Ushuhuda wa breakthrough!

Ushuhuda wa breakthrough!

kuna watu wengi sana wanakuja DM wanaandika msg wakielezea matatizo yao na wanataka niwape pesa. Ninajua ni kweli mnaweza kuwa kwenye matatizo, lakini hamtakiwi kuniomba mimi, mwombe Mungu huyo ndiye anaweza kutatua tatizo lako jumla. mwanadamu hawezi kukusaidia. hata mimi nitakusaidia kama nikiguswa na Mungu. kuna watu wengine wanapitia kwenye majangwa kwasababu Mungu anawapitisha kuwafundisha maisha ili atakapowabariki wakumbuke. au ni njia tu ya shule anawafundisha.

ila wengine wanapitia kwenye matatizo kwasababu wamegombana na Mungu na wanapata adhabu. hakuna mtu anaweza kukuokoa kutoka kwenye mkono wa Mungu kama ameamua kukushughulikia. unachotakiwa ni kutengeneza uhusiano wako na Mungu akusamehe na kukuondolea tatizo lako. kuna watu mmeua, mmezini, mmeiba na kuumiza mioyo ya watu, watu hao wamelia kwa Mungu na Mungu ameshuka kuwapambania and you think mwanadamu anaweza kukurescue toka mikononi mwa Mungu? No. cha ajabu ni kwamba, Mungu ni Mungu wa rehema, huwa anasamehe kila anayekuja kwake kutubu.

ila kwa wale wote ambao kiukweli wanapita tu kwenye jangwa, Mungu labda anawafundisha, usimwombe mwanadamu chochote. utapita kwenye jangwa hilo hadi utakapomaliza mtihani wako ndipo Mungu atakuondoa kwasababu labda Mungu ana makusudi. na pengine unapita hivyo kwasababu ameona unaweka macho yako kwa wanadamu, msaada wetu hautoki kwa wanadamu, unatoka kwa Mungu. msaaada wa mwanadamu haudumu, ila msaada toka kwa Mungu hata kama ametumia mwanadamu kukubariki unadumu na hauna majuto. jua kwamba, Mungu hubariki kwa kutumia wanadamu pia, lakini ni mpaka hao wanadamu waguswe na Mungu kufanay hivyo nandio maana utukufu unatakiwa kwenda kwa Mungu kwasababu ni yeye ametoa kwa kupitia mwanadamu. hata mimi leo hii Mungu akinielekeza kwa namna atakayojua yeye nitoe kitu, nitatoa, ila asiponielekeza siwezi.

Kama vile Musa alivyomwinua nyoka wa shaba ndivyo Mwana wa Adam alivyoinuliwa ili kila amwaminiye apate uzima wa milele. mwangalie Yesu, huyo ndiye msaada wako, ukiangalia wanadamu na kutegemea misaada toka kwa wanadamu ni dharau na tusi kwa Mungu.

katika maisha yangu nilishapita kwenye majangwa mara nyingi, kuna kipindi nilikuwa nategemea wanadamu na elimu na kazi. Mungu akaona kumbe sijamwelewa vizuri, akaweka ugumu mioyo kwa wanadamu (ndugu zangu ambao ni matajiri), nilipita kwenye tatizo ambalo hakuna mwanadamu aliyekuwa msaada, nilichekwa na kudharauliwa hadi na watoto wadogo. ndugu zangu walikuwa tayari kusaidia watu wengine ila sio mimi. wale niliowasaidia wakafanikiwa sana ndio walikuwa wakwanza kunicheka na kunitupa. hadi pale nilipoondoa macho yangu kwenye elimu, ndugu na wanadamu, nikawa nimebaki mimi na Mungu tu, nilipoangalia macho yangu kwa Mungu tu ndipo alikuja kuniokoa mazima. that was 12 years ago. nikajifunza kuwa kumbe hatutakiwi kuangalia au kutegemea msaada toka kwa wanadamu. hata hili fungu la kumi naongelea, ni kwamba nilishawahi kubarikiwa, nikawa natoa fungu, nilipokuja kusimama miaka kadhaa ndio milango ikafungwa, hadi mwishoni mwa mwaka jana na mwezi januari mwaka huu 2022 nilipoazimia kuanza. na nimejifunza kitu kwa vitendo, hakuna mtu atakuja kunidanganya tena.

nitayainua macho yangu nitazame milima, msaada wangu utatoka wapi? msaada wangu utatoka kwa Bwana, aliyeziumba mbingu na nchi, asiuache mguu wako usogezwe, asisinzie akulindaye, Bwana ndiye mlinzi wako.

mwenye kunielewa amenielewa, asiyenielewa kuna siku atautafuta ukweli huu.
 
Hakuna next time rafiki time ni hii tupe ushuhuda maana sisi wakatoliki ndo tunaongoza kutangatanga .tunahitaji sana shuhuda tupatie

Ngoja nikushambulie kidogo....

Ogopa sana kuhisi huko uliko ndio sahihi kuliko pengine....

Hata mimi niwewahi kupata manufaa makubwa baada Tu ya kutoa sehemu ya 10% ya mapato yangu....

Ngoja nikupe uhalisia...

Mwezi wa 8 mwaka jana mmoja wa marafiki zangu alikuja kunitembelea ofisini na hivyo kufanya uhalifu wa kuiba fedha (mapato) ya taasisi ninayoifanyia kazi.... Hali iliyonipekea kuwa na changamoto ya kukosa usingizi kwasababu ya fedha iliyoibiwa ijapokuwa uongozi wa Taasisi uliamua kuisamehe ile fedha baada ya mimi kumtajia muhisiwa ambaye wao wanamfahamu vyema kutokana na matukio yaliyowahi kutokea hapo nyuma kabla ya Mimi kuwa muajiriwa ndani ya hiyo taasisi...

So kuanzia August mpaka December sikuwa vizuri kifedha kwasababu nilijikuta naingia kwenye madeni yasiyoeleweka.... Nakumbuka yalifikia kama laki 756,000 sasa December 20 nilikuwa kwenye lindi la mawazo hivyo nikawa nawaza naanzaje 2022 nikiwa na madeni?

Ila neno ninalolitumia kila siku ninapokuwa kwenye changamoto ni MUNGU ANAJUA NI KIPI UNASTAHILI, MUAMINI ATATENDA.... Jioni niko kwenye kibarua ikapigwa simu nahitajika kwenye kikao cha siku 3 nje ya mkoa.... Lakini changamoto sina hata Mia mbovu.... Kawaida ofisi inafungwa saa kumi na mbili Ila Mimi nikajikuta nazidisha mpaka saa moja na nusu still niko kibaruani na huku nikiwa nawaza ni wapi nitaenda kupiga sound nipate atleast laki 2.5?

Mungu si athumani alikuja MTU saa mbili kasoro usiku akaniuliza kama naweza mpatia huduma hivyo nilimpa na akaongeza angependa watoto wake kama watano hivi wafanyiwe procedure ndani ya week hiyo nikamwambia inawezekana na akaomba aniachie advance ya laki 1.2 hivi so halafu akaondoka ... Naapa mbele ya Mungu nililia na nikajiuliza hivi inawezekana mimi ni mtoto wa mwisho wa Mungu mbona ananijali hivyo?

In short, ukienda kwenye seminar usisahau na ona umuhimu wa kuweka TGS kubwa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] utanishukuru

Paap baada ya seminar tukaingiziwa mpunga mrefu nilioweza kukamilisha madeni yote na kuwapatia fedha ya Christmas na mwaka mpya ndugu zangu....

Ninachotaka kusema hasa kwetu sisi wakatoliki tunao Hama Hama bila sababu, tusali kwa kukiri kweli na tuamini kweli tuache huu mchezo wa kusali kwa mazoea....

Next time, nitajatoa ushuhuda wa Ekarist Takatifu uliowahi kunitokea nikiwa mtumikiaji (ministrant) Parokia moja iliyopo Jimbo kuu la Dar es salaam

Ushuhuda mwingine, mbele ya Groto la Bikirira Maria 2019

Mwingine 2020

Na huu niliouelezea ni December 20, 2021


Amini katika unachokiamini usikubali kuyumba...
 
Hakuna next time rafiki time ni hii tupe ushuhuda maana sisi wakatoliki ndo tunaongoza kutangatanga .tunahitaji sana shuhuda tupatie
Kuna shetani mmoja huwa anawadanganya kwamba kwenda kusali nje ya catholic ni kutangatanga,matokeo yake mnabaki hivyoivyo bila kujua ukweli. Catholic awali ilianza vzr lkn karne hizo walishapoteza foundation,wameacha kuabudu Mungu,wanaabudi dini.

mnasoma Biblia inayowataka muokoke lkn ninyi mnapinga wokovu. Ole wenu,siku yaja,mtajilaumu why mlipoteza muda.

Mwenye hekima atatafuta kweli had I aijue,na pale ilipo. Asiye na hekima ataona ni kutangatanga.
 
Unamtolea Mungu kwa wrong reasons, kwamba akupe vitu vya mwilini? Earthly things ndo zinakusukuma kutoa na sio kwamba unampenda Mungu? Kornelio alitoa ili apete vitu? Je dorkas alitoa sadaka nyingi na kusaidia watu ili apate faida bnafsi za dunia hii? Soma vizuri biblia yako
 
Naomba niweke hapa ushuhuda huu, hata akiusoma mtu mmoja tu kwangu inatosha, unaweza kubadilisha maisha yake kwa namna moja au nyingine. ni juu ya yale Mungu amenitendea leo hii, siwezi kunyamaza.

kwa muda wa miezi kadhaa nimekuwa nikipitia kwenye kipindi fulani cha jangwani, na januari hii ikaja kuongeza makali yake. hii inatokana na kuyumba fulani kwenye biashara yangu fulani, na ilitokana na makosa niliyoyafanya ya kupeleka pesa nyingi kwenye ujenzi wa nyumba Dodoma na viwanja viwili besides ya hiyo nyumba (namshukuru Mungu kwa hilo pia). na niwe muwazi, nilishaachaga kutoa fungu la kumi (zaka) zamani tu pamoja na kwamba nilikuwa nasali.

kutokana na ujenzi na manunuzi ya viwanja, niliyumba sana kipesa na nikapitia wakati mgumu sana. Mimi nimeokoka, ninasali kanisa la kilokole lakini sio hayo ya mafuta na manabii wa kisasa.

nilipita kwenye mitandao nikakutana na mchungaji mmoja anahubiri kwamba fungu la kumi ni lazima kutoa na kwa kutoa fungu hil (Malaki 3:10-12) ni njia ya kumjaribu Mungu, Mungu ametangaza agano ambalo hawezi kutengua kwasababu yeye sio mwanadamu hata aseme uongo, kwamba kwa mtu anayetaka kumjaribu ili amwone kama hatafungua madirisha ya mbinguni, atoe fungu la kumi (hata kama kuna sadaka zingine) ili kiwemo chakula katika nyumba yake.

as soon as nilipoamua moyoni kuwa mtoaji, nikapita sehemu tena mchungaji mwingine akawa anafundisha kwamba fungu la kumi lilikuwa kwa ajili ya agano la kale tu, wakati wa agano jipya hatulazimiki kutoa, lakini nilishasoma pia Mathayo 23:23 na Luka 11:42, Yesu aliwaambia mafarisayo kuwa besides wanayotakiwa kuyafanya, hawatakiwi kuneglect fungu la kumi. hivyo nilikuwa kwenye njiapanda, na nilivyo mdadisi, mchungaji mmoja anasema fungu la kumi ni agizo la Mungu, mwingine anasema sio lazima kwa sasa. ila nikaazimia moyoni lazima nipate ukweli kwa kufanya practical. Mungu alinijalia fedha fulani kufikia kam 4m ambayo iliisha hata sikujua iliishaje ni kama ilipitia kwenye mfuko uliotoboka, lakini ikatakiwa nitoe fungu la kumi lake sasa mwishoni mwa mwezi wa kwanza huu kwasababu nilidhamiria kujaribu kurudi kule awali ambako nilikuwa natoaga fungu. actually, zamani nilipokua natoa fungu la kumi nilikuwa sijawahi kuishiwa pesa sasa nafikiri sikuwa najua kama ndio zilikuwa baraka za Mungu nikaachana nalo na ukiacha kuja kuanza tena ni mbinde kwasababu shetani hataki uanze kwasababu anajua ukianza kutoa tu utabarikiwa.

kupunguza maneno mengi, nilichodhamiria kufanya ni kuanza kutoa fungu la kumi sambamba na Neno la Mungu linavyosema ili nimjaribu Mungu kama alivyosema tumjaribu, sio kwasababu Mungu ananidai, bali kwasababu Mungu amesema tufanye hivyo kama namna ya kumjaribu ili tuone kama hatafungua madirisha ya mbinguni na kutumwagia baraka hata isiwepo nafasi ya kutosha. nikatoa fungu la kumi kwenye 4m hiyo, tena nilikuwa nahitaji sana hiyo potion na tayari nilishaitumia hivyo nikahisi mwisho wa mwezi nipate pesa nitoe, nikapata ile inayotosha fungu la kumi tu, ikabidi nitoe kwa imani ili mimi nibaki na Mungu tukiangaliana usoni.....

baada ya kutoa fungu linalouma na ambalo wakati huo nilikuwa nalihitaji mno, nikaanza kuangalia Mungu atafanyaje, I was like testing to see whether Mungu bado anahitaji sisi katika agano jipya tutoe au la, manake kama Mungu angereact in accordance with his word ni uthibitisho kwamba anataka tutoe, kama singereact nisingefuata. hivyo nilimjaribu Mungu kama yeye alivyosema tumjaribu.

wandugu, baada tu ya kufanya hivyo, ndio kipindi kigumu kilizidi, nilipita kwenye jangwa moja hatari ambalo nilishawahi pitaga miaka 12 iliyopita, na nilikuwa sioni njia kabisa, akili yangu yote ilishindwa kupata suluhisho, elimu, marafiki, career, ndugu n.k vilishindwa. nikaingia kwenye maombi na kuanza kumuuliza Mungu mbona sasa huonekani kama ulivyoahidi kwenye Neno lako wakati mimi nimekujaribu? au hukuwa unamaanisha nilivyofanya? nilivyomaliza tu maombi, nikakutana na clip moja ya mchungaji anatoa ushuhuda kwamba, UKIWA UMEOMBA UKAONA MUNGU KAMA HATOKEI, Jua kuna mambo mawili. aidha, haupo kwenye njia sahihi hivyo Mungu hajasikia, au kama wewe unaona upo kwenye njia sahihi, jua Mungu ameshajibu, hivyo relax subiri kuona matokeo. gafla moyoni nikashuhudiwa kuwa Mungu ameshajibu na atakushangaza muda si mrefu, kuna sauti ya Roho Mtakatifu yenye uhakikisho huwa inaongea, wale waliookoka wanajua ninachosema. nikaamua kurelax.

SASA LEO majira tarehe 04/02/2022 majira ya saa kumi na moja jioni, Mungu ameamua kunishangaza, amefungua mlango wa pesa mahali ambapo sikutegemea kabisa kwamba pangetoa pesa, sikustahili kuzipata, amenipa tu na wala sikuzitolea jasho, kama huwa unasikia kuwa Mungu alishawahi kutoa maji kwenye mwamba wana wa Israel wakanywa jangwani, ndio imekuwa kwangu, sikutegemea kupata ile pesa, sikustahili kuipata, na sikuitolea jasho, imekuja tu, na kwasababu imekuja siwezi kunyamaza kama haijaja, Mungu ameamua iwe hivyo, naona shetani alikuwa amepafunga tu nilango na madirisha ya mbinguni ya baraka zangu kwa hila zake, Mungu kafumua lango hilo na nimepata millions of money ndugu zangu. sisemi uongo. Mungu amenifanyia sapraizi jamani.

sasa, nina uhakika wa kurevive biashara yangu yote kwasababu hela niliyopewa na Mungu (ambayo hata sikustahili ni neema yake tu na nilikuwa sitegemei kwasabbu sikuifanyia kazi), millions, inatosha kufufua biashara yangu, inatosha kujenga nyumba zingine kwenye viwanja viwili besides ile niliyokuwa najenga, inatosha kuongeza mtaji mkubwa tu kwenye biashara ya mke wangu.

na zaidi ya yote, hata kwa hiyo nayo, nitamtolea Mungu fungu la kumi. Mungu anisaidie nisiache kwasababu hapo ndio nimethibitishiwa na Mungu kwamba ndiko eneo la kumjaribu Mungu. Malaki 3:10-12) anasema leteni zaka kamili ghalani mwangu ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo muone kama sitafungua madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka hata isiwepo nafasi ya kutosha, namni nitamkemea yeye alaye na kuharibu mazao yenu..., hivyo kumbe Mungu amemkemea shetani aliyekuwa amefunga milango ya baraka, sasaivi ninaye mkemeaji kwenye biashara yangu, kwenye career yangu etc. Jina la Bwana litukuzwe.

ushauri wangu kwako msomaji, uanze kutoa fungu la kumi, ila toa kwenye udongo mzuri, kwa maana kwamba utoe sehemu ambayo watu wanamwabudu Mungu katika roho na kweli, kwa upande wangu mimi huko huwa naamini ni sehemu ambayo watu wameokoka wanaenda mbinguni (nikiwa muwazi tu) sio sehemu watu wanaabudu dini na Mungu hayupo, utapoteza pesa yako kwasababu haitaenda kwenye kazi/ghala la Mungu. kwa aliyeelewa, usiache fungu la kumbi, usiache fungu la kumi, usiache fungu la kumi ! utakuja kunishukuru.

Sifa na utukufu kwa Mungu. ushuhuda huu ni wa kweli kabisa na umenitokea leo hii, kwa atakayeamini aamini, kwa atakaye neglect aneglect ila mimi nimeshautoa.
Mungu hujibu aisee
 
Sadaka inaanzia nyumbani ..ushamaliza mambo ya fungu la kumi.. angalia watu wako wa karibu (ndugu zako) wasaidie uhimarishe zaidi imani na uchumi wako
 
Hilo fungu nipe hata mimi mjane, si umeona pia kwenye Biblia kuwa wajane tunasitahili hilo
 
Naomba niweke hapa ushuhuda huu, hata akiusoma mtu mmoja tu kwangu inatosha, unaweza kubadilisha maisha yake kwa namna moja au nyingine. ni juu ya yale Mungu amenitendea leo hii, siwezi kunyamaza.

kwa muda wa miezi kadhaa nimekuwa nikipitia kwenye kipindi fulani cha jangwani, na januari hii ikaja kuongeza makali yake. hii inatokana na kuyumba fulani kwenye biashara yangu fulani, na ilitokana na makosa niliyoyafanya ya kupeleka pesa nyingi kwenye ujenzi wa nyumba Dodoma na viwanja viwili besides ya hiyo nyumba (namshukuru Mungu kwa hilo pia). na niwe muwazi, nilishaachaga kutoa fungu la kumi (zaka) zamani tu pamoja na kwamba nilikuwa nasali.

kutokana na ujenzi na manunuzi ya viwanja, niliyumba sana kipesa na nikapitia wakati mgumu sana. Mimi nimeokoka, ninasali kanisa la kilokole lakini sio hayo ya mafuta na manabii wa kisasa.

nilipita kwenye mitandao nikakutana na mchungaji mmoja anahubiri kwamba fungu la kumi ni lazima kutoa na kwa kutoa fungu hil (Malaki 3:10-12) ni njia ya kumjaribu Mungu, Mungu ametangaza agano ambalo hawezi kutengua kwasababu yeye sio mwanadamu hata aseme uongo, kwamba kwa mtu anayetaka kumjaribu ili amwone kama hatafungua madirisha ya mbinguni, atoe fungu la kumi (hata kama kuna sadaka zingine) ili kiwemo chakula katika nyumba yake.

as soon as nilipoamua moyoni kuwa mtoaji, nikapita sehemu tena mchungaji mwingine akawa anafundisha kwamba fungu la kumi lilikuwa kwa ajili ya agano la kale tu, wakati wa agano jipya hatulazimiki kutoa, lakini nilishasoma pia Mathayo 23:23 na Luka 11:42, Yesu aliwaambia mafarisayo kuwa besides wanayotakiwa kuyafanya, hawatakiwi kuneglect fungu la kumi. hivyo nilikuwa kwenye njiapanda, na nilivyo mdadisi, mchungaji mmoja anasema fungu la kumi ni agizo la Mungu, mwingine anasema sio lazima kwa sasa. ila nikaazimia moyoni lazima nipate ukweli kwa kufanya practical. Mungu alinijalia fedha fulani kufikia kam 4m ambayo iliisha hata sikujua iliishaje ni kama ilipitia kwenye mfuko uliotoboka, lakini ikatakiwa nitoe fungu la kumi lake sasa mwishoni mwa mwezi wa kwanza huu kwasababu nilidhamiria kujaribu kurudi kule awali ambako nilikuwa natoaga fungu. actually, zamani nilipokua natoa fungu la kumi nilikuwa sijawahi kuishiwa pesa sasa nafikiri sikuwa najua kama ndio zilikuwa baraka za Mungu nikaachana nalo na ukiacha kuja kuanza tena ni mbinde kwasababu shetani hataki uanze kwasababu anajua ukianza kutoa tu utabarikiwa.

kupunguza maneno mengi, nilichodhamiria kufanya ni kuanza kutoa fungu la kumi sambamba na Neno la Mungu linavyosema ili nimjaribu Mungu kama alivyosema tumjaribu, sio kwasababu Mungu ananidai, bali kwasababu Mungu amesema tufanye hivyo kama namna ya kumjaribu ili tuone kama hatafungua madirisha ya mbinguni na kutumwagia baraka hata isiwepo nafasi ya kutosha. nikatoa fungu la kumi kwenye 4m hiyo, tena nilikuwa nahitaji sana hiyo potion na tayari nilishaitumia hivyo nikahisi mwisho wa mwezi nipate pesa nitoe, nikapata ile inayotosha fungu la kumi tu, ikabidi nitoe kwa imani ili mimi nibaki na Mungu tukiangaliana usoni.....

baada ya kutoa fungu linalouma na ambalo wakati huo nilikuwa nalihitaji mno, nikaanza kuangalia Mungu atafanyaje, I was like testing to see whether Mungu bado anahitaji sisi katika agano jipya tutoe au la, manake kama Mungu angereact in accordance with his word ni uthibitisho kwamba anataka tutoe, kama singereact nisingefuata. hivyo nilimjaribu Mungu kama yeye alivyosema tumjaribu.

wandugu, baada tu ya kufanya hivyo, ndio kipindi kigumu kilizidi, nilipita kwenye jangwa moja hatari ambalo nilishawahi pitaga miaka 12 iliyopita, na nilikuwa sioni njia kabisa, akili yangu yote ilishindwa kupata suluhisho, elimu, marafiki, career, ndugu n.k vilishindwa. nikaingia kwenye maombi na kuanza kumuuliza Mungu mbona sasa huonekani kama ulivyoahidi kwenye Neno lako wakati mimi nimekujaribu? au hukuwa unamaanisha nilivyofanya? nilivyomaliza tu maombi, nikakutana na clip moja ya mchungaji anatoa ushuhuda kwamba, UKIWA UMEOMBA UKAONA MUNGU KAMA HATOKEI, Jua kuna mambo mawili. aidha, haupo kwenye njia sahihi hivyo Mungu hajasikia, au kama wewe unaona upo kwenye njia sahihi, jua Mungu ameshajibu, hivyo relax subiri kuona matokeo. gafla moyoni nikashuhudiwa kuwa Mungu ameshajibu na atakushangaza muda si mrefu, kuna sauti ya Roho Mtakatifu yenye uhakikisho huwa inaongea, wale waliookoka wanajua ninachosema. nikaamua kurelax.

SASA LEO majira tarehe 04/02/2022 majira ya saa kumi na moja jioni, Mungu ameamua kunishangaza, amefungua mlango wa pesa mahali ambapo sikutegemea kabisa kwamba pangetoa pesa, sikustahili kuzipata, amenipa tu na wala sikuzitolea jasho, kama huwa unasikia kuwa Mungu alishawahi kutoa maji kwenye mwamba wana wa Israel wakanywa jangwani, ndio imekuwa kwangu, sikutegemea kupata ile pesa, sikustahili kuipata, na sikuitolea jasho, imekuja tu, na kwasababu imekuja siwezi kunyamaza kama haijaja, Mungu ameamua iwe hivyo, naona shetani alikuwa amepafunga tu nilango na madirisha ya mbinguni ya baraka zangu kwa hila zake, Mungu kafumua lango hilo na nimepata millions of money ndugu zangu. sisemi uongo. Mungu amenifanyia sapraizi jamani.

sasa, nina uhakika wa kurevive biashara yangu yote kwasababu hela niliyopewa na Mungu (ambayo hata sikustahili ni neema yake tu na nilikuwa sitegemei kwasabbu sikuifanyia kazi), millions, inatosha kufufua biashara yangu, inatosha kujenga nyumba zingine kwenye viwanja viwili besides ile niliyokuwa najenga, inatosha kuongeza mtaji mkubwa tu kwenye biashara ya mke wangu.

na zaidi ya yote, hata kwa hiyo nayo, nitamtolea Mungu fungu la kumi. Mungu anisaidie nisiache kwasababu hapo ndio nimethibitishiwa na Mungu kwamba ndiko eneo la kumjaribu Mungu. Malaki 3:10-12) anasema leteni zaka kamili ghalani mwangu ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo muone kama sitafungua madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka hata isiwepo nafasi ya kutosha, namni nitamkemea yeye alaye na kuharibu mazao yenu..., hivyo kumbe Mungu amemkemea shetani aliyekuwa amefunga milango ya baraka, sasaivi ninaye mkemeaji kwenye biashara yangu, kwenye career yangu etc. Jina la Bwana litukuzwe.

ushauri wangu kwako msomaji, uanze kutoa fungu la kumi, ila toa kwenye udongo mzuri, kwa maana kwamba utoe sehemu ambayo watu wanamwabudu Mungu katika roho na kweli, kwa upande wangu mimi huko huwa naamini ni sehemu ambayo watu wameokoka wanaenda mbinguni (nikiwa muwazi tu) sio sehemu watu wanaabudu dini na Mungu hayupo, utapoteza pesa yako kwasababu haitaenda kwenye kazi/ghala la Mungu. kwa aliyeelewa, usiache fungu la kumbi, usiache fungu la kumi, usiache fungu la kumi ! utakuja kunishukuru.

Sifa na utukufu kwa Mungu. ushuhuda huu ni wa kweli kabisa na umenitokea leo hii, kwa atakayeamini aamini, kwa atakaye neglect aneglect ila mimi nimeshautoa.
Maelezo marefu...!!
 
utaniwia radhi, lakini penye ukweli naomba niseme ili ninawe mikono kwako. siku utakapokuja kugundua kuwa ulipoteza muda sana kuamini bikira maria na ekarist za kidini, it will be too late for you. unahitaji kuokoka na sehemu ulipo hapana wokovu, hata wale wana uamsho wanaojaribu wanafukuzwa.

wengi tulikuwa huko kwenye dini hatukumwona Mungu, tulipokuja kwenye nuru tunamwona Mungu. Kumwona Mungu sio lazima iwe kwenye vitu, these material things are just a bonus, ni bonasi tu lakini kumwona Mungu kiuhalisia ni kumwona moyoni kwasaababu sisi ni hekalu lake kama tukimkaribisha aingie ndani yetu. hakuna wokovu kwenye ukatoliki, trust me and you know it in your heart. pia huku tuliko sio kwamba ni dini inayokupeleka mbinguni hapana, ila at least misingi yao na mafundisho yao yapo kibiblia na Roho Mtakatifu ambaye ndiye Mungu mwenyewe anahusika kwenye maisha ya watu.

asiye na roho wa Kristo huyo sio mwana wa Mungu na hataenda Mbinguni. mtanishambulia lakin ukweli ndio huo. don't just shambulia, jaribisha kuingia kwenye wokovu uone tunachosema ni cha kweli au uongo, usibishe wakati upo huko. ukiwa kwenye shimo mtu akitaka kukurushia kamba utoke hautakiwi kubisha kupokea kamba labda kwa kuamini kama ni yakweli wakati bado upo kule shimoni. naongea hivi sio kwasababu nataka kutanishi ushuhuda wangu, huu nimeusema sio ili nisifiwe na mtu au vyovyote, nimeshindwa kunyamaza hadi nitangaze yale Mungu aliyonitendea na walio nielewa wamenielewa wasionielewa hata siwalazimishi kuamini au kuelewa. lakini wale watakaojaribu kufuata Maneno ya Mungu ndio watakaokuja na ushuhuda kama nimedanganya au la. I am not a pastor, wala nabii wala mtume, just an ordinary person. la mwisho ninalowaambia wale wanaomwamini Mungu ni kwamba, Wamtumaninio Bwana watapata nguvu mpya, watapaa juu kwa mbawa zao kama tai, watapiga mbio wala hawatachoka". Mungu awabariki.
"Siku utakapokuja kugundua kuwa ulipoteza muda sana kuamini bikira maria , it will be late for you "

Yanii hadi nimelia niliye mdogo kwake ambaye si stahili kuona hata uso wake

JE YEYE AMBAE KUPITIA YEYE AKATULETEA MWANA KONDOO AMBAE KILA AMWAMINIYE ANA UZIMA MILELE sijui ata kuwa amelipokeje neno hilo

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
kuna baraka na pesa za aina nyingi. kuna pesa zinatokana na mashetani, freemason, majini n.k, pia kuna pesa zinatoka kwa Mungu kabisa. sisi tunaomwamini Mungu tunaamini kwamba, "baraka za Mungu hazina majuto". yani Mungu akikubariki hutajuta, hutatoa kafara, ni furaha. unaweza usiwe na pesa kama za hao matajiri wa dunia lakini ukawa tajiri kwa kuwa na Mungu anayekupa provisions, na pia anayekupa uzima. Mungu ndiye ameshikilia pumzi za wote, na Biblia inasema Mungu ndiye atupaye utajiri. namshukuru Mungu kwasababu ananipa baraka na ninaye yeye kwenye maisha yangu, kuliko mabilioni ningekuwa nayo lakini sina Mungu...sihitaji hilo.

Mashetani,freemason na majini pesa wanagawa wapi?
 
Hebu tueleze ukweli kuhusu hizo pesa ambazo hujui hata zilipotokea. Je, uliziokota njiani au kuna mtu tualikupa pesa hizo au uliamka ukazikuta nyumbani kwako? Tukishapata hiyo taarifa ambayo umeificha sana katika maelezo yako, na sisi tutafuata ushauri wako.
 
Hizo foundation ni njia yakukwepa kodi sababu ya charity
Wafia dini huwa hawana akili. Charity sio fungu la kumi wala watoaji wengi sio waamini wa dini. Hata mashoga, wamiliki wa kampuni za silaha, watengenezaji wa zana za ngono ni watoaji wa misaada. Bill Gates mwenyewe anatoa misaada kuhusu mimba na uzazi wa mpango
 
Sijaona justification ya kunifanya nitoe fungu la 10. Kwa jinsi unavyodai umeona muujiza, bado aliyesalia kwa Bikira Maria naye kadai aliona muujiza, bado anayemuomba Allah anaona muujiza sijui nao wanaita hivyo, na SDA ataona muujiza, na Buddha, Hindu wataona miujiza, hata team mizizi wataona miujiza.

Justification ya kuamini muujiza wako ni genuine na wote tufuate njia yako ni nini?
 
Nna uhakika na ww mimi sitoagi hilo Fungu na tena kusali ni mvivu sana ila kuna watu nawapaga kidogo changu ila trust me kila nikiwapa napitia magumu lakini kisima cha fedha japo kidogo lakini hakikauki.Kuna mambo Mungu atakutendea yani hata hustahili acha aitwe Mungu tu
 
Nna uhakika na ww mimi sitoagi hilo Fungu na tena kusali ni mvivu sana ila kuna watu nawapaga kidogo changu ila trust me kila nikiwapa napitia magumu lakini kisima cha fedha japo kidogo lakini hakikauki.Kuna mambo Mungu atakutendea yani hata hustahili acha aitwe Mungu tu
kuna principle moja ya Biblia inaitwa "the principle of giving". Yesu alisema, wapeni watu vitu nanyi mtapewa vingi hadi kumwagika vifuani mwenu. hii haijalishi wewe ni mtu wa Mungu au la, kama unapenda kusaidia wengine, kuna siku na wewe ukipata shida utasaidiwa. inaweza kuwa shida ya kipesa, shida ya kiafya, kikazi n.k. this principel is alive.
 
Sijaona justification ya kunifanya nitoe fungu la 10. Kwa jinsi unavyodai umeona muujiza, bado aliyesalia kwa Bikira Maria naye kadai aliona muujiza, bado anayemuomba Allah anaona muujiza sijui nao wanaita hivyo, na SDA ataona muujiza, na Buddha, Hindu wataona miujiza, hata team mizizi wataona miujiza.

Justification ya kuamini muujiza wako ni genuine na wote tufuate njia yako ni nini?
aliyesalia kwa bikira maria hajaona muujiza wowote, hakuna muujiza maria anaweza kutoa, ameshakufa, na ameoza. Yesu Kristo pekee ndiye alifufuka na ndiye yu hai hadi leo. wanaoabudu maria wanaabudu sanamu, wanaabudu wafu na ni dhambi.
 
Hilo fungu nipe hata mimi mjane, si umeona pia kwenye Biblia kuwa wajane tunasitahili hilo
Mamdanyi, fungu huwa hawepi mjane, fungu la kumi sio charity, unatakiwa upeleke kwenye ghala/store ya kanisa ili litumike kwenye kazi ya Mungu. ukishatoa fungu la kumi, pia unatakiwa kuwajali wajane kama wewe sana. hivyo ni vitu viwili tofauti.
 
Wafia dini huwa hawana akili. Charity sio fungu la kumi wala watoaji wengi sio waamini wa dini. Hata mashoga, wamiliki wa kampuni za silaha, watengenezaji wa zana za ngono ni watoaji wa misaada. Bill Gates mwenyewe anatoa misaada kuhusu mimba na uzazi wa mpango
do not mix charity with tithe/fungu la kumi. ni vitu viwili tofauti.
 
Back
Top Bottom