Zee la Mandandu
JF-Expert Member
- Nov 30, 2022
- 1,064
- 2,603
Elezea haya ya maji ya kina kirefu na maji mapana yapoje kiongozi?Hii nchi imerogwa na kufanyiwa makafara makubwa mno na kafara kubwa kuliko yote ni lile la bagamoyo la kukimbiza moto, likifuatiwa na la Tanganyika maji ya kina kirefu kisha la Lindi maji mapana
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu tuwekee link nasi tukajioneeNimeamua kuuandika kwa vile upo YouTube, lakini sikubaliani wala kupingana na msimuliaji.
Ni ushuhuda wa bwana mmoja anayejiita Shehe Omari Mnyeshani, Mchawi wa "zamani".
Anadai kuwa kabla ya kuukimbia uchawi, alikuwa Mwenyekiti wa wachawi Tanzania na nje ya Tanzania.
Ikiwa anayoyaongea yana ukweli, basi nchi yetu inahitaji "ukombozi" wa Kimungu. Lakini ikiwa tu ayasemayo ni ya kweli.
Anadai kuwa kabla ya kuachana na uchawi, kuna mwaka walifanya tambiko la Kitaifa la kuisindika nchi, tambiko ambalo lilifanyikia mkoani Lindi. Shughuli hiyo iliwahusisha wachawi wote wa Tanzania. Nafikiri ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 90, kama sijakosea.
Katika hilo tambiko, waliazimia mambo kadhaa, ikiwemo la Waziri Mkuu wa Tanzania kutokushika madaraka ya Urais.
Kwamba, haijalishi Waziri Mkuu atajitahidi kiasi gani, haitakaa itokee awe Raisi wa JMT. Akishaushika tu Uwaziri Mkuu, na Urais anakuwa ameshaukosa. Kama ndivyo, na ikiwa nguvu kubwa kuliko ya wachawi haitaingilia kati, Majaliwa hayakuwa Rais wa JMT. Vile vile, isingewezekana kwa John Malecella, David Msuya, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na Mizengo Pinda kukushika Urais wa Tanzania. Wote hao walishashika nafasi za Uwaziri Mkuu.
Hilo tambiko lilikuwa na athari kwa mkoa wa Lindi, kwamba watu wake hawatakuwa na uwezo mzuri kiakili.
Ardhi ya Lindi ilitolewa kama kafara kufuatia hilo tambiko la kichawi kufanyikia huko.
Inasemekana kuna kipindi Serikali iliweka jitihada ya kuwasisitiza watu wa huko kutumia chumvi ya viwandani ili kuwaongezea uwezo wa kufikiri, kwa kudhaniwa kuwa ni ukosefu wa madini muhimu ndiyo uliokuwa ukiwapelekea watoto wa huko kuwa chini kimasomo. Lakini kwa mujibu wa huyo mchawi wa zamani, ni kwa sababu Lindi ilitolewa kama Kafara wakati wa hilo tambiko.
Wachawi wa Lindi walijulishwa kabla ya hilo tambiko kuwa hayo madhara yatawatokea wana Lindi, na wakataka likafanyikie Tanga au Tabora lakini wachawi wa hiyo mikoa wakajitetea kuwa nao walishatoa michango yao siku za nyuma. Wachawi wa Lindi japo hawakutaka mkoa wao uwe duni, walishindwa kulikwepa hilo la tambiko kufanyikia kwao.
Jambo lingine aliloliongelea ni uchaguzi wa 1995. Anadai kuwa katika rada yao ya kichawi, waligundua kuwa mtu aliyekuwa amekusudiwa na Mungu awe Rais wa Tanzania kipindi hicho ni Jackson Makweta. Lakini walipobaini kuwa Makweta anaweza akawa kero kwao, waliamua kupambana naye kwa kumwondolea wazo la Urais, na wakafanikiwa.
Aliyeyasema hayo ni Shehhe Omari Mnyeshani!
Japo sijakubali wala kukataa, nina maswali kadhaa kuhusu hayo madai yake.
1. Ni kweli kuwa watu wa Lindi wana uwezo mdogo kiakili? Mbona Mama Salam Kikwete na marehemu Bernard Membe ni watu wa Lindi lakini wako vizuri upstairs?
2. Unafikiri kwa hoja yake kuwa katika tambiko la mwisho la kuisindika Tanzania kichawi walikubaliana kuwa mtu aliyeshika nafasi ya Uwaziri Mkuu asifanikiwe kuwa Rais wa JMT, inaweza kuwa na mashiko?
3. Kwa mujibu wa simulizi yake, Makweta ndiye aliyekusudiwa na Mungu awe Rais wa JMT 1995. Unafikiri Makweta angefanya vizuri kumzidi Mkapa?
4. Japo masimulizi yake hayawezi kuthibitishwa Kisayansi, unafikiri nguvu za giza zina nafasi kwenye utawala wa Tanzania?
Nashukuru. Nilikuwa sijaiona hiyo typing error. Nitairekebisha....Ni KUZINDIKA Sio KUSINDIKA...Mengine yote ni Stupidity ! [emoji57][emoji57]
Natamani ukutane na Mshana Jr ili akuelimishe kiufasaha.Hawa wanaojiita wachawi hakuna cha uchawi wala nini, hao ni wajanja fulani tu wa kuunganisha dot na kucheza vizuri na historia.
Kwenye hili la waziri mkuu kutokuwa raisi, Ukiangalia historia ya Tanganyika baada ya uhuru ni kweli hakuna waziri mkuu aliyewahi kuwa raisi.
Sasa kwenye uhalisia huo unaweza kutengeneza hadithi lukuki za kimtizamo (dini, uchawi, laana n,k) na watu wakaamini.
Kwa hiyo huyu naye ni wale wale wa kurubuni watu kwa story za kutunga kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Video hiyo hapoMkuu tuwekee link nasi tukajionee
hao walawi wapo hapa hapa bongo au ndio mnataka muongeze wakimbizi?Huo ndo UKWELI, ikiwa huamini kaa hivyo hivyo.
Jambo muhimu ni kuwa, funguo za kuondoa uchawi huo zimepatikana,
Tutapitia mtikisiko kidogo, yanakuja majanga, Matetemeko, sunami, njaa ,mtikisiko wa Muungano nk nk
Baada ya hayo kupita, Nchi yetu itastawi sana,
Mwiko wa kutawala nje ya mwislam au catoliki utavunjwa, atatawala Mlawi.
Tusubiri.
Hahaaa, Mlawi ni code.hao walawi wapo hapa hapa bongo au ndio mnataka muongeze wakimbizi?
Mambo mengine si ya kuandika kiundani elewa hivyo.Elezea haya ya maji ya kina kirefu na maji mapana yapoje kiongozi?
Anaitwa Omari Mnyashani kutoka Tanga.Nimeamua kuuandika kwa vile upo YouTube, lakini sikubaliani wala kupingana na msimuliaji.
Ni ushuhuda wa bwana mmoja anayejiita Shehe Omari Mnyeshani, Mchawi wa "zamani".
Anadai kuwa kabla ya kuukimbia uchawi, alikuwa Mwenyekiti wa wachawi Tanzania na nje ya Tanzania.
Ikiwa anayoyaongea yana ukweli, basi nchi yetu inahitaji "ukombozi" wa Kimungu. Lakini ikiwa tu ayasemayo ni ya kweli.
Anadai kuwa kabla ya kuachana na uchawi, kuna mwaka walifanya tambiko la Kitaifa la kuizindika nchi, tambiko ambalo lilifanyikia mkoani Lindi. Shughuli hiyo iliwahusisha wachawi wote wa Tanzania. Nafikiri ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 90, kama sijakosea.
Katika hilo tambiko, waliazimia mambo kadhaa, ikiwemo la Waziri Mkuu wa Tanzania kutokushika madaraka ya Urais.
Kwamba, haijalishi Waziri Mkuu atajitahidi kiasi gani, haitakaa itokee awe Raisi wa JMT. Akishaushika tu Uwaziri Mkuu, na Urais anakuwa ameshaukosa. Kama ndivyo, na ikiwa nguvu kubwa kuliko ya wachawi haitaingilia kati, Majaliwa hayakuwa Rais wa JMT. Vile vile, isingewezekana kwa John Malecella, David Msuya, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na Mizengo Pinda kukushika Urais wa Tanzania. Wote hao walishashika nafasi za Uwaziri Mkuu.
Hilo tambiko lilikuwa na athari kwa mkoa wa Lindi, kwamba watu wake hawatakuwa na uwezo mzuri kiakili.
Ardhi ya Lindi ilitolewa kama kafara kufuatia hilo tambiko la kichawi kufanyikia huko.
Inasemekana kuna kipindi Serikali iliweka jitihada ya kuwasisitiza watu wa huko kutumia chumvi ya viwandani ili kuwaongezea uwezo wa kufikiri, kwa kudhaniwa kuwa ni ukosefu wa madini muhimu ndiyo uliokuwa ukiwapelekea watoto wa huko kuwa chini kimasomo. Lakini kwa mujibu wa huyo mchawi wa zamani, ni kwa sababu Lindi ilitolewa kama Kafara wakati wa hilo tambiko.
Wachawi wa Lindi walijulishwa kabla ya hilo tambiko kuwa hayo madhara yatawatokea wana Lindi, na wakataka likafanyikie Tanga au Tabora lakini wachawi wa hiyo mikoa wakajitetea kuwa nao walishatoa michango yao siku za nyuma. Wachawi wa Lindi japo hawakutaka mkoa wao uwe duni, walishindwa kulikwepa hilo la tambiko kufanyikia kwao.
Jambo lingine aliloliongelea ni uchaguzi wa 1995. Anadai kuwa katika rada yao ya kichawi, waligundua kuwa mtu aliyekuwa amekusudiwa na Mungu awe Rais wa Tanzania kipindi hicho ni Jackson Makweta. Lakini walipobaini kuwa Makweta anaweza akawa kero kwao, waliamua kupambana naye kwa kumwondolea wazo la Urais, na wakafanikiwa.
Aliyeyasema hayo ni Shehhe Omari Mnyeshani!
Japo sijakubali wala kukataa, nina maswali kadhaa kuhusu hayo madai yake.
1. Ni kweli kuwa watu wa Lindi wana uwezo mdogo kiakili? Mbona Mama Salam Kikwete na marehemu Bernard Membe ni watu wa Lindi lakini wako vizuri upstairs?
2. Unafikiri kwa hoja yake kuwa katika tambiko la mwisho la kuisindika Tanzania kichawi walikubaliana kuwa mtu aliyeshika nafasi ya Uwaziri Mkuu asifanikiwe kuwa Rais wa JMT, inaweza kuwa na mashiko?
3. Kwa mujibu wa simulizi yake, Makweta ndiye aliyekusudiwa na Mungu awe Rais wa JMT 1995. Unafikiri Makweta angefanya vizuri kumzidi Mkapa?
4. Japo masimulizi yake hayawezi kuthibitishwa Kisayansi, unafikiri nguvu za giza zina nafasi kwenye utawala wa Tanzania?
Hapo chini ni moja ya shuhuda zake
Sawa sawaNi muhubiri.
Mbona kama ni kweli?Maeneo yote waliyofanya matambiko nchini hayana maendeleo.
Bagamoyo,lindi,Tanga,tabora kigoma
😀😀😀Umasikini wa watanzania ni kafara lililofanywa na ccm.
Ccm ni muunganiko wa vyama vya kichawi mwaka 1977.
Ibada ya kichawi iliyozaa mwenge ilifanyikia Bagamoyo kabla ya uhuru.Ni kabla ya tambiko
Mwenge ni uchawi kamiliAnachosema ni kweli tupu.
Alikuwa Gwiji haswa.
Mwenge hauna faida yoyote zaidi ya kupoteza pesa na kuwapumbaza watu.
💪Ahsante kwa kunirekebisha
Tufanyeje mkuu kuiponya nchi yetu?Hii nchi imerogwa na kufanyiwa makafara makubwa mno na kafara kubwa kuliko yote ni lile la bagamoyo la kukimbiza moto, likifuatiwa na la Tanganyika maji ya kina kirefu kisha la Lindi maji mapana
Sent using Jamii Forums mobile app
🤣🤣🤣Hahaaa, Mlawi ni code.
Fungua code, usipende vitu laini😀
Ukiona kasema hivyo ujue yeye pia ni Mlawi.hao walawi wapo hapa hapa bongo au ndio mnataka muongeze wakimbizi?