Usianze kuwatajia madaktari ugonjwa... Hawapendi

Usianze kuwatajia madaktari ugonjwa... Hawapendi

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,346
"Daktari nina maumivu makali ya tumbo, nahisi hivi vitakuwa vidonda vya tumbo kabisa"... Maelezo ya namna hii humkera daktari na inaweza kusababisha usipate huduma vizuri. Madaktari hawapendi kuelekezwa ugonjwa. Unachotakiwa kufanya ni kueleza dalili za matatizo yako ya kiafya.

Maumivu, uvimbe, kiungo kushindwa kufanya kazi... pia elezea ni kwa muda gani (usiogope kuambiwa kwanini hukuwa umeenda hospitali siku zote), elezea kwa ufasaha sehemu, upande na kama maumivu ni ya moja kwa moja au ya kuja na kupoa.

Unaweza pia kutoa historia ya watu wa famili yako, au watu wa karibu na wewe kama waliwahi kuwa na matatizo kama uliyo nayo. Lakini usikimbilie kutaja ugonjwa unaohisi kuwa unaumwa...
 
Sawa Daktari Mkuu.@Tuko Mimi nina Ugonjwa wa matatizo ya kupenda Mke wangu Daktari Tuko utaweza kunisaidiaje? Nikimpenda mtu mke mpaka anajuwa kama nina mpenda nifanyeje ili tatizo hilo liniondokee Daktari wangu tuko?
 
Mzizimkavu,eti njia bora ya uzazi wa mpango ni hipi naombba ufafanuzi na athari zaki,kondom isiweke hapo
 
Kwa kweli mimi huwa nakasirika sana, na akijifanya mbishi namwandikia dawa kadri alivyosema na mwacha. Coz kusema hivi unamislead at the end of the day visit kibao kumbe tatizo ni jingine
 
Sawa Daktari Mkuu.@Tuko Mimi nina Ugonjwa wa matatizo ya kupenda Mke wangu Daktari Tuko utaweza kunisaidiaje? Nikimpenda mtu mke mpaka anajuwa kama nina mpenda nifanyeje ili tatizo hilo liniondokee Daktari wangu tuko?
pole tatizo hilo limekuanza lini?na umewahi kutumia dawa za aina gani!!kuna historia kama hiyo katika ukoo wako...?
 
Ni kweli chief TUKO...Hata madaktari pia hawaanzi na diagnosis(ugonjwa) wa naanza na History(dalili za ugonjwa) alafu examination(Uchunguzui kwa kuona au kushika) alafu invesigation( uchunguzi wa kimaabara au vipimo vingine) ndo daktari anajua mgonjwa anaumwa nini....japo sio magonjwa yote yanafata huo mtiririko.....sasa ukiend ana diagnosis(ugonjwa wako) unaharibu mtiririko...lakin pia unaweza kuta unaugojwa mwingine tofauti na unavyoona...mfano homa huweza kuletwa na malaria au UTI, otitis media(infection s kwnye maskio) sasa ukija na diagnosis hta daktari anakua biased kutafuta magonjwa mengine...
 
Kwa kweli mimi huwa nakasirika sana, na akijifanya mbishi namwandikia dawa kadri alivyosema na mwacha. Coz kusema hivi unamislead at the end of the day visit kibao kumbe tatizo ni jingine

Nina mashaka na taaluma yako mkuu.Na huenda wewe huwezi kabisa kufanya kazi kwa watu wa vijijini ambapo mf. huku kanda ya ziwa magonjwa mengi yanatambulika kwa majina mbalimbali mf.tumbo kuuma,kuhara,kifafa,kichefu chefu,nk yanajulikana kama mchango au nyoka!(nzoka),ama magonjwa ya kifua, njia ya hewa na mgongo na koo wanasema wanavidonda ama hata wengine wanaenda mbali na kusema wana Inzi walioingia kwenye njia ya hewa na kumsumbua mgonjwa kifuani na mgongoni!Sasa kama una tabia ya kukasirika kasirika utafanyaje kazi wewe?Unatakiwa kumsikiliza mgonjwa bila kumbeza hata kama amekwambia ugonjwa wake.Wewe ni jukumu lako kufanya kwa mujibu wa taaluma yako ili kumwonesha kuwa si rahisi tu kuja na diagnosis kwa kila tatizo hata kama linaonekana dogo.Na nikuhakikishie,utajenga heshima kubwa kwa mteja wako kuliko kumwandikia dawa ukiwa umemzira!kitu ambacho wengi hufanya si wewe peke yako.Pia kumbuka kwamba siku hizi baadhi ya watu hu google kutafuta maelezo juu ya matatizo yao na hata maelezo ya dawa kabla hajaenda kwa daktari!Kwa hiyo ni jambo la busara madajtari mkawa watulivu na kuheshimu kile mgonjwa anachokueleza.Msitamani kurambwa miguu tu eti kwa kudhani mna akili zaidi kuliko wateja wenu kwa vile tu ninyi ni madaktari!Badilikeni!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Utatuua Barca, huo sio udaktari

Kwa kweli mimi huwa nakasirika sana, na akijifanya mbishi namwandikia dawa kadri alivyosema na mwacha. Coz kusema hivi unamislead at the end of the day visit kibao kumbe tatizo ni jingine
 
Sawa Daktari Mkuu.@Tuko Mimi nina Ugonjwa wa matatizo ya kupenda Mke wangu Daktari Tuko utaweza kunisaidiaje? Nikimpenda mtu mke mpaka anajuwa kama nina mpenda nifanyeje ili tatizo hilo liniondokee Daktari wangu tuko?

hahaha Jf raha sana, asante MziziMkavu kwa kunichekesha...ngoja tumsubiri Dr Tuko aje
 
Last edited by a moderator:
..."Daktari nina maumivu makali ya tumbo, nahisi hivi vitakuwa vidonda vya tumbo kabisa"... Maelezo ya namna hii humkera daktari na inaweza kusababisha usipate huduma vizuri. Madaktari hawapendi kuelekezwa ugonjwa. Unachotakiwa kufanya ni kueleza dalili za matatizo yako ya kiafya... Maumivu, uvimbe, kiungo kushindwa kufanya kazi... pia elezea ni kwa muda gani (usiogope kuambiwa kwanini hukuwa umeenda hospitali siku zote), elezea kwa ufasaha sehemu, upande na kama maumivu ni ya moja kwa moja au ya kuja na kupoa.

Unaweza pia kutoa historia ya watu wa famili yako, au watu wa karibu na wewe kama waliwahi kuwa na matatizo kama uliyo nayo. Lakini usikimbilie kutaja ugonjwa unaohisi kuwa unaumwa...

Tatizo hata ukijieleza kwa saa nzima ataishia kukuandiakia kupima BS - Yaani malaria. Ndio maana siku nyingine tunajaribu kuwasaidia.
 
pole tatizo hilo limekuanza lini?na umewahi kutumia dawa za aina gani!!kuna historia kama hiyo katika ukoo wako...?
Mkuu Zamaulid tatizo langu ninalo siku nyingi nikimpenda mwanamke huwa ninamuonyesha kwa vitendo na

yeye huyo mwanamke huwa hanionyeshi kuwa ananipenda. niliwahi kumuuliza mke wangu siku moja tupo kitandani.Nilimwambia

Mke wangu ninakupenda lakini wewe kwanini hunipendi? Alinijibu hivi na mimi pia ninakupenda lakini sikuonyeshi kama ninakupenda

utapata kichwa. Haa nilishangaa sana, katika ukoo wetu Marehemu Mama yangu alikuwa anampenda Marehemu Dingi wangu huku

akimuonyesha mapenzi lakini dingi wangu hakuwa anamuonyesha mapenzi mama yangu ingawa Dingii wangu alikuwa anampenda

Mama yangu. Sasa itakuwa mimi nimerithi kwa marehemu Mama yangu mkuu?
 
MziziMkavu mmmmh
hivi wasema ya ukweli au unatuzuga tu hapa?

Mkuu Zamaulid tatizo langu ninalo siku nyingi nikimpenda mwanamke huwa ninamuonyesha kwa vitendo na

yeye huyo mwanamke huwa hanionyeshi kuwa ananipenda. niliwahi kumuuliza mke wangu siku moja tupo kitandani.Nilimwambia

Mke wangu ninakupenda lakini wewe kwanini hunipendi? Alinijibu hivi na mimi pia ninakupenda lakini sikuonyeshi kama ninakupenda

utapata kichwa. Haa nilishangaa sana, katika ukoo wetu Marehemu Mama yangu alikuwa anampenda Marehemu Dingi wangu huku

akimuonyesha mapenzi lakini dingi wangu hakuwa anamuonyesha mapenzi mama yangu ingawa Dingii wangu alikuwa anampenda

Mama yangu. Sasa itakuwa mimi nimerithi kwa marehemu Mama yangu mkuu?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kibaravumba,
Nadhani hoja si mgonjwa kuwa na uelewa kuhusu dalili alizonazo ni ugonjwa gani, shida ni kumng'ang'aniza daktari kuandika vipimo, dawa kulingana na "matakwa ya mgonjwa", bila kujali maamuzi ya daktari(clinical, intellectual judgement).

Mf. daktari, ninaumwa ninatapika, nina harisha, tumbo linauma, homa na ninachoka, hii Malaria, unajua juzi niliumwa na mbu wengi sana katika msiba..hebu nianzishie dawa za Malaria,.."

Kulingana na vitu fulani
1. Kuumwa na mbu
2. Homa na dalili nyinginezo
hapa mgonjwa anataka dawa kama alivyosema..wengi hufikiri hivi, ni kweli Malaria yaweza kuwa gonjwa mojawapo lakini inaweza kuwa, si Malaria kwa kuwa;
1. Muda wa mbu kumuuma hadi kujitokeza kwa dalili ni mfupi.
2. Magonjwa mengine mengi yanaweza kuwa yana dalili hizo.

Pili, Uwapo kwa daktari, huwa unajieleza kwa daktari sababu iliyo/zilizokufanya wewe (kama mgonjwa/mteja) kwenda hospitali hizi huitwa main complaint/chief complaints, sasa mojawapo ya vitu tusivyovipenda ni mtu/mgonjwa kusema dakari nimekuja nina Malaria, Typhoid, Sina Damu, n.k bafala yake kueleza dalili/vitu vikivyokufanya wewe ufikirie hivyo...mf. kichwa kuuma, kutapika, kuharisha, kichefu chefu, kujisikia/kuona kizungu zungu n.k

Tatu, dunia ya sasa magonjwa yanaandikwa kila mahali panoja na matibabu yake, jambo kuu la msingi madaktari wengi tunasema.."Treatment is individualized"..hii ikiwa na maana Ingawaje mgonjwa amekuja ana tatizo la kiafya mfano ana kisukari na Malaria pia, mwingine ana tatizo la Pneumonia lakini ana shida ya Pumu(Asthma) pia, au ana Tatizo la uoungufu wa damu lakini ana tatizo la Sickle cell, ...wagonjwa kama hawa matibabu yao si rahisi ("not straight forward") kama utavyosoma katika mitandao na kumshawishi daktari.

Jambo la muhimu ni kujielimisha (mgonjwa/mteja) kama unaweza, lakini kama huwezi omba msaada kwa watu wa taaluma hiyo.Na mwisho si vyema sana 'kumlazimisha' daktari kuandika kipimo, matibabu kulingana tu na 'kuhisi' kwako (hata kama mgonjwa ni daktari), vipimo na matibabu yafanyike kulingana na vipaumbele lakini zaidi kutegemeana na muonekano wa kiafya wa mgonjwa.
 
Last edited by a moderator:
MziziMkavu mmmmh
hivi wasema ya ukweli au unatuzuga tu hapa?
hahahaah umekuja kipenzi Mamndenyi akikusikia mke mwenzako bibie@Madame B utaleta hapa ugomvi shauri yako lakini, mchanga wa pwani huo mimi simo lakini. Marehemu yangu alikuwa anampenda sana marehemu Baba yangu lakini kama ujuavyo mwanamke akimuonyesha mwaname mapenzi basi yule Mwanamme atapata kichwa ni kweli kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo hata ukijieleza kwa saa nzima ataishia kukuandiakia kupima BS - Yaani malaria. Ndio maana siku nyingine tunajaribu kuwasaidia.

Mkuu, inakuwaje unaumwa wewe, then "unamsaidia" daktari, nilitegemea kusikilizwa hasa ndiyo kuna umuhimu kabla ya vipimo(maana magonjwa mengine yana epukika, mengine ni ya kudumu, n.k..lakini kama nia ingekuwa "kusaidia" ingekuwa ujisikiapo dalili unaenda Maabara kupima tu na kununua dawa.
 
uke wenza ndo ulionikimbiza kwako,
ngoja kwanza umalizane na Madame B nitakuja.

kweli mwanaume akipendwa sana huwa anaringa
sasa hapa nitafanyaje na mimi huwa siwezi kuigawa roho yangu
nikipenda mmoja ndo huyo huyo daah mitihani ya maisha hii tena.

hahahaah umekuja kipenzi Mamndenyi akikusikia mke mwenzako bibie@Madame B utaleta hapa ugomvi shauri yako lakini, mchanga wa pwani huo mimi simo lakini. Marehemu yangu alikuwa anampenda sana marehemu Baba yangu lakini kama ujuavyo mwanamke akimuonyesha mwaname mapenzi basi yule Mwanamme atapata kichwa ni kweli kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom