Ushuhuda: Kusomesha mtoto shule ya kiingereza yenye walimu wa Zambia/Malawi /Kenya /Uganda kuna afadhali zaidi kuliko walimu wa hapa kwetu

Ushuhuda: Kusomesha mtoto shule ya kiingereza yenye walimu wa Zambia/Malawi /Kenya /Uganda kuna afadhali zaidi kuliko walimu wa hapa kwetu

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Hiki kitu nimeshuhudia kuna mtoto wa ndugu yangu anasoma shule flani ya msingi darasa la nne, ni shule ya mtaala wa kiingereza ila walimu ni wa hapa kwetu, huwa anafaulu vizuri tu lakini kuna maswali aliniletea nimsaidie ya social studies (maarifa ya jamii) sasa nikawa namweleza swali linamaanisha nini kwa kiswahili ili nione kama kaelewa ndio nimsaidie lakini alikuwa anapata wakati mgumu, ajabu ni kwamba nikimuliza maswali ya homework zake za zamani majibu ananipa vizuri ila nikumuuliza maana ya maswali niliyomuuliza inakuwa taabu kidogo.

Pia katika maswali nimeona kwa level ambayo yupo walimu wao wa hapa kwetu wana complicate sana mambo kwenye lugha hasa kwa kutumia misamiati migumu kidogo kwa mtoto wa darasa la tatu.

Kwa upande wa mtoto wangu, nae yupo darasa la nne shule yao ni ya mtaala wa kiingereza ila walimu wengi wametokea Zambia, kiukweli kwenye lugha hata kunipa tafsiri huwa sio tabu na walimu wao sio kwamba hizi kugha wamejifunzia ukubwani bali ni lugha za nchi yao kwa hio kuna njia rahisi zaidi wanatumia ili watoto waelewe.

kuna siku kulikuwa na mhubiri anaeongea kiingerea ilibidi awe anatafsiriwa na , basi mtoto wangu alikuwa nae anatafsiria wenzake vizuri kabisa kiukweli nilikuwa nafarijika, mtu kama kiingereza kimepanda kutafsiri ni ishu ndogo tu.

Mapendekezo:

Ni bora zaidi kumpeleka mtoto kwenye shule ya kiingereza yenye walimu ambao asili ya nchi zao kiingereza ni mojawapo ya lugha za taifa tangu utotoni mtu anaitumia. kama ni kumpeleka mtoto shule ambazo walimu ni wenye asili ya hapa kwetu ambako wengi huanza kujifunza kiingereza sekondari basi tuwe tunajihakikishia lugha wanaielewa vizuri.
 
Elimu ya msingi ya kenya ya shule zao za serikali tu. Ni nzuri sana shida mtoto mdogo anasomaje mbali
Ni kuhusu asili ya walimu wanaofundisha kwemye shule za English Medium hapa nchini, ni bora upeleke mtoto shule ambayo walimu wake wametokea nchi tajwa kuliko walimu wenye asili ya hapa kwetu.
 
Ni kuhusu asili ya walimu wanaofundisha kwemye shule za English Medium hapa nchini, ni bora upeleke mtoto shule ambayo walimu wake wametokea nchi tajwa kuliko walimu wenye asili ya hapa kwetu.
Wabongo kwa kudharau vya kwenu bwana😅 we kama ulikuwa hata presentations unajificha nyuma ya ubao usichukulie kizembe kwa wenzio!

Tupo ambao tunaichapa lugha vizuri tu na tupo njema sana kwenye kufundisha.
 
Wabongo kwa kudharau vya kwenu bwana😅 we kama ulikuwa hata presentations unajificha nyuma ya ubao usichukulie kizembe kwa wenzio!

Tupo ambao tunaichapa lugha vizuri tu na tupo njema sana kwenye kufundisha.
najua wapo wabongo ambao wapo fresh kwenye ngeli lakini wengi ni hawa ze ze ze ze, due to, nadhani umeona hata watu wazito kiingereza kinavyowapiga chenga.

Nakumbuka nilienda kwenye hafla flani pale shuleni kwa mwanangu dj alipiga ngoma ya future - mask. off, kuna mwalimu alimkataza haraka sana asirudie hio ngoma na kweli maneno yaliyokuwa ya kizungumzwa hayafai kwa watoto, lakini muda huo huo nilikumbuka zamani kuna mwalimu wa kiingereza shuleni kwetu inapigwa ngoma ya in da club ya 50 cent kwenye mahafali yeye wala hana hata anachokijua yani mziki umejaa matusi acha tu
 
najua wapo wabongo ambaonwapo fresh kwenye ngeli lakini wengi ni hawa ze ze ze ze, due to, nadhani umeona hata watu wazito kiingereza kinavyowapiga chenga.

Nakumbuka nilienda kwenye hafla flani pale shuleni kwa mwanangu dj alipiga ngoma ya future - mask. off, kuna mwalimu alimkataza haraka sana asirudie hio ngoma na kweli maneno yaliyokuwa ya kizungumzwa hayafai kwa watoto
Huyo DJ kilaza kweli sasa anapigaje mask off kwenye hafla ya watoto😅
 
Ulichofail Ni kumuelezea mtoto kwa kiswahili wakati yy kafundishwa na kielezewa kwa kiingereza siku nyingine jaribu kumfafanulia kwa kiingereza uone km hataelewa asilimia kubwa Hawa watoto vitu vingi wanakuwa wanavijua kwa lugha ya kiingereza ukiwaambia au kuwapa kwa kiswahili huwa wanashindwa.
 
Huyo DJ kilaza kweli sasa anapigaje mask off kwenye hafla ya watoto😅
Sio kilaza, wabongo wengi hip hop ya marekani tunachopendea labda beats na flows pekee, lyrics wachache sana wanaelewa, haya mambo ni mpaka mahakamani huko kiingereza kinapiga sana chenga, rejea interviews za waziri wa elimu aligonga A ya kiingereza lakini kiingereza anachoongea unabaki hoi
 
Sio kilaza, wabongo wengi hip hop ya marekani tunachopendea labda beats na flows pekee, lyrics wachache sana wanaelewa, haya mambo ni mpaka mahakamani huko kiingereza kinapiga sana chenga, rejea interviews za waziri wa elimu aligonga A ya kiingereza lakini kiingereza anachoongea unabaki hoi
Hahahhaha waziri wa mchongo😅. Ananyonga sana kikristo ze pipo is becoz we need zem to be cleva!
 
Ulichofail Ni kumuelezea mtoto kwa kiswahili wakati yy kafundishwa na kielezewa kwa kiingereza siku nyingine jaribu kumfafanulia kwa kiingereza uone km hataelewa asilimia kubwa Hawa watoto vitu vingi wanakuwa wanavijua kwa lugha ya kiingereza ukiwaambia au kuwapa kwa kiswahili huwa wanashindwa.
Ndio maana nmeanzisha hii maada tujue kuna tatizo kubwa sama kwenye hizo shule, binafsi mtoto wangu anateleza tu fresh na uwezi wake darasani ni wastani tu ila lugha anaimudu, kuna siku kulikuwa na mhubiri anaongea kiingereza anatafsiriwa basi kabla hajatafsiriwa mtoto wangu alikuwa anatafsiria wenzake wa karibu kwa kiswahili, pia hata hizi muvi huwa anamtafsiria house girl bila tatizo lolote.
 
Pendekeza, nini Serikali tufanyee!!!??
Ni bora zaidi kumpeleka mtoto kwenye shule ya kiingereza yenye walimu ambao asili ya nchi zao kiingereza ni mojawapo ya lugha za taifa tangu utotoni mtu anaitumia. kama ni kumpeleka mtoto shule ambazo walimu ni wenye asili ya hapa kwetu ambako wengi huanza kujifunza kiingereza sekondari basi tuwe tunajihakikishia lugha wanaielewa vizuri
 
Ni bora zaidi kumpeleka mtoto kwenye shule ya kiingereza yenye walimu ambao asili ya nchi zao kiingereza ni mojawapo ya lugha za taifa tangu utotoni mtu anaitumia. kama ni kumpeleka mtoto shule ambazo walimu ni wenye asili ya hapa kwetu ambako wengi huanza kujifunza kiingereza sekondari basi tuwe tunajihakikishia lugha wanaielewa vizuri
Usisahau kulipia hili tangazo
 
Duh, tunakoelekea mtawapeleka watoto hadi nje ya nchi kutafuta kingereza tu.
 
Back
Top Bottom