USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

We mdada na wewe unaweza kufuga!!!? Mimi nadhani wewe ni wale wanaovaa viatu virefu na jeans huku wakiwa na kucha za kubandikiza. Karibu kwenye ujasiriamali.
Looh hisia zako zinakudanganya jamani.... Santeee ntakaribia muda si mrefu
 
kuku wa kienyeji wanalipa ikiwa utapata chakula cha kutosha kutengeza viini ili viwe vinawapa hali ya kuihitaji kutaga, kuku hawa inabidi kwanza uwachanganye na kuku wa kienyeji wa malawi, alafu akianza kutaga, jaribu kuhesabu mayai mara nyingi hutaga kumi na mbili hadi 14, chunga sauti yake akianza sauti ya kulalia, ukimukuta unamchukua unamwogesha na sabuni ya homo siku mbili , anapoteza ile joto iliyotayarishwa kwa ajiri ya mayai, baada ya siku tatu huanza utaga tena.
 
Umenitoa matongo-tongo katika hii industry. Nitakutafuta
 
Mkuu shukrani kwa maelezo mazuri, yanatia Moyo kwa ambao tunataka kuanzisha miradi ya kuku wa Kienyeji. Tunaweza kujifunza mengi kupitia watu kama nyie wenye uzoefu kama wewe na Ginner
 
Kuku wangu mmoja ameanza tena kulalia mayai tena nimempa mayai 23 nategemea atotoe yote. Nitawatumia picha ya namna ya kumwekea mayai kwa beseni la kunawia.
Picha ya kuku alolalia mayai 23.
 

Attachments

  • 1473772610003.jpg
    34.6 KB · Views: 324
  • 1473772630265.jpg
    50.7 KB · Views: 346
  • 1473772670693.jpg
    56.4 KB · Views: 315
Nitakutafuta ndg nimekuelewa. Huyo jamaa kachemka lkn nae niuelewa wake..
 
Mkuu shukrani kwa maelezo mazuri, yanatia Moyo kwa ambao tunataka kuanzisha miradi ya kuku wa Kienyeji. Tunaweza kujifunza mengi kupitia watu kama nyie wenye uzoefu kama wewe na Ginner
Asante kwa mchango wako mkuu.kiukweli kama unataka kua mfugaji usiogope wala kusikia maneno yenye kukatisha tamaa.mm nilipata maelezo mengi na maandiko mengi tena humu jf hasa jamaa mmoja aitwae Gazeti ana uzi wake humu.nilisoma makala yote bila kuacha hata coment moja.nikaanza kufuga.kiukweli mwanzo nilipata changamoto saana nakumbuka mara ya kwanza nilianza na kuku wawili baada ya kama miezi minne nikawa na kuku zaid ya 40. Kilichotokea ni malaika wako ndo wanajua maana wooooote walikufa baada ya kupata ugonjwa.nilikula kuku mpaka wakanikina moja leo mm hua Sili firigisi maana zilinikifu kabisaaa!mama yoyo akapata hasira akaniambia hakuna kufuga tena mpka tuhamie kwetu coz nilikua nimepanga! Nami ckua na ubishi maana yy ndo mhudumiaj mkuu hapa hom.nikawa nasoma makala mblmbl kujiongezea maujuzi.nikshamia hom kwangu nikaanza na kuku wawili tena baada ya miezi 4 nikapata kama 60 pamoja na makinda nao pia nikapata mtikisiko wakapata ugonjwa nikabak na mmoj nikaanza tena. Sasa nimeanza kutulia maana nimejifunZa mengi.hakuna kukata tamaa.
 
Mkuu kipekee nimejifunza mengi kupitia hii makala yako, na kama ntakua na plani ya kufuga kuku ni dhahiri ntakutafuta nipate mwongozo na matirio zaidi
 
Safi Sana Mkuu, Tunashukuru kwa kututia moyo, Miaka mi3 inatosha kabisa kukupa ujuzi na uzoefu kuhusu huu mradi, Ni dhahiri tutajifunza mengi
 

Dah! Safi Sana Mkuu, Kuku wangu wako mbioni kuanza kutaga, Naamin huu muongozo utanisaidia sana. Kiukweli mwanzoni wakiwa na miezi mi3 walikuwa wanakufa sana, karibia 30 hivi. ila sasa nashukuru mungu wamekuwa wakubwa vifo zimekoma na walibakia kama 100 hivi.

Mkuu kwa Kilo 100 baada ya kuzichanganya zinatosha kulisha kuku wangapi na kwa muda gani? Na je chokaa ni chokaa tuu hata hii inayotumika kwenye Ujenzi inafaa. Nauliza kaama huwa nasikia kuna chokaa maalumu kwa ajili ya kuku, Kwa kipindi chote hicho tumekuwa tukiwapa chakula kilichoandaliwa tayari
 
Hongera mkuu! Huna hiyana Mungu atakuongezea! Mm sio mfugaji wa kuku, na wala sitegemei kufuga kuku kwa maengo ya biashara, ila nimeukubari mchango Wako!
 

mkuu naomba nitolee maelezo maeneo machache kuhusu bandiko lako hapo juu ulilokuwa kwa wema kabisa ukikosoa baadhi ya Hoja zangu. nashukuru sana kwa maelezo yako mazuri yaliyojitosheleza, ila ningependa kuzungumza mambo machache juu ya hoja zako kama ifuatavyo

“Ningefarijika sana kama unge declare interest kuwa wewe ni mfanya biashara wa hao kuku uliowapigia debe, hata ukaweka na picha zao na namba yako, kuliko kuwakatisha tamaa wafugaji waliojikita ktk ufugaji mdogo mdogo wa kuku wa kienyeji.
Pia nawatia moyo wafugaji wote wasikatishwe tamaa na maandiko kama hayo bali yawe chachu ya wao kujua zaidi mbinu mbali mbali za kupata kuku wengi ndani ya muda mfupi na wasichoke kujifunza.

kama utanataka kujua chochote kuhusu kuku wa kienyeji njoo in box nitakusaidia bila ya malipo yoyote, mimi sio mfanya biashara, nami nakaribisha kukosolewa. “




Kwa namna dunia na taifa linavyohimiza juu ya kilimo cha kibiashara, nitashangaa sana kama mfugaji au mkulima aone aibu kukiri kuwa yeye ni mfanyabiashara ya kilimo na ufugaji.

Dunia ya sasa tunaondokana na dhana ya kilimo na ufugaji wa mazoea ambao umekuwa unatumika na kwa miaka kadhaa, na kufanya shughuli hizi kuwa rasmi na kufuga au kulima kwa kulenga soko.

Nitoe angalizo tu, kwa wafugaji na wakulima, kama utaingia kwenye shughuli hizi za kilimo na ufugaji bila ya kuwa na mpangilio mzuri wa namna ya kuendesha shughuli hizi kibiashara nakuhakikishia unafanya mchezo wa mdako. Utatelekeza shamba kama wakulima wa nyanya uko dumila

Ifikie hatua hizi shughuli zifanyike kibiashara, wakulima wawekeze kwenye mbinu za kuendesha miradi yao kibiashara Zaidi na si kwa mazoea. Hivyo basi, naomba nikuunge mkono kwa hoja yako ya kudeclare interest ya kuwa mfanyabiashara.



I declare interest: “Mimi ni mfanya biashara ya ufugaji, najitahidi kuepukana na mbinu za ufugaji zisizo na tija. Nimejitajidi kuepukana na madalali waliokuwa wakirudisha nyuma jitihada zangu za biasahra hii ya ufugaji kwa kujijengea utegemezi kwenye mnyororo wote thamani.



Namiliki kampuni ya ufugaji, Backyard (T) LTD, inayojishughulisha na ufugaji mdogo mdogo wa majumbani hasa at the backyards, hivyo basi,ufugaji wangu ni biashara rasmi kabisa na naiiendesha kitaalamu.



Ili kuondokana na utegemezi katika ufugaji, nimeweza kufungua kiwanda kidogo kwa ajili ya uzalishaji wa vifaranga na kwa sasa nazalisha wastani wa vifaranga 1000 chotara kila wiki (kila jumatatu).



Pili,nimekuwa nanyonywa sana na madalali wa kuku hasa wanapokuja kununua kwa bei isiyo ya soko. Kutatua hili, nimefanikiwa kumiliki machinjio yangu ya kisasa kwaajili ya kuprocess nyama ya kuku na kusambaza kwenye masoko rasmi hasa high profile hotels, restaurants supermarkets etc. brand yangu ya kuku inaitwa backyard frozen chicken. Machinjio yangu si makubwa sana,ila yana uwezo wa kuprocess mpaka kuku mia tatu kwa saa. Kwa mahitaji yangu yanatosha kwa sasa.

Mimi si mfugaji, ila Ninafanya biashara ya ufugaji, na ninajivunia hili.



“kuku wa kienyeji wanataga mayai 15 hadi 20 na sio kwa siku za mfululizo kuna siku nyingine huwa hatagi na hii inatokana na kutokushiba vizuri, nakubali kuhusu muda wa kulea kuwa ni siku 50 hadi 60. unachotakiwa kufanya siku tatu baada ya kuku kutotoa vifaranga, mnyang'anye vifaranga na uviweke mbali nae huko vipatie chakula cha kukuzia stater, maji ya kunywa changanya na glucose, pia weka na chanzo cha joto kama ile mtungi wenye mkaa wa moto ndani yake.ukifanya hivyo itamchukua kuku huyo uliemnyang'anya vifaranga wiki mbili na kuanza tena utagaji.kwa mwaka atatoa kati ya mayai 100 hadi 160 kwa uhakika.”



Nakubaliana na wewe kuhusu kutumia mbinu mbadala kumfanya kuku aongeze Zaidi utagaji, ikiwa ni pamoja na kumnyanganya vifaranga kila baada ya siku tatu baada ya utotoleshwaji. Swali, does it worth your efforts? Wakuu tusiangalie ule ufugaji wa mazoea ambao tumeshauzoea hapa nchini wa kuwa na kuku wawili mpaka kumi bandani ambao mbinu hizi zinaweza kuwa applicable, tuzungumzie kwa context ya ufugaji wa kibiashara, pale unapokuwa na kuku 500-1000 bandani, kwenye hali kama iyo tunafanyaje. Tuzungumzie kuhusu efficiency katika utotoleshwaji wa mayai, tujiulize kuhusu variation ya umri wa vifaranga, maana kwa mbinu iyo unaweza ukawa na batch Zaidi ya nne kwa week ya vifaranga vilivyotofautiana umri, vipi kuhusu kuwahudumia kwa vitu kama chanjo na madawa etc. Mkuu master the trade. Ufugaji ni biashara.





“uhifadhi wa mayai ya kienyeji sio mgumu, yanakaa bila ya kuharibika kwa muda wa mwezi mmoja, unachotakiwa kufanya, hifadhi mayai yako ktk trey ya mayai, pia chunguza kama yai lina ufa hilo usilihifadhi litumie kwa kula mwenyewe na familia, pia weka mayai yako sehemu ya wazi ambayo ina mwangaza wa kutosha, kuyaweka mayai sehemu isiyo na mwangaza kutapelekea mayai kuanza kutunga kifaranga ndani yake (hiyo ni kwa mayai ya kuuza kwa matumizi ya lishe)
kama unahifadhi yai la kutotolesha hilo halitakiwi lizidi siku 14 uwe tayari ushampa kuku kwa ajili ya kuatamia.
kwa faida yako na wengine si lazima kuku wa kienyeji apandwe na jogoo ndio atage, umri wake wa kutaga ukifika tu ataanza kutaga, ambao ni miezi sita hadi saba
.”


Kinachofanya yai la kuku wa kienyeji liharibike ni kwa vile liko fertilized. Its just a simple biology na iko wazi kabisa. Mara nyingi yai la kuku wa kienyeji huwa limerutubishwa na jogoo. (nikimanisha lina mbegu). Hivyo yai hili lililorutubishwa linahitaji kiasi flani cha joto ili zile mbegu kuanza kujijenga na kuwa zygote, embryo na baadae kuwa kifaranga kamili.

Nitaweka attachment ya stages za ukuaji wa kifaranga ndani ya yai hapa baadae kidogo, ila ni siku ya nne tu kama eneo lina joto la juu, (kwanzia nyuzi joto 30 kuendelea) yai huanza kutengeneza mishipa midogo ya damu na siku ya sita baadhi ya viungo vya kifaranga vinaanza kuonekana. Hivyo basi, kuweza kulihifadhi yai hili, ni lazma lihifadhiwe kwenye mazingira yenye baridi ikiwezekana chini ya nyuzi joto 26 ili kusimamisha development ya kifaranga ndani ya yai.

Ili yai liwe kifaranga, linahitaji kiwango cha nyuzi joto cha 37.8 kisichobadilika sana kwa muda wa siku 21, kwa vile joto la mazingira hupanda na kushuka, na mara nyingi haifiki kiwango kinachohitajika ili kifaranga kizidi kujijenga, maendeleo ya ukuaji wa kifaranga husimama ndani ya yai na baada ya muda uoza na kuywa viza.



Uwezo wa wafugaji kuweza kumaintain kiwango hiki cha joto si mkubwa, kwa wakazi wa maeneo yenye joto ni ngumu sana kuhifadhi mayai haya bila kuwa na chumba kilichofungwa air condition.

Kwaiyo kwa hili la uhifandhi kuwa changamoto sitafuta kauli yangu.



Pia bei ya kuku wa kienyeji zaidi kutokana na ladha yake na wala sio kilo zake”.



Ndugu yangu, kilimo na ufugaji ni biashara, liweke hili kichwani kwanza ndipo uchallenge baadhi ya hoja zangu. Kama hutakuwa na malengo ya kufuga kibiashara kamwe hatuwezi kuongea lugha moja. Naomba nikujibu kama ifuatavyo.



Ladha ya kuku hutokana na chakula anachokula na si vinginevyo. Leo hii ukichukua kifaranga wa kuku asilia toka singida mfano, ukamlisha chakula cha layers kwa muda wake wote wa ufugaji, hatakuwa na ladha ya kuku wa kienyeji, hivyo hivyo kuwa kuku wa kisasa, ukimchukua broiler leo, au layers, kwanzia akiwa kifaranga akawa anafugwa ka mazingira asilia, kumwachia nje akala majani, panzi na wadudu wengineyo, ukija kumla kuku huyu akishakomaa ladha yake haitakuwa tofauti na kuku wa kienyeji. Kuna baadhi ya wafugaji wanawapa kuku wao wa kisasa majani tu ilimradi kiini cha mayai yao kiwe cha njano na iwe na ladha asilia. Kwaiyo ndugu yangu ladha hutokana na unachomlisha kuku na wala haitokani na aina ya kuku.



Pili umezungumzia bei ya kuku, kwa hapa sitatumia nguvu nyingi kutoa maelezo kwani umeshadeclare interest kuwa, wewe si mfanyabiashara.

Ukiwa mfanyabiashara ya ufugaji soon or later, utagundua soko la kuku si hili la kumuuzia jirani yako kuku wawili kwaajili ya sikukuu kwa sh 30,000 ukaona inalipa, kwani soko la mtaani halina standards.

Mfanyabiashara ya ufugaji huu ni wakati wa kufikiria kupata soko la rasmi la hotels au super markets wanaotaka mzigo wa Zaidi ya kuku 500 kwa week au kwa mwezi.

Au soko la export ambalo wao wanasema supply tani tano za kuku wala hawako interested kujua watakuwa kuku wangapi, kama ni wawili sawa, kama ni 20,000 sawa ila wanataka uzito. Sasa ndugu sijajua unafanya ufugaji kwa malengo gani na unatarget soko gani, nisingependa kukupinga maana sijajua malengo yako ya ufugaji ni ya nini, either ni kwaajili ya passion tu ya kuona kuku wako bandani au unalenga soko.





Pamoja na hayo yote, nashukuru sana kwa challenge, kwenye biashara si vyema kuwa na rigid mind, lazma kusikiliza wengine wanafanya nini iliujifunze Zaidi. Nakiri nimejifunza mengi kwa hoja zako na ninaahidi kuzifanyia kazi.

Pia nashauri, wanajaamii kupima, kwamba wapi wanaweza kufanya study za mbinu za ufugaji holela na wapi wanaweza kupata mbinu za ufugaji wa kibiashara.
 
Ginner amenikosha, ila nawe umenikuna haswaaa! Sasa nakupataje?​
 
Mkuu ningeanza kukupongeza kwa makala au tafiti yako hii. Kisha ningependa nitoe maoni yangu kama mfugaji anaejifunza kufuga kuku wa kienyeji (pure). Kuhusu muda wa kuharibika mayai imekuwa tofauti kwa upande wangu, hukaa zaidi ya wiki mbili bila kuharibika kwa kipindi chote cha kiangazi sijui nisubiri msimu wa joto kali. Kuhusu bei pia ya kuku wa kienyeji nadhani koo/mtetea anaanzia 14,000/- hadi 17,000/- kutegemea na mahali unapouzia na matukio ya nyakati kama sherehe za kidini. Bei hiyo ni kwa Dar na kuku sio lazima azidi uzito 1kg. Wateja wako kama ni supermarkets au hotel labda ndio hupima uzito lakini masokoni kama Kisutu, Mwenge, na mitaani hawapimi uzito kwa mizani wakati wa kununua. Majogoo waliokomaa vizuri bei ni 17,000/- hadi 25,000/- bila kujali uzito bali umbo. Huwa wananuliwa sana hivyo soko sio tatizo. Changamoto kubwa kuliko zote ni malisho/chakula ni gharama kubwa sana ukizingatia inabidi wafungiwe ktk sehemu flani lakini wale pumba na majani/nyasi pamoja na wadudu ili kutunza ladha yao na rangi ya mayai yao. Pia bei za samaki ulizosema ni za zamani sana kwani sasa 1kg ya samaki aina ya tilapia(sato) inafika 10,000/- lakini siku chache zijazo itashuka kufika 8,000/- hadi 9,000/-. Mwisho wa yote ningependa kuuunga mkono mengi uliyoyaeleza katika tafiti yako. Angalizo ni kuwa mimi ndio kwanza nimeanza ufugaji wa kuku wa kienyeji miezi michache hivyo mengi siyajui. Hapo awali nilianza kununua vijijini na kuwauza moja kwa moja nikaona bora nianze kufuga.
 
Kwa nyongeza ningependa nimuunge mkono mdau "Mfuga kuku" maelezo yako ya kuku mbadala kiasi fulani na baadhi ya hoja zako zimekuwa na mlengo wa kufanya PROMO ya bidhaa zako yaani hao Cross breed e.t.c. Kitu ambacho sio dhambi lakini ingekuwa vema ungekuwa neutral flani au ungeweka tangazo lako la hao kuku kule jukwaa la matangazo ya biashara. Pili kulikuwa hakuna ulazima wa kusema umri wako kujaribu kuonesha mafanikio uliyopata haraka kwa hii biashara na elimu yako, hii ni kama aina ya majivuno/majigambo flani. Kwani sisi tunaweza kuthibitisha vipi umri wako hapa JF? Na je ulifanikiwa haraka bila kuwezeshwa na mtu/familia? Pia hatuwezi kuthibisha kama umefanikiwa kiuchumi ktk biashara zako kwani kuwa na kampuni au kiwanda haimaanishi vinaleta faida kubwa na havileti madeni makubwa kwako. Kumalizia sio dhambi kuwa na majigambo na mafanikio yako kiuchumi na kielimu lakini it sounds unprofessional, though it might inspire young fellows.
 
Chokaa c ile ya ujenzi IPO maalum maduka ya vyakula vya kuku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…