USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

Naomba ni tofauti ane na mtoa mada na bahati nzuri mm mwenyewe binafsi nimeshafuga kuku wote hao nilisha fuga kuanzia kuku wa nyama, mayai chotara na kienyeji na matokeo yake kuku wa kienyeji waliyo mbegu bora wamekua ni wa faida kubwa kuliko wote waliotajwa hapo juu mkihitaji ufafanuzi nitawapa
 
FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU KWA NJIA YA KIENYEJI


Kuku huleta faida kwa jamii. Zaidi ya hayo, ufugaji wa kuku na nguruwe waweza kuimarishwa pasipo gharama nyingi ukilinganisha na mifugo wengine.
· Hutupatia fedha kwa kuuza nyama na mayai
· Mayai ni chakula kilicho na madini muhimu na kisicho ghali katika soko lolote. (madini kama methionine na cystine), madini haya ni muhimu sana kwa afya ya watu hasa watoto wachanga. Pia hutupatia protini.
· Kinyesi cha kuku ni mbolea safi
· Kiwanda asilia cha kutotoa vifaranga
· Gharama za kuanzisha na kuendeleza ni nyepesi
· Kitoweo chepesi na rahisi kwa wageni, kitoweo hakihitaji hifadhi hutumika mlo mmoja au miwili na kumalizika
· Jogoo hutumika kama saa inapowika
· Manyoya ya kuku hutumika kutengenezwa mapambo mbalimbali, mito na magodoro

Kuku ndiye mnyama wa kipekee anayeweza kuishi mahali popote hapa bila kuadhiriwa
na viwango vya hali ya hewa. Ufugaji wa kuku ndio shughuli inayofanyika kwa wingi duniani kuliko ufugaji wa aina yeyote. Mayai yaweza kuwekwa mahali kwa muda mrefu bila kuhitaji barafu. Hautahitaji kuhifadhi kuku kwa njia yoyote, kwani nyama yake hupatikana pale unapohitaji kwa kuchinja.

Upungufu wa kuku wa kigeni ukilinganisha na wale wa kienyeji ni kama ufuatao:
• Kuku wa kigeni hawawezi kukalia na kuangua mayai, hivyo basi wahitajika kununua vifaranga
• Vifaranga wa kigeni huhitaji utunzaji maalum na vyakula maalum
• Kuku waliozalishwa kwa njia ya kisasa huhitaji chakula kingi ili kutaga mayai
• Kuku wa kisasa huhitaji zaidi kuchanjwa dhidi ya magonjwa ukilinganisha na wa kienyeji (japo nao huhitaji chanjo);
• Kuku wa kutaga mayai huhitaji mwangaza wa stima (saa 14 kwa siku) ili kutaga mayai
Kwa kuongezea, rangi ya nyama na mayai ya kuku wa kienyeji huvutia kuliko ile ya kuku wa kisasa.

Hivyo basi najaribu kuendeleza na kuhimiza ufugaji wa kuku wa kienyeji.
Iwapo mkulima ana jogoo mmoja na kuku kumi na mbili, basi kila mwezi waweza kupata kuku
akikalia mayai 10-12 kwa mwezi (mayai yote kwa wakati mwingi hayataanguliwa) kuna hakikisho la
kupata vifaranga vinne kila mwezi. Kuku mzima atachukua miezi minne kuchunga vifaranga
walioanguliwa. Kwa hivyo, kati ya kuku wote kumi na mbili kila mara kutakuwa na kuku wanne
wakitunza vifaranga, huku wale wengine wanane wakitaga mayai.
Kuku waliofugwa kwa njia ya kitamaduni hupata vyakula vyao kwa kutafuta mbegu, wadudu
nyongonyongo, n.k; Lakini kuku hawa hukosa vyakula vya kutosha vilivyo na nguvu ili waweze
kutaga mayai. Vyakula vya kutoa nguvu daima huwa ni haba.
Waweza kuwalisha kuku kwa nafaka ili wapate chakula cha nguvu (mfano kilo moja ya nafaka
iliyopondwa kila siku kwa kuku 10), nafaka hii yapaswa kuwa kavu. Vifaranga wapewe kiasi kidogo
cha nafaka au mchele wiki za kwanza. Kuku wanaolishwa nafaka baada ya kujitafutia chakula nje
huongeza idadi ya mayai (kutoka asilimia 20-25% hadi 40-50%). Kuna umuhimu wa kuhifadhi
nafaka kama lishe badala ya kuuza kwani utapata mayai mengi ambayo baadaye utaweza kuuza.
Hautahitaji kununua vyakula vya protini kwani kuku hujitafutia lishe la protini.
Ikiwa hauna nafaka, waweza kutumia vyakula vya mzizi au ndizi. Vyakula vya aina hii hata hivyo,
huwatatiza kuku wanapovitonogoa, kiwango cha mayai sio kikubwa kama cha wale wanaolishwa
nafaka.
Kwa kuwalisha kuku kwa nafaka utapata hakikisho la mayai manne kwa siku kutoka kwa wale kuku
wanane. Iwapo hakuna nafaka, kati ya kuku wanane wanaotaga utapata mayai mawili tu kwa siku.
Ni bora kutumia nafaka hii kama lishe kuliko kuuza na hatimaye kununua vyakula vya dukani.
Kuku kumi na mbili na jogoo mmoja wanaolishwa kwa kilo moja ya nafaka kila siku waweza
kuelezwa hivi:
• Waweza kuuza kuku wanne kila mwezi na kujaza pengo hilo na wale vifaranga (vifaranga
wanne huanguliwa kila mwezi) na
• Dazani kumi za mayai kila mwezi (mayai manne kila siku).
 
Tatizo si kuku, bali namna ya kuwatunza kwa gharama nafuu.
Wengi wa kuku chotara wanakula, hata zaidi ya 150g, kwa siku. Ili hali hao kienyeji pure wanakula takribani 100g kwa siku.
Yote kwa yote, chakula kamili cha kuku ni bei kubwa sana, na inachukua miezi mingi kwa kuku kienyeji pure kukua ikilinganishwa na hao chotara.
 
Nashukuru kwa kukubali kupokea challenge,
kwa ufupi andiko lako limejaa upotoshaji mkubwa na linalenga kuwakatisha tamaa, wajasiriamali wadogo wadogo ambao wanapendelea kufuga kuku wa kienyeji.
Pia nimegundua mambo makubwa mawili,
1. Bila shaka utakuwa unauza hiyo aina ya kuku amabayo unadai kuwa ni wazuri.
2. Bado hujajua mbinu mbali mbali za ufugaji wenye tija.

Hebu tazama hapa, ulichoandika.

Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

kuku wa kienyeji wanataga mayai 15 hadi 20 na sio kwa siku za mfululizo kuna siku nyingine huwa hatagi na hii inatokana na kutokushiba vizuri, nakubali kuhusu muda wa kulea kuwa ni siku 50 hadi 60. unachotakiwa kufanya siku tatu baada ya kuku kutotoa vifaranga, mnyang'anye vifaranga na uviweke mbali nae huko vipatie chakula cha kukuzia stater, maji ya kunywa changanya na glucose, pia weka na chanzo cha joto kama ile mtungi wenye mkaa wa moto ndani yake.
ukifanya hivyo itamchukua kuku huyo uliemnyang'anya vifaranga wiki mbili na kuanza tena utagaji.
kwa mwaka atatoa kati ya mayai 100 hadi 160 kwa uhakika.

Tizama na hapa.

'Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.

uhifadhi wa mayai ya kienyeji sio mgumu, yanakaa bila ya kuharibika kwa muda wa mwezi mmoja, unachotakiwa kufanya, hifadhi mayai yako ktk trey ya mayai, pia chunguza kama yai lina ufa hilo usilihifadhi litumie kwa kula mwenyewe na familia, pia weka mayai yako sehemu ya wazi ambayo ina mwangaza wa kutosha, kuyaweka mayai sehemu isiyo na mwangaza kutapelekea mayai kuanza kutunga kifaranga ndani yake (hiyo ni kwa mayai ya kuuza kwa matumizi ya lishe)
kama unahifadhi yai la kutotolesha hilo halitakiwi lizidi siku 14 uwe tayari ushampa kuku kwa ajili ya kuatamia.
kwa faida yako na wengine si lazima kuku wa kienyeji apandwe na jogoo ndio atage, umri wake wa kutaga ukifika tu ataanza kutaga, ambao ni miezi sita hadi saba.

Pia bei ya kuku wa kienyeji zaidi kutokana na ladha yake na wala sio kilo zake.

Mwisho.

Ningefarijika sana kama unge declare interest kuwa wewe ni mfanya biashara wa hao kuku uliowapigia debe, hata ukaweka na picha zao na namba yako, kuliko kuwakatisha tamaa wafugaji waliojikita ktk ufugaji mdogo mdogo wa kuku wa kienyeji.
Pia nawatia moyo wafugaji wote wasikatishwe tamaa na maandiko kama hayo bali yawe chachu ya wao kujua zaidi mbinu mbali mbali za kupata kuku wengi ndani ya muda mfupi na wasichoke kujifunza.

kama utanataka kujua chochote kuhusu kuku wa kienyeji njoo in box nitakusaidia bila ya malipo yoyote, mimi sio mfanya biashara, nami nakaribisha kukosolewa.







 
Nisaidieni;
kuna kila dalili kuwa bandani kwangu kuna kuku anakula mayai;
naomba msaada ili kuondoa hii kitu.
 
search kwenye web ya hawa jamaa wameweka mchanganuo wa vyakula vya kuku aina zote na kinafanya kazi kweli sema wengi huwa hatuamini hizi vitu bila kujaribu www.rldc.co.tz

Hiyo website haifunguki
 
Nisaidieni;
kuna kila dalili kuwa bandani kwangu kuna kuku anakula mayai;
naomba msaada ili kuondoa hii kitu.

Wape vyakula vyenye calcium kwa wingi kama unga wa mifupa.

Hii itasaidia wao waachane na tabia ya kula mayai ambayo maganda yake yana calcium.

Wanakula mayai kwasababu wanapungukiwa na calcium.
 
Wape vyakula vyenye calcium kwa wingi kama unga wa mifupa.

Hii itasaidia wao waachane na tabia ya kula mayai ambayo maganda yake yana calcium.

Wanakula mayai kwasababu wanapungukiwa na calcium.
Asante kwa ushauri; nitafanya hivyo.
 
N kwel,kuna watu sasa macho yanawatoka balaa,wamekopa na faida ya kuku hawaioni
 
Kwa speed ya kila mtu anafuga Miaka Miwili mingi bidhaa Kama nyama ya kuku na mayai Itakuwa Kama nyanya kwa mwaka huu.. Ingawa ufugaji unalipa Sana
 
Back
Top Bottom