Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,307
- 25,932
Simba na Yanga walikuwemo kwenye michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika. Wote walianza kwenye hatua ya kwanza kwa kupepetena na timu za Msumbiji na Botswana.
Mechi za awali zilishuhudia Simba na Yanga zikipata suluhu na sare. Simba ilipata suluhu ugenini na Yanga ikapata sare nyumbani.
Yanga, wakithibitisha kuwa wao ni wa kimataifa, walipata ushindi wa bao moja huko Botswana. Wakasonga mbele. Simba, wakiwa nyumbani Taifa,waliambulia sare ya moja kwa noja na kufurushwa mashindanoni.
Hadi hapo, Yanga ndiyo wa kimataifa. Simba hubebwa na mashabiki wa Yanga kwenye michuano ya kimataifa. Hata kuwazomea huwafanya kuchachamaa. Kuwepo mashindanoni wote, ni kumaliza ubishi.
Yanga wamedhihirisha kuwa wao ni zaidi ya Simba kwenye uga wa kimataifa. Pole ni sana Simba, ni zamu yetu Yanga kuwabeba mwaka huu!
Mechi za awali zilishuhudia Simba na Yanga zikipata suluhu na sare. Simba ilipata suluhu ugenini na Yanga ikapata sare nyumbani.
Yanga, wakithibitisha kuwa wao ni wa kimataifa, walipata ushindi wa bao moja huko Botswana. Wakasonga mbele. Simba, wakiwa nyumbani Taifa,waliambulia sare ya moja kwa noja na kufurushwa mashindanoni.
Hadi hapo, Yanga ndiyo wa kimataifa. Simba hubebwa na mashabiki wa Yanga kwenye michuano ya kimataifa. Hata kuwazomea huwafanya kuchachamaa. Kuwepo mashindanoni wote, ni kumaliza ubishi.
Yanga wamedhihirisha kuwa wao ni zaidi ya Simba kwenye uga wa kimataifa. Pole ni sana Simba, ni zamu yetu Yanga kuwabeba mwaka huu!