Ushindi wa Ethiopia jimbo la Tigray uko wazi

Ushindi wa Ethiopia jimbo la Tigray uko wazi

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Yawezekana madai ya jimbo la Tigray nchini Ethiopia chini ya chama kikongwe cha uasi cha TPLF yakawa na mantiki katika kile wanachokitetea, hata hivyo hawana nguvu ya kupigana na serikali kuu ya Ethiopia chini ya waziri wake mkuu Abiy Ahmed.

Tigray ni jimbo la kaskazini magharibi ya Ethiopia na limepakana na nchi ya Eritrea kwa masafa marefu na sehemu ndogo imepakana na Sudan.Tangu kuanza kwa mzozo huo baina yake na serikali kuu ya Ethiopia hawaonekani kufanya mashambulizi yoyote ya maana na huenda hasa baada ya kushambuliwa kwa mahodhi makuu ya silaha ya kambi za jeshi zilizo jimboni humo.

Kibaya zaidi vijana wengi wa Tigray ambao wangekuwa askari wa kupambana na jeshi la Ethiopia wamekuwa wakikimbia kuingia nchi ya Sudan kukimbia vita.Kwa upande mwengine jimbo hilo halionekani kuwa na uhusiano mzuri na nchi ya Eritrea ambayo karibuni imerudhisha uhusiano na Ethiopia uliopotea kwa miaka mingi tangu pale Eritrea ijitenge na Ethiopia kuliko sababisha vita baiana yao.

Hivyo mzozo huu wa Tigray kwa Ethiiopia huenda ikawa ni moja ya mambo yatakayomuongezea sifa waziri mkuu Abiy Ahmed kimataifa na nchini mwake pale atakapomaliza kuzima uasi wa jimbo hilo.

Si rahisi kwa Tigray kupata nguvu ya kujitenga kutoka Ethiipia kama vile ilivyokuwa kwa Eeritrea ambayo ina kitega uchumi kikubwa cha kupakana na bahari nyekundu.

Vijana wa Tigray wakipanga foleni kukimbia vita ili waingie Sudan.

1605783562570.png
 
Mbona hawa waethiopia ni masiki hivi aisee ndio kila siku wanakimbilia kusini.

Na nchi yao inajinadi imeendelea kumbe maendeleo ya watu ni kidogo hapa Ethiopia naona ni maendeleo ya vitu tu..
 
Kwani sudani na misri wana semaje kuhusu ili
Sudan na Misri naona kama hawana maslahi na mgogoro huu.Kama ni maslahi basi ni Eritrea na Somalia ambao wana udugu wa karibu na watu wa Tigray.Mojawapo wakiamua kuwaunga mkono waTigray basi mambo yanaweza kuharibika kwa upande wa Ethiopia.
 
Mbona hawa waethiopia ni masiki hivi aisee ndio kila siku wanakimbilia kusini...
Na nchi yao inajinadi imeendelea kumbe maendeleo ya watu ni kidogo hapa Ethiopia naona ni maendeleo ya vitu tu..
Hata ukimbizi wao si wa maana.Wanakimbia kiovyo ovyo kama nyati wanavyomkimbia Simba.Tofauti na wenzao wasomali ambao hutafuta nchi zenye utajiri.Waethiopia wanaweza kukimbia kwao na wakakimbilia nchi za jangwa na zenye shida na njaa kama kwao
 
Hivi ndivyo massiemu yangefanywa baada ya Lissu kushika mpini

Yangetaka eti chatto iwe nchi kama ilivyo Lethoto amabayo ni nchi ndani ya nchi nyingine
 
Sudan na Misri naona kama hawana maslahi na mgogoro huu.Kama ni maslahi basi ni Eritrea na Somalia ambao wana udugu wa karibu na watu wa Tigray.Mojawapo wakiamua kuwaunga mkono waTigray basi mambo yanaweza kuharibika kwa upande wa Ethiopia.
Eritrea anasapoti wa Tigray wapewe kichapo wapo pamoja na Serikali kuu ya Ethiopia
 
Eritrea anasapoti wa Tigray wapewe kichapo wapo pamoja na Serikali kuu ya Ethiopia
Hapo basi ndio ugumu kwa Tigray.Na ugomvi wa Eritrea na waTigray ni upi au ndiye yule Mangestu aliyepigana na Eritrea alitokea huko.
 
Hapo basi ndio ugumu kwa Tigray.Na ugomvi wa Eritrea na waTigray ni upi au ndiye yule Mangestu aliyepigana na Eritrea alitokea huko.
Kipindi cha vita ya Ethiopia na Eritrea wa Tigray na majenerali wao ndo waliokua mstari wa mbele kuwachapa wa eritrea...........
 
Hivi ndivyo massiemu yangefanywa baada ya Lissu kushika mpini

Yangetaka eti chatto iwe nchi kama ilivyo Lethoto amabayo ni nchi ndani ya nchi nyingine
Angalia farasi huyu nae,yani kuna watu hua mnakurupuka kifala kweli yani,kama lijinga jinga hivi
 
Kipindi cha vita ya Ethiopia na Eritrea wa Tigray na majenerali wao ndo waliokua mstari wa mbele kuwachapa wa eritrea...........
Eritrea kwa sasa ina maslahi makubwa na nchi ya Ethiopia hasa katika uwanja wa kiuchumi kwani kwa kuwa Ethiopia haina bahari wanapitishia bidhaa zao Eritrea na wao wa Eritrea wanatumia ndege za Ethiopia kufika nchi za mbali kwa maana shirika la ndege la Ethiopia lina abiria wengi sana wa Eritrea.Hata biashara za kuvuka mipaka baina ya nchi mbili hizo ni kubwa.
 
Eritrea kwa sasa ina maslahi makubwa na nchi ya Ethiopia hasa katika uwanja wa kiuchumi kwani kwa kuwa Ethiopia haina bahari wanapitishia bidhaa zao Eritrea na wao wa Eritrea wanatumia ndege za Ethiopia kufika nchi za mbali kwa maana shirika la ndege la Ethiopia lina abiria wengi sana wa Eritrea.Hata biashara za kuvuka mipaka baina ya nchi mbili hizo ni kubwa.
Sasa kama hao watigray wakiziba njia ya kwenda Eritrea ndio basi tena kama namuona kwa mbaaaali mkenya akiangalia namna ya kuwasapoti watigray
 
Tigray haiwezi kupambana na serikali kuu ikishinda hilo lipo wazi.

Ila kitendo cha wapiganaji kutoka kabila la Amhara kuungana na serikali kuu kushirikiana vita dhidi ya Tigray huoni kama kitazidisha zaidi uhasama wa kikabila?
 
Tigray haiwezi kupambana na serikali kuu ikishinda hilo lipo wazi.

Ila kitendo cha wapiganaji kutoka kabila la Amhara kuungana na serikali kuu kushirikiana vita dhidi ya Tigray huoni kama kitazidisha zaidi uhasama wa kikabila?
Hao wanachapwa na makabila yote hadi wa Oromo nao wameungana na serikali....shida wa Tigray walikua wanajiona keki kwenye hio nchi hamna kabila linalowasapoti
 
Hao wanachapwa na makabila yote hadi wa Oromo nao wameungana na serikali....shida wa Tigray walikua wanajiona keki kwenye hio nchi hamna kabila linalowasapoti
Shida sio kujiona 'keki' ila ni uhasama wa kudumu wa kikabila.
 
Shida sio kujiona 'keki' ila ni uhasama wa kudumu wa kikabila.
Katika hali zote watigray hawana nafasi ya kushinda.Kikabila na namna nyenginezo.Kabila lao ni dogo na hawana uchumi wa kuvutia watu wa mbali kuwaunga mkono ili na wao wafaidi hizo mali.
 
Hao vijana huko Sudan wataenda kupata mafunzo nadhimu ya kijeshi na watapata ufadhiri wa silaha kutoka nchi za magharibi, watakaporudi for revenge ndo utaelewa.... Kiufupi ushindi wa kijeshi ni kama adui anajisalimisha kwako, sio akimbie nchi nyingine ambayo huwezi kumfata.
 
Back
Top Bottom