Ushuhuda wa kweli: Jinsi mdudu mchwa alivyobadirisha maisha ya watu kimaendeleo na kutoa ajira kwa vijana

Ushuhuda wa kweli: Jinsi mdudu mchwa alivyobadirisha maisha ya watu kimaendeleo na kutoa ajira kwa vijana

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,778
Reaction score
7,145
Wana JF.

Katika pita pita zangu nimeweza kudadisi kudadisi ni kwanini kumeibuka ujenzi wa kasi namna hii iliyopo hasa maeneo ya kanda ya ziwa hususani Kagera na Geita. Ningeweza kusema Kagera tu lakini kile kipande kilichochotwa na kupeleka Geita kimebadili stori.

Kwanini mchwa ndio chanzo? Sababu ni kwamba watu wa zamani walidhani kujenga nyumba ya udongo ni bei nafuu mno kwani vitu vingi unavipata bure. Haya yalikuja kubadilika baada ya ukataji miti hovyo imara na ya asili, hivyo vijiji vingi vilijikuta hakuna miti ya kujengea tena, hakuna misitu ya kukata miti kama tulivyozoea.

Miti inayochukua muda mfupi nayo haiwezi kuimili vishindo, wadudu watafunao miti, mchwa. Kilichofuata nyumba nyingi zilizojengwa kwa miti dhaifu zote zilidondoka, ndipo wakatokea wabunifu wa kupasua mawe na wengine kuanza kufyatua tofari kwenye mashamba yao.

Katika harakati za kukimbia mdudu mchwa kukatokea dharura ya kutakiwa wataalum zaidi wa kufyatua tofari za udongo na kuchoma. Haijaishia hapo, hadi kuna wataalum wa kupima udongo kama unafaa kufyatua tofari. Ajira nyingi zikatokea sababu ya mdudu mchwa.

Haikuishia hapo wakatokea wataalum wa kubuni ramani za ndani na wengine wakaongeza ujuzi zaidi wa kuremba paa, tena kwa ujenzi wa gharama nafuu wa mbao za mtindo mmoja wa 2 kwa 2. Vijana hawa wapya wamekuwa tishio kwa mafundi wa zamani, tena wenye kisomo cha juu.

Kwa sasa watu wanaojenga mjini wanawafuata vijana wa vijijini kuja kuezeka nyumba Dar na Arusha kutoka Bukoba na Geita. Vijana hawa wameleta mvuto kwa jamii, kwani ni wepesi kumaliza kazi, ni watu waaminifu na hesabu zao za nyenzo wako vizuri, kwani hawazidishi vitu ili kupata cha juu.

Kama watu hamwamini. Tembelea Kagera, Geita, Kahama ujionee kasi ya ujenzi wa nyumba bora zenye ufanisi wa paa imara zisizoezuliwa na upepo.
 

Attachments

  • Screenshot_20221009-104300_Facebook.jpg
    Screenshot_20221009-104300_Facebook.jpg
    88.4 KB · Views: 22
  • Screenshot_20221009-110038_Chrome.jpg
    Screenshot_20221009-110038_Chrome.jpg
    109.5 KB · Views: 25
Hata mdudu mbu anawatajirisha wenye mahospitali Sana, huku akizidi kuwatia ufukara masikini
 
Unamaanisha mchwa watu au mchwa mdudu
Mchwa Mdudu. Kitendo cha kutafuna miti dhaifu kimewafanya watu waachane na ujenzi wa nyumba za tembe kwa kutumia miti na nyasi, mabadiriko makubwa tukapata wataalum wa kufyatua tofari bora kwa ajiri ya ujenzi,,tukapata vijana wataalum wa kuezeka nyumba wasio wasomi lakini weledi wao mkubwa katika kucheza na nakshi za paa. Tayari nyumba nyingi mafundi ujenzi wanawafuata vijijini na hawana hasara kwani hawaibi material. Kwa sasa majumba mengi mazuri yanazaliwa kasi wilaya ya Muleba na kahama kwa sababu ya matokeo ya mdudu mchwa.
 
Wana JF.

Katika pita pita zangu nimeweza kudadisi kudadisi ni kwanini kumeibuka ujenzi wa kasi namna hii iliyopo hasa maeneo ya kanda ya ziwa hususani Kagera na Geita. Ningeweza kusema Kagera tu lakini kile kipande kilichochotwa na kupeleka geita kimebadiri story.

Kwanini Mchwa ndio chanzo? Sababu ni kwamba watu wa zamani walidhani kujenga nyumba ya udongo ni bei nafuu mno kwani vitu vingi unavipata bure.
Haya yalikuja kubadirika baada ya ukataji miti hovyo imara na ya asili, hivyo vijiji vingi vilijikuta hakuna miti ya kujengea tena , hakuna misitu ya kukata miti kama tulivyozoea. Miti inayochukua muda mfupi nayo haiwezi kuimili vishindo wadudu watafunao miti MCHWA. Kilichofuata nyumba nyingi zilizojengwa kwa miti dhaifu zote zilidondoka, ndipo akatokea wabunifu wa kupasua mawe na wengine kuanza kufyatua tofari kwenye mashamba yao.

Katika harakati za kukimbia mdudu mchwa kukatokea dharura ya kutakiwa wataalum zaidi wa kufyatua tofari za udongo na kuchoma, aijaishia hapo hadi kuna wataalum wa kupima udongo kama unafaa kufyatua tofari. Ajira nyingi zikatokea sababu ya mdudu mchwa. Haikuishia hapo akatokea wataalum wa kudesgn ramani za kilocal na wengine wakaongeza ujuzi zaidi wa kulemba paa tena kwa ujenzi wa gharama nafuu wa mbao za mtindo mmoja 2 by 2. Vijana hawa wapya wamekuwa tishio kwa mafundi wa zamani tena wenye kisomo cha juu. Kwa sasa watu wanaojenga mjini wanawafuata vijana wa vijijini kuja kuezeka nyumba dar na arusha kutoka Bukoba na Geita. Vijana hawa wameleta mvuto kwa jamii kwani ni wepèsi kumaliza kazi, ni watu waaminifu na hesabu zao za material wako vizuri kwani hawazidishi vitu ili kupata cha juu. Kama watu hamwamini tembelea Kagera, Geita, Kahama ujionee kasi ya ujenzi wa nyumba bora zenye ufanisi wa paa imara zisizoezuliwa na upepo.
Nshomile vipi zao la vanilla?
 
Nshomile vipi zao la vanilla?
Yaani hili zao ni machimbo madogo ya dhahabu ya kijani. BK inaendelea kimya kimya wakati watu wakiinanga kuwa BK maskini kumbe siri kubwa Vanilla hazijulikana kama zipo na serikali inakosa mapato. Bukoba ndiyo imeipandisha Uganda kuonekana ni wazalishaji wakubwa wa vanilla kumbe afisa ugani wa tz wamezubaa hawana record. NEI Limited kaipa kisogo Moshi kwa sasa anavuna maela kagera. Kwa sasa umahasishaji ni mkubwa ila tu Mkuu wa Mkoa aliyepita alikuwa dhaifu sana. Wafanyabiqshara walimwingiza mjini akasahau kuwa wakulima wanateseka. Hivi sasa tumefundisha vijana kukausha vanilla sasa wanaonanga wahaya wakae mkao wa kuachwa kama wamesimama kwenye maendeleo. Tunashukru ujio wa Bashe kwani amegundua wanaosema kagera maskin kwa sababu hawataki kubadirika amewaona waongo. Hata mkuu wa mkoa alilishwa maneno mapema baada ya kutembea akakata kauli ameanza kusifia. Kwa sasa viwanda vingi vya kuchakata kahawa vipo vya kutosha Muleba.
 
Back
Top Bottom