USHUHUDA: Ninavyoyamudu maisha kupitia kilimo cha mbogamboga ndani ya ekari moja tu

USHUHUDA: Ninavyoyamudu maisha kupitia kilimo cha mbogamboga ndani ya ekari moja tu

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,587
Wakuu , pole na hongereni na weekend !

Mimi nimeamua kudeal na kilimo cha mazao ya mbogamboga kwenye eneo langu lenye ukubwa wa ekari moja ninalolimiliki mwenyewe baada ya kulima kwa kukodi mashamba ya watu.

Nalimia Chekereni - Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro.Kandolando ya barabara kuu ya Moshi - Dsm. Ni mbele kidogo ya Njia Panda ya Himo (Kwa wale wenyeji).

Niliacha kazi niliyokuwa nimeajiliwa baada ya kutofautiana na mwajiri wangu (TPC - Moshi) na kuamua nilime tu.

Nilianza Kwa kukodi shamba la ekari 1 kwa TZS 300,000 kwa msimu nikapanda pilipili Hoho aina ya F1.Zao hili huhitaji roughly siku 100 na huendelea kuzaa na ukachuma hata michumo 10 endapo unaendelea kutoa huduma nzuri. Roba 1 la hoho ni kati ya 80 mpaka 100k. Hapa nilipiga hela nzuri sana, zaidi ya 2 mil.

Msimu uliofuata nikaweka cabbage na kuipa matunzo vizuri.Mungu si athumani nikapatamo hela nzuri tu.


Misimu miwili iliyofuata nikalima kitunguu maji aina ya Neptune. Hii mbegu inatoa vitinguu vikubwa na vizuri sana , hupendwa sana na wafanyabishara wa Kenya.

Kifupi ndo hivyo , mambo yanaenda.

Tujikite na kilimo.

Start with small but very smart !
 
Safi, unaendelea kutufundisha tuache uoga, tukimbilie ndoto zetu. Ila unamwagilia au unategemea mvua? Vipi changamoto ya magonjwa ya mimea?

Nguvu kazi, mwingine anaweza kudhani kilimo ni rahisi kama kunywa maji. Kuna kuku wa wiki 4 wametoa watu kamasi. Ila naamini ukiwa na taarifa sahihi na mtaji inawezekana.
 
Mkuu umerahisisha sana yaani baada kukodi shamba laki tatu halafu ikawaje sasa??

Dawa, mbegu,maji,vibarua, wezi, muda,nk vyote hujataja vilikugharimu kiasi gani ila nimeona tu umewekeza laki tatu na kupata faida ya milioni mbili. Hongera sana mkuu.
 
Safi, unaendelea kutufundisha tuache uoga, tukimbilie ndoto zetu. Ila unamwagilia au unategemea mvua? Vipi changamoto ya magonjwa ya mimea? Nguvu kazi, mwingine anaweza kudhani kilimo ni rahisi kama kunywa maji. Kuna kuku wa wiki 4 wametoa watu kamasi. Ila naamini ukiwa na taarifa sahihi na mtaji inawezekana.
Ni kitu gani au kazigani ya kuingiza mapene ambayo haina changamoto ndugu.? au tukae tu pe,beni tukiziogopa hizo changamoto?
 
Mkuu umerahisisha sana yaani baada kukodi shamba laki tatu halafu ikawaje sasa??

Dawa, mbegu,maji,vibarua, wezi, muda,nk vyote hujataja vilikugharimu kiasi gani ila nimeona tu umewekeza laki tatu na kupata faida ya milioni mbili. Hongera sana mkuu.
Ndio kawaida ya kilimo cha WhatsApp na Instagram
 
Back
Top Bottom