Ushirikina Uwanja wa Taifa Usiku huu kuelekea Derby ya Kariakoo

Chukwu emeka

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2018
Posts
24,314
Reaction score
38,919
Nimepita hapa Uwanja wa Taifa kuna kundi la watu linazozana kumbe ni Makomandoo wa Yanga na Simba wamekuja kulinda Uwanja ili kuzuia vitendo vya kishirikina,hizi timu kwa Tanzania imekuwa zaidi ya imani za dini kiasi kwamba kila upande unatumia nguvu nyingi ambazo wangewekeza kwenye mechi za kimataifa timu hizi zingekuwa zinafika hadi fainali.

Ukizaliwa Tz lazima uwe upande mmoja kama si Yanga basi utakuwa Simba mtu akikwambia hana timu kati ya hizi anakudanganya.Basi acha tuendelee kuziabudu tu na porojo za kina Hajji Manara na Dismas Ten.
 
Ushirikina ndiyo dini yenye wafuasi wengi sana Tanzania
 
Katika hili naomba umuondoe Dismas Ten bali Haji Manara linamhusu zaidi.
 
Kuna kadogo ka simba kana preach ushirikina humu ndani hamjakaona tu??
 
Mkuu, wengine Jana usiku walikuwa pale makaburi kinondoni wakichawia.. Yaan duuh bongo Nyosso
 
Nijuavyo mimi huwezi kulinda kwa style hiyo wala kumzuia mchawi kwa kuweka makomandoo muda ukifika hata hao makomandoo hawatajua kitu.
Wazee wa kazi wanaingia na chopa hapo biashara inaisha au madude yanaagizwa tu hapo kazi inaisha.Msilete mchezo na uchawi ni nguvu ya maombi pekee ndiyo inayoweza siyo mabondia wenu hao.
Nijuavyo anayefanikiwa ni yule mwenye skills kubwa kumpita mwingine.
 

Hao watakuwa kina Team Genta, kuna uzi wake humu akitaadharisha kitu walichofanya hapo kwa Mchina ati lazima mtu afe ikiwa Yanga wakitaka kutegua mitego yao. Ukistaajabu y'a Musa....
 
Mkuu acha uongo mbona tumeingia hapo na kuzika mbuzi katikati ya uwanja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…