Usia wa Roma Mkatoliki kwa wanaojiandaa kuoa

Usia wa Roma Mkatoliki kwa wanaojiandaa kuoa

Raymanu KE

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2022
Posts
8,611
Reaction score
16,118
Salute comrades!

Hitmaker wa NIPENI MAUA YANGU, Roma Zimbabwe kupitia ukurasa wake wa Instagram amewausia vijana wa kiume wanaojiandaa kuoa kwamba wasikurupuke tu kufanya maamuzi ya kuoa bali wawafanyie wachumba wao " vetting" ya kutosha.

Roma amesema kabla hujamuoa huyo mchumba wako na kumfanya mkeo na mama ya watoto wako,Kwanza jiulize maswali muhimu yafuatayo;

👉Je, huyu mchumba wako ataweza kuwa mama Bora kwa watoto wako?
Ataweza kutekeleza majukumu yake ipasavyo kama mama kwa watoto wenu?

👉Kwa mfano ikitokea siku ukapatwa na msala mzito utakaopelekea wewe kufungwa jela kwa miaka kadhaa,Je,huyo mkeo ataendelea kuwa mwaminifu kwako kwa kukutunzia tunda lako pamoja kulea watoto au ndo ataanza kuhanya hanya?
Au atakuwa anachepuka kisiri Siri ili angalau apate Cha kuwalisha watoto wenu akisubiria umalize kifungo?

👉Ukikumbwa na anguko la kiuchumi ukafilisika kabisa,je, huyo mkeo ataendelea kukupenda na kukutia moyo upambane mpaka pale utakapoinuka tena kiuchumi au ndo atakuacha upambane na umasikini wako?

Ukishajiuliza hayo maswali matatu hapo juu then unaweza kufanya tathmini yako ili ubaine Kama huyo unayetaka kumfanya mkeo anaweza shinda hayo majaribu endapo yatatokea.

Kijana usiangalie tu shape na sura ya mwanamke Kisha ukakurupuka kuoa, maana unaweza ukajutia uamuzi wako baadae.
 
Wanawake wote ni nyoka,
Kuna bifu la maisha kati ya nyoka na binadamu,
Yeyote anayemuona mwenzake humshambulia,
Nyoka hutaka kumnga'ta binadamu,
Binadamu hutaka kumuua nyoka,


Lakini kuna watu wanaishi na nyoka,
Wanawafuga na kuwachezea watakavyo,

Kuna watu wameoa wanawake pasua kichwa ila wanawacontrol vizuri kabisa,
Unapoishi na mwanamke ndani jua unaishi na nyoka,
Muda wowote anaweza kukugeuka au kukuangusha ama kukuua kabisa

Kama Hauwezi kuishi na nyoka usioe,
Wanawake wote ni nyoka

Biblia inasema tuishi nao kwa akili
 
Yeye al
Salute comrades!

Hitmaker wa NIPENI MAUA YANGU, Roma Zimbabwe kupitia ukurasa wake wa Instagram amewausia vijana wa kiume wanaojiandaa kuoa kwamba wasikurupuke tu kufanya maamuzi ya kuoa bali wawafanyie wachumba wao " vetting" ya kutosha.

Roma amesema kabla hujamuoa huyo mchumba wako na kumfanya mkeo na mama ya watoto wako,Kwanza jiulize maswali muhimu yafuatayo;

👉Je, huyu mchumba wako ataweza kuwa mama Bora kwa watoto wako?
Ataweza kutekeleza majukumu yake ipasavyo kama mama kwa watoto wenu?

👉Kwa mfano ikitokea siku ukapatwa na msala mzito utakaopelekea wewe kufungwa jela kwa miaka kadhaa,Je,huyo mkeo ataendelea kuwa mwaminifu kwako kwa kukutunzia tunda lako pamoja kulea watoto au ndo ataanza kuhanya hanya?
Au atakuwa anachepuka kisiri Siri ili angalau apate Cha kuwalisha watoto wenu akisubiria umalize kifungo?

👉Ukikumbwa na anguko la kiuchumi ukafilisika kabisa,je, huyo mkeo ataendelea kukupenda na kukutia moyo upambane mpaka pale utakapoinuka tena kiuchumi au ndo atakuacha upambane na umasikini wako?

Ukishajiuliza hayo maswali matatu hapo juu then unaweza kufanya tathmini yako ili ubaine Kama huyo unayetaka kumfanya mkeo anaweza shinda hayo majaribu endapo yatatokea.

Kijana usiangalie tu shape na sura ya mwanamke Kisha ukakurupuka kuoa, maana unaweza ukajutia uamuzi wako baadae

Yeye alijuliza kabla hajaimba Kikwete K

USSR
 
Wanawake wote ni nyoka,
Kuna bifu la maisha kati ya nyoka na binadamu,
Yeyote anayemuona mwenzake humshambulia,
Nyoka hutaka kumnga'ta binadamu,
Binadamu hutaka kumuua nyoka,


Lakini kuna watu wanaishi na nyoka,
Wanawafuga na kuwachezea watakavyo,

Kama Hauwezi kuishi na nyoka usioe,
Wanawake wote ni nyoka

Biblia inasema tuishi nao kwa akili
Babako aliwezaje kuishi na nyoka mpaka ukazaliwa wewe?
Jibu atakalokupa baba yako lifanyie kazi ipasavyo ili na wewe uishi na mwanamke vizuri Kama baba yako alivyoweza kuishi na mama yako.
 
Babako aliwezaje kuishi na nyoka mpaka ukazaliwa wewe?
Jibu atakalokupa baba yako lifanyie kazi ipasavyo ili na wewe uishi na mwanamke vizuri Kama baba yako alivyoweza kuishi na mama yako.
Mzee wangu alitumia akili sana sana sanaa najua hautaweza kunielewa kwa sasa pengine upo kwenye kipindi cha huba subiri shubiri

Ahsante
 
Watu wanabadilika, ni vigumu kutabili juu ya kesho. Ingawa Kuna viashiria ambavyo havina uhusiano wa moja kwa moja na fikra za mwanadamu kuhusu kesho. Jambo la msingi ni kuangalia kama ni mgumba tasa au lah.
 
Back
Top Bottom