USHUHUDA: Watanzania tuwe wakweli juu ya ufugaji wa kuku

USHUHUDA: Watanzania tuwe wakweli juu ya ufugaji wa kuku

Hiyo gharama uliyotaja ni ya juu sana na haiwafanyi watanzania kudhubutu. Niliposoma ile post ya kuku 6 kukupatia kuku 200 nilivutiwa sana. Uwezo wa hao kuku nilikuwa nao; hivyo nilipowanunua nilitumia Tshs. 48,000/= kununua kuku, 30,000/= kununua sehemu ya kuku kushinda, 10,000/ kifaa cha maji na Tshs. 4,500/= kununua kifaa cha chakula. Sehemu ya kulala nilikuwa nawalaza jikoni. Chakula nilikuwa nanunua kila wiki nachanganya mwenyewe pale nyumbani.
Walipoongezeka kufikia 50, ndo nilijenga banda dogo mita 3 x 4 kwa ajili ya kulaza wale kuku wasiohatamia.
Hivyo sikubaliani na mtoa mada kuwa unahitaji mil 1.5 kuanza - HAPANA. Hicho ni kiasi kukubwa sana; unataka kuwaogopesha watu wasijaribu kufuga eti kwa sababu hawana hiyo pesa.
 
Tanzania kuna upotoshaji mkubwa sana, wengi wetu ni waongo waongo sana. Penye ukweli tunapindisha.

Ili ufuge kuku wa kienyeji, tena kwa banda la hali ya chini kabisa, ni lazima uwe na vitu vifuatavyo :-

(Kwa banda la mita 9 kwa mita 3)

1. Eneo la kutosha kwa ajili ya banda

2. Muda wa kutosha kuwahudumia kuku

3. Uwe na mtaji wa siyo chini ya Milioni 1.5 kwa ajili ya kujengea banda tu

Gharama ya fundi siyo chini ya laki 1.5 , mabati used siyo chini ya mabati 15 @ 8,000 TZS , matofali ya kuchoma 800 300 TZS, misumari ya bati 2 kg @ 5,000 TZS , Binding wire , bawaba , cement 12 bags , kufuli 1 @ 5,000 TZS , kitasa 1 @ 4,000, mbao ( 2 x 2 , 3 x 2 ) 800 Rft , mirunda 12 @ 5,000 TZS , Chicken mesh 1 Roller 80,000 TZS , Wavu mgumu 2 Rollers @ 12,000 , usafiri na mengineyo madogo madogo.


4. Uwe na walau laki 3 za kununua kuku wakubwa wanaokaribia kutaga

Ikumbukwe tu , kuku 1 ni kati ya TZS 10 - 15,000


Watanzania tuwe wakweli , tuache uongo na ushabiki wa vitu tusivyovijua kwa vitendo.
Kitendo tu cha kuwaza unafuga kuku wa kienyeji tayari umeshafeli.
Ni lazima kila utakachoambiwa hakitaendana na mawazo yako!

Ufugaji wa kuku=Breed inahusu kwa asilimia kubwa!

,Ndo maana mahindi ya kisasa ni tofauti na mahindi ya kienyeji kwa maana ya productivity!

Hivo pata elimu kwanza uelewe sawa sawa,ufugaji lisayansi ni utajiri wa wazi kabisa!No stories,its factual!
 
Tena usipojipanga kwenye chakula utasema umelogw maana kuku wanakula hatari kama viwavi unaeza nunua gunia la pumba ukatengeneza chakula manina hat mwezi gunia halitoboi daah,hakuna jambo rahisi chini ya jua
Kwa kuwa wafugaji wengi hawahitaji kujifunza ndo maana wanahangaika na chakula. Mimi natumia ngano, naotesha chakula (Hydroponics Fodder) - ambapo kilo mbili za ngano zinanipatia chakula kilo 14/16. Hizo ngano kilo moja naipata kwa gharama ya Tshs. 1,200 / 1,500. Hivyo suala la chakula kwangu sio shida; labda changamoto inakuja kwenye muda wa kuotesha - zoezi hili la kuotesha ni endelevu kama kupiga mswaki kila siku ila unapata chakula bora kwa gharama nafuu.
Kuhusu virutubisho natumia EM.1 ambayo lita moja inanipatia lita 20 za virutubisho ambavyo naweza kutumia mwaka mzima na kiasi kingine nikawauzia wafugaji majirani wanaoona umuhimu wa hivyo virutubisho.
Kwa ujumla nimekuwa mfugaji kwa muda mrefu hadi nimeona kuwa kufuga ni namna unavyoji-tune kufanya hiyo kazi.
 
Wapo kazini. Wasiporahisisha siku nyingine utalipaje kiingilio. Pia wanafadhiliwa na wenye maduka ya madawa.
Sikubaliani na wewe hata siku moja. Ufugaji wa kuku inabidi kila siku ujifunze. Nenda Uganda uone waganda wanavyofuga kwenye mazingira ya kawaida sana.
Tatizo kwenye mitaa mingine ni vibaka!
 
Hiyo gharama uliyotaja ni ya juu sana na haiwafanyi watanzania kudhubutu. Niliposoma ile post ya kuku 6 kukupatia kuku 200 nilivutiwa sana. Uwezo wa hao kuku nilikuwa nao; hivyo nilipowanunua nilitumia Tshs. 48,000/= kununua kuku, 30,000/= kununua sehemu ya kuku kushinda, 10,000/ kifaa cha maji na Tshs. 4,500/= kununua kifaa cha chakula. Sehemu ya kulala nilikuwa nawalaza jikoni. Chakula nilikuwa nanunua kila wiki nachanganya mwenyewe pale nyumbani.
Walipoongezeka kufikia 50, ndo nilijenga banda dogo mita 3 x 4 kwa ajili ya kulaza wale kuku wasiohatamia.
Hivyo sikubaliani na mtoa mada kuwa unahitaji mil 1.5 kuanza - HAPANA. Hicho ni kiasi kukubwa sana; unataka kuwaogopesha watu wasijaribu kufuga eti kwa sababu hawana hiyo pesa.
Ww tayari hata jikoni unapo. Kwa mpangaji wa vyumba viwili atawaweka sebuleni? Obvious atahitaji shamba kabisa. Si rahisi bro
 
Kwa kuwa wafugaji wengi hawahitaji kujifunza ndo maana wanahangaika na chakula. Mimi natumia ngano, naotesha chakula (Hydroponics Fodder) - ambapo kilo mbili za ngano zinanipatia chakula kilo 14/16. Hizo ngano kilo moja naipata kwa gharama ya Tshs. 1,200 / 1,500. Hivyo suala la chakula kwangu sio shida; labda changamoto inakuja kwenye muda wa kuotesha - zoezi hili la kuotesha ni endelevu kama kupiga mswaki kila siku ila unapata chakula bora kwa gharama nafuu.
Kuhusu virutubisho natumia EM.1 ambayo lita moja inanipatia lita 20 za virutubisho ambavyo naweza kutumia mwaka mzima na kiasi kingine nikawauzia wafugaji majirani wanaoona umuhimu wa hivyo virutubisho.
Kwa ujumla nimekuwa mfugaji kwa muda mrefu hadi nimeona kuwa kufuga ni namna unavyoji-tune kufanya hiyo kazi.
Wewe utakuwa walewale, hao yote unayafanyia hewani? Weka wazi hilo eneo unayofanyia yote hayo umeme au unakodisha? Swala hapa ni kudanganya watu kuwa hufugaji huitaji mtaji mkubwa kitu ambacho siyo kweli!
 
Wewe utakuwa walewale, hao yote unayafanyia hewani? Weka wazi hilo eneo unayofanyia yote hayo umeme au unakodisha? Swala hapa ni kudanganya watu kuwa hufugaji huitaji mtaji mkubwa kitu ambacho siyo kweli!
Kama ni hivyo, basi hata mil 1.5 haitoshi kwa sababu hakuna kiwanja utakachonunua na kuanza ujenzi kwa pesa hiyo; labda vijijini huko. Mara nyingi mimi huwa napenda kuwashauri wale ambao tayari wana sehemu ya kufugia.
 
Kwa kuwa wafugaji wengi hawahitaji kujifunza ndo maana wanahangaika na chakula. Mimi natumia ngano, naotesha chakula (Hydroponics Fodder) - ambapo kilo mbili za ngano zinanipatia chakula kilo 14/16. Hizo ngano kilo moja naipata kwa gharama ya Tshs. 1,200 / 1,500. Hivyo suala la chakula kwangu sio shida; labda changamoto inakuja kwenye muda wa kuotesha - zoezi hili la kuotesha ni endelevu kama kupiga mswaki kila siku ila unapata chakula bora kwa gharama nafuu.
Kuhusu virutubisho natumia EM.1 ambayo lita moja inanipatia lita 20 za virutubisho ambavyo naweza kutumia mwaka mzima na kiasi kingine nikawauzia wafugaji majirani wanaoona umuhimu wa hivyo virutubisho.
Kwa ujumla nimekuwa mfugaji kwa muda mrefu hadi nimeona kuwa kufuga ni namna unavyoji-tune kufanya hiyo kazi.
wenye akili tumekuelewa sana...thank very much
 
Hahaha Nimecheka sana mkuu
Nimeongea ukweli mkuu nina fuga hao jamaa ni balaa Angalia picha apo ni saa moja wamegoma kuingia ndani wana juwa wakishaingia tu ndio mwisho wa kula.
Ka toto ka bata ka miezi 3 kanaweza kula sawa na Kuku wa 2 sema na usipo wapa msosi wana angaliaga kwa huruma kama vile ume mnyima mtoto pipi ukala wewe!
IMG_20181127_190548.jpg

Sema uzuri wa bata nyama sio tatizo kabisa kama ilivyo kwa kuku unaweza fuga kuku ukakosa wa kumla bata hukosi nyama hata siku moja!
Kuku unaweza kusema dah huyu Ana Angua sana au ana taga sana bata wote sawa ukichukuwa kisu atakaye jilengesha unaondoka naye bila kuangalia ni mweusi au mweupe labda useme bado nina penda kumuona!
Ukifuga Bata vizuri ukawa na kajiko kapisa!
IMG_20181118_183546.jpg
 
Hahaaaa nilipewa dili la kufuga bata nikajenga banda nikanzungushia eneo langu chicken wire nikanunua bata km kumi nikaanza kuwalisha ebhana wakafika 80 nia yangu wafike 100 niuze ikaja mvua ikapiga ile mbaya sikua najua mvua na bata hazipatani walikufa bata km hamsin kumbuka hao nilikua nanunua gunia la pumba kila wiki plus cost za ujenzi wa banda nikajikuta nimebaki na bata wadogo 18 na wakubwa 12 nilishikwa na hacra nikawagawa tu.Sasa hivi nafuga kuku wa kienyeji siwazingatii kivile ila naona wamekubali nao km 32.Ufugaji bila kujipanga ni hasara na tafuta mtaalamu sio hao waongo wa kwenye mitandao akufundishe kabla ya kuanza ufugaji.
 
uko sahihi kabisa, kwa mtu ambaye hakufanya hizi shughuli ataona uongo
Motivational speakers wanaharibu sana....
Kajitu kanagongea rimoti ya tecno kanaingia mtandaoni akisoma ufugaji wa kuku anafikiri ni kupika maandazi izo garama hapi juu bado chakula na madawa na vyombo vya chakula na maji ya bahari mimi mwenyewe mfugaji og
tatizo baadhi ya watu wanafuga kuku kwa kutumia vipeperushi na ukibahatika kuvisoma bila kufanya upembuzi yakinifu utaishia kuchukia ufugaji.
 
Hahaaaa nilipewa dili la kufuga bata nikajenga banda nikanzungushia eneo langu chicken wire nikanunua bata km kumi nikaanza kuwalisha ebhana wakafika 80 nia yangu wafike 100 niuze ikaja mvua ikapiga ile mbaya sikua najua mvua na bata hazipatani walikufa bata km hamsin kumbuka hao nilikua nanunua gunia la pumba kila wiki plus cost za ujenzi wa banda nikajikuta nimebaki na bata wadogo 18 na wakubwa 12 nilishikwa na hacra nikawagawa tu.Sasa hivi nafuga kuku wa kienyeji siwazingatii kivile ila naona wamekubali nao km 32.Ufugaji bila kujipanga ni hasara na tafuta mtaalamu sio hao waongo wa kwenye mitandao akufundishe kabla ya kuanza ufugaji.
Pole Sana mkuu ndio changa moto hizo!
 
Wewe utakuwa walewale, hao yote unayafanyia hewani? Weka wazi hilo eneo unayofanyia yote hayo umeme au unakodisha? Swala hapa ni kudanganya watu kuwa hufugaji huitaji mtaji mkubwa kitu ambacho siyo kweli!
Aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo. Karibu kituoni kwetu nikupeleke sehemu ninapofanyia shughuli hizo uone kwa macho yako. Sifichi chochote kwa sababu najua watanzania ni wazembe kutenda. Hata ukiona najua hutakuwa mshindani kwangu kwa sababu tayari umelemaa fikra.
 
KUna mtu kanambia bata wakiwa bandani bila kuruhusiwa kuzunguka hawatagi. Ni kweli????
 
Back
Top Bottom