Ushirikiano wa BRICS waleta fursa mpya kwa Afrika

Ushirikiano wa BRICS waleta fursa mpya kwa Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111332674211.jpg
Mkutano wa 14 wa viongozi wa nchi za BRICS utafanyika hapa Beijing kwa njia ya mtandao. Kaulimbiu ya mwaka huu ya BRICS ni “Kujenga uhusiano wa kiwenzi wa hali ya juu, kuanzisha kwa pamoja zama mpya ya maendeleo ya kimataifa”.

Likiwa jukwaa la ushirikiano kati ya nchi zinazoendelea, BRICS inabeba jukumu la kutatua changamoto ya umaskini inayokabili nchi zinazoendelea na kutimiza maendeleo endelevu. Kwa kuwa Afrika ni bara lenye nchi zinazoendelea nyingi zaidi, ushirikiano wa BRICS umeiletea fursa mpya.

Afrika Kusini ni nchi mwanachama wa kwanza wa upanuzi wa BRICS, na tangu kujiunga na BRICS, nchi hiyo imeimarisha ushirikiano na nchi zilizoibukia kiuchumi duniani, haswa China ambayo ni nchi ya pili kwa ukubwa wa uchumi duniani, na kuhimiza maendeleo ya uchumi. Baada ya China kutoa pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja”, Afrika Kusini imezidisha ushirikiano na China katika biashara na uwekezaji kupitia utaratibu wa BRICS, na kuhimiza ujenzi wa miundombinu, pamoja na maendeleo ya sekta za uzalishaji za viwanda, zikiwemo vifaa vya nyumbani, magari, vifaa vya ujenzi, na vifaa vya nishati ya jua.

Ushirikiano wa BRICS si kama tu umehimiza maendeleo ya Afrika Kusini, bali pia umetoa fursa pana ya ushirikiano kwa nchi nyingine za Afrika. Katika miaka ya hivi karibuni, nchi za Afrika zimeshiriki kwa hatua madhubuti katika utaratibu wa ushirikiano wa BRICS kupitia tawi la Benki Mpya ya Maendeleo ya BRICS barani Afrika. Maendeleo endelevu ni msingi wa mikakati ya maendeleo ya kikanda ya Afrika kama vile Ajendaya 2063 ya Umoja wa Afrika, na Ajenda ya Pamoja ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika. Kuanzishwa kwa tawi la Benki Mpya ya Maendeleo ya BRICS barani Afrika kunamaanisha kuwa huduma za benki hiyo zinapatikana kwa nchi za Afrika. Hadi sasa, nchi nyingine za Afrika ikiwemo Misri zimetangaza kujiunga na Benki hiyo, na nchi nyingi zaidi za Afrika zitapata mikopo kutoka Benki hiyo katika siku zijazo. Wakati wa kutoa huduma za kifedha, tawi la Benki Mpya ya Maendeleo ya BRICS barani Afrika pia ni njia ya nchi nyingine ya Afrika, na mashirika ya kikanda ya Afrika kushiriki katika ushirikiano wa BRICS.

Licha ya uchumi, uratibu wa sera pia ni njia muhimu kwa nchi za Afrika kushiriki na kufaidika na mfumo wa “BRICS+”. Katika miaka ya hivi karibuni, nchi za Afrika zimebadilishana maoni na kuratibu misimamo na nchi za BRICS katika mikutano ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa kuhusu masuala muhimu mbalimbali yakiwemo mabadiliko ya hali ya hewa, mazungumzo ya WTO, na kutoa sauti ya pamoja ya nchi zinazoendelea duniani.
 
Bila shaka wanachama wa huu muungano pia ndio wenye hazina Kubwa ya chuma Duniani maana ukiingia top 5 ndio nchi hizi zinaongoza kuchimba vanadium steel chuma kigumu kinachotumika kwa engine za rocket, crankshaft, gear na hata magari magumu ya kazi za ujenzi au kijeshi
 
Taratiiibu mnyama anauawa bila huruma, masikini jamani hiki kitakuwa kifo kibaya Sana kwa mnyama mwenye mikwala mingi 🤔🤔🤔
 
Hamna ushirikiano hapo ni uzugaji tu,

China na India Wana mgogoro muda wowote kinawaka,

Russia ndio huyo, vita vya Ukraine vishamshinda muda wowote anatemeshwa bungo.

South Africa ni mshiriki dhaifu,

Wapo pale kuonekana wapo lkn hawapo
 
Hakuna kitu hapo ni propaganda tupu. China hawezi kumsaidia mtu kwa sababu ana mamilioni ya watu wasio na hili wala lile na China siku zote hataki mtu mweusi afaidi hata akikuajiri ujue una shida.

Muhindi ndio wale wale hata siku moja mhindi hawezi kukubali mwafrika apige hatua yoyote kimaendeleo tunao hapa tunawaona.

Mrussia ni mtu ambaye haamini kwamba kuna mtu anaweza akasaidiwa katika dunia hii yeye anaamini kama huwezi kujikwamua kiuchumi mwenyewe basi hiyo ni shauri yako na wala haimhusu.

Brazil ndio bado wanajua kwamba bado wana safari ndefu kufikia malengo yao na shida za kiuchumi walizonazo na madeni makubwa kwa mashirika ya kifedha duniani, hawana uwezo wa kusaidia mtu.

Afrika Kusini ndio kabisa, watu wenye roho mbaya ni hakuna mfano afadhali hata kama ingekuwa utawala wa makaburu, hata waafrika wanaotoka kwenye mataifa mengine hawawataki. Leo hii wanawathamini wachina kuliko hata watanzania waliojinyima kuwapigania dhidi ya ubaguzi wa rangi.

Hiyo Bricks kama mtu anaota ndoto kwamba inaweza ikaisaidia Afrika basi anajidanganya sana kwani hiyo Bricks iliundwa kwa ajili ya maslahi ya mataifa hayo tu na haituhusu sisi na wala tusitegemee kupata chochote hapo.
 
Hakuna kitu hapo ni propaganda tupu. China hawezi kumsaidia mtu kwa sababu ana mamilioni ya watu wasio na hili wala lile na China siku zote hataki mtu mweusi afaidi hata akikuajiri ujue una shida.

Muhindi ndio wale wale hata siku moja mhindi hawezi kukubali mwafrika apige hatua yoyote kimaendeleo tunao hapa tunawaona.

Mrussia ni mtu ambaye haamini kwamba kuna mtu anaweza akasaidiwa katika dunia hii yeye anaamini kama huwezi kujikwamua kiuchumi mwenyewe basi hiyo ni shauri yako na wala haimhusu.

Brazil ndio bado wanajua kwamba bado wana safari ndefu kufikia malengo yao na shida za kiuchumi walizonazo na madeni makubwa kwa mashirika ya kifedha duniani, hawana uwezo wa kusaidia mtu.

Afrika Kusini ndio kabisa, watu wenye roho mbaya ni hakuna mfano afadhali hata kama ingekuwa utawala wa makaburu, hata waafrika wanaotoka kwenye mataifa mengine hawawataki. Leo hii wanawathamini wachina kuliko hata watanzania waliojinyima kuwapigania dhidi ya ubaguzi wa rangi.

Hiyo Bricks kama mtu anaota ndoto kwamba inaweza ikaisaidia Afrika basi anajidanganya sana kwani hiyo Bricks iliundwa kwa ajili ya maslahi ya mataifa hayo tu na haituhusu sisi na wala tusitegemee kupata chochote hapo.
Wamagharib ukishirikiana nao wanataka uwe shoga,eidha uwabomoe au wakubomoe.

Nadhan kila upande una changamoto zake chakuzungatia ni maslah ya nchi bila ya kuuza utu.
 
Africa Kusini Ilishaendelezwa muda mrefu na makaburu kabla BRICS haijafikiriwa kuwepo.

Halafu nchi nyingine za Africa ukiondoa Africa Kusini zitafaidikia vipi na huo muungano uchwara??
 
Back
Top Bottom