mtamu ni ushindani katika uwanja sawa, sio ule wa mezani. Magufuli, kasi yako ni ushindi wa kishindo. Ruhusu ushindani wa haki, sawa na wazi

Nafikiri chuki ikizidi inapoteza umakini wa kufanya jambo,paskali uwafungulie uzi siku nyingine nao wawe makini,zaidi ya hapo baba kijana ataendelea kutimua mbio zake za kawaida kumshinda mwanawe!
 
Nchi inahitaji maendeleo ya watu ...tumejichelewesha sana kusaka kiki za demokrasia kwani ndio upuuz waliotaka tuufikirie.

Kwa hiyo hayo maendeleo ya vitu yanaletwa kwa kunajisi box la kura? Kuna uzi huku jukwaani unasema kama tunajenga miradi kwa pesa zetu za ndani iweje, deni la taifa lipande kwa 20t ndani ya miaka minne? Nenda huko maana sio mada ya kidemokrasia, praise team wenzako huko wanatukana tu maana hawana majibu. Mada hii tuachie tunaojadili demokrasia.
 
Huyu bwana ni mzuri wa kutengeneza tatizo na kulitatua ili apate umaarufu zaidi. Sitashangaa nikisika Dr Abasi akisema “Mheshimiwa rais Dk John Pombe Magufuli amewasamehe wote waliojaza fomu kimakosa”.

Hata akisema hivyo haitasaidia maana wapiga kura wengi hatujajiandikisha kwa sababu tulijua fika uchaguzi utahujumiwa, na hilo limedhihirika.
 
Daraja la juu la ubungo litanisaidia Nini mkulima wa chikichi Kigoma?
Hizi ni dalili za ubinafsi wa kipuuzi!!! Hujui kuwa gharama kubwa inayotokana na matumizi makubwa ya nishati ya mafuta kwenye foleni pale makutano Ubungo itapungua sana!? Upungufu huo utasidia ela zilizokuwa zinatumika kununulia mafuta za zitatumika kununulia vitu vingine vya muhimu kwa watanzania wote hata na huyo mkulima wa chikichi Kigoma!?

Acha ubinafsi wa kipuuzi!!!
 
Nchi inahitaji maendeleo ya watu ...tumejichelewesha sana kusaka kiki za demokrasia kwani ndio upuuz waliotaka tuufikirie.
Africa kuna nchi gani ilikuwa na maendeleo ya watu kama Libia, nchi gani taja moja tu. Lakini kutokana na kukosekana kwa demokrasia tumeona nini kimetokea hadi sasa wananchi wamebaki madhalili. Demokraisia si jambo la kupuuza hata kidogo.
 
1111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111111
 
Hakubaliki kwani uchaguzi wa urais huo? Kujaza mkosee nyie lawama mumpe magu. Mjitafakari muache kuishi kwa mazoea.
 
Hujamuelewa Paskal, ameandika kwa mfumo wa fasihi, kimsingi Paskal anamkejeli tu mwananzengo mwenzake kama anaamini yeye ndio ajaye aache Watanzania wachaguwane kwa haki watamduwaza kwenye sanduku LA kura.

Kilichowazi kwa sasa ccm haina imani na Watanzania, sijui unaelewa lugha hii? Si kwamba tu Watanzania hawana imani na ccm, Bali ccm pia haina imani na Watanzania.
 
Walio Jitoa Ni Wachache Sana kuliko walio Ondolewa. A.C.T Walio ondolewa ni 94%, CHADEMA Ni 82 % kama sikosei.

Je! Hapo Kuna Uchaguzi Au Kuna Uchafuzi?.
Ziliwekwa taratibu ili zifuatwe. Ukishindwa kiziguata, unaondolewa tu. Hata Bunge la Congress la Marekani sasa liko kwenye mchakato wa kutaka kimuondoa Rais Trump madarakani kwasababu amekiuka utaratibu. Simple!
 
Baada ya Gaddafi kufa libya imekuwa na demokrasia?
Haikuwa kwa sababu hakueka misingi mizuri tangia mwanzo ya kidemokrasia amesabisha chuki kwa wananchi na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Unapoanzisha makundi mawili moja unalifavor na jengine unalikandamiza matokeo yake baada ya muda wale wanaokandamizwa watakuja juu na wakifanikiwa lile kundi jengine wataona haiwezekani. Hapo ndio msingi wa vita unapoanza so inatakiwa misingi ya haki na uwazi iwepo mapema ili kila mmoja aone thamani yake.
 
P sio kwamba hapendi kutoa uhuru huo ila anajua nn kitatokea chama kishapotea mvuto ndio njia pekee ya kujinasua pia sio kila mtu anaweza kuhimili presssure ya matokeo katika uchaguzi huru chochote chaweza tokea.
 
Miaka nenda rudi ambayo sisi tumekuwa tukiishi taabuni Ni sababu ya foleni ya Ubungo kumaliza hela za serikali?
Ninachojua Mimi Ni hiki, ili nchi ipate pesa nilazima iuze vitu nje. Bila kuuza vitu nje hamna pesa itakayoingia.
Ninachosema Mimi serikali iboreshe miundombinu c, tupate pembejeo kwa gharama nafuu, tulime kwa wingi (massive production) ili tuweze ku enjoy economies of scale, na tuweze kusafirisha bidhaa zetu kwa wepesi, zifike kwa wateja wa ndani na nje ya nchi kwa wakati.
Huwezi kuendesha nchi wala kuhudumia taifa lako kwa kutegemea hela ya kubana matumizi ya mafuta, hizo ni fikra za kifukara kabisa na za kibwege.
 
Hata akiwasamehe wapinzani wasikubali ,wakikubali ndo mwisho wao na 2020 wakaze moyo wajitoe tena japo najua ni ngumu kwa kuwa wengi wanategemea siasa kuishi
Huyu bwana ni mzuri wa kutengeneza tatizo na kulitatua ili apate umaarufu zaidi. Sitashangaa nikisika Dr Abasi akisema “Mheshimiwa rais Dk John Pombe Magufuli amewasamehe wote waliojaza fomu kimakosa”.
 
Asalaam Aleykum mzee wangu, out of topic, hivi hamuwezi kumuomba Sheikh Alhad Musa awaombee masheikh wetu wa Uamsho watolewe gerezani? Watakaa huko mpaka lini? Hivi huyu sheikh Alhad kila siku yupo ikulu anashindwa kuwatetea masheikh wenzake waachiwe wakati mpaka wabakaji Babu seya wameachiwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…