Ushuhuda wa breakthrough!

kuna watu wengi sana wanakuja DM wanaandika msg wakielezea matatizo yao na wanataka niwape pesa. Ninajua ni kweli mnaweza kuwa kwenye matatizo, lakini hamtakiwi kuniomba mimi, mwombe Mungu huyo ndiye anaweza kutatua tatizo lako jumla. mwanadamu hawezi kukusaidia. hata mimi nitakusaidia kama nikiguswa na Mungu. kuna watu wengine wanapitia kwenye majangwa kwasababu Mungu anawapitisha kuwafundisha maisha ili atakapowabariki wakumbuke. au ni njia tu ya shule anawafundisha.

ila wengine wanapitia kwenye matatizo kwasababu wamegombana na Mungu na wanapata adhabu. hakuna mtu anaweza kukuokoa kutoka kwenye mkono wa Mungu kama ameamua kukushughulikia. unachotakiwa ni kutengeneza uhusiano wako na Mungu akusamehe na kukuondolea tatizo lako. kuna watu mmeua, mmezini, mmeiba na kuumiza mioyo ya watu, watu hao wamelia kwa Mungu na Mungu ameshuka kuwapambania and you think mwanadamu anaweza kukurescue toka mikononi mwa Mungu? No. cha ajabu ni kwamba, Mungu ni Mungu wa rehema, huwa anasamehe kila anayekuja kwake kutubu.

ila kwa wale wote ambao kiukweli wanapita tu kwenye jangwa, Mungu labda anawafundisha, usimwombe mwanadamu chochote. utapita kwenye jangwa hilo hadi utakapomaliza mtihani wako ndipo Mungu atakuondoa kwasababu labda Mungu ana makusudi. na pengine unapita hivyo kwasababu ameona unaweka macho yako kwa wanadamu, msaada wetu hautoki kwa wanadamu, unatoka kwa Mungu. msaaada wa mwanadamu haudumu, ila msaada toka kwa Mungu hata kama ametumia mwanadamu kukubariki unadumu na hauna majuto. jua kwamba, Mungu hubariki kwa kutumia wanadamu pia, lakini ni mpaka hao wanadamu waguswe na Mungu kufanay hivyo nandio maana utukufu unatakiwa kwenda kwa Mungu kwasababu ni yeye ametoa kwa kupitia mwanadamu. hata mimi leo hii Mungu akinielekeza kwa namna atakayojua yeye nitoe kitu, nitatoa, ila asiponielekeza siwezi.

Kama vile Musa alivyomwinua nyoka wa shaba ndivyo Mwana wa Adam alivyoinuliwa ili kila amwaminiye apate uzima wa milele. mwangalie Yesu, huyo ndiye msaada wako, ukiangalia wanadamu na kutegemea misaada toka kwa wanadamu ni dharau na tusi kwa Mungu.

katika maisha yangu nilishapita kwenye majangwa mara nyingi, kuna kipindi nilikuwa nategemea wanadamu na elimu na kazi. Mungu akaona kumbe sijamwelewa vizuri, akaweka ugumu mioyo kwa wanadamu (ndugu zangu ambao ni matajiri), nilipita kwenye tatizo ambalo hakuna mwanadamu aliyekuwa msaada, nilichekwa na kudharauliwa hadi na watoto wadogo. ndugu zangu walikuwa tayari kusaidia watu wengine ila sio mimi. wale niliowasaidia wakafanikiwa sana ndio walikuwa wakwanza kunicheka na kunitupa. hadi pale nilipoondoa macho yangu kwenye elimu, ndugu na wanadamu, nikawa nimebaki mimi na Mungu tu, nilipoangalia macho yangu kwa Mungu tu ndipo alikuja kuniokoa mazima. that was 12 years ago. nikajifunza kuwa kumbe hatutakiwi kuangalia au kutegemea msaada toka kwa wanadamu. hata hili fungu la kumi naongelea, ni kwamba nilishawahi kubarikiwa, nikawa natoa fungu, nilipokuja kusimama miaka kadhaa ndio milango ikafungwa, hadi mwishoni mwa mwaka jana na mwezi januari mwaka huu 2022 nilipoazimia kuanza. na nimejifunza kitu kwa vitendo, hakuna mtu atakuja kunidanganya tena.

nitayainua macho yangu nitazame milima, msaada wangu utatoka wapi? msaada wangu utatoka kwa Bwana, aliyeziumba mbingu na nchi, asiuache mguu wako usogezwe, asisinzie akulindaye, Bwana ndiye mlinzi wako.

mwenye kunielewa amenielewa, asiyenielewa kuna siku atautafuta ukweli huu.
 
Hakuna next time rafiki time ni hii tupe ushuhuda maana sisi wakatoliki ndo tunaongoza kutangatanga .tunahitaji sana shuhuda tupatie

 
Hakuna next time rafiki time ni hii tupe ushuhuda maana sisi wakatoliki ndo tunaongoza kutangatanga .tunahitaji sana shuhuda tupatie
Kuna shetani mmoja huwa anawadanganya kwamba kwenda kusali nje ya catholic ni kutangatanga,matokeo yake mnabaki hivyoivyo bila kujua ukweli. Catholic awali ilianza vzr lkn karne hizo walishapoteza foundation,wameacha kuabudu Mungu,wanaabudi dini.

mnasoma Biblia inayowataka muokoke lkn ninyi mnapinga wokovu. Ole wenu,siku yaja,mtajilaumu why mlipoteza muda.

Mwenye hekima atatafuta kweli had I aijue,na pale ilipo. Asiye na hekima ataona ni kutangatanga.
 
Unamtolea Mungu kwa wrong reasons, kwamba akupe vitu vya mwilini? Earthly things ndo zinakusukuma kutoa na sio kwamba unampenda Mungu? Kornelio alitoa ili apete vitu? Je dorkas alitoa sadaka nyingi na kusaidia watu ili apate faida bnafsi za dunia hii? Soma vizuri biblia yako
 
Mungu hujibu aisee
 
Sadaka inaanzia nyumbani ..ushamaliza mambo ya fungu la kumi.. angalia watu wako wa karibu (ndugu zako) wasaidie uhimarishe zaidi imani na uchumi wako
 
Hilo fungu nipe hata mimi mjane, si umeona pia kwenye Biblia kuwa wajane tunasitahili hilo
 
Maelezo marefu...!!
 
"Siku utakapokuja kugundua kuwa ulipoteza muda sana kuamini bikira maria , it will be late for you "

Yanii hadi nimelia niliye mdogo kwake ambaye si stahili kuona hata uso wake

JE YEYE AMBAE KUPITIA YEYE AKATULETEA MWANA KONDOO AMBAE KILA AMWAMINIYE ANA UZIMA MILELE sijui ata kuwa amelipokeje neno hilo

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 

Mashetani,freemason na majini pesa wanagawa wapi?
 
Hebu tueleze ukweli kuhusu hizo pesa ambazo hujui hata zilipotokea. Je, uliziokota njiani au kuna mtu tualikupa pesa hizo au uliamka ukazikuta nyumbani kwako? Tukishapata hiyo taarifa ambayo umeificha sana katika maelezo yako, na sisi tutafuata ushauri wako.
 
Hizo foundation ni njia yakukwepa kodi sababu ya charity
Wafia dini huwa hawana akili. Charity sio fungu la kumi wala watoaji wengi sio waamini wa dini. Hata mashoga, wamiliki wa kampuni za silaha, watengenezaji wa zana za ngono ni watoaji wa misaada. Bill Gates mwenyewe anatoa misaada kuhusu mimba na uzazi wa mpango
 
Sijaona justification ya kunifanya nitoe fungu la 10. Kwa jinsi unavyodai umeona muujiza, bado aliyesalia kwa Bikira Maria naye kadai aliona muujiza, bado anayemuomba Allah anaona muujiza sijui nao wanaita hivyo, na SDA ataona muujiza, na Buddha, Hindu wataona miujiza, hata team mizizi wataona miujiza.

Justification ya kuamini muujiza wako ni genuine na wote tufuate njia yako ni nini?
 
Nna uhakika na ww mimi sitoagi hilo Fungu na tena kusali ni mvivu sana ila kuna watu nawapaga kidogo changu ila trust me kila nikiwapa napitia magumu lakini kisima cha fedha japo kidogo lakini hakikauki.Kuna mambo Mungu atakutendea yani hata hustahili acha aitwe Mungu tu
 
kuna principle moja ya Biblia inaitwa "the principle of giving". Yesu alisema, wapeni watu vitu nanyi mtapewa vingi hadi kumwagika vifuani mwenu. hii haijalishi wewe ni mtu wa Mungu au la, kama unapenda kusaidia wengine, kuna siku na wewe ukipata shida utasaidiwa. inaweza kuwa shida ya kipesa, shida ya kiafya, kikazi n.k. this principel is alive.
 
aliyesalia kwa bikira maria hajaona muujiza wowote, hakuna muujiza maria anaweza kutoa, ameshakufa, na ameoza. Yesu Kristo pekee ndiye alifufuka na ndiye yu hai hadi leo. wanaoabudu maria wanaabudu sanamu, wanaabudu wafu na ni dhambi.
 
Hilo fungu nipe hata mimi mjane, si umeona pia kwenye Biblia kuwa wajane tunasitahili hilo
Mamdanyi, fungu huwa hawepi mjane, fungu la kumi sio charity, unatakiwa upeleke kwenye ghala/store ya kanisa ili litumike kwenye kazi ya Mungu. ukishatoa fungu la kumi, pia unatakiwa kuwajali wajane kama wewe sana. hivyo ni vitu viwili tofauti.
 
do not mix charity with tithe/fungu la kumi. ni vitu viwili tofauti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…