Ushindi wa kishindo bungeni 2020, Lipumba adai yalikuwa maandalizi ya kubadili katiba aliyepo aendelee

Ushindi wa kishindo bungeni 2020, Lipumba adai yalikuwa maandalizi ya kubadili katiba aliyepo aendelee

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Prof. Ibrahim Lipumba leo ameuelezea uchaguzi wa 2020 akiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na TCD. Lipumba ametolea mfano Pemba ambako CCM walikuwa hawapati viti lakini 2020 wakabeba viti 12 ilhali Tanzania bara kati ya viti 214 upinzani uliambulia viti viwili pekee mpaka Unyanyembe wakaja na methali 'CCM hawana haya' jinsi hali ilivyokuwa ngumu.

Lipumba amesema hadi Kilimanjaro ambapo huwa wanatoka wapinzani safari hii vyote vimeenda CCM akidai hata kama wangechukua basi wangedanganya walau kidogo.

Lipumba amedai labda mama Kate Kamba(CCM) walikuwa wanajua ajenda iliyokuwepo lakini anaamini hata kubadilisha katiba ingekuwa nyepesi na tayari kulikuwa kuna maneno tuna Rais mzuri na vipindi viwili viwekwe kando na aliyepo aendelee kama China ilivyowezekana.

Lipumba amesema uchaguzi wa 2020, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliuita Tsunami
 
Huyo Lipumba ni mpuuzi fulani, yeye na Mbatia walikubali kutumika na Magufuli kuhalalisha uchaguzi ule wa kihayawani. Baada ya kuona hata makubaliano yake na Magufuli yametupiliwa mbali ndio anaishia kukalia. Ameshapoteza mvuto saa hia anatazama atoke vipi.
 
Amejifia, afe na afe tena huko aliko.
Kama sio MUNGU jamaa angetufanya kitu mbaya sana

Ikiwa huamin kuna MUNGU mkumbuke magufoul.
 
Pamoja na kwamba Jiwe alihusika na ubomoaji wa nyumba yangu lakini kuna vitu vingi sana alikuwa anaviweka kwenye mstari hilo halina ubishi. Saivi nipo hapa na umeme hamna tangu sambili asbh.
 
Back
Top Bottom